Mipaka ya Zanzibar imeanzia wapi na inaishia wapi?

Mipaka ya Zanzibar imeanzia wapi na inaishia wapi?

Sheria ya 1992
Na.4 ib.3
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.
(2) Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali
ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Rais aweza kuigawa Jamhuri ya Muungano katika
mikoa, wilaya na maeneo mengineyo, kwa kufuata utaratibu
uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na
Bunge:
Isipokuwa kwamba Rais atashauriana kwanza na Rais
wa Zanzibar kabla ya kuigawa Tanzania Zanzibar katika
Mikoa, Wilaya au maeneo mengineyo.
Tangazo la nchi
yenye Mfumo wa
vyama vingi
Sheria ya 1992
Na.4 ib.5
Kuna kitu umenote kuwa katiba
Ya Zanzibar ni batili?.
P
Katiba ya Zanzibar nayo inampa mamlaka Rais wa Zanzibar kuigawa Zanzibar wilaya na Mikoa bila ya kumshauri Mtu yeyote
Ni kweli Eneo lote la Tanzania bara na Zanzibar ndio linalofanya Jamhuri ya Muungano. Kama Umenisoma vizuru hoja yangu ni kuwa eneo la Zanzibar linalopakana na Tanzania bara limeanzia wapi linaishia wapi? Ndio hoja ya Msingi ndugu yangu. Hatuna shida na Eneo lote la Mkoa wa Arusha linaeleweka eneo lote la Manyara pia linaeleweka mipaka yake. Shida ipo hapa Eneo la Zanzibar linaishia wapi au limeanzia wapi kwa sababu Zanzibar imepakana na baadhi ya Mikoa ya Tanzania Bara kwa upande wa Baharini mfano Zanzibar imepakana na Mkoa wa Daresalam, Mkoa wa Pwani , Mkoa wa Tanga Mkoa Lindi na Mtwara na kadhalika sasa hapa tunahitaji kuelewa mipaka ya Zanzibar imeanzia wapi na inaishia wapi ??? Kuna Ramani yoyote inayoonyesha mipaka ya mikoa ya Tanzania Bara iliyopakana na Zanzibar? Kama hamna ni kwa nini ? Wakati mikoa yote mipaka yake iko wazi?
 
Zanzibar ni nchi?
Jibu ni hapana, maana kuna kitu kinaitwa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Na muungano=(x+y)=z hapa x inapaswa ife na y pia inapaswa ife.
Kama sio nchi ni nini?
Je, Tanzania ni Shirikisho?
No!!
Kwanini?
Shirikisho =(A,B)=AB, kwa ufafanuzi ni kwamba nchi mbili zilizounda federation zote zitaendelea kuwepo. Na hapa tukitazama Tanganyika hatuioni.
Je, Zanzibar ni mkoa?
Uliyeuliza swali nahitaji jibu hapa
Jibu ndugu yangu nimeshakuwekea hapo juu Kama umesoma Uzi vizuri Ibara ya kwanza na ya pili ya Katiba ya Zanzibar inafafanua hili. Zisome hizi ibara MBILI ni muhimu sana.
 
Unasema Zanzibar ni nchi!?huo ni uhaini
Sijasema Mimi Zanzibar ni Nchi !!! Katiba ya Zanzibar ndio iliyotamka hivo. Nimenukuu Ibara ya Kwanza na ya pili nakushauri uisome vizuri siyo Mimi, Rafiki.
 
Mpaka upo baharini.Inapoishia Tanganyika na inapoanza Zanzibar.Wakoloni walishaweka kabla hujazaliwa
Umejitahidi kidogo ila tufahamishe ikoje hapa ndio napata tabu leta Evidence
 
