Mirambo arithi mikoba ya Profesa Lipumba CUF

Mirambo arithi mikoba ya Profesa Lipumba CUF

Elias Msuya

Senior Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
173
Reaction score
672
Aliyekuwa mwenyekiti wa uchaguzi huo, Said Miraji akitangaza matokeo leo Februari 22, 2026.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa dharura wa Chama cha Wananchi (CUF) wamemchagua Mirambo Camil Yusuf kuwa Mwenyekiti wa chama hicho akichukua nafasi iliyoshikiliwa na Profesa Ibrahim Lipumba tangu mwaka 1999.

Mirambo, ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Kigoma Mjini, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa nne wa chama hicho, akipata kura 257 amewashinda Othman Omar Dunga aliyepata kura , 177 na Nkunyunyika Siwale, aliyepata kura 6.
Uchaguzi huo uliofanyika katikaukumbi wa hoteli ya Lekham Buguruni jijini Dar es Salaam ulihudhuriwa na wajumbe 456, ambapo kura halali zilikuwa 448, huku kura sita zikiharibika.

Akizungumza baada ya kuchaguzuliwa, Mirambo amesema atahakikisha kunakuwa na matumizi sahihi ya fedha za chama na kwamba kipaumbele chake kitakuwa ni kuhakikisha watumishi wanalipwa kwa wakati ili kuongeza ari na morali ya kazi, pamoja na kuimarisha ngazi za chini za chama.

“Nataka kujenga taasisi inayoaminika na kupata wadau sahihi watakaosaidia chama kupiga hatua kwa kupata rasilimali fedha,” amesema.

Ameeleza pia kuwa siasa za Tanzania zinapaswa kuwa siasa za ukombozi kwa kujenga mtandao wa ngazi za chini utakaopanua wigo wa kura, badala ya kujikita zaidi katika siasa za upinzani.

“Mimi ni muumini wa siasa za ukombozi na ninaamini zinaweza kutuvusha kutoka hapa tulipo na kutufikisha hatua nyingine. Nitakuwa kiongozi bora kupitia fursa nitakayopata ili tufikie maendeleo endelevu,” amesema.

Vilevile, amesema amejipanga kutatua migogoro ndani ya chama kwa kuanza kuchunguza chanzo chake ili kupata suluhu ya kudumu kupitia njia sahihi zitakazowezesha kufikia hatua bora.

Mirambo ambaye ni mkazi wa Kigoma na alizaliwa mkoani Tabora mwaka 1971. Kitaaluma, ni mwandishi wa habari na mtaalamu wa lugha za Kiswahili, Kifaransa na Kiarabu. Pia ni mwalimu wa mpira wa miguu.

Aidha, amekuwa Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Kigoma Ujiji kwa miaka 10, ambapo alikiongoza chama katika vuguvugu la Muungano wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ulioshirikisha vyama vya Chadema na NLD.
09a41fda-8676-420a-bc47-a5cd58423230.jpg

Mirambo Yusufu (mwenye shati la Kitenge) akipongezwa na baadhi ya Wanachama.


Nafasi nyingine
Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Miraji Mtibwiliko alipata kura 264 na kuwashinda Mohammed Ngulangwa aliyepata kura 88 pamoja na Mussa Mbarouk aliyepata kura 82.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar imechukuliwa na Haroub Mohamed Shamsi aliyepata kura 256, akimshinda Mbarouk Seif Salim aliyepata kura 171, huku Amina Rashid Salim akijitoa kabla ya upigaji kura.
 
View attachment 3547069
Aliyekuwa mwenyekiti wa uchaguzi huo, Said Miraji akitangaza matokeo leo Februari 22, 2026.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa dharura wa Chama cha Wananchi (CUF) wamemchagua Mirambo Camil Yusuf kuwa Mwenyekiti wa chama hicho akichukua nafasi iliyoshikiliwa na Profesa Ibrahim Lipumba tangu mwaka 1999.

Mirambo, ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Kigoma Mjini, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa nne wa chama hicho, akipata kura 257 amewashinda Othman Omar Dunga aliyepata kura , 177 na Nkunyunyika Siwale, aliyepata kura 6.
Uchaguzi huo uliofanyika katikaukumbi wa hoteli ya Lekham Buguruni jijini Dar es Salaam ulihudhuriwa na wajumbe 456, ambapo kura halali zilikuwa 448, huku kura sita zikiharibika.

