Misamaha ya kodi Bakwata na Taasisi nyingine

Misamaha ya kodi Bakwata na Taasisi nyingine

Tutoe michango yetu kwa busara na kuheshimiana. Huo ndo ustaraabu.
 
Ishu iliyopo sio kwamba bakwata wameagiza magari mangapi ila wameshindwa kuitolea maelezo ya kutosha hiyo starlis iveco waliyoagiza simply..

Yaani hawa badala ya kuuliza kwanini wamefukuzwa, yeye anaweka jicho la kidini
 
Hao wengine waliwahi kuombwa kutolea maelezo magari yao? Hamna chochote ni unafiki waache kuomba maelezo waliosamehewa magari 2000 na kitu watake maelezo kwa waliosamehewa magari 82!

Kwa kuwa hawakuombwa, ina maana waliisha toa maelezo, umeona ni nani amesaini hiyo barua?
 
Hii Ndio Tanzania ya Leo, tunalilia Amani na Utulivu, lakini Watanzania hasa ( Raia) lazima tukumbuke kwamba Amani haiji ikiwa Serikali zetu zitafanya Ubaguzi juu ya kundi Fulani.

Ifuatayo hapo chini ni Orodha ya makisio ya MISAMAHA YA KODI kwa magari (TU)?yaliyoingizwa nchini kupitia Taasisi za Dini kuanzia mwaka 2006-2015 (hadi sasa).

1. BAKWATA na Taasisi zake (Shule, Vyuo, Hospitali, misikiti etc)
-magari 82 ya aina tofauti yenye thamani ya Bil 6.8 (Kodi iliyosamehewa Bil 1.9),
2. Kanisa Katoliki na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, parokia etc) ? Magari 691 yenye thamani ya Bil 59.5 (Kodi iliyosamehewa Bil 19.3),
3. CCT na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, makanisa etc), magari 527 yenye thamani ya Bil.42.9 (kodi iliyosamehewa Bil.13.8),
4. Makanisa ya Pentecoste na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, makanisa etc) ? magari 2,719 ya aina mbalimbali yenye thamani ya Bil 186.1 (kodi iliyosamehewa Bil 57.4),
5. Taasisi nyingine za dini (Hindu, Budha etc) magari 203 ya aina mbalimbali yenye thamani ya Bil 36.4 (kodi iliyosamehewa Bil 9.01).

JAUMLA ya Magari yaliyoingizwa nchini kwa mwavuli wa Taasisi za dini tangu Mwaka 2006 (Magari 4,222).
JUMLA ya Kodi iliyosamehewa BIL 102.41. Na ‎Hizi‬ ni pesa zinazotosha kujenga Mabunge matatu yenye hadhi sawa na Bunge la Dodoma na chenge ikabaki.

Kumbuka hii ni misamaha ya Kodi kwa magari tu bado vitu vingine kama Vifaa vya Hospitalini, Vitabu vya mashuleni na vyuoni,biashara za ujenzi na etc?

N:B Je TRA itaomba nyaraka kwa taasisi nyengine za kidini? kwani misamaha kwa taasisi za hizo nyengine inatisha na hayo kuna watu waliuliza bakwata na magani 82 ni ya kazi gani.. Sasa sijui watasemaje na magari 2719, 203, 527 na 691.

Tujadili hili na najua wengine watasema udini kwa sababu limewagusa wao

Uamuzi wa TRA kweli kwa mtazamo unaonyesha ubaguzi. Zoezi hili lilifaa liwe kwa Taasisi zote zinazopata Misamaha Nchi Nzima.
Haya magari mengine utashangaa ziko huku uswahili na zikiendeshwa na warembo au Mashamba boi wenyewe kazi maalum wenye mahusiano na watendaji wa hizi Taasisi.


Nadhani eneo hili la misamaha ya kodi naona Magufuli hajakumbushwa kama Jipu la huku nalo ni Balaa!
Umepata kusikia hadi Toile Paper ilipata kusamehewa Kodi?


Nadhani huku ni kukimbizana perege na kuwaacha Kabare akijinafasi.



RIPOTI YA CAG Ni madudu kila kona - Mtanzania-Gazeti la ...

mtanzania.co.tz/?p=4508


Translate this page
May 20, 2015 - Kuhusu misamaha ya kodi, Profesa Assad alisema iliyotolewa kwa mafuta ... kati ya Sh milioni 465.23, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ...


Misamaha ya kodi Tanzania: - Twaweza.org

www.twaweza.org/.../Misamaha%20ya%20kodi%20T...


