Mimi ni muathirika wa UKIMWI

Mimi ni muathirika wa UKIMWI

Mwaka jana 2018 nilikutana na mwanaume wa ndoto zangu. Mtanzania, mzuri mcheshi msomi. Maongezi yalinoga sana. Tulikwenda dinner, mara ya pili tulikwenda picnic park. Siku nilipomkaribisha dinner nyumbani baada ya glass ya wine nilifinguka .

Yule kaka alikuwa hakustuka. Baada ya kuondoka aliniambia kwenye simu kuwa hataweza kunioahivyo asinipotezee muda.

Niliumia sana.
pole sana Protein
hongera kwa kuwa muwazi.
 
Aisee pole sana. ....mojawapo ya matokea ya ku jiweka wazi ndio kama hizo rejections.

Usikate tamaa muda bad unao na utabarikiwa mtu muelewa na mtakuwa na familia yenu.

Jitahidi kumsamehe na ujisamehe wewe pia, kwa maana ni jukumu lako kujilinda afya yako kwanza.

Ni muda sasa tujifunze kuacha kuwa nyanyapa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi na kuwaona kama wamemkosea Mungu au walikuwa na maienendo michafu kufika maambukizi.

Kila la kheri Protein
 
Ndio maana watu hawawezi kuleta testimonies hapa, hukuwa na sababu ya kumshambulia mleta mada, ujana unakuja na mengi, wengi tumeleteza na baadhi wameangukia kwenye maradhi kama hayo.

Relax na umshauri na kumpa moyo mwenzetu, don't attack her.
Umesoma Aya ya mwisho ?
 
Yaani ulikwenda kwa daktari baada ya kupata kazi?
Kuna utaratibu wa kupima ukipata kazi Sweden?Daktari ndio alikupa fomu?
Daktari umuambie tiki kote sina wasiwasi?Ndio alijibu una uhakika hauna ukimwi?
Prata sanningen. Det är inte så svårt att veta att du prata inte sanning..
Nimeandika kiswidish
"Sema ukweli.
Sio ngumu kujua kwamba husemi ukweli."
Sweden hamna utaratibu huo unaousimulia.Sweden hamna kitengo.Watu wote wanapimwa kwenye vårdcentral magonjwa yote.
Vårdcentral- Zahanati
 
Mkuu nilipima mwaka 2005 na baada ya hapo Zabron ndiye niliye lala nae. Mengine nimeongoa kama finzo
Ok vyema umeshajigundua mapema, nadhani pia umeshajikubali !!! Kikubwa jali Sana afya, jiepushe na ngono, ikishindikana shiriki aghalabu ngono salama !

Kwa Sasa afya yako ndio iwe kipaumbele, zingatia mlo pia ukipata muda jipangie ratiba ya mazoezi ! All the best
 
Yaani ulikwenda kwa daktari baada ya kupata kazi?
Kuna utaratibu wa kupima ulipata kazi Sweden?Daktari ndio alikupa fomu?
Daktari umuambie tiki kote sina wasiwasi?Ndio alijibu una uhakika hauna ukimwi?
Pratar sanningen. Det är inte så svårt att veta att du pratar inte sanning..
Nimeandika kiswidish
"Sema ukweli.
Sio ngumu kujua kwamba husemi ukweli."
Sweden hamna utaratibu huo unaousimulia.
Form ina maswali mengi lakini kinga ya lazima ilikuwa hepatitis B, ila niliamua kufanya full medical check up.
 
Sasa huko sindo wanasemaga kila siku wamepata kinga sijui nini

Sent using Jamii Forums mobile app
Labda huko tuendako. Nilipoanza tiba nilipewa vidonge viwili kimoja asubuhi kimoja jioni. December niliambiwa tiba imeimarishwa kidonge cha asubuhi na jioni kimechangnywa ni uamuzi wangu tu kunywa asubuhi au jioni. Lakini ni mara moja kwa siku.

Daktari alisema wengi walikuwa wanasahau dose moja kati ya hizi mbili hivyo wataalamu waliamua kuzichanganya iwe kidonge kimoja.
 
Labda huko tuendako. Nilipoanza tiba nilipewa vidonge viwili kimoja asubuhi kimoja jioni. December niliambiwa tiba imeimarishwa kidonge cha asubuhi na jioni kimechangnywa ni uamuzi wangu tu kunywa asubuhi au jioni. Lakini ni mara moja kwa siku.

Daktari alisema wengi walikuwa wanasahau dose moja kati ya hizi mbili hivyo wataalamu waliamua kuzichanganya iwe kidonge kimoja.
Hao watu wanatuvuruga tu akili zetu kama wameweza kuchanga vidonge viwili kuwa kimoja wanashindwa vitu kuchanga na vingine kuleta dawa kamili wanazingua tu wanazo ziko store ila wanataka wabongo tufe kwanza waje kuchukua bara lao kwa upya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao watu wanatuvuruga tu akili zetu kama wameweza kuchanga vidonge viwili kuwa kimoja wanashindwa vitu kuchanga na vingine kuleta dawa kamili wanazingua tu wanazo ziko store ila wanataka wabongo tufe kwanza waje kuchukua bara lao kwa upya

Sent using Jamii Forums mobile app
Research ya hizi dawa inagharimu pesa nyingi hivyo inawezekana wenye licences wamezuia tiba kamili mpaka warudishe faida yao.
 
Zabron si jina lake halisi. Ameniumza sana. Kila nikijaribu kumsamehe ninajikuta ninalia.
Mtaje tuu yeye .Yeye aliamua kukufanyia ukatili hivyo. Hakuna haja ya kumuwekea privacy. Unaweza kuja na Id mpya na nyuzi nyingine ukamtaja tuu. Alikufanyia ukatili Sana
 
Ndugu huku Tz wapo wazee vijijini ambao wanatibu hiyo kitu unakuwa mzima kabisa lakini wazee wenyewe hawana umaarufu wala mbwembwe wapo kigoma, Mtwara, nk jitahidi ukipata likizo uje bongo ukakae bush kwa hawa wazee ndani ya mwezi tu unakuwa HIV Neg

Kulalamika na kutuhumu watu bila ya ushahidi wenye mashiko haitakusaidia kitu sanasana utaletewa kejeli na maneno mbofu mbofu

Maadamu umeshajijua afya yako jitahidi kujihifadhi sasa usianze kuusambaza kwa watu kwa kulipa kisasi
 
Back
Top Bottom