Mipaka ya Zanzibar imeanzia wapi na inaishia wapi?

Mipaka ya Zanzibar imeanzia wapi na inaishia wapi?

Torero

Senior Member
Joined
Dec 22, 2017
Posts
122
Reaction score
138
"Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar" Ibara ya Kwanza ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 toleo la 2010 inasema hivi.

Wakati Ibara ya pili inasema : " Zanzibar ni Miongoni mwa Nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" Kwa lengo la kuelew baadhi tu ya Sheria Sheria nawaombeni Masada kuweza kutambua kwa uhalisia hasa mipaka ya Zanzibar na Tanganyika.

Oh! Sorry Tanzania bara. Wala siyo dhambi kutaka kuelewa kwa sababu mipaka yote kati ya mkoa na Mkoa naelewa kwa mfano Sina shida mipaka iliyopo kati ya Mkoa wa Iringa na Mbeya naielewa shida IPO kati ya mipaka ya Zanzibar na Tanzania Bara.

Wajuzi naomba msaada. Katiba ya Jamhuri ya Muungano, 1977 inasemaje kuhusu jambo hili? Sheria za Kimataifa Zinasemaje ?
 
Hakuna hiyo mipaka mkuu.wewe ishi tu.
Ni muhimu kuelewa jographia ya mipaka ni muhimu sana kuelewa na ndio maana mikoa yote ya Tanzania mipaka yake iko wazi. Kwa mfano kuna Sheria nyingi zinatumika Zanzibar tu hazitumiki Bara sasa hapo ndio nataka kuelewa wapi Zanzibar imeishia na wapi imeanzia ?na huwezi kulijua hili mpaka uelewe mipaka
 
Mipaka ya Zanziba na pemba ni kilomita moja toka Tanga badarini na Darisalama bandarini na Kilwa bandarini. Huko kwingine ni Zenj. Unasemaje? Unataka kwenda kufanya utafiti wa mafuta?? Kwa nini huulizi mipaka ya ziwa Nyasa na Nyasaland??
Chokochoko hatutaki. Nyiye ndo mnasema ati Zanziba siyo nchi!! Kuna siku mtaitambua tu. Hakuna mkoa wenye wimbo wa taifa ni Zenj tu
 
Mipaka ya Zanziba na pemba ni kilomita moja toka Tanga badarini na Darisalama bandarini na Kilwa bandarini. Huko kwingine ni Zenj. Unasemaje? Unataka kwenda kufanya utafiti wa mafuta?? Kwa nini huulizi mipaka ya ziwa Nyasa na Nyasaland??
Chokochoko hatutaki. Nyiye ndo mnasema ati Zanziba siyo nchi!! Kuna siku mtaitambua tu. Hakuna mkoa wenye wimbo wa taifa ni Zenj tu
Kwa Ushahidi Gani? Lete Evidence kaka! Nimeuliza kisheria zaidi siyo politics
 
"Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar" Ibara ya Kwanza ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 toleo la 2010 inasema hivi.

Wakati Ibara ya pili inasema : " Zanzibar ni Miongoni mwa Nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" Kwa lengo la kuelew baadhi tu ya Sheria Sheria nawaombeni Masada kuweza kutambua kwa uhalisia hasa mipaka ya Zanzibar na Tanganyika.

Wajuzi naomba msaada. Katiba ya Jamhuri ya Muungano, 1977 inasemaje kuhusu jambo hili? Sheria za Kimataifa Zinasemaje ?
Sheria ya 1992
Na.4 ib.3
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.
(2) Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali
ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Rais aweza kuigawa Jamhuri ya Muungano katika
mikoa, wilaya na maeneo mengineyo, kwa kufuata utaratibu
uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na
Bunge:
Isipokuwa kwamba Rais atashauriana kwanza na Rais
wa Zanzibar kabla ya kuigawa Tanzania Zanzibar katika
Mikoa, Wilaya au maeneo mengineyo.
Tangazo la nchi
yenye Mfumo wa
vyama vingi
Sheria ya 1992
Na.4 ib.5
Kuna kitu umenote kuwa katiba
Ya Zanzibar ni batili?.
P
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Tanganyika ni bonge moja la nchi lakini limepoteza utaifa wake kwa kiini macho cha muungano.
 
Ni muhimu kuelewa jographia ya mipaka ni muhimu sana kuelewa na ndio maana mikoa yote ya Tanzania mipaka yake iko wazi. Kwa mfano kuna Sheria nyingi zinatumika Zanzibar tu hazitumiki Bara sasa hapo ndio nataka kuelewa wapi Zanzibar imeishia na wapi imeanzia ?na huwezi kulijua hili mpaka uelewe mipaka
Narudia tena mkuu,wewe ishi tu.
Ukiulizwa hilo swali kwenye mtihani utajua vya kujibu lakini haipo.
 
Mpaka upo baharini.Inapoishia Tanganyika na inapoanza Zanzibar.Wakoloni walishaweka kabla hujazaliwa
 
Sheria ya 1992
Na.4 ib.3
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.
(2) Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali
ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Rais aweza kuigawa Jamhuri ya Muungano katika
mikoa, wilaya na maeneo mengineyo, kwa kufuata utaratibu
uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na
Bunge:
Isipokuwa kwamba Rais atashauriana kwanza na Rais
wa Zanzibar kabla ya kuigawa Tanzania Zanzibar katika
Mikoa, Wilaya au maeneo mengineyo.
Tangazo la nchi
yenye Mfumo wa
vyama vingi
Sheria ya 1992
Na.4 ib.5
Kuna kitu umenote kuwa katiba
Ya Zanzibar ni batili?.
P
Mimi mwenyewe nashindwa kuelewa!

hivi wanashindwa nini kusema kuwa Zanzibar ni moja ya mikoa iliyopo Tanganyika?

maana utaifa wa zanzibar hata sielewi
kuna siku niliulizwa swali na rai wa kigeni kuhusu Muungano wa Tz na Zanzibar ...yaani alibaki kushangaa kuhusu huu Muungano..

lakini kwa yote yale Mr nyerere alikuwa MJANJA sanaaa kutupatia mkoa wa zanzibar kwa kiinii macho cha Muungano..

Bila Shaka angeendelea kuwepo taifa tungekuwa mbali Sanaa ki jasusi na li uchumi...japo na uhakika zile sera zake angezibadilisha
 
Mipaka halisi ya Zanzibar ya enzi za Sultani ni visiwa Pemba na Unguja eneo lote la mwambao kuanzia kilwa hadi Tanga yani kifupi Dar yote ni Zanzibar mpaka wa Tanganyika na Zanzibar umepita kibaha
 
Mipaka halisi ya Zanzibar ya enzi za Sultani ni visiwa Pemba na Unguja eneo lote la mwambao kuanzia kilwa hadi Tanga yani kifupi Dar yote ni Zanzibar mpaka wa Tanganyika na Zanzibar umepita kibaha
Zanzibar ni mkoa tu kama lindi
 
Zanzibar ni nchi?
Jibu ni hapana, maana kuna kitu kinaitwa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Na muungano=(x+y)=z hapa x inapaswa ife na y pia inapaswa ife.
Kama sio nchi ni nini?
Je, Tanzania ni Shirikisho?
No!!
Kwanini?
Shirikisho =(A,B)=AB, kwa ufafanuzi ni kwamba nchi mbili zilizounda federation zote zitaendelea kuwepo. Na hapa tukitazama Tanganyika hatuioni.
Je, Zanzibar ni mkoa?
Uliyeuliza swali nahitaji jibu hapa
 
Back
Top Bottom