Translate this page
taifa au TZS 695 bilioni zilitolewa kama misamaha ya kodi. Ukubwa wa ... Misamaha ya kodi inayotolewa na Mamlaka ya Mapato (TRA) katika visiwa vya.
 
Daaahh kazibao umemaliza
 
Last edited by a moderator:
Sidhani kama TRA wamekurupuka katika kuibana Bakwata na hii misamaha.

Kwa kuiangalia tu ile barua nahisi kuwa yale maombi hayakuwa ba maelezo ya kutosha kuhusiana na matumizi ya gari tajwa.

Kuna kosa pia ambalo ninaliona hapa. Bakwata inatumika kama mwamvuli wa kupatia misamaha ya kodi kwa niaba ya taasisi nyingine. Jambo hili ni makosa.
Msamaha unapaswa kuomba na 'mlipa kodi' mwenyewe. Na akivunja masharti ya msamaha basi 'mlipa kodi' ndio anapaswa awajibike. Ninaamini ni kosa katika 'Tax Compliance and Administration' kuipa Bakwata misamaha ya kodi kwa niaba ya walipa kodi wengine.

Kumekuwa na hoja kuwa makanisa na taasis za kikristo zimepewa misamaha ya magari lukuki na hivyo Bakwata wanaonewa kwa sababu ya dini yao.
Hili nalipinga. Bakwata naamini kabisa kuwa Bakwata hawajanyimwa sababu ya DINI. Bali kutokana na maombi ya msamaha kutoendana na shughuli zilizosajiliwa za Bakwata. Hiyo inaleta shaka na kuhitaji kufanya "audit" ya msamehewa na misamaha aliyopewa.
Kwa mfano shule moja ya kidini (taasis) haiwezi pewa misamaha ya magari 30 bila maelezo ya kutosha na kuthibitisha kufuata masharti ya misamaha iliyopita.

Hata taasisi hizo nyingi za kikiristo kila moja huomba na mara kadha wa kadha taasisi hizo mbali mbali hunyimwa pia. Ni kwa sababu tu watu hawaweki mitifuano yao na TRA kwenye mitandao.

Na hata wafanyakazi wanaostahili misamaha ya kodi za magari nao hunyima misamaha hiyo pale maelezo au vigezo vinapokuwa havikidhi.

Tuache kuleta udini kwenye mambo ya kiutawala na udhibiti hasa wa kodi.
Tuwe makini na misamaha yote. Mambo ya NGO za Ukimwi yatajirudia kwa kasi, ambapo watu walijinufaisha na misaada lukuki ikiwa ni pamoja na misamaha ya kodi.

Toa ushahidi wa hizo taasisi za kikristo zilizonyimwa/kukataliwa ?hatutaki maneno ya kufikirika hapo!lete facts tujiridhishe!
 
Toa ushahidi wa hizo taasisi za kikristo zilizonyimwa/kukataliwa ?hatutaki maneno ya kufikirika hapo!lete facts tujiridhishe!

Kweli wewe ni kipofu aliyekubuhu na uliyejaa udini.
Siwezi bandika jukwaani hivi sasa bila idhini ya wahusika.
Lakini nina amini jukwaa hili lina watu wengi wa taasisi zilizonyima misamaha ya kodi kwa nyakati tofauti na watathibitisha maneno yangu.
Badilika ndugu yangu.😡
 
mtoa mda umewai kujulza kwa nn mh rais avamie bandarn huko ndiko kwenye shda! why bakwata not kwingme? viva tra go ahead
 
Watu kam wanachngia dini flani imeonewa ila mm naona kam ni jambo kufeel proud unapoona dini yako inatekeleza sheria za nchi ipasavyo maana apo naona kama kulkuwa na uchafu ndani unasafishwa tukibak chombo safi mbele ya mwenyezi najisifia dini ni safi...
 
Toa ushahidi wa hizo taasisi za kikristo zilizonyimwa/kukataliwa ?hatutaki maneno ya kufikirika hapo!lete facts tujiridhishe!

Kweli wewe ni kipofu aliyekubuhu na uliyejaa udini.
Siwezi bandika jukwaani hivi sasa bila idhini ya wahusika.
Lakini nina amini jukwaa hili lina watu wengi wa taasisi zilizonyima misamaha ya kodi kwa nyakati tofauti na watathibitisha maneno yangu.
Badilika ndugu yangu.😡

Na wenzio washakujibu hapa
https://www.jamiiforums.com/showthread.php?p=14821242
 
Hivo Hatuna haja ya Kubisha na kusema kwamba Serikali ya CCM au Serikali ya Muungano Haina Dini.. Ushahidi Mdogo ambao ulikuwa Unajulikna kutokana na Unawiri wa Kundi la Dini Fulani na Unyonyaji au UDhoofishaji wa Kundi la Dini Nyengine ni Huu hapa.

