Mimi sio mtoto wa kufikia. (Tafakuri)

Jokajeusi

JF-Expert Member
Jun 1, 2018
6,305
10,582
Habari wakuu!

Wachungaji na makasisi wametufanya tuwe watoto wakufikia. Kama haitoshi Mashekhe na maimamu wametugeuza watoto haramu katika nyumba ya Baba yetu. Wameturubuni kwa maneno ya uongo na hadithi za kutunga. Nasi tumekubali kuishi kama watumwa katika nyumba yetu.

Wamejipa haki ya umiliki wa ukweli. Eti ukweli wa Neno la Baba yetu ambaye wamemfanya kwetu kama Bosi wetu kumbe ni Baba yetu. Si kwamba hawajui yakuwa yeye ni Baba mzazi na mwenye kutulea katika nyumba hii. Na mali zote alituwekea sisi lakini wamemficha hata hatumuoni ili kujilimbikizia mali zake kusudi sisi tuishi kwa taabu katika nyumba yetu.

Eti tukirudi nyumbani tukakuta hakujapikwa tusiulize kwa nini hakujapikwa kisa Baba yetu haulizwi na hapaswi kuulizwa. Je Baba yangu mzazi na mlezi nisimuulize kuhusu chanzo cha njaa yangu, chanzo cha matatizo yangu. Je nikikosa mavazi pia nisimuulize. Mimi sio mtoto wa kufikia nasema. Ninayo haki ya kuuliza yanayonihusu.

Huko Kwenye mahekalu nikiuliza kwa nini Baba yangu aliondoka na kuniacha mkiwa. Nikiuliza kwa nini naumwa, na kupatwa na mikosi kama sio majanga ya kila namna. Naambiwa napaswa kushukuru kwa kila jambo kwani ni mipango ya Baba yangu na ipo siku ataniokoa katika utumwa na taabu zote. Iweje niishi kwa tabu katika nyumba aliyojenga Baba yangu.

Mimi sio mtoto wa kufikia. Ni mtoto halali wa Baba yangu. Nitauliza na kuomba chochote nikitakacho. Nikisema hivi naambiwa namkufuru Baba yangu aliyeenda mbali. Niacheni nimkufuru, yeye ndio anajua namna ya kunishughulikia kama mwanae. Iweje nyie mnisemee na kunichongea kwa Baba yangu.

Mnanipa vitisho eti nitakufa kifo kibaya, eti Baba yangu hadhihakiwi hivyo atanipa fresh ya shamba. Sijajua mnamzungumzia Baba yake nani. Ila kama ni Baba yangu mtasubiri sana. Baba yangu alinipa mali nyie mkanituliza kwa maneno yenu ya hila yenye utamu na huruma ya kiutu.

Mkaniambia nitoe Kodi ambayo mliita sijui zaka na sadaka looh! Hivi tokea lini Mwana akalipa kodi kwenye nyumba ya Baba yake. Mimi sio Mtoto wa kufikia ili nilipe Kodi mliyoiita zaka na sadaka. Baba yangu anamali nyingi sana ndio maana akanijengea nyumba ya kuishi sasa nilipe vipi Kodi.

Mambo yanayomhusu Baba yangu mnajifanya mnayajua sana. Mara Baba yangu yupo Mbinguni, sijui kila mahali, sijiu ana wapambe zake ambao ninyi mliwaita malaika. Mnanichonganisha na Baba yangu eti sifuati taratibu zake. Yeye alinambia kuwa niishi kwa raha mustarehe katika nyumba yake ambayo ni yangu kwa sasa. Lakini mwanifundisha elimu ya kijinga sana.

Mimi sio Mtoto wa kufikia. Eti Kuhoji kama Baba ananipenda au la ni kosa langu. Kwani mimi kujua napendwa ni kosa. Hivi nikipatwa na majanga makubwa na Baba yangu akaniangalia tuu bila kufanya lolote wakati anauwezo wa kuyazuia alafu nikiuliza upendo wa Baba kwangu ninyi mnasema nakufuru tena mnasema nitachomwa na Baba yangu mpenzi.

Nataka niuambie ulimwengu. mimi sio mtoto wa kufikia. Huyu ni Baba yangu. Hizo hadithi za kanisani na kwenye mahekalu. Hadithi za kwenye misikiti na masinagogi msiniambie mimi.
Mnachekesha sana.

Iwafikie wote wenye Baba kama Mimi.

