Mipapai huu ni ugonjwa au nini?

Mipapai huu ni ugonjwa au nini?

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,707
Reaction score
1,729
Wakuu tokea masika tu kuisha mipapai yangu imekuwa na muonekano huu. Nilimtafuta kijana mmoja mlima bustani na kumuomba aliulizie wataalam wa mimea kama ni shambulio, jibu likawa ni ukungu. Sasa naomba wataalam humu JF maana pana wajuzi hapa waliobobea wanijuze.
IMG_20160902_071826_0.jpg
IMG_20160902_162410_0.jpg
IMG_20160902_162421_0.jpg
 
Mkuu hao ni kuvu wa mipapai na hapo wameshambulia sana mpaka majani yananyauka unaweza kutumia dawa za kuzuia kuvu kama mancozeb au farmzeb na aina nyingne kama hzo katika dozi nzito kidogo ili kucontrol vyema ugonjwa huo
 
Huo Ugonjwa unaitwa Powder Mildew unashambulia mazao mengi unatakiwa uspray na sulphur kabla haujatokea au ukiwa katika hatua za awali. Mwenye zaidi atakuja ongezea
Aksante mkuu, kwa hali hii sasa nifanyeje? Hakuna dawa yake?
 
Mkuu hao ni kuvu wa mipapai na hapo wameshambulia sana mpaka majani yananyauka unaweza kutumia dawa za kuzuia kuvu kama mancozeb au farmzeb na aina nyingne kama hzo katika dozi nzito kidogo ili kucontrol vyema ugonjwa huo
Poa mkuu nitajaribu na husababiswa na nini?
 
Huo ni ugonjwa wa kuvu kwa kua ushauata tumia dawa ya kutibu aina ya metalaxyl!!
 
Huo ni ugonjwa wa kuvu kwa kua ushauata tumia dawa ya kutibu aina ya metalaxyl!!
Ni vema ukatumia majina ya biashara sio ya kitaalam. Unaweza kuuliza metalaxyl hata dukani muuzaji akakwambia haipo kumbe ipo. Dawa zenye metalaxyl kama active ingredient kwa kawaida huwa pia na mancozeb. Mfano ni Ridomil Gold, Ivory 72 ( Sio Ivory 80), na nyinginezo nyingi.
 
Mkuu hiki kichwa cha habari umekiandika kama unayauliza hayo mapapai yakujibu.
 
Iv mpapai ukiwa dume unafanyaje uubarishe il uwe jike
 
Ni vema ukatumia majina ya biashara sio ya kitaalam. Unaweza kuuliza metalaxyl hata dukani muuzaji akakwambia haipo kumbe ipo. Dawa zenye metalaxyl kama active ingredient kwa kawaida huwa pia na mancozeb. Mfano ni Ridomil Gold, Ivory 72 ( Sio Ivory 80), na nyinginezo nyingi.
Shukran CORAL
 
Na mimi ilo tatizo lilinipata mipapai mingi imekuwa dume
Mkuu,

Huwezi badili jinsia ya mapapai. Ukigundua ni dume, ng'oa tu.

Ile ya kuweka vigunzi sijui 'haifanyagi' kazi. Utajisumbua bure...
 
Iv mpapai ukiwa dume unafanyaje uubarishe il uwe jike
Unaweza kuupa stress kwa kuugonga na msumari au kuufunga na kitu kizito kama jiwe au gunzi la hindi. Fanya hivi pale unapoona mpapai wako una dalili ya kuwa dume inaweza kusaidia.
 
Back
Top Bottom