Hapa tunaweza kuona Tofauti kubwa ya Misamaha ya Kodi ya Taifa Baina ya BAKWATA na MAKANISA. Na Hii nataka niwambie Wasomaji kwamba sio FITINA ya Kidini bali Tunataka Nchi Zetu Mbili Tuzipendazo yaani Tanganyika na Zanzibar na Serikali ya Muungano. Ziwe INVIGILANT na kadhia hii.

Nakufanya FAIRNESS (Haki) juu ya Misamaha hii. Kwasababu Nchi Nyingi za Ulaya Zina Makanisa mengi kuliko Misikiti au Vikundi Vingi vya NGO za Wakristu kuliko Waislamu. Lakini Ruzuku ya Serikali inapogaiwa Hugaiwa Sawa Sawa Nor Matter Who is Religion are?

Kodi za Nchi huwa hazisamehewi Ovyo Ovyo kwasababu tu ya Udini, Ukabila au Ucheo.. Nchi ya Tanzania imekuwa masikini kushindwa hata kumiliki Ndege yake Wenyewe. Na Wananchi Wake Wamekuwa na hali dhaifu na hata kukosa Basic Services kama vile Maji Safi. Na Tanzania imekuwa Omba omba kwa Serikali yake ya CCM, ambayo imetutawala zaidi ya miaka 52 sASA- kukosa democrasia na kukataa maendeleo.

Isipokuwa kufanya Ufisadi kutudunisha sisi Wananchi wa kawaida dhidi ya Umasikini.. Matajiri Wanazidi kutajirika na Masikini wanazidi kumasikinika.. Wananchi wenye asili ya Kikristo Wanazidi Kunawiri kwa Vyeo na Elimu za Juu na Wale Nduguzao Waislamu Wanazidi Kudhalilishwa, kufelishwa na kukamatwa wakiwekwa Jela.

Hii Ndio Tanzania ya Leo, tunalilia Amani na Utulivu, lakini Watanzania hasa ( Raia) lazima tukumbuke kwamba Amani haiji ikiwa Serikali zetu zitafanya Ubaguzi juu ya kundi Fulani.

Ifuatayo hapo chini ni Orodha ya makisio ya MISAMAHA YA KODI kwa magari (TU)?yaliyoingizwa nchini kupitia Taasisi za Dini kuanzia mwaka 2006-2015 (hadi sasa).

1. BAKWATA na Taasisi zake (Shule, Vyuo, Hospitali, misikiti etc)
-magari 82 ya aina tofauti yenye thamani ya Bil 6.8 (Kodi iliyosamehewa Bil 1.9),
2. Kanisa Katoliki na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, parokia etc) ? Magari 691 yenye thamani ya Bil 59.5 (Kodi iliyosamehewa Bil 19.3),
3. CCT na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, makanisa etc), magari 527 yenye thamani ya Bil.42.9 (kodi iliyosamehewa Bil.13.8),
4. Makanisa ya Pentecoste na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, makanisa etc) ? magari 2,719 ya aina mbalimbali yenye thamani ya Bil 186.1 (kodi iliyosamehewa Bil 57.4),
5. Taasisi nyingine za dini (Hindu, Budha etc) magari 203 ya aina mbalimbali yenye thamani ya Bil 36.4 (kodi iliyosamehewa Bil 9.01).

JAUMLA ya Magari yaliyoingizwa nchini kwa mwavuli wa Taasisi za dini tangu Mwaka 2006 (Magari 4,222).
JUMLA ya Kodi iliyosamehewa BIL 102.41. Na ‎Hizi‬ ni pesa zinazotosha kujenga Mabunge matatu yenye hadhi sawa na Bunge la Dodoma na chenge ikabaki.

Kumbuka hii ni misamaha ya Kodi kwa magari tu bado vitu vingine kama Vifaa vya Hospitalini, Vitabu vya mashuleni na vyuoni,biashara za ujenzi na etc?

