Mining jobs

Kitu kingine ambacho wachangiaji mmeshindwa kuelewa ni kuwa, hapa nimelenga uchimbaji mdogo yaani kama wewe hapo unaamua kuwekeza katika uchimbaji locally sasa badala ya kuchimba kwa mazoea ya kubashiri tu hivi sasa nimeshuhudia maeneo ya Bulyanhulu (vijijini) watu wanaungana (wasomi na wajasiriamali) na kuanzisha uchimbaji. Geologist anatafutwa na analipwa lkn anashawishiwa kuwa shareholder ili kuwapa elemu hawa wengine. Mimi nilishiriki kuambatana na Geologist kunionyesha "Mark" za eneo la kuchimba pamoja na hayo namtumia sana kila baada ya kuongeza kimo cha shimo anapeleka samples maabara. Mimi nilikuwa na lengo kuwa badala ya huyo Geologist kuwaza kuajiliwa ni vizuri akaungane na wachimbaji wadogo wenye PLANTS za kuchenjua dhahabu kuanzisha uchimbaji mdogo na baadae atakuja kujikuta ashakuwa mfanyabiashara. Haiwezekani kila anayesoma na kuhitimu awaze tu kuajiriwa
Sasa nimekuelewa sana mkuu.
Asante kwa kunipa darasa la local mining
 
majority ya watu wenye GPA hizo huwaza siku zote kuwa ni bora zaidi na hivyo kutozingatia kuwa wanapaswa kujifunza kazi mpya wanazopewa na mwisho wa siku wanashindwa kudeliver!! Kwenye ulimwengu wa leo,your deliverance matters,GPA zinafundisha vyuoniiiiiiii

Huo ni mtazamo wako na wengine kama wewe, ni sawa kabisa watu wa kawaida kimaisha kuwalaumu/ kuwasingizia matajiri, ni kauli tu za mtu aliekosa, ni kweli wanaweza wakawa na madhaifu kama ilivyo binadamu wa kawaida, tatizo kubwa jamii zetu hawajui NAMNA ya kuwatumia hawa watu adimu.

Mfano unampa kazi nyingi zakutumia nguvu na usanii (kukarim wateja, kuchangamkia shughuli fasta fasta) badala ya kumpa kazi za kutumia AKILI (Plannng, kutatua changamoto za kazi zilizoshindikana, ubunifu, )

Unamshindanisha akili ndogo na kubwa ? ? Engineer na Msanii ? ? huyo kazi yake ya mwezi mmoja wewe utafanya miaka 3 ,

Mafanikio ya mtu inategemea na malengo yake yeye SIO MALENGO YAKO,
 
Mkuu ungeainisha hapa angalau hiyo kiasi ya mtaji wengi tunatamani kuwekeza huko, hasa hiyo shareholding.

Mfn mimi nazitambua zile za kufungua plant ambayo min sana at least 10M unaweza kuanza nayo maeneo kama chunya kule.

Na zile nyingine za shinyanga huko mnaweka share kwa kuchanga kusapoti shughuli zote za uchimbaji alafu kitakacho patikana kinagawanya kwa asilimia kutokana na kile ulicho kitoa.. Lkn hii mimi naiterm kama betting maana unaweza weka milioni 1 yako mkachimba mkatoka patupu
Kwanza kabisa unapokuwa na ndoto za kumiliki Plant ya dhahabu na baadae kuuza dhahabu yenyewe baada ya kuchenjua hatua ambayo naiona itakupaisha haraka ni hizi:
1: Tafuta eneo lenye madini (mtumie Geologist na itapendeza ukipata Geologist hasa aliyefanya kazi serikalini akaamua kujiajiri mwenyewe maana wanakuwa na ramani ya madini na uzoefu mkubwa)
2: Baada ya kuelewana na Geologist na kumlipa chake afakuonyesha sehemu ya kuchimba (kuanzisha shimo) hii itaendana na kila shimo utalipia kutokana na maelewano yako na yeye mimi nilikuwa namlipa 600,000/= kila mark.
3: Tafuta wachimbaji wadogo wastani weka wachimbaji wanne kila shimo. Pia mpishi. Wachimbaji wengi hawataki kulipwa isipokuwa uwape asilimia (hisa) maana wanafahamu wakifikia uzalishaji watapata faida kubwa kuliko mshahara.
4: Nunua chakula na vitendea kazi. Ni vizuri ukatengeneza vibanda vya kulala huko huko
5: Ukifikia uzalishaji na kuwepo kwa madini ni vizuri ununue Crushers hata mbili au uingie ubia na mwenye ma crusher na utengeneze mwalo ambapo utapata mabaki ya mchanga utakaoutumia katika plant yako endapo huna uwezo wa kununua vifusi vyenya madini
6: Uchimbaji ni gharama hasa ukichimba eneo lenye tabia ya maji mengi.
7: Mtaji ukipanuka ni vizuri ukawa na leseni ya kumiliki eneo ili kuepuka kuja kuvamiwa na wajanja hasa pale uzalishaji wako wa dhahabu utakuwa mkubwa
 
Mwenye namba ya B52 wa Shy naomba anitumie mie nakachukue Crusher langu nikapige kazi. Mie shule sijaenda na wala chuo sikijui nyie endeleenii kutunishana misuli na GPA za 4 plus
 
Back
Top Bottom