Mimi na Mgahawa wa Chef Pride

Mimi na Mgahawa wa Chef Pride

Ukitaka kujua Jiji la dar es salaam, nyuzi kama hizi binafsi zinanikosha... Mimi wa kuja ndo unajua mambo.

Hongera
 
Bonta nilijua tu nitakukumbusha enzi za Best Bite mafafa yote full mass nondo kati hapo.
Kulikuwa na sehemu ile opp na Serena sahv ilikuwa inaitwa Bush trekker kama sijakosea jina ilikuwa meeting point nzr sana pia
Baadaye posta ikaja food world

Ova
 
Kulikuwa na sehemu ile opp na Serena sahv ilikuwa inaitwa Bush trekker kama sijakosea jina ilikuwa meeting point nzr sana pia
Baadaye posta ikaja food world

Ova
Zile sehemu ilikuwa ukipita nje tu unaipata ile harufu unataka kuingia mwenyewe.
 
Oh nami umenikumbusha,mimi sheikh said nilikujulia hapo salamander kwa akina hashim sagaf,nilikuwa nakuja hapo na kaka yangu wakati huo nikisoma nje ya nchi,nikawa a bit rafiki kwako kutokana na uwezo wako wako wa kuchambua mambo,pia nikamfahamu jamaa mmoja akiitwa tamim,na kijana mmoja kama msomali hivi akiitwa mohamed akiaandikia magazeti.Kaka yangu akanipeleka hapo chef pride chagga street,aisee kulikuwa na kila aina ya chakula na ndipo nikakutana na watu wengi sana maarufu,na kabla sijasahau pale salamander nilikutana na jakaya na tukawa marafiki sana nadhani wakati huo alikuwa waziri wa madini.

Hapo chef pride nje kulikuwa na shoeshiner wengi na vijana wa kutafuta parking za magari.

Baadae nikamfahamu huyo mmiliki wa chef pride.

Sasa hapo pembeni ya chef pride kulikuwa na tea room mmoja maarufu sana,ambayo ilikuwa maarufu kwa aina fulani ya chai kwenye tu vikombe tudogo na kababu za kunde,aiseeee ile chai haina mfano,watu walikuwa wanagombania nafasi na mara kwa mara nilikuwa nakuta foleni nje.Pia walikuwa na mzee mmoja weita mmoja ambae alikuwa ana kichwa cha kompyuta,bili za watu alikuwa anakariri tu na akiulizwa anatoa hesabu kamili.Miaka ya zamani klabu ya yanga ilikuwa na seneti yake ikiongozwa na mohamed virani,nao walikuwa wakija wote hapo yea room kunywa chai.

Nami hapo nilipata dada mmoja wa kihindi nikazaa nae.Basi sheikh said asante sana kwa uzi wako
Mzee Abdul yupo mpaka leo ni mhudumu. Huyu Mzee anayo kumbukumbu mpaka ya Malcom X alipotembelea Tanzania mwaka 1965 siku chache kabla ya kifo chake huo USA
 
Ya kale ni dhahabu.
Umenikumbusha mgahawa maarufu mtaa wa uhuru na Swahili uliojuilikana kama Salim Tea Shop. Juzi kati nimepita pale nimekuta ghorofa la msajili NHC limebomolewa na ujenzi mpya unaendelea wakati mgahawa haupo tena kiukweli machozi yalinitoka na huzuni ilinijaa.
Kwa zaidi ya miaka 40 tumekuwa tukija kariakoo basi lazima tuingie tule au kupata chochote pale Salim Tea Shop.
Historia imepotea.
 
Kulikuwa na sehemu ile opp na Serena sahv ilikuwa inaitwa Bush trekker kama sijakosea jina ilikuwa meeting point nzr sana pia
Baadaye posta ikaja food world

Ova
bushtrekker kila jumapili palikuwa na live banda nzuri sana
 
Leo njoo tujumuike kwenye 40 ya mwapachu Mohamed Said

Ova

Leo njoo tujumuike kwenye 40 ya mwapachu Mohamed Said

Ova
KHITMA YA JUMA MWAPACHU

Ndugu na jamaa leo walikusanyika nyumbani kwa Juma Mwapachu kusoma khitma.

Mtume SAW kifo kinatosha kuwa mawaidha.

Kwangu binafsi kuwa kwenye nyumba ile kulirejesha kumbukumbu nyingi za furaha nikiwa na marehemu ukumbini kwake tukizungumza mengi.

Halikadhalika katika hadhira ile niliwaona watu wengi ambao kwa namna moja au nyingine walirejesha fikra zangu kwa marehemu.

Katika wengi tuliohudhuria khitma hii sisi wakati wa uhai wake Juma Mwapachu alikuwa kaka mkubwa kwetu kwa kila hali.

Juma Mwapachu alitutangulia sisi kwa kila kitu kuanzia kuingia Chuo Kikuu hadi katika ajira iwe serikalini, shirika la umma au binafsi.

Juma Mwapachu alikuwa mwanafunzi wa University of East Africa wakati sisi wengi wetu tuko sekondari.

Katika niliowaona pale khitmani waliosoma University of East Africa alikuwa Mohamed Ismail na Prof. Issa Shivji.

Waliobakia niliowafahamu walisoma Dar es Salaam University na hatukulikuta hata vumbi lake pale chuoni.

