Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Jamaa mmoja akiwa kwenye gari yake aliwaona watu wawili kando ya barabara wakila nyasi.Akamuamuru dereva asimame;akashuka na kwenda kuwahoji:kwa nini mnakula nyasi?Wale wakamjibu:hatuna hela ya chakula.Akawambia wapande kwenye gari awapeleke kwake.Wale jamaa kuona wanaenda pewa msaada,wakaomba jamaa akawapitie wake zao wawili na watoto 13.Jamaa akasema haina shida,akaenda akawachukua wote.Akiwa njiani kuwapeleka kwake,mmoja wa wale jamaa akaamua kumshukuru kwa msaada mkubwa anaoenda kuwapa.Jamaa akajibu;kwa nini niwaache ndugu zangu mkipata shida na nyasi chafu za barabarani wakati nyumbani kwangu kuna nyasi ndefu zenye kimo cha mita moja!