"MIRUNGI" ni Biashara huria Moshi na Arusha??

"MIRUNGI" ni Biashara huria Moshi na Arusha??

Mandla Jr.

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2013
Posts
3,098
Reaction score
631
Kama ndio mara ya kwanza kufika Moshi au Arusha utashangaa sana, vijana wanakula majani kama mbuzi...Hatari sana kumbe sio majani ni Mirungi!!!

Huku polisi sio wakali kabisa juu ya utafunaji majani haya, na uuzaji wa mirungi maarufu kama "Miraa".
Na wauzaji wanafahamika na mitaa wanayouzia inafahamika. Ila hakuna mkono wa sheria juu yao.

Kwa wanaojua nini madhara ya matumizi ya mmea huu?? Na kisheria Tanzania inaruhusiwa kuliwa na kuuzwa??
 
Isijekuwa imeshamiri kiasi hicho na kupelekea kila mara uvunjifu wa amani Arusha.

Ila hata Dar maeneo ya Kariakoo, ilala na magomeni hupatikana kwa wingi sana hayo majani, hususan usiku kuanzia saa mbili mpaka alfajiri.
 
Nilinusurika kutumia 'gomba' nikiwa Darasa la Sita, 2001. Ifahamike 'gomba' ya hapo inatoka Tanga, pia ifahamike Kenya ni karibu sana; hata watu wanakwenda kwa miguu, na baiskeli.
Madhara ya 'gomba' ni sawa na madhara ya madawa mengine ya kulevya.
 
Hapa same eneo linaitwa gavao wanalima mirungi kama mahindi yanavyolimwa watu wa eneo hili wanaendesha maisha yao kwa kilimo cha mirungi
 
Inakata usingizi yaani ukila unaweza ukawa unakesha kama pakajizi.
 
Kama ndio mara ya kwanza kufika Moshi au Arusha utashangaa sana, vijana wanakula majani kama mbuzi...Hatari sana kumbe sio majani ni Mirungi!!!

Huku polisi sio wakali kabisa juu ya utafunaji majani haya, na uuzaji wa mirungi maarufu kama "Miraa".
Na wauzaji wanafahamika na mitaa wanayouzia inafahamika. Ila hakuna mkono wa sheria juu yao.

Kwa wanaojua nini madhara ya matumizi ya mmea huu?? Na kisheria Tanzania inaruhusiwa kuliwa na kuuzwa??
Miraa inaliwa mpaka na mapolisi hivyo ni vigumu sana kudhibiti. Kuna kipindi polisi ndio wanasafirisha miraa kutoka namanga hadi ngaramtoni ambapo ndio kitovu chama ugawji wa miraa. Kwa uchunguzi mdogo nilioufanya polisi ndio wahusika wahusika wakubw kwani wauza miraa wameweka viwango vya fedha vya kuwapa baada ya miraa kufika. Vituo vinavoongoza kufanikisha biashara hii ni Namanga polce station, longido, Oldonyo Sambu na Ngaramtoni.
 
Kama ndio mara ya kwanza kufika Moshi au Arusha utashangaa sana, vijana wanakula majani kama mbuzi...Hatari sana kumbe sio majani ni Mirungi!!!

Huku polisi sio wakali kabisa juu ya utafunaji majani haya, na uuzaji wa mirungi maarufu kama "Miraa".
Na wauzaji wanafahamika na mitaa wanayouzia inafahamika. Ila hakuna mkono wa sheria juu yao.

Kwa wanaojua nini madhara ya matumizi ya mmea huu?? Na kisheria Tanzania inaruhusiwa kuliwa na kuuzwa??

Pombe na sigara zina madhara makubwa kuliko mirungi.

Ni chanzo kizuri sana cha mapato kwa raia na kodi kwa Serikali. Kenya, Uganda, Ethiopia na nchi nyingine za Ulaya ni ruksa.

Hapa Mrema alichemka kuipiga marufuku.
 
Gombaaaaa!!!! Hakuna kama gomba....Mleta mada sema hujawahi onja hii mambo....Unatafuna na Big G pembeni unasoda ya Sprite...Ni laana tupu..
 
