Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,305
- 10,582
Habari wakuu!
Wachungaji na makasisi wametufanya tuwe watoto wakufikia. Kama haitoshi Mashekhe na maimamu wametugeuza watoto haramu katika nyumba ya Baba yetu. Wameturubuni kwa maneno ya uongo na hadithi za kutunga. Nasi tumekubali kuishi kama watumwa katika nyumba yetu.
Wamejipa haki ya umiliki wa ukweli. Eti ukweli wa Neno la Baba yetu ambaye wamemfanya kwetu kama Bosi wetu kumbe ni Baba yetu. Si kwamba hawajui yakuwa yeye ni Baba mzazi na mwenye kutulea katika nyumba hii. Na mali zote alituwekea sisi lakini wamemficha hata hatumuoni ili kujilimbikizia mali zake kusudi sisi tuishi kwa taabu katika nyumba yetu.
Eti tukirudi nyumbani tukakuta hakujapikwa tusiulize kwa nini hakujapikwa kisa Baba yetu haulizwi na hapaswi kuulizwa. Je Baba yangu mzazi na mlezi nisimuulize kuhusu chanzo cha njaa yangu, chanzo cha matatizo yangu. Je nikikosa mavazi pia nisimuulize. Mimi sio mtoto wa kufikia nasema. Ninayo haki ya kuuliza yanayonihusu.
Huko Kwenye mahekalu nikiuliza kwa nini Baba yangu aliondoka na kuniacha mkiwa. Nikiuliza kwa nini naumwa, na kupatwa na mikosi kama sio majanga ya kila namna. Naambiwa napaswa kushukuru kwa kila jambo kwani ni mipango ya Baba yangu na ipo siku ataniokoa katika utumwa na taabu zote. Iweje niishi kwa tabu katika nyumba aliyojenga Baba yangu.
Mimi sio mtoto wa kufikia. Ni mtoto halali wa Baba yangu. Nitauliza na kuomba chochote nikitakacho. Nikisema hivi naambiwa namkufuru Baba yangu aliyeenda mbali. Niacheni nimkufuru, yeye ndio anajua namna ya kunishughulikia kama mwanae. Iweje nyie mnisemee na kunichongea kwa Baba yangu.
Mnanipa vitisho eti nitakufa kifo kibaya, eti Baba yangu hadhihakiwi hivyo atanipa fresh ya shamba. Sijajua mnamzungumzia Baba yake nani. Ila kama ni Baba yangu mtasubiri sana. Baba yangu alinipa mali nyie mkanituliza kwa maneno yenu ya hila yenye utamu na huruma ya kiutu.
Mkaniambia nitoe Kodi ambayo mliita sijui zaka na sadaka looh! Hivi tokea lini Mwana akalipa kodi kwenye nyumba ya Baba yake. Mimi sio Mtoto wa kufikia ili nilipe Kodi mliyoiita zaka na sadaka. Baba yangu anamali nyingi sana ndio maana akanijengea nyumba ya kuishi sasa nilipe vipi Kodi.
Mambo yanayomhusu Baba yangu mnajifanya mnayajua sana. Mara Baba yangu yupo Mbinguni, sijui kila mahali, sijiu ana wapambe zake ambao ninyi mliwaita malaika. Mnanichonganisha na Baba yangu eti sifuati taratibu zake. Yeye alinambia kuwa niishi kwa raha mustarehe katika nyumba yake ambayo ni yangu kwa sasa. Lakini mwanifundisha elimu ya kijinga sana.
Mimi sio Mtoto wa kufikia. Eti Kuhoji kama Baba ananipenda au la ni kosa langu. Kwani mimi kujua napendwa ni kosa. Hivi nikipatwa na majanga makubwa na Baba yangu akaniangalia tuu bila kufanya lolote wakati anauwezo wa kuyazuia alafu nikiuliza upendo wa Baba kwangu ninyi mnasema nakufuru tena mnasema nitachomwa na Baba yangu mpenzi.
Nataka niuambie ulimwengu. mimi sio mtoto wa kufikia. Huyu ni Baba yangu. Hizo hadithi za kanisani na kwenye mahekalu. Hadithi za kwenye misikiti na masinagogi msiniambie mimi.
Mnachekesha sana.
Iwafikie wote wenye Baba kama Mimi.
Joka Jeusi ni mtoto wa pekee katika familia ya Baba aliyeenda nchi za mbali. Lakiji anakabiliwa na changamoto ya madalali wanaojifanya wanamjua Baba yake.