Katiba ya Zanzibar nayo inampa mamlaka Rais wa Zanzibar kuigawa Zanzibar wilaya na Mikoa bila ya kumshauri Mtu yeyote
Ni kweli Eneo lote la Tanzania bara na Zanzibar ndio linalofanya Jamhuri ya Muungano. Kama Umenisoma vizuru hoja yangu ni kuwa eneo la Zanzibar linalopakana na Tanzania bara limeanzia wapi linaishia wapi? Ndio hoja ya Msingi ndugu yangu. Hatuna shida na Eneo lote la Mkoa wa Arusha linaeleweka eneo lote la Manyara pia linaeleweka mipaka yake. Shida ipo hapa Eneo la Zanzibar linaishia wapi au limeanzia wapi kwa sababu Zanzibar imepakana na baadhi ya Mikoa ya Tanzania Bara kwa upande wa Baharini mfano Zanzibar imepakana na Mkoa wa Daresalam, Mkoa wa Pwani , Mkoa wa Tanga Mkoa Lindi na Mtwara na kadhalika sasa hapa tunahitaji kuelewa mipaka ya Zanzibar imeanzia wapi na inaishia wapi ??? Kuna Ramani yoyote inayoonyesha mipaka ya mikoa ya Tanzania Bara iliyopakana na Zanzibar? Kama hamna ni kwa nini ? Wakati mikoa yote mipaka yake iko wazi?
Kama katiba ya JMT imesema Tanzania ni nchi moja na Zanzibar ni sehemu ya JMT, na mwenye mamlaka ya kuigawa JMT ni rais wa JMT ila kwenye kuigawa Zanzibar atashauriana na rais wa Zanzibar, then kitendo cha katiba ya Zanzibar kusema Tanzania ni nchi mbili ni batili, kitendo cha kuuita Zanzibar ni nchi na kuitaja mipaka yake ni batili, kitendo cha kusema rais wa Zanzibar ana mamlaka ya kuigawa Zanzibar ni batili kwa sababu Zanzibar ni sehemu ya JMT.

Mipaka ya Zanzibar baada ya Mkutano wa Berlin wa 1884 ilikuwa eneo last visiwa vyote vya pwani ya Africa Mashariki na eneo la maili 10 ya pwani hiyo ikijumuisha Dar es Salaam, Mombasa hadi Lamu.

Kwa vile Tanganyika ilikuwa ni koloni chini ya Ujerumani na Kenya ni koloni chini ya Uingereza wakati Zanzibar hauingizwa kwenye ukoloni ilibaki kuwa mamlaka ya Sultanete of Zanzibar na 10 miles ya costal strip, Uingereza ikafanya urafiki na Zanzibar kwa ahadi ya kuilinda, protectorate hivyo ikawa inajivinjari pwani yote, Ujerumani ana Tanganyika hana pwani, hana bandari.

Ndipo Mjerumani na Muingereza wakaingia mkataba wa Hellingoland wa July 1, 1990, Mjerumani akawapa Waingereza kisiwa cha Witu, na Waingereza wakawapa Wajerumani zile maili 10 za Pwani ya Dar es Salaam, ndipo mipaka ya Zanzibar ikabadilika na hadi kati kati ya bahari kati ya Dar na Zanzibar na visiwa vya vyote vilivyo karibu na Tanganyika vikiwemo Kilwa na Mafia kuangukia Tanganyika, kisiwa cha Lamu kuangukia Mombasa, Kisiwa cha Ngazija kikaangukia Comoro, Sultanete of Zanzibar ikabakiwa na visiwa vya Unguja na Pemba tuu.

Na ili kuwafidia Waingereza kwa kuchukua pwani yao, Waingereza wakabadili mipaka ya Ziwa Nyasa ya Mkutano wa Berlin ambao nchi ziligawana kati kati na kuibadili kuwa maji yote ni ya Waingereza na Ujerumani ikabakiwa na nchi kavu tuu na ndio mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na sisi hadi leo.

Chanzo cha mgogoro ni Waingereza kuligawa eneo la Sultanete of Zanzibar bila kuishirikisha Zanzibar halafu kujimegea eneo la Ziwa Nyasa bila kuishirikisha Ujerumani, hivyo tulipata uhuru Ile 1961 tulikataa kuutambua huo mpaka wa nchi kavu huku Banda wa Malawi akidai Ziwa lote ni lake. Tulimtungia hadi wimbo "Banda wa Malawi katuvalia ngozi ya chui kututishia Watanzania, hatujali hatujali.
P
 
Kama katiba ya JMT imesema Tanzania ni nchi moja na Zanzibar ni sehemu ya JMT, na mwenye mamlaka ya kuigawa JMT ni rais wa JMT ila kwenye kuigawa Zanzibar atashauriana na rais wa Zanzibar, then kitendo cha katiba ya Zanzibar kusema Tanzania ni nchi mbili ni batili, kitendo cha kuuita Zanzibar ni nchi na kuitaja mipaka yake ni batili, kitendo cha kusema rais wa Zanzibar ana mamlaka ya kuigawa Zanzibar ni batili kwa sababu Zanzibar ni sehemu ya JMT.