Kiukweli mirungi haina ubaya ila utajapoizidisha ndo ina madhara hata wali maharage ukila ukavimbewa lazma utalewa tu na utalala kwa stimu au uongo jaman
 
Wenzetu wa Kenya mirungi aka MIRAA kwao ni zao la biashara kuna ndege maalum zinazosafirisha mirungi kwenda ulaya, america, china, pakistani, yemeni, saudia kwa mfano kuna ndege 3 zinapeleka mirungi JAMHURI YA WATU WA SOMALILAND, NA NYINGINE INAPELEKA SOMALIA, DJIBOUT. SISI TUMELALA TU NA MIRUNGI YETU INAYOPATINA KOROGWE, SAME NA LUSHOTO KAMA NASISI TUNGESAFIRSHA TUNGEPAT PESA NYINGI KWA WAKULIMA WETU WANO LIMA MAENEO YA MOMBO & SAME TANZANIA tuna product zuri sana, kama vile Shamba rungu, maua, hizi zingewasadia sana wananchi wa maeneo ya korogwe na same , mwanga, lushoto. Kuna watu wamekula hii kitu kwa miaka zaidi ya 70 na hawakupata madhari, stimu yake piya haimusiri mtu kwenye kazi zake
 
Wenzetu wa Kenya mirungi aka MIRAA kwao ni zao la biashara kuna ndege maalum zinazosafirisha mirungi kwenda ulaya, america, china, pakistani, yemeni, saudia kwa mfano kuna ndege 3 zinapeleka mirungi JAMHURI YA WATU WA SOMALILAND, NA NYINGINE INAPELEKA SOMALIA, DJIBOUT. SISI TUMELALA TU NA MIRUNGI YETU INAYOPATINA KOROGWE, SAME NA LUSHOTO KAMA NASISI TUNGESAFIRSHA TUNGEPAT PESA NYINGI KWA WAKULIMA WETU WANO LIMA MAENEO YA MOMBO & SAME TANZANIA tuna product zuri sana, kama vile Shamba rungu, maua, hizi zingewasadia sana wananchi wa maeneo ya korogwe na same , mwanga, lushoto. Kuna watu wamekula hii kitu kwa miaka zaidi ya 70 na hawakupata madhari, stimu yake piya haimusiri mtu kwenye kazi zake

Kwa maelezo yako, Soko lake liko nchi gani mkuu???
 
Gombaaaaa!!!! Hakuna kama gomba....Mleta mada sema hujawahi onja hii mambo....Unatafuna na Big G pembeni unasoda ya Sprite...Ni laana tupu..

Ni kweli sijawahi kutumia.
Ila nimeshangaa jinsi vijana wanavyoishambulia. Mwanzo nilijua ni dawa fulani
kumbe ni Miraa aka gomba.
 
Kuna bablish/bgiii nimeona zimeandikwa "GOMBA"
Ni maalumu kwa ajili ya utafunaji mirungi au ni jina tu?????
 
Kama ndio mara ya kwanza kufika Moshi au Arusha utashangaa sana, vijana wanakula majani kama mbuzi...Hatari sana kumbe sio majani ni Mirungi!!!

Huku polisi sio wakali kabisa juu ya utafunaji majani haya, na uuzaji wa mirungi maarufu kama "Miraa".
Na wauzaji wanafahamika na mitaa wanayouzia inafahamika. Ila hakuna mkono wa sheria juu yao.

Kwa wanaojua nini madhara ya matumizi ya mmea huu?? Na kisheria Tanzania inaruhusiwa kuliwa na kuuzwa??

Hiyo mirungi iko katika kundi la madawa ya kulevya hapa nchini hivyo ni kosa kuuzwa. Tatizo ni kwamba kama ilivyo pombe moshi aka Gongo-ni chanzo cha mapato ya ziada kwa askari polisi wetu! Wanajikusanyia mapato toka kwa wauzaji kama wabia wa mradi!
 
Back
Top Bottom