Miradi mingi ya Magufuli haina tija? Ni white elephant?

inchaji

JF-Expert Member
Jul 5, 2019
2,420
4,922
Wanandugu.

Serikali ya awamu ya 5 imejipambanua kama ya wanyonge na imekuja na miradi lukuki inayotafuna mabilioni ya pesa za walalahoi, lakini miradi hii haina na wala haionyeshi dalili ya kuwa na tija yoyote huko mbeleni. miaka mitano hiyo inakatika tunapigwa porojo lakini mabilioni yanateketea.

Daraja la Mfugale
Huu ni mradi wa hovyo niliowahi kuuona na unareflect hisia kwamba utawala huu umejaa ubinafsi.

Daraja limejengwa kimkakati kuwapa upendeleo wanasiasa wanaowahi ndege airport.

Wanyonge wanaotoka na kwenda Tandika na maeneo mengine ya Temeke inawachukua wastani wa dakika 45 kuvuka Tazara, ni kero kuliko ilivyokuwa kabla halijajengwa.

Rais ajae alibomoe ndani ya siku 100 lijengwe upya watu wote walifaidi.

SGR
Huu mradi miaka minne sasa inaenda mitano hakuna cha maana zaidi ya kuona minguzo na minondo tu inasimikwa kila siku.

Nguzo zenyewe zinaonekana kujengwa sehemu zinazopitwa na watu wengi ionekane kuna kitu kinajengwa kumbe ni uzugaji.

Ndege
Kila nikilitizama anga naona ndege za biashara ni zilezile tu: SwisAir, Turkish, Emirates.

Hizi za Rubondo island mbona hatuzioni zinabeba nini kwenda wapi?

Dar es salaam
Huu ni mji lakini ni mradi tosha. Toto pendwa hajatatua hata kero moja; foleni, maji, mafuriko na hata usafi siku za jumamosi umemshinda.

Miaka mitano inakatika bado miradi inayowapa unafuu watanzania inabaki kuwa ile ile iliyobuniwa awamu zilizopita; daraja la Kigamboni, mwendokasi, shule za kata, barabara za lami kila kona, treni za Mwakyembe, watu wengi wameajiriwa sekta binafsi awamu zilizopita.

Sasa huu utawala kuna mradi gani wa maana umefanya ukafanikisha? Muda unaenda miaka mitano hiyo inakatika jamani.
 
Miradi yote hata wawakilishi wa nchi za nje walipopelekwa wakashangaa kuona mambo ya ulaya yanawekwa hapa Tanzania

Kwa mujibu wa kituo cha dunia cha uwekezaji wanakubali kuwa katika bara zima la Africa Tanzania ndio inatumia pesa zake kwenye miradi yenye tija

Mungu mpemaisha marefu jpm

State agent
 
kwenye swala miradi ndugu yangu Jiwe yupo sawa kosa lake ni kutumia fedha za ndani, kitumia wachina na jamii kama hao ambao fee zao ni ndogo na wamejawa na ubinaFsi, pesa yote inaenda China na watu wachache wanaajiriwa na kulipwa pesa kiduchu

Mkuu hiyo miradi kweli ni pesa za ndani? kama ni pesa za ndani imekuwaje deni la taifa limepaa kwa 20t kwa miaka minne? Deni la taifa jumla ni karibia kabisa na 60t. Hivyo yeye pekee kaleta 1/3 ya deni lilipotikana chini ya marais wote wanne. Toka nje ya box ndugu unangizwa mjini.
 
SGR tuliambiwa Disemba mwaka huu tutaenda na treni ya umeme kutoka Dar mpaka Morogoro. Na kulingana na mkataba ni kuwa Mkandarasi Yapi Merkezi alitakiwa akabidhi awamu ya kwanza ya mradi tarehe 1, Novemba mwaka huu. Mbona kimya?
 
