Mishahara ya watumishi wa umma haitakaa ilingane

Mishahara ya watumishi wa umma haitakaa ilingane

Mukulu wa Bakulu

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2014
Posts
4,050
Reaction score
12,966
Tuwe wakweli, mishahara ya watumishi wa umma haitakaa ikawa sawa au kakaribiana.

Baada ya magufuri kuingi ikulu baadhi ya watu hasa watumishi wa umma wameanza kupata ndoto za mchana na kuanza kuomba magufuri kuondoa tofauti iliyopo katika mishahara ya watumishi wa umma.

Ni kweli kwamba kuna tofauti kubwa sana katika mishahara ya watumishi wa umma. Lakini lazima tuwe wakweli, haiwezekani mfanyakazi wa halmashauri,mfano mhasibu ukalingana mshahara sawa na mhasibu wa dawasco au ttcl.

Halmashauri ni sehemu ambapo ni kwa ajili ya matumizi tu na hakuna uzalishaji wa pesa,haiwezekani ikawa sawa na dawasco au tanesco au tpdc ambao wanafanya biashara,wanazalisha na kuuza.

Haiwezekani mkusanya kodi wa tra anaekutana na wateja,kujadiliana nao kiwango cha kulipa na kumshawishi mtu kulipa kodi alingane mshahara na mhasibu wa halmashauri.

Tuangalie aina ya kazi wanayoifanya watu na mishahara yao,tusitake kujilinganisha nao.

Wenye ndoto za mchana kama hizo achaneni nazo.
 
CHUKUA KOPO Ingiza Ndani Kisha Kalale, Usikojoe Kitandani Kojolea Kwenye Hl Kopo Sawa Mtoto
 
Ni sawa lkn basi Hiyo tofaut isiwe kwa kiwango kilichopo jaman, kunatofaut kubwa sana ambayo inaumiza sana watu
 
Haya mambo ya kijinga sana na ni hoja dhaifu sana, unafikiri mtumishi gani hataki kufanya kazi katika shirika la umma?je kwa nini mashirika hayo yanaendeshwa kwa hasara ingali wanapewa mishshara mikubwa?je ni kweli waajiriwa kwenye mashirika wanakusanya fedha?
Huu nasema ilikuwa mradi wa watoto wa vigogo, haiwezekani mshahara wa certificate wa shirika la umma ulingane na degree holder wa local or central government.Madhara ya serikali dhaifu ndiyo namkumbuka Mwigulu alilisemea kuwa atakomesha sana ila sasa yuko kilimo na uvuvi sijui watamsikiliza kwenye baraza la mawaziri.
 
darasa la kwanza hadi la saba mpo pamoja.....fom one had 4 mko pamoja....fom six mnaenda kibaha kusoma CBA pamoja...chuo kikuu mko sokoine university morogoro mnasomea mazao...then zinatangazwa ajira wizara ya kilimo..mnaitana mna apply kwa bahati nzuri mnapewa wote ajira...
mmoja anapewa idara ya utafiti anaanza na milion moja..
mwingine idara ya afisa kilimo mshahara laki nne na nusu...
kaka ni pasua kichwa..
hujajua hili swala vile limekaa
 
Hivi na wewe ni mwanafunzi uliye maliza chuo kikuu? Kazi ipo kwa kweli
 
Kwani nchi gani ambayo mishahara yao inalingana,tuanzie hapo ndugu muanzisha mada
 
darasa la kwanza hadi la saba mpo pamoja.....fom one had 4 mko pamoja....fom six mnaenda kibaha kusoma CBA pamoja...chuo kikuu mko sokoine university morogoro mnasomea mazao...then zinatangazwa ajira wizara ya kilimo..mnaitana mna apply kwa bahati nzuri mnapewa wote ajira...
mmoja anapewa idara ya utafiti anaanza na milion moja..
mwingine idara ya afisa kilimo mshahara laki nne na nusu...
kaka ni pasua kichwa..
hujajua hili swala vile limekaa

Hili mbona rahisi, kasheshe ni jinsi kazi hizo za TRA zinavyopatikana. Halafu huyo anayepata mara 10 ya mwenzake ndiye ana first class au upper second?

