Mimi CPA KITALIKA, TITHO.E nimekusudia kugombea nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA)

Jun 25, 2019
14
20
KUSUDIO LA KUTANGAZA NIA YA KUGOMBEA NAFASI YA KATIBU MKUU BARAZA LA VIJANA WA CHADEMA (BAVICHA).


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia Katibu mkuu kimetoa tangazo la uchaguzi wa Chama ngazi ya Taifa utakayoanza tarehe 09 Desemba na kuhitimishwa tarehe 19 mwezi huo huo kwa uchaguzi wa Katibu Mkuu wa Chama na manaibu katibu wawili. Uchaguzi wa taifa utahusisha pia mabaraza ya Chama.

Mimi CPA KITALIKA, TITHO.E nimekusudia kugombea nafasi ya Ukatibu mkuu wa Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA). Nimejipima mimi mwenyewe pamoja na kupata ushauri kutoka kwa watu wangu wa karibu wanaofahamu uwezo wangu wa kiuongozi na dhamira yangu ya kukitumikia chama na kujiridhisha kwamba nafasi hii ndiyo sahihi Zaidi kwangu.

Nafahamu yapo mafanikio yaliyofikiwa na viongozi walioshika nafasi ndani ya baraza lakini vile vile kuna mambo yanatakiwa kufanyika. Nikifanikiwa kuteuliwa kuwa mgombea nitaeleza dhamira na maono yangu kama nitachaguliwa kuwa katibu mkuu wa BAVICHA.

KAZI NA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHAMA

  • 2011: Wakati nikiwa mwanafunzi wa A’level wakati wa likizo nilishirikiana na viongozi wa Chama wilaya ya Mufindi Kueneza chama katika majimbo ya Mufindi Kusini na Kaskazini.

  • 2012: Niliteuliwa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA NI MSINGI kata ya Mtwango katika jimbo la Mufindi Kusini na nimeshiriki kuaanzisha matawi imara na tegemeo kwa chama katika jimbo la Mufindi Kusini mfano Nyololo na Ihowanza.


  • 2013: Nimeshiriki katika uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Themi Jimbo la Arusha Mjini, nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa CHASO tawi la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), nilishiriki kuanzisha CHASO MKOA WA ARUSHA na kuchaguliwa kuwa mratibu wa kwanza wa CHASO Mkoa wa Arusha.

  • 2014: Nimeshiriki kutafuta wanachama na kuwapa kadi katika jimbo la Longido Mkoa wa Arusha, nimeshiriki kampeni za uchaguzi serikali za mitaa katika Jimbo la Nyang’wale, Arumeru Magharibi na Arusha Mjini na nilichaguliwa kuwa mratibu wa CHASO Mkoa wa Arusha kwa mara nyingine.


  • 2015: Nilishiriki kampeni za ubunge katika jimbo la Mafinga Mjini kama mjumbe wa kamati ya kampeni na kuzunguka na mgombea ubunge na madiwani katika kata zote sita za jimbo. Na mara kadhaa katika jimbo la Mufindi Kaskazini.

  • 2016/2019: Nimeshiriki katika uchaguzi mdogo katika kata ya Saranga jimbo la Kibamba, uchaguzi wa marudio wa jimbo la Kinondoni katika kampeni za nyumba kwa nyumba katika kata ya Hananasifu, magomeni na Ndugumbi


  • 2019: Nimeshiriki katika kuwezesha viongozi wa chama kata ya Mtwango Jimbo la Mufindi kusini wanapata wagombea katika uchaguzi wa serikali za mitaa na vijiji.

  • 2019: Mjumbe wa Kamati Tendaji Jimbo la Mufindi Kusini na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa (Wilaya ya Mufindi)

MAFANIKIO KATIKA UONGOZI WANGU NDANI YA CHAMA.

2013/2015 MRATIBU CHASO ARUSHA.