Akizungumza baada ya kuchaguzuliwa, Mirambo amesema atahakikisha kunakuwa na matumizi sahihi ya fedha za chama na kwamba kipaumbele chake kitakuwa ni kuhakikisha watumishi wanalipwa kwa wakati ili kuongeza ari na morali ya kazi, pamoja na kuimarisha ngazi za chini za chama.

“Nataka kujenga taasisi inayoaminika na kupata wadau sahihi watakaosaidia chama kupiga hatua kwa kupata rasilimali fedha,” amesema.

Ameeleza pia kuwa siasa za Tanzania zinapaswa kuwa siasa za ukombozi kwa kujenga mtandao wa ngazi za chini utakaopanua wigo wa kura, badala ya kujikita zaidi katika siasa za upinzani.

“Mimi ni muumini wa siasa za ukombozi na ninaamini zinaweza kutuvusha kutoka hapa tulipo na kutufikisha hatua nyingine. Nitakuwa kiongozi bora kupitia fursa nitakayopata ili tufikie maendeleo endelevu,” amesema.

Vilevile, amesema amejipanga kutatua migogoro ndani ya chama kwa kuanza kuchunguza chanzo chake ili kupata suluhu ya kudumu kupitia njia sahihi zitakazowezesha kufikia hatua bora.

Mirambo ambaye ni mkazi wa Kigoma na alizaliwa mkoani Tabora mwaka 1971. Kitaaluma, ni mwandishi wa habari na mtaalamu wa lugha za Kiswahili, Kifaransa na Kiarabu. Pia ni mwalimu wa mpira wa miguu.

Aidha, amekuwa Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Kigoma Ujiji kwa miaka 10, ambapo alikiongoza chama katika vuguvugu la Muungano wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ulioshirikisha vyama vya Chadema na NLD.
View attachment 3547071
Mirambo Yusufu (mwenye sahti jekundu, akipongezwa na baadhi ya wanachama.


Nafasi nyingine


Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Miraji Mtibwiliko alipata kura 264 na kuwashinda Mohammed Ngulangwa aliyepata kura 88 pamoja na Mussa Mbarouk aliyepata kura 82.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar imechukuliwa na Haroub Mohamed Shamsi aliyepata kura 256, akimshinda Mbarouk Seif Salim aliyepata kura 171, huku Amina Rashid Salim akijitoa kabla ya upigaji kura.
Tàkataka🚮🚮🚮🚮
 
View attachment 3547069
Aliyekuwa mwenyekiti wa uchaguzi huo, Said Miraji akitangaza matokeo leo Februari 22, 2026.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa dharura wa Chama cha Wananchi (CUF) wamemchagua Mirambo Camil Yusuf kuwa Mwenyekiti wa chama hicho akichukua nafasi iliyoshikiliwa na Profesa Ibrahim Lipumba tangu mwaka 1999.

Mirambo, ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Kigoma Mjini, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa nne wa chama hicho, akipata kura 257 amewashinda Othman Omar Dunga aliyepata kura , 177 na Nkunyunyika Siwale, aliyepata kura 6.
Uchaguzi huo uliofanyika katikaukumbi wa hoteli ya Lekham Buguruni jijini Dar es Salaam ulihudhuriwa na wajumbe 456, ambapo kura halali zilikuwa 448, huku kura sita zikiharibika.

Akizungumza baada ya kuchaguzuliwa, Mirambo amesema atahakikisha kunakuwa na matumizi sahihi ya fedha za chama na kwamba kipaumbele chake kitakuwa ni kuhakikisha watumishi wanalipwa kwa wakati ili kuongeza ari na morali ya kazi, pamoja na kuimarisha ngazi za chini za chama.

“Nataka kujenga taasisi inayoaminika na kupata wadau sahihi watakaosaidia chama kupiga hatua kwa kupata rasilimali fedha,” amesema.

Ameeleza pia kuwa siasa za Tanzania zinapaswa kuwa siasa za ukombozi kwa kujenga mtandao wa ngazi za chini utakaopanua wigo wa kura, badala ya kujikita zaidi katika siasa za upinzani.