Karibuni kwa Mada
Wachungaji na makasisi wametufanya tuwe watoto wakufikia. Kama haitoshi Mashekhe na maimamu wametugeuza watoto haramu katika nyumba ya Baba yetu. Wameturubuni kwa maneno ya uongo na hadithi za kutunga. Nasi tumekubali kuishi kama watumwa katika nyumba yetu.
Wamejipa haki ya umiliki wa ukweli. Eti ukweli wa Neno la Baba yetu ambaye wamemfanya kwetu kama Bosi wetu kumbe ni Baba yetu. Si kwamba hawajui yakuwa yeye ni Baba mzazi na mwenye kutulea katika nyumba hii. Na mali zote alituwekea sisi lakini wamemficha hata hatumuoni ili kujilimbikizia mali zake kusudi sisi tuishi kwa taabu katika nyumba yetu.
Eti tukirudi nyumbani tukakuta hakujapikwa tusiulize kwa nini hakujapikwa kisa Baba yetu haulizwi na hapaswi kuulizwa. Je Baba yangu mzazi na mlezi nisimuulize kuhusu chanzo cha njaa yangu, chanzo cha matatizo yangu. Je nikikosa mavazi pia nisimuulize. Mimi sio mtoto wa kufikia nasema. Ninayo haki ya kuuliza yanayonihusu.
Huko Kwenye mahekalu nikiuliza kwa nini Baba yangu aliondoka na kuniacha mkiwa. Nikiuliza kwa nini naumwa, na kupatwa na mikosi kama sio majanga ya kila namna. Naambiwa napaswa kushukuru kwa kila jambo kwani ni mipango ya Baba yangu na ipo siku ataniokoa katika utumwa na taabu zote. Iweje niishi kwa tabu katika nyumba aliyojenga Baba yangu.
Mimi sio mtoto wa kufikia. Ni mtoto halali wa Baba yangu. Nitauliza na kuomba chochote nikitakacho. Nikisema hivi naambiwa namkufuru Baba yangu aliyeenda mbali. Niacheni nimkufuru, yeye ndio anajua namna ya kunishughulikia kama mwanae. Iweje nyie mnisemee na kunichongea kwa Baba yangu.
Mnanipa vitisho eti nitakufa kifo kibaya, eti Baba yangu hadhihakiwi hivyo atanipa fresh ya shamba. Sijajua mnamzungumzia Baba yake nani. Ila kama ni Baba yangu mtasubiri sana. Baba yangu alinipa mali nyie mkanituliza kwa maneno yenu ya hila yenye utamu na huruma ya kiutu.
Mkaniambia nitoe Kodi ambayo mliita sijui zaka na sadaka looh! Hivi tokea lini Mwana akalipa kodi kwenye nyumba ya Baba yake. Mimi sio Mtoto wa kufikia ili nilipe Kodi mliyoiita zaka na sadaka. Baba yangu anamali nyingi sana ndio maana akanijengea nyumba ya kuishi sasa nilipe vipi Kodi.
Mambo yanayomhusu Baba yangu mnajifanya mnayajua sana. Mara Baba yangu yupo Mbinguni, sijui kila mahali, sijiu ana wapambe zake ambao ninyi mliwaita malaika. Mnanichonganisha na Baba yangu eti sifuati taratibu zake. Yeye alinambia kuwa niishi kwa raha mustarehe katika nyumba yake ambayo ni yangu kwa sasa. Lakini mwanifundisha elimu ya kijinga sana.
Mimi sio Mtoto wa kufikia. Eti Kuhoji kama Baba ananipenda au la ni kosa langu. Kwani mimi kujua napendwa ni kosa. Hivi nikipatwa na majanga makubwa na Baba yangu akaniangalia tuu bila kufanya lolote wakati anauwezo wa kuyazuia alafu nikiuliza upendo wa Baba kwangu ninyi mnasema nakufuru tena mnasema nitachomwa na Baba yangu mpenzi.
Nataka niuambie ulimwengu. mimi sio mtoto wa kufikia. Huyu ni Baba yangu. Hizo hadithi za kanisani na kwenye mahekalu. Hadithi za kwenye misikiti na masinagogi msiniambie mimi.
Mnachekesha sana.
Iwafikie wote wenye Baba kama Mimi.
Joka Jeusi ni mtoto wa pekee katika familia ya Baba aliyeenda nchi za mbali. Lakiji anakabiliwa na changamoto ya madalali wanaojifanya wanamjua Baba yake.
Karibuni kwa Mada