N:B Je TRA itaomba nyaraka kwa taasisi nyengine za kidini? kwani misamaha kwa taasisi za hizo nyengine inatisha na hayo kuna watu waliuliza bakwata na magani 82 ni ya kazi gani.. Sasa sijui watasemaje na magari 2719, 203, 527 na 691.
Tujadili hili na najua wengine watasema udini kwa sababu limewagusa wao

Kwenye suala la kodi zinazohusisha Taasisi za kidini Nchini tufikie mahali sasa tuione Tanzania Kwanza.
Taasisi hizi zimekuwa zinasamehewa kodi kwa malengo mazuri ila baadhi zimefikia kutumia vibaya matumizi ya misamaha hiyo ya kodi,Tumeona baadhi wakijisifu kwa magari ya kifahari yanayotumiwa na Matajiri huko ulaya kwa anasa BMW, Range Rover Vogue, Land Cruiser V8 ,Benz magari zaidi ya mawili, Tunashuhudia Taasisi hizi zenye kupewa misamaha ya kodi kwenye Mahospitali yao Gharama za matibabu zinaenda sawa na Hospitali Binafsi zenye kulipa kodi, Tunashuhudia Gharama za mashule ya taasisi hizi zikiwa juu kabisa Taasisi ambazo zingempa unafuu fulani Mtanzania,Tufikie suala la misamaha hiyo kuangaliwa upya Taasisi hizi zilipe kodi kwa kuwa inayojengwa ni Tanzania.
 
hapo bado wanapitisha na unga ni hatar hii misamaha ifutwe kama awataki wasiagize ivyo vitu vyao bil 57 aisee
 
mkuu mashirika ya dini yanafanya kazi nying za kuisaidia serikali hasa
elimu na afya
hospital kama
bugando
kcmc
tumaini
hydom
selian
etc zinatibu mamilioni ya watu bila kujali imani
vyuo au shule kama
marian
mau semimary
loyola
st agustine
tumaini
ruaha
bugando heath college
kcm etc
wanasoma maelfu ya watoto so si jambo jema kuwadai kodi vingnevyo serikali iendeshe shule zote na hospipali zote
 
Swala sio ukubwa wa misamaha. Bakwata hawajahojiwa kwa nini wamevuka kiwango cha misamaha, la hasha.
Swala ni vigezo vya msamaha wa kodi na masharti yake.
Ukivunja masharti ya msamaha wa kodi ni msala. Haijalishi we ni mkristo au muislam.
Kama wamevunja sheria ya kodi basi wamevunja tu, dini haihusu.
Tutakujaleta dini hadi kwenye ICD na makontena eti mbona watuhumiwa wengi wana majina ya dini ya kiislam. Basi wanaonewa.
Hiyo ni dhana potofu. Ulipaji kodi na ufuata sheria haujali dini.
Bakwata watekeleze matakwa ya kisheria na mjadala upite.


swaga zao huwa ni kukimbilia kuonewa wanapenda kubebwa
 
Haya makanisa ya Pentecoste kwann yasifungiwe jamani,
Maana mtu anaanzisha kanisa anajibana kwny kichochoro yan mtaa mmoja una makanisa hata 10 matokeo yake wanaanza kurushiana vijembe,

Nadhani serikali iangalie upya juu ya haya makanisa yanayoibuka kila uchwao,
Ndio na mafisadi wanajichomeka humo humo kufanya yao.


mkuu uhuru wa kaabudu kasome tena katiba ya nchi
 
hvi taasis ya kiislam ni bakwata peke yake?wale wanaotoaga matamko nyakati za uchaguzi wapo taasis zipi?
 
Hivo Hatuna haja ya Kubisha na kusema kwamba Serikali ya CCM au Serikali ya Muungano Haina Dini.. Ushahidi Mdogo ambao ulikuwa Unajulikna kutokana na Unawiri wa Kundi la Dini Fulani na Unyonyaji au UDhoofishaji wa Kundi la Dini Nyengine ni Huu hapa.

Hapa tunaweza kuona Tofauti kubwa ya Misamaha ya Kodi ya Taifa Baina ya BAKWATA na MAKANISA. Na Hii nataka niwambie Wasomaji kwamba sio FITINA ya Kidini bali Tunataka Nchi Zetu Mbili Tuzipendazo yaani Tanganyika na Zanzibar na Serikali ya Muungano. Ziwe INVIGILANT na kadhia hii.

Nakufanya FAIRNESS (Haki) juu ya Misamaha hii. Kwasababu Nchi Nyingi za Ulaya Zina Makanisa mengi kuliko Misikiti au Vikundi Vingi vya NGO za Wakristu kuliko Waislamu. Lakini Ruzuku ya Serikali inapogaiwa Hugaiwa Sawa Sawa Nor Matter Who is Religion are?

Kodi za Nchi huwa hazisamehewi Ovyo Ovyo kwasababu tu ya Udini, Ukabila au Ucheo.. Nchi ya Tanzania imekuwa masikini kushindwa hata kumiliki Ndege yake Wenyewe. Na Wananchi Wake Wamekuwa na hali dhaifu na hata kukosa Basic Services kama vile Maji Safi. Na Tanzania imekuwa Omba omba kwa Serikali yake ya CCM, ambayo imetutawala zaidi ya miaka 52 sASA- kukosa democrasia na kukataa maendeleo.

