Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,650
- 21,011
Huku kwetu zamani kwenye misiba watu walikuwa wanaenda na kuni, mahindi na maharage, mbao zinanunuliwa na watu wanashirikiana na seremala wa karibu jeneza linatengenezwa. Pia sehemu zote ardhi ya kuzikia ilikuwa bure.
Leo bila pilau au wali nyama msima unaonekana 'haujanoga 'na watu hawaji na mchele wala nyama. Gharama karibu zote ni wafiwa. Majeneza bei juu. Sehemu fulani za kuzikia zinauzwa. Na kumezuka tabia ya kukodi magari ya muziki ambayo huwa na mike yakitangaza majonzi barabarani na kupiga nyimbo za huzuni. Mbaya zaidi msiba huja ghafla so hakuna michango kama ya harusi hivyo wafiwa huwa na mzigo mzito.
Nini kimetokea? ubepari, mabadiliko ya kawaida au ndiyo masuala ya showoff?
Leo bila pilau au wali nyama msima unaonekana 'haujanoga 'na watu hawaji na mchele wala nyama. Gharama karibu zote ni wafiwa. Majeneza bei juu. Sehemu fulani za kuzikia zinauzwa. Na kumezuka tabia ya kukodi magari ya muziki ambayo huwa na mike yakitangaza majonzi barabarani na kupiga nyimbo za huzuni. Mbaya zaidi msiba huja ghafla so hakuna michango kama ya harusi hivyo wafiwa huwa na mzigo mzito.
Nini kimetokea? ubepari, mabadiliko ya kawaida au ndiyo masuala ya showoff?