“Mimi ni muumini wa siasa za ukombozi na ninaamini zinaweza kutuvusha kutoka hapa tulipo na kutufikisha hatua nyingine. Nitakuwa kiongozi bora kupitia fursa nitakayopata ili tufikie maendeleo endelevu,” amesema.

Vilevile, amesema amejipanga kutatua migogoro ndani ya chama kwa kuanza kuchunguza chanzo chake ili kupata suluhu ya kudumu kupitia njia sahihi zitakazowezesha kufikia hatua bora.

Mirambo ambaye ni mkazi wa Kigoma na alizaliwa mkoani Tabora mwaka 1971. Kitaaluma, ni mwandishi wa habari na mtaalamu wa lugha za Kiswahili, Kifaransa na Kiarabu. Pia ni mwalimu wa mpira wa miguu.

Aidha, amekuwa Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Kigoma Ujiji kwa miaka 10, ambapo alikiongoza chama katika vuguvugu la Muungano wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ulioshirikisha vyama vya Chadema na NLD.
View attachment 3547071
Mirambo Yusufu (mwenye sahti jekundu, akipongezwa na baadhi ya wanachama.


Nafasi nyingine


Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Miraji Mtibwiliko alipata kura 264 na kuwashinda Mohammed Ngulangwa aliyepata kura 88 pamoja na Mussa Mbarouk aliyepata kura 82.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar imechukuliwa na Haroub Mohamed Shamsi aliyepata kura 256, akimshinda Mbarouk Seif Salim aliyepata kura 171, huku Amina Rashid Salim akijitoa kabla ya upigaji kura.
kila la kheri mh. Prof. Ibrahimu Haruna Lipumba kwa kustaafishwa kwa lazima bila kupenda.
Ni vizuri viongozi wa kisiasa kujifunza kusoma alama za nyakati kwa usahihi :1Head:
 
CUF bado inaonekana ya kidinidini tu hadi leo! Pamoja na udinidini wake imepoteza umaarufu wake. CUF ilikuwa kali enzi za maalimu seif kabla hajatimkia ACT. Kwa sasa chama hicho ni chama mfu kisichokuwa na mvuto kwa wananchi, ni kama hakipo!
 
View attachment 3547069
Aliyekuwa mwenyekiti wa uchaguzi huo, Said Miraji akitangaza matokeo leo Februari 22, 2026.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa dharura wa Chama cha Wananchi (CUF) wamemchagua Mirambo Camil Yusuf kuwa Mwenyekiti wa chama hicho akichukua nafasi iliyoshikiliwa na Profesa Ibrahim Lipumba tangu mwaka 1999.

Mirambo, ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Kigoma Mjini, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa nne wa chama hicho, akipata kura 257 amewashinda Othman Omar Dunga aliyepata kura , 177 na Nkunyunyika Siwale, aliyepata kura 6.
Uchaguzi huo uliofanyika katikaukumbi wa hoteli ya Lekham Buguruni jijini Dar es Salaam ulihudhuriwa na wajumbe 456, ambapo kura halali zilikuwa 448, huku kura sita zikiharibika.

Akizungumza baada ya kuchaguzuliwa, Mirambo amesema atahakikisha kunakuwa na matumizi sahihi ya fedha za chama na kwamba kipaumbele chake kitakuwa ni kuhakikisha watumishi wanalipwa kwa wakati ili kuongeza ari na morali ya kazi, pamoja na kuimarisha ngazi za chini za chama.

“Nataka kujenga taasisi inayoaminika na kupata wadau sahihi watakaosaidia chama kupiga hatua kwa kupata rasilimali fedha,” amesema.

Ameeleza pia kuwa siasa za Tanzania zinapaswa kuwa siasa za ukombozi kwa kujenga mtandao wa ngazi za chini utakaopanua wigo wa kura, badala ya kujikita zaidi katika siasa za upinzani.

“Mimi ni muumini wa siasa za ukombozi na ninaamini zinaweza kutuvusha kutoka hapa tulipo na kutufikisha hatua nyingine. Nitakuwa kiongozi bora kupitia fursa nitakayopata ili tufikie maendeleo endelevu,” amesema.

Vilevile, amesema amejipanga kutatua migogoro ndani ya chama kwa kuanza kuchunguza chanzo chake ili kupata suluhu ya kudumu kupitia njia sahihi zitakazowezesha kufikia hatua bora.