Joka Jeusi ni mtoto wa pekee katika familia ya Baba aliyeenda nchi za mbali. Lakiji anakabiliwa na changamoto ya madalali wanaojifanya wanamjua Baba yake.

Karibuni kwa Mada
 
Nilishasomaga maandiko tofauti tofauti mara nyingi tu na ninaendelea kusoma maybe nitabadilisha mawazo siku moja.
lla kwa sasa naamini Baba yetu anayetajwa kwenye vitabu maarufu vinavyotumika huko makanisani na misikitini simuoni kama ana upendo kwetu sisi wanae tusio wa kufikia.
Namuona katili zaidi kuliko kutupenda kama inavyodaiwa.
 
Nilishasomaga maandiko tofauti tofauti mara nyingi tu na ninaendelea kusoma maybe nitabadilisha mawazo siku moja.
lla kwa sasa naamini Baba yetu anayetajwa kwenye vitabu maarufu vinavyotumika huko makanisani na misikitini simuoni kama ana upendo kwetu sisi wanae tusio wa kufikia.
Namuona katili zaidi kuliko kutupenda kama inavyodaiwa.
Nimeshusha pumzi ndefuuuu
 
Nilishasomaga maandiko tofauti tofauti mara nyingi tu na ninaendelea kusoma maybe nitabadilisha mawazo siku moja.
lla kwa sasa naamini Baba yetu anayetajwa kwenye vitabu maarufu vinavyotumika huko makanisani na misikitini simuoni kama ana upendo kwetu sisi wanae tusio wa kufikia.
Namuona katili zaidi kuliko kutupenda kama inavyodaiwa.


Baba anayesubiria kukuchoma moto dooh!
 
Nilishasomaga maandiko tofauti tofauti mara nyingi tu na ninaendelea kusoma maybe nitabadilisha mawazo siku moja.
lla kwa sasa naamini Baba yetu anayetajwa kwenye vitabu maarufu vinavyotumika huko makanisani na misikitini simuoni kama ana upendo kwetu sisi wanae tusio wa kufikia.
Namuona katili zaidi kuliko kutupenda kama inavyodaiwa.

Baba sio katili na hawezi kuwa katili, tatizo lipo kwa wawakilishi wake wanaojifanya madalali..
 
Hoja ni ya kufikirisha sana. Kuna ndugu zetu pia,ndugu zetu kabisa wa damu wamejiita baba ,yaani wanatutisha,wanasema wakiamua jambo ,baba analibariki,hao ambao wanajiita baba sisi ndio tunawalisha kwa kodi zetu. Wanadai wako sawa na baba kabisa,lakini mbona ni wakatili ,na wanadai wakipenda wanaweza kukupandisha daraja ukawa kama wao. Hata ukifa wanaweza fanya namna Fulani ukapanda cheo. Wengine ni marehemu na wakati wapo nasi wakatuagiza tukitaja jina lao tumalizie na kibwagizo cha kuwambea kwa baba. Kwa kweli kuna maajabu sana
 
JOka jeusi baba yake atakuwa joka jeusi tiiiiiiiiiiii - baba yako yuko kuzimu mfuate huko huko; hapa duniani ni milki ya wanadamu. Tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge; minyororo ya shetani (joka jeusi tiiiii) imeshindwa!
 
Hoja ni ya kufikirisha sana. Kuna ndugu zetu pia,ndugu zetu kabisa wa damu wamejiita baba ,yaani wanatutisha,wanasema wakiamua jambo ,baba analibariki,hao ambao wanajiita baba sisi ndio tunawalisha kwa kodi zetu. Wanadai wako sawa na baba kabisa,lakini mbona ni wakatili ,na wanadai wakipenda wanaweza kukupandisha daraja ukawa kama wao. Hata ukifa wanaweza fanya namna Fulani ukapanda cheo. Wengine ni marehemu na wakati wapo nasi wakatuagiza tukitaja jina lao tumalizie na kibwagizo cha kuwambea kwa baba. Kwa kweli kuna maajabu sana
sala za marehemu unazijua?
 
Habari wakuu!

Wachungaji na makasisi wametufanya tuwe watoto wakufikia. Kama haitoshi Mashekhe na maimamu wametugeuza watoto haramu katika nyumba ya Baba yetu. Wameturubuni kwa maneno ya uongo na hadithi za kutunga. Nasi tumekubali kuishi kama watumwa katika nyumba yetu.

