Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 22,454
- 32,980
MIMI NA CHEF PRIDE
Historia yetu sasa nadhani ina kiasi cha miaka 30 na zaidi.
Mgahawa ulikuwa Mosque Street, Zahir Hotel.
Katika miaka ya 1980/90 ndipo kilipokuwa kijiwe chetu cha mazungumzo, kula na kunywa.
Mwendeshaji wa mgahawa kijana mwenzetu Salim Mahsen.
Vyama vingi vilipoanza 1992 mgahawa ukawa uwanja wa siasa wanachama na wapenzi wa vyama vyote huwapungui hapo.
Mijadala moto moto ikiunguruma.
Unachagua mwenyewe ukae meza ipi.
NCCR Mageuzi na Augustino Mrema ilikuwa imepamba moto, NRA kisha CUF ya Maalim Seif na Kaka Mkubwa CCM.
Salim anatununulia magazeti yote wa nyakati zile anatuwekea mezani - Shaba, Rai, Bahari, Uhuru na haya magazeti yalikuwa yana mkondo wake katika siasa changa za vyama vingi.
Ukifika Zahir asubuhi kunywa chai unapata taarifa zote katika ulimwengu wa siasa za Tanzania.
Salim akiijua saikolojia ya sisi wateja wake.
Wakati mwingine akitutania anasema, "Nimekuwekeeni hizi meza ziwe mbali ili msiibiane sera."
Siku alipotuambia kuwa anairudisha hoteli kwa mwenyewe ilikuwa msiba.
Wateja wote tulitawanyika.
Hatukuwa na mahali pa kukutana.
Mgahawa ulikuwapo lakini haikuwa kama alipokuwa Salim.
Uwanja hakika ulikuwapo lakini magoli yameng'olewa.
Salim akafungua Chef Pride, Chagga Street.
Haba jana.
Tukapata uhai mpya.
Kisha akafungua Chef Pride nyingine Lumumba Avenue karibu na CCM.
Chef Pride hakika leo ni sehemu ya historia ya Dar-es-Salaam.
Hapati mtu mgeni sharti atampeleka Chef.
Chai ya asubuhi haipiti ila inywewe Chef.
Halikadhalika chakula cha mchana na usiku ukiwa na mgeni.
Nimeweka hapo chini picha ya Salim na Dr. Harith Ghassany nilipomfikisha Chef miaka michache ya nyuma nikamjulisha kwa Salim.
Chef ni mahali utamuona kila mtu.
Ni suala la subra na muda.
Kulia Dr. Harith Ghassany na Salim Mahsen
Historia yetu sasa nadhani ina kiasi cha miaka 30 na zaidi.
Mgahawa ulikuwa Mosque Street, Zahir Hotel.
Katika miaka ya 1980/90 ndipo kilipokuwa kijiwe chetu cha mazungumzo, kula na kunywa.
Mwendeshaji wa mgahawa kijana mwenzetu Salim Mahsen.
Vyama vingi vilipoanza 1992 mgahawa ukawa uwanja wa siasa wanachama na wapenzi wa vyama vyote huwapungui hapo.
Mijadala moto moto ikiunguruma.
Unachagua mwenyewe ukae meza ipi.
NCCR Mageuzi na Augustino Mrema ilikuwa imepamba moto, NRA kisha CUF ya Maalim Seif na Kaka Mkubwa CCM.
Salim anatununulia magazeti yote wa nyakati zile anatuwekea mezani - Shaba, Rai, Bahari, Uhuru na haya magazeti yalikuwa yana mkondo wake katika siasa changa za vyama vingi.
Ukifika Zahir asubuhi kunywa chai unapata taarifa zote katika ulimwengu wa siasa za Tanzania.
Salim akiijua saikolojia ya sisi wateja wake.
Wakati mwingine akitutania anasema, "Nimekuwekeeni hizi meza ziwe mbali ili msiibiane sera."
Siku alipotuambia kuwa anairudisha hoteli kwa mwenyewe ilikuwa msiba.
Wateja wote tulitawanyika.
Hatukuwa na mahali pa kukutana.
Mgahawa ulikuwapo lakini haikuwa kama alipokuwa Salim.
Uwanja hakika ulikuwapo lakini magoli yameng'olewa.
Salim akafungua Chef Pride, Chagga Street.
Haba jana.
Tukapata uhai mpya.
Kisha akafungua Chef Pride nyingine Lumumba Avenue karibu na CCM.
Chef Pride hakika leo ni sehemu ya historia ya Dar-es-Salaam.
Hapati mtu mgeni sharti atampeleka Chef.
Chai ya asubuhi haipiti ila inywewe Chef.
Halikadhalika chakula cha mchana na usiku ukiwa na mgeni.
Nimeweka hapo chini picha ya Salim na Dr. Harith Ghassany nilipomfikisha Chef miaka michache ya nyuma nikamjulisha kwa Salim.
Chef ni mahali utamuona kila mtu.
Ni suala la subra na muda.
Kulia Dr. Harith Ghassany na Salim Mahsen