Mirambo ambaye ni mkazi wa Kigoma na alizaliwa mkoani Tabora mwaka 1971. Kitaaluma, ni mwandishi wa habari na mtaalamu wa lugha za Kiswahili, Kifaransa na Kiarabu. Pia ni mwalimu wa mpira wa miguu.

Aidha, amekuwa Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Kigoma Ujiji kwa miaka 10, ambapo alikiongoza chama katika vuguvugu la Muungano wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ulioshirikisha vyama vya Chadema na NLD.
View attachment 3547071
Mirambo Yusufu (mwenye sahti la Kitenge) akipongezwa na baadhi ya wanachama.


Nafasi nyingine


Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Miraji Mtibwiliko alipata kura 264 na kuwashinda Mohammed Ngulangwa aliyepata kura 88 pamoja na Mussa Mbarouk aliyepata kura 82.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar imechukuliwa na Haroub Mohamed Shamsi aliyepata kura 256, akimshinda Mbarouk Seif Salim aliyepata kura 171, huku Amina Rashid Salim akijitoa kabla ya upigaji kura.
Lipumba katoswa na mfumo.
 
ahamie ccm akawe mzee mshauri wa mambo ya siasa ya uchumi
Gentleman,
nadhani CCM in hazina ya kutosha ya vijana na wazee mahiri na wabobevu wa masuala ya siasa na uchumi na haina upungufu wa watu wa kada hizo, tena ina watu wenye uzoefu na weledi zaidi ya king"ang"anizi Lipumba.

KIUKWELI hana nafasi na kwakweli hahitajiki kabisa CCM, labda acheki chadema na vyama vingine vinavyotumika kama vituo vya mamaluki na vibaraka wa mabwenyenye ya magharibi :1Head:
 
CUF bado inaonekana ya kidinidini tu hadi leo! Pamoja na udinidini wake imepoteza umaarufu wake. CUF ilikuwa kali enzi za maalimu seif kabla hajatimkia ACT. Kwa sasa chama hicho ni chama mfu kisichokuwa na mvuto kwa wananchi, ni kama hakipo!
Ni tawi la ccm, wanagombania fursa za vijisent toka ccm. Na wote ni imani moja ya dini ya Mwenyaaaaaazi Mungu
 
Hivi magdalena sakaya aliingiaje kwenye hicho chama chenye sura ya kidini waziwazi? Chama kimetawaliwa na kanzu na vibaraghashia vitupu plus hijabu/juba! Chama kinatakiwa kiwe na sura ya kitaifa walau kama ccm na chadema vimejaza watu wa imani na dini tofauti mpaka wachawi na wanga wapo humo!
 
Maswali ambayo hata google search au AI yameshindikana kupata majibu. Labda ukubwa wa JamiiForums utaweza kutegua maswali haya chini kumhusu:
Mirambo Camil Yusuf
  • Elimu yake
  • Pia mbali ya siasa anapata kipato chake kutokana na ni shughuli gani?
  • Lugha je Mirambo Camil Yusuf anaongea lugha ngapi za kimataifa?
  • N.k
 
Ni tawi la ccm, wanagombania fursa za vijisent toka ccm. Na wote ni imani moja ya dini ya Mwenyaaaaaazi Mungu

Msimamizi wa uchaguzi wa mwenyekiti wa CUF Taifa, Bw. Said Miraji akitangaza matokeo


View: https://m.youtube.com/watch?v=4ZG5IXCWFyI

Matokeo hayo yametangazwa Februari 22, 2026 na Mwenyekiti wa Uchaguzi wa chama hicho, mchambuzi mkongwe tajwa wa siasa katika televisheni Bw. Said Miraji, baada ya mkutano mkuu wa dharura uliohudhuriwa na wajumbe 456.

jamiiforums__2026-02-14T125505.000Z.jpg

Picha : Profesa Ibrahim Haruna Lipumba

Chama cha Wananchi (CUF) kimempata Mwenyekiti mpya wa Taifa, ambapo Mirambo Camil Yusuf amechaguliwa kushika nafasi hiyo akichukua mikoba ya Ibrahim Lipumba, aliyekuwa akiiongoza tangu mwaka 1999.
 
Back
Top Bottom