Mipaka ya Zanzibar baada ya Mkutano wa Berlin wa 1884 ilikuwa eneo last visiwa vyote vya pwani ya Africa Mashariki na eneo la maili 10 ya pwani hiyo ikijumuisha Dar es Salaam, Mombasa hadi Lamu.

Kwa vile Tanganyika ilikuwa ni koloni chini ya Ujerumani na Kenya ni koloni chini ya Uingereza wakati Zanzibar hauingizwa kwenye ukoloni ilibaki kuwa mamlaka ya Sultanete of Zanzibar na 10 miles ya costal strip, Uingereza ikafanya urafiki na Zanzibar kwa ahadi ya kuilinda, protectorate hivyo ikawa inajivinjari pwani yote, Ujerumani ana Tanganyika hana pwani, hana bandari.

Ndipo Mjerumani na Muingereza wakaingia mkataba wa Hellingoland wa July 1, 1990, Mjerumani akawapa Waingereza kisiwa cha Witu, na Waingereza wakawapa Wajerumani zile maili 10 za Pwani ya Dar es Salaam, ndipo mipaka ya Zanzibar ikabadilika na hadi kati kati ya bahari kati ya Dar na Zanzibar na visiwa vya vyote vilivyo karibu na Tanganyika vikiwemo Kilwa na Mafia kuangukia Tanganyika, kisiwa cha Lamu kuangukia Mombasa, Kisiwa cha Ngazija kikaangukia Comoro, Sultanete of Zanzibar ikabakiwa na visiwa vya Unguja na Pemba tuu.

Na ili kuwafidia Waingereza kwa kuchukua pwani yao, Waingereza wakabadili mipaka ya Ziwa Nyasa ya Mkutano wa Berlin ambao nchi ziligawana kati kati na kuibadili kuwa maji yote ni ya Waingereza na Ujerumani ikabakiwa na nchi kavu tuu na ndio mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na sisi hadi leo.

Chanzo cha mgogoro ni Waingereza kuligawa eneo la Sultanete of Zanzibar bila kuishirikisha Zanzibar halafu kujimegea eneo la Ziwa Nyasa bila kuishirikisha Ujerumani, hivyo tulipata uhuru Ile 1961 tulikataa kuutambua huo mpaka wa nchi kavu huku Banda wa Malawi akidai Ziwa lote ni lake. Tulimtungia hadi wimbo "Banda wa Malawi katuvalia ngozi ya chui kututishia Watanzania, hatujali hatujali.
P
Bwana Pascal Mayala Ngoja nikwambie jambo moja hizi ni katiba MBILI zilizohuru hakuna katiba iliyokuwa iko juu ya Nyengine. Na kwa msingi huo inapotokea Mgongano wa katiba hizi MBILI ya Tanzania, 1977 na ile ya Zanzibar,1984 Ipi inayo Prevail ? Jawabu ni hapana. Constitutional Lawyers kama Akina Professor Shivji wanalifaham hili.
Kwa ajil hii Katiba ya URT 1977 Haiko juu ya Katiba Zanzibar na kinyume chake Katiba ya Zanzibar pia Haiko juu ya katiba ya TZ.
Hili "kosa" nafkiri wameliona walio draft katiba mpya baada ile Draft ya Katiba ya Tume ya Jaji Warioba wamelirekebisha na sina hakika kama Zanzibar wataikubali ibara ile inayoipa UKUU Katiba ya Tanzania na UDOGO katiba ya Zanzibar. Katiba mpya inayopendekezwa ambayo Imewekwa kiporo Wameweka ibara ambayo inaipa nguvu katiba ya Muungano endapo itatokea Mgongano . Wamesoma "makosa" ya Katiba ya Sasa.

All in All nakubaliana na wewe kwamba kuna Mgongano Mkubwa kati ya Katiba ya Zanzibar na katiba ya Muungano.
 
Sheria ya 1992
Na.4 ib.3
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.
(2) Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali
ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Rais aweza kuigawa Jamhuri ya Muungano katika
mikoa, wilaya na maeneo mengineyo, kwa kufuata utaratibu
uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na
Bunge:
Isipokuwa kwamba Rais atashauriana kwanza na Rais
wa Zanzibar kabla ya kuigawa Tanzania Zanzibar katika
Mikoa, Wilaya au maeneo mengineyo.
Tangazo la nchi
yenye Mfumo wa
vyama vingi
Sheria ya 1992
Na.4 ib.5
Kuna kitu umenote kuwa katiba
Ya Zanzibar ni batili?.
P
Hapa kama una kitu mkuu
 
Back
Top Bottom