Milion 3 biashara gani naweza kufanya?