Mheshimiwa anajitahidi kuweka miundombinu vizuri japo zipo changamoto nyingi kwenye utawala wake ni kama mambo mengi hayapo wazi. Kwa issue ya daraja la mfugale ile ni grants from JP sema kwakuwa vitu vingi tunachukulia kisiasa sana. Upanuzi wa bagamoyo road ukiwa mradi moja wapo kutoka JP
 
sasa huu utawala kuna mradi gani wa maana umefanya ukafanikisha? muda unaenda miaka mitano hiyo inakatika jamani.
Nilisoma mada yako nikiwa natafuta "Viwanda 4,000". Sikusoma popote katika mada yako kuhusu viwanda hivyo, sasa sijui katika mradi huo wa viwanda unakubaliana na majigambo na misifa anayojitangazia?

Mimi natamani sana kusoma habari za viwanda hivi vilivyoanzishwa nchini katika muda wa miaka minne. Hii ina maana vijana wamepata ajira ya kutosha, (sijui wangapi wameajiriwa huko), na sasa tutakuwa tumepunguza kuagiza nje baadhi ya mahitaji yetu ya vitu vinavyozalishwa kwenye viwanda hivyo, na pato letu litaongezeka kwa kuuza nje bidhaa zinazozalishwa viwandani humo.

Mkuu 'Inchaji,' unaweza kutuelezea lolote kuhusu viwanda hivi?
 
Miradi yote hata wawakilishi wa nchi za nje walipopelekwa wakashangaa kuona mambo ya ulaya yanawekwa hapa Tanzania

Kwa mujibu wa kituo cha dunia cha uwekezaji wanakubali kuwa katika bara zima la Africa Tanzania ndio inatumia pesa zake kwenye miradi yenye tija

Mungu mpemaisha marefu jpm

State agent
Mbona deni linakuwa au mnapiga huku mnakopa kuzuga
 
Mkuu hiyo miradi kweli ni pesa za ndani? kama ni pesa za ndani imekuwaje deni la taifa limepaa kwa 20t kwa miaka minne? Deni la taifa jumla ni karibia kabisa na 60t. Hivyo yeye pekee kaleta 1/3 ya deni lilipotikana chini ya marais wote wanne. Toka nje ya box ndugu unangizwa mjini.
Eeenh, 'Tindo', hawa watu ni 'wasomi', wamehitimu na wana digrii au diploma zao; lakini bado huwaambi lolote kuhusu taarifa za upotoshaji kama hizo.
Na Jiwe anajuwa watu hawa wapo wengi ndani ya nchi hii, ndio maana haoni aibu kuendelea na upotoshaji anaoufanya kama wa 'ujenzi wa viwanda 4,000', tokea achukue madaraka!

Na kwa kuwa amewatia woga watu na kujitungia sheria za ukandamizaji, hakuna mwandishi wa habari yeyote anayeweza kuchunguza juu ya taarifa hiyo na kuiandikia makala. Huyu Jiwe nikama alijiandaa maisha yake yote kupanga jinsi ambavyo angefanikisha mipango yake ya upotoshaji pindi alipopewa madaraka. Kila kitu kimapangiliwa kimkakati.
 
Kwenye ilo daraja la mfugale upo sahihi ni moja ya mradi wa kipumbavu sana njia ya kutoka buguruni kwenda magorofani kulitakiwa rotation ya highway sio magari kusimama kweny mataa.
 
Miradi yote hata wawakilishi wa nchi za nje walipopelekwa wakashangaa kuona mambo ya ulaya yanawekwa hapa Tanzania

Kwa mujibu wa kituo cha dunia cha uwekezaji wanakubali kuwa katika bara zima la Africa Tanzania ndio inatumia pesa zake kwenye miradi yenye tija

Mungu mpemaisha marefu jpm

State agent
Mnatumia pesa za ndani, sasa kinachofanya deni la taifa liongezeke kwa kasi ni nini? Danganyeni wengine, hakuna cha miradi wala nini zaidi ya teni pasenti za Jiwe, miradi yote ni hewa tupu, feki tupu.
 
SGR tuliambiwa Disemba mwaka huu tutaenda na treni ya umeme kutoka Dar mpaka Morogoro. Na kulingana na mkataba ni kuwa Mkandarasi Yapi Merkezi alitakiwa akabidhi awamu ya kwanza ya mradi tarehe 1, Novemba mwaka huu. Mbona kimya?
Jiwe anaandaa treni used za umeme aje kudanganyia wajinga, vichwa feki nimevikuta vinashushwa bandarini ni vichekesho.
 
Back
Top Bottom