Madikizela
JF-Expert Member
- Jul 4, 2009
- 675
- 439
MAHAKAMA TANZANIA YASEMA HAKUNA MWANAHARAMU, ILA KUNA WAZAZI HARAMU TU.
Kuna hukumu-rejea ilitolewa tarehe 28/5/2020 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupitia Mh. Jaji Mlyambina.
Ni hukumu ya kesi ya mirathi no. 50 ya mwaka 2016 (ina maana kesi ilichukua miaka 4 kwisha).
Ishu ya msingi katika kesi hiyo ni kuna mume wa mtu alifariki bila ya kuacha wosia. Aliacha mke ambaye alikuwa amemuoa kwa ndoa ya kikristo na watoto wa ndoa hiyo, na wengine wa michepuko (nje ya ndoa).
Watoto wa nje ya ndoa wakaweka pingamizi la mirathi maana walikuwa wameenguliwa wasipate kitu na msimamizi wa mirathi hiyo ambaye ni mtoto wa ndoa.
Wakati wa uhai wake, marehemu alikuwa anawasomesha watoto hao (ambapo wengine tayari walikuwa ni watu wazima), vyeti vyao vya kuzaliwa vilikuwa na jina la marehemu kama baba mzazi, na alishawatambulisha kwa mama yake na ndugu zake wengine.
Mahakamani mama na dada wa marehemu walitoa ushahidi kwamba wanawatambua hao watoto kama watoto wa marehemu.
Upande wa wa kwenye ndoa walikataa DNA test kufanyika kupima kama hao ni watoto wa marehemu.
Katika hukumu yake, Mahakama ikatumia sheria zifuatazo:
1. Katiba ambayo inasema watu wote ni sawa
2. Sheria ya Mtoto kifungu cha 5 ambacho kinakataza kubagua watoto
3. Sheria ya Mtoto kifungu cha 10 ambacho kinampa mtoto haki ya "ku-enjoy" mali ya mzazi wake.
4. Mikataba ya kimataifa kuhusu haki za mtoto ambayo Tanzania imeridhia.
Katika majumuisho yake, Mahakama ikasema, "Watoto hawana hatia maana hawachagui kuzaliwa au kwamba watazaliwa wapi. Msemo wa "kitanda hakizai haramu" maana yake ni hakuna watoto haramu. Ila kuna wazazi haramu."
Kwa hiyo mama za watoto wa nje ndoa ndo wakatambuliwa kwamba ni wazazi haramu na hawastahili kurithi mali ya marehemu. Ila watoto wa nje ya ndoa wakaingizwa katika orodha ya warithi, ambayo ilijumuisha na mjane wa marehemu na mama wa marehemu.
Pia ikaonekana mtoto wa ndani ya ndoa kusimamia mirathi hiyo haitakuwa vyema, ikateua Kabidhi Wasii Mkuu (yaani serikali) awe msimamizi.
------------------------------
Kwa kuwa hii ni hukumu-rejea kwa sasa hii ndo tafsiri ya sheria nchini Tanzania, mpaka pale itakapoamuliwa vinginevyo na Mahakama ya Rufaa, au mpaka Bunge litakapotunga sheria tofauti na tafsiri hii ya mahakama.
Je wewe unaonaje? Mahakama iko sahihi, au tuendelee kufuata misimamo ya kidini ambayo inawabagua watoto wa nje ya ndoa na watoto wanaozaliwa kabla ya ndoa?
Hukumu hii inapatikana hapa:
https://tanzlii.org/tz/judgment/hig...me-mwimbe-other-prob-admincause-no50-2016.pdf
Sent from my HUAWEI VNS-L31 using JamiiForums mobile app
Kuna hukumu-rejea ilitolewa tarehe 28/5/2020 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupitia Mh. Jaji Mlyambina.
Ni hukumu ya kesi ya mirathi no. 50 ya mwaka 2016 (ina maana kesi ilichukua miaka 4 kwisha).
Ishu ya msingi katika kesi hiyo ni kuna mume wa mtu alifariki bila ya kuacha wosia. Aliacha mke ambaye alikuwa amemuoa kwa ndoa ya kikristo na watoto wa ndoa hiyo, na wengine wa michepuko (nje ya ndoa).
Watoto wa nje ya ndoa wakaweka pingamizi la mirathi maana walikuwa wameenguliwa wasipate kitu na msimamizi wa mirathi hiyo ambaye ni mtoto wa ndoa.
Wakati wa uhai wake, marehemu alikuwa anawasomesha watoto hao (ambapo wengine tayari walikuwa ni watu wazima), vyeti vyao vya kuzaliwa vilikuwa na jina la marehemu kama baba mzazi, na alishawatambulisha kwa mama yake na ndugu zake wengine.
Mahakamani mama na dada wa marehemu walitoa ushahidi kwamba wanawatambua hao watoto kama watoto wa marehemu.
Upande wa wa kwenye ndoa walikataa DNA test kufanyika kupima kama hao ni watoto wa marehemu.
Katika hukumu yake, Mahakama ikatumia sheria zifuatazo:
1. Katiba ambayo inasema watu wote ni sawa
2. Sheria ya Mtoto kifungu cha 5 ambacho kinakataza kubagua watoto
3. Sheria ya Mtoto kifungu cha 10 ambacho kinampa mtoto haki ya "ku-enjoy" mali ya mzazi wake.
4. Mikataba ya kimataifa kuhusu haki za mtoto ambayo Tanzania imeridhia.
Katika majumuisho yake, Mahakama ikasema, "Watoto hawana hatia maana hawachagui kuzaliwa au kwamba watazaliwa wapi. Msemo wa "kitanda hakizai haramu" maana yake ni hakuna watoto haramu. Ila kuna wazazi haramu."
Kwa hiyo mama za watoto wa nje ndoa ndo wakatambuliwa kwamba ni wazazi haramu na hawastahili kurithi mali ya marehemu. Ila watoto wa nje ya ndoa wakaingizwa katika orodha ya warithi, ambayo ilijumuisha na mjane wa marehemu na mama wa marehemu.
Pia ikaonekana mtoto wa ndani ya ndoa kusimamia mirathi hiyo haitakuwa vyema, ikateua Kabidhi Wasii Mkuu (yaani serikali) awe msimamizi.
------------------------------
Kwa kuwa hii ni hukumu-rejea kwa sasa hii ndo tafsiri ya sheria nchini Tanzania, mpaka pale itakapoamuliwa vinginevyo na Mahakama ya Rufaa, au mpaka Bunge litakapotunga sheria tofauti na tafsiri hii ya mahakama.
Je wewe unaonaje? Mahakama iko sahihi, au tuendelee kufuata misimamo ya kidini ambayo inawabagua watoto wa nje ya ndoa na watoto wanaozaliwa kabla ya ndoa?
Hukumu hii inapatikana hapa:
https://tanzlii.org/tz/judgment/hig...me-mwimbe-other-prob-admincause-no50-2016.pdf
Sent from my HUAWEI VNS-L31 using JamiiForums mobile app