Wamejipa haki ya umiliki wa ukweli. Eti ukweli wa Neno la Baba yetu ambaye wamemfanya kwetu kama Bosi wetu kumbe ni Baba yetu. Si kwamba hawajui yakuwa yeye ni Baba mzazi na mwenye kutulea katika nyumba hii. Na mali zote alituwekea sisi lakini wamemficha hata hatumuoni ili kujilimbikizia mali zake kusudi sisi tuishi kwa taabu katika nyumba yetu.

Eti tukirudi nyumbani tukakuta hakujapikwa tusiulize kwa nini hakujapikwa kisa Baba yetu haulizwi na hapaswi kuulizwa. Je Baba yangu mzazi na mlezi nisimuulize kuhusu chanzo cha njaa yangu, chanzo cha matatizo yangu. Je nikikosa mavazi pia nisimuulize. Mimi sio mtoto wa kufikia nasema. Ninayo haki ya kuuliza yanayonihusu.

Huko Kwenye mahekalu nikiuliza kwa nini Baba yangu aliondoka na kuniacha mkiwa. Nikiuliza kwa nini naumwa, na kupatwa na mikosi kama sio majanga ya kila namna. Naambiwa napaswa kushukuru kwa kila jambo kwani ni mipango ya Baba yangu na ipo siku ataniokoa katika utumwa na taabu zote. Iweje niishi kwa tabu katika nyumba aliyojenga Baba yangu.

Mimi sio mtoto wa kufikia. Ni mtoto halali wa Baba yangu. Nitauliza na kuomba chochote nikitakacho. Nikisema hivi naambiwa namkufuru Baba yangu aliyeenda mbali. Niacheni nimkufuru, yeye ndio anajua namna ya kunishughulikia kama mwanae. Iweje nyie mnisemee na kunichongea kwa Baba yangu.

Mnanipa vitisho eti nitakufa kifo kibaya, eti Baba yangu hadhihakiwi hivyo atanipa fresh ya shamba. Sijajua mnamzungumzia Baba yake nani. Ila kama ni Baba yangu mtasubiri sana. Baba yangu alinipa mali nyie mkanituliza kwa maneno yenu ya hila yenye utamu na huruma ya kiutu.

Mkaniambia nitoe Kodi ambayo mliita sijui zaka na sadaka looh! Hivi tokea lini Mwana akalipa kodi kwenye nyumba ya Baba yake. Mimi sio Mtoto wa kufikia ili nilipe Kodi mliyoiita zaka na sadaka. Baba yangu anamali nyingi sana ndio maana akanijengea nyumba ya kuishi sasa nilipe vipi Kodi.

Mambo yanayomhusu Baba yangu mnajifanya mnayajua sana. Mara Baba yangu yupo Mbinguni, sijui kila mahali, sijiu ana wapambe zake ambao ninyi mliwaita malaika. Mnanichonganisha na Baba yangu eti sifuati taratibu zake. Yeye alinambia kuwa niishi kwa raha mustarehe katika nyumba yake ambayo ni yangu kwa sasa. Lakini mwanifundisha elimu ya kijinga sana.

Mimi sio Mtoto wa kufikia. Eti Kuhoji kama Baba ananipenda au la ni kosa langu. Kwani mimi kujua napendwa ni kosa. Hivi nikipatwa na majanga makubwa na Baba yangu akaniangalia tuu bila kufanya lolote wakati anauwezo wa kuyazuia alafu nikiuliza upendo wa Baba kwangu ninyi mnasema nakufuru tena mnasema nitachomwa na Baba yangu mpenzi.

Nataka niuambie ulimwengu. mimi sio mtoto wa kufikia. Huyu ni Baba yangu. Hizo hadithi za kanisani na kwenye mahekalu. Hadithi za kwenye misikiti na masinagogi msiniambie mimi.
Mnachekesha sana.

Iwafikie wote wenye Baba kama Mimi.

Joka Jeusi ni mtoto wa pekee katika familia ya Baba aliyeenda nchi za mbali. Lakiji anakabiliwa na changamoto ya madalali wanaojifanya wanamjua Baba yake.

Karibuni kwa Mada
Ukishaelewa habari ya jumla kwamba baba Mungu (mjuzi wa yote, mwenye uwezowote na upendo wote) kuwepo ni uzushi tu, hizi stories nyingine za rejareja hazitakusumbua.
 
Back
Top Bottom