Majipu ya nchi hii ni mengi kiasi kwamba hata msukuma asipolala kwa miaka 5 hawezi kutumbua hadi 25%.
 
Mshahara uwe sawa kwa kazi za umma kama mtu hataki akafanye kazi shambani kwake.
Katika kutumikia umma kila mtu ni muhimu.
Hakuna TRA bila mwalimu. Bila polisi fedha zote wanazokusanya TRA zitaibiwa na vibaka wasio na ajira.
Bila wanajeshi mipaka ya nchi haitakua salama.
Bila Madaktari wafanyakazi na wananchi watakua na afya duni.
Huu mradi wa mishahara kuwa tofauti ulikua ni mradi wa kutengeneza madaraja na kudharauliana kwenye kulitumikia taifa . Kamwe haikubaliki kwenye taifa la kijamaa kuwa na watumishi wanaoneemeka kwa rasilimali za umma huku wengine wakiteseka kwa watumikia wengine.
Huu ni mfumo mbaya sana sana. Wizara na idara zote ni muhimu.
Kama mtu ataona hawezi kulitumikia taifa hili kwa uaminifu kwa sababu tu ya kutaka kuwa awe tofauti na mwenzake mwenye elimu sawa na ya kwake basi awapishe wenye moyo wa kizalendo ambao ni wengi mno.
Tutapinga huu unyonyaji wa watumishi wa idara ndani ya mashirika ya umma kunyonya rasilimali za nchi na kuwafanya wengine ni vibarua wao.
Hali hii ya Wachache wanaojilimbikizia mamishahara na kujenga nyumba 73 Kwenye eneo moja huku watumishi wengine wakijenga nyumba moja tu kwa tabu na mikopo yenye riba kubwa inapoteza uzalendo.
Kila mtu anataka kula vizuri na kuishi kama binadamu na alee watoto wake kama wengine.
 
Tuwe wakweli, mishahara ya watumishi wa umma haitakaa ikawa sawa au kakaribiana.

Baada ya magufuri kuingi ikulu baadhi ya watu hasa watumishi wa umma wameanza kupata ndoto za mchana na kuanza kuomba magufuri kuondoa tofauti iliyopo katika mishahara ya watumishi wa umma.

Ni kweli kwamba kuna tofauti kubwa sana katika mishahara ya watumishi wa umma. Lakini lazima tuwe wakweli, haiwezekani mfanyakazi wa halmashauri,mfano mhasibu ukalingana mshahara sawa na mhasibu wa dawasco au ttcl.

Halmashauri ni sehemu ambapo ni kwa ajili ya matumizi tu na hakuna uzalishaji wa pesa,haiwezekani ikawa sawa na dawasco au tanesco au tpdc ambao wanafanya biashara,wanazalisha na kuuza.

Haiwezekani mkusanya kodi wa tra anaekutana na wateja,kujadiliana nao kiwango cha kulipa na kumshawishi mtu kulipa kodi alingane mshahara na mhasibu wa halmashauri.

Tuangalie aina ya kazi wanayoifanya watu na mishahara yao,tusitake kujilinganisha nao.

Wenye ndoto za mchana kama hizo achaneni nazo.

We mleta mada ni mpuuzi sana. Kwahyo unaona sawa kutupigia vumbi ssi walimu wakati wote tuna degree eti kisa uko TRA?
 
Inawezekana tena sana2 swala ni kwamba mwisho wa siku wote ni watumishi wa umma..kikubwa levo zao za elimu2 sioni sababu ya msingi ya mwalimu wa shahada kupishana na mwenye shahada wa TRA zaid ya laki 4
 
Wanaota kweli

levo zilizopangwa kikazi na ukubwa wa eneo wanalokava au mji au nayo inaingiaga ila haitofautiana kuoshia kusema kuwa mtu yulr na yule cheo sawa mishahara imepishana sanaaaaa.

Kuna mengi natumaini wanaopanga mishahara wanajua wanachofanya na sio kuonea.
 
Mishahara isulingane ni sawa ila mimi wa kima cha chini ambae ninakwenda soko moja la bidhaa pamoja na huyo wa tra niwezeshwe kupanga nyumba, kulipa bill zangu, kununua chakula, kuvaa na nauli za kwenda job.
 
Back
Top Bottom