Isipokuwa kufanya Ufisadi kutudunisha sisi Wananchi wa kawaida dhidi ya Umasikini.. Matajiri Wanazidi kutajirika na Masikini wanazidi kumasikinika.. Wananchi wenye asili ya Kikristo Wanazidi Kunawiri kwa Vyeo na Elimu za Juu na Wale Nduguzao Waislamu Wanazidi Kudhalilishwa, kufelishwa na kukamatwa wakiwekwa Jela.

Hii Ndio Tanzania ya Leo, tunalilia Amani na Utulivu, lakini Watanzania hasa ( Raia) lazima tukumbuke kwamba Amani haiji ikiwa Serikali zetu zitafanya Ubaguzi juu ya kundi Fulani.

Ifuatayo hapo chini ni Orodha ya makisio ya MISAMAHA YA KODI kwa magari (TU)?yaliyoingizwa nchini kupitia Taasisi za Dini kuanzia mwaka 2006-2015 (hadi sasa).

1. BAKWATA na Taasisi zake (Shule, Vyuo, Hospitali, misikiti etc)
-magari 82 ya aina tofauti yenye thamani ya Bil 6.8 (Kodi iliyosamehewa Bil 1.9),
2. Kanisa Katoliki na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, parokia etc) ? Magari 691 yenye thamani ya Bil 59.5 (Kodi iliyosamehewa Bil 19.3),
3. CCT na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, makanisa etc), magari 527 yenye thamani ya Bil.42.9 (kodi iliyosamehewa Bil.13.8),
4. Makanisa ya Pentecoste na Taasisi zake (vyuo, shule, hospitali, makanisa etc) ? magari 2,719 ya aina mbalimbali yenye thamani ya Bil 186.1 (kodi iliyosamehewa Bil 57.4),
5. Taasisi nyingine za dini (Hindu, Budha etc) magari 203 ya aina mbalimbali yenye thamani ya Bil 36.4 (kodi iliyosamehewa Bil 9.01).

JAUMLA ya Magari yaliyoingizwa nchini kwa mwavuli wa Taasisi za dini tangu Mwaka 2006 (Magari 4,222).
JUMLA ya Kodi iliyosamehewa BIL 102.41. Na ‎Hizi‬ ni pesa zinazotosha kujenga Mabunge matatu yenye hadhi sawa na Bunge la Dodoma na chenge ikabaki.

Kumbuka hii ni misamaha ya Kodi kwa magari tu bado vitu vingine kama Vifaa vya Hospitalini, Vitabu vya mashuleni na vyuoni,biashara za ujenzi na etc?

N:B Je TRA itaomba nyaraka kwa taasisi nyengine za kidini? kwani misamaha kwa taasisi za hizo nyengine inatisha na hayo kuna watu waliuliza bakwata na magani 82 ni ya kazi gani.. Sasa sijui watasemaje na magari 2719, 203, 527 na 691.

Tujadili hili na najua wengine watasema udini kwa sababu limewagusa wao

Mi nadhani TRA wameanza na bakwata lakini watahoji kila taasisi!
Labda kwa kuwa bakwata ilikuwa na idadi ndogo ya magari kuhoji imekuwa nyepesi, wengine uchunguzi unaendelea wakiwa tayari wataombwa nao walete vielelezo!
Shida ya watanzania wengi hawajui wanamtumikia nani?
Wapo ambao Tanzania nafasi yake ni ya tatu baada ya dini na kabila, wengine ya NNE, baada ya kabila, dini na chama! Etc!
Hayo sio tatizo Ila linapokuja suala la kuwa Tanzania imedhulumiwa na dini, kabila au chama au mtu binafsi, tunaomba muipe haki yake jamhuri!
Mimi ni muislam na nimeipenda dini yangu na Tanzania ya pili lkn kama dini yangu Imeidhulumi Tanzania basi ijiandae kulipa, au kama wajanja wachache ndani ya taasisi wamefanya hivyo, wawajibisjwe na nchi, na taasisi!
Wale wakristo wakiwemo viongozi wa nchi, nao pia wajue haki ya Tanzania italindwa na dhamana ya vyeo vyao, wote tutoe ushirikiano kwa TRA kukamilisha kurejesha mapato yaliyokwepwa na inapobidi kuzisaidia mahakama na vyombo vya uchunguzi kuhakikisha haki inatendeka kwa mtu, taasisi na nchi yetu!
 
Back
Top Bottom