  • Pamoja na viongozi wenzangu tulisaidia kuongea matawi ya CHASO kutoka manne mpaka kumi
  • Kuongeza ushiriki wa wanaCHASO katika kujenga chama matharani wanaCHASO kushiriki katika chaguzi ndogo za udiwani katika mikoa ya Tanga, Arusha na Manyara.
  • Kuanzisha kanuni za CHASO MKOA zilizozinduliwa na mh.Tundu lissu tofauti na mikoa mingine ambayo hutegemea nyaraka na miongozo kutoka kwa katibu Mkuu BAVICHA.
  • Kuwezesha wanaCHASO kushinda nafasi za uongozi katika serikali za wanafunzi katika vyuo mf. IAA, MMU, St Joseph (Kisongo) na Jomo Kenyatta.
  • Kuandaa mapendekezo ya KANUNI ZA KUONGOZA CHASO na kuziwasilisha kwa mjumbe wa kamati kuu Prof.Mwesige Baregu.


UONGOZI NJE YA CHAMA

2008/2009-
Amekuwa kiongozi katika serikali ya wanafunzi shule ya sekondari Mdabulo

2010/2011- Amekuwa kiongozi wa Afya na Mazingira shule ya sekondari Azani.

2012/2013- Amekuwa mwakilishi wa Taaluma wa Darasa (Uchumi na Fedha) katika Kamati ya Taaluma ya Serikali ya wanafunzi.

2019- -Mjumbe wa Board na mshauri wa kifedha wa NGO iitwayo Every Child Tanzania (ECT)



ELIMU YA MGOMBEA

2018/2019: MBA Corporate Management (IP)-
Mzumbe University

2016/2018: Certified Public Accountant (CPA)-National Board of Accountants and Auditors.

2012/2015: Bachelor of Economics and Finance-Institute of Accountancy Arusha

2006/2012: O’level & A ‘level- Mdabulo Secondary School/Azania High School
 
Kila LA heri, hiyo ndo demokrasia.jambo LA msingi utambue kuna kupata Na kushindwa.pia ukishinda hakikisha unahudumu kwa miaka mitano yote.mchezo Wa kuunga juhudi kama katambi sio saws.
 
..huyu kijana ameshiriki ktk shughuli za chama na ana elimu nzuri.

..Nataka kumsikiliza kama ana uwezo wa mzuri wa kujenga hoja na kulitawala jukwaa.
 
Is he a person of INTEGRITY????? sababu ya kuuliza hii swali ni hii, kaa hana integrity ya kutosha basi anaweza nunuliwa na wanaccm, kaa vile waitara na wengine walivyonunuliwa, elimu pekee haitoshi, kuwa na UNSHAKABLE POLITCAL STAND is aslo very vital
 
Cha ajabu anaweza kushinda halafu akanunuliwa kwa Bei chee na kuunga juhudi
Tunakwenda na Mdude BAVICHA
Aisee siku hizi wanasiasa ni Kama bidhaa wanataka kupata fursa tu ya
kuonekana,wakionekana wauzike kwa bei nzuri.
'Any way' hongera mgombea Mungu awe pamoja nawe uendeleze chama chenu.
 
Cha ajabu anaweza kushinda halafu akanunuliwa kwa Bei chee na kuunga juhudi
Tunakwenda na Mdude BAVICHA

..huyu anagombea ukatibu mkuu.

..dawa ya ushawishi wa pesa za ccm ni cdm kuwa na vijana wengi wanaoweza kuziba nafasi za wanaonunuliwa.

..wakati wa vita ya Vietnam Marekani alikuwa akiua askari wengi sana wa Vietcong.

..Lakini Vietcong walikuwa na uwezo wa ku-recruit askari kwa idadi kubwa mara 10 ya waliokuwa wakiuawa na Wamarekani.

..Matokeo yake Marekani alichoshwa na vita vyisivyokuwa na kikomo, wakaamua kutimka na Vietcong wakaiteka Vietnam nzima.

..Kwa hiyo, cdm wakiwa na vijana wengi wa kuziba nafasi za wanaonunuliwa, itafika wakati ccm watachoka na ndiyo itakuwa ushindi kwa cdm.
 
Good CV
Nakumbuka Bwana mmoja aliwahi kusema huko kwao kuna utaratibu wa kujuwa kama mtu ni raia au siyo hata kama chombo cha serikali kama kimethibitisha
CHADEMA.....ukiandika hivi umekosea
Chadema......kwa nini usitumie herufi kubwa zoote
Pull up your socks
 
..huyu kijana ameshiriki ktk shughuli za chama na ana elimu nzuri.

..Nataka kumsikiliza kama ana uwezo wa mzuri wa kujenga hoja na kulitawala jukwaa.
Kazi Hana Ni jobless pamoja na elimu yake
 
Back
Top Bottom