Juma Mwapachu kwa wengi wetu tuliokuwa pale kama nilivyosema alikuwa kaka.

Sasa nawaangalia wale wa rika la kaka Juma Mwapachu Yusuf Kalala, Mohamed Ismail, Prof. Issa Shivji wote wamejikusanya wamekaa pamoja.

Miaka imekwenda lakini wanapendeza.

Katika hawa kwangu mimi kila mtu ana historia ya yake ya kupendeza.

Kaka Yusuf Kalala mwanafunzi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School kipi asichokijua kuhusu Dar-es-Salaam?

Siku moja namwambia Bi Bahai keshafariki.

Akaniambia yu hai.

(Kulikuwa na Bahia wawili na wote maarufu - Bi. Bahia Lumelezi na Bi. Bahia mke wa Sheikh Mzee Ali Comorian.

Mmoja katika hawa ndiye aliyekuwa kutangulia mbele ya haki).

Juma Mwapachu alipanda mabega ya Mohamed Ismail kukwea mlingoti uliokuwa unapeperusha Union Jack kuiteremsha chini katika maandamano dhidi ya Uingereza kutochukua hatua Ian Smith alivyotangaza uhuru wa Southern Rhodesia yaani "Uniletaral Declaration of Independence," maarufu UDI.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu walikuwa wameandamana kutoka Mlimani kuja Ubalozi wa Uingereza.

Wanafunzi walikuwa wamejaa ghadhabu.

Huu ulikuwa mwaka wa 1965.

Juma Mwapachu na Mohamed Ismail wote wanafunzi wa sheria walikuwa vijana wadogo.

Kisa hiki alinihadithia Mzee Ahmad Rashaad Ali aliyeshuhudia tukio hilo kwa macho akiwa na akiwajua hawa watoto kama alivyopenda kuwaita.

Mzee Rashaad akisema Juma Mwapachu alikuwa akiendeleza vile vita vya baba yake Hamza Kibwana Mwapachu dhidi ya Waingereza wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Tulipokuwa tunachukua chakula akanijia mtu akaniuliza kwa nini nimekataa kuzungumza.

Nilikuwa nimesimama na Chief Edward "Ted" Makwaia wa Siha, Usukuma.

(Ted ndiye aliyenijulisha kwa Juma Mwapachu mwaka wa 1967).

Nilimjibu kuwa sikukataa ila nasaa walizotoa masheikh zetu zilitosha.

Lakini kama ingekuwa hadhira nyingine si khitma ningeeleza kisa hiki cha kutunguliwa bendera ya Mwingereza Juma Mwapachu kapanda mabega ya Mohamed Ismail kuuparamia mlingoti wa Union Jack.

Lakini kisa hiki ningekieleza kwa urefu kama alivyonihadithia Mzee Rashaad kuanzia jana yake Mzee Ahmed Rashaad akiwa Deputy Permanent Secretary Information alipokwenda nyumbani kwa Mwalimu Nyerere kutaka kauli yake kuhusu tatizo la Rhodesia ili Wizara ya Habari itoe "Press Release."

Rashaad alikumkuta Mwalimu nyumbani kwake anazungumza na Dossa Aziz na Lucy Lameck.

Kuna stori kubwa Nyerere alimhadithia Mzee Ahmed Rashaad Ali.
 
Oh nami umenikumbusha,mimi sheikh said nilikujulia hapo salamander kwa akina hashim sagaf,nilikuwa nakuja hapo na kaka yangu wakati huo nikisoma nje ya nchi,nikawa a bit rafiki kwako kutokana na uwezo wako wako wa kuchambua mambo,pia nikamfahamu jamaa mmoja akiitwa tamim,na kijana mmoja kama msomali hivi akiitwa mohamed akiaandikia magazeti.Kaka yangu akanipeleka hapo chef pride chagga street,aisee kulikuwa na kila aina ya chakula na ndipo nikakutana na watu wengi sana maarufu,na kabla sijasahau pale salamander nilikutana na jakaya na tukawa marafiki sana nadhani wakati huo alikuwa waziri wa madini.

Hapo chef pride nje kulikuwa na shoeshiner wengi na vijana wa kutafuta parking za magari.

Baadae nikamfahamu huyo mmiliki wa chef pride.

Sasa hapo pembeni ya chef pride kulikuwa na tea room mmoja maarufu sana,ambayo ilikuwa maarufu kwa aina fulani ya chai kwenye tu vikombe tudogo na kababu za kunde,aiseeee ile chai haina mfano,watu walikuwa wanagombania nafasi na mara kwa mara nilikuwa nakuta foleni nje.Pia walikuwa na mzee mmoja weita mmoja ambae alikuwa ana kichwa cha kompyuta,bili za watu alikuwa anakariri tu na akiulizwa anatoa hesabu kamili.Miaka ya zamani klabu ya yanga ilikuwa na seneti yake ikiongozwa na mohamed virani,nao walikuwa wakija wote hapo yea room kunywa chai.

Nami hapo nilipata dada mmoja wa kihindi nikazaa nae.Basi sheikh said asante sana kwa uzi wako
Fimbo...
Umenikumbusha mbali.
 
Chif pride enzi zile za ikifika saa 4 vyakula vyoote ni buku 2, extrems balaaa.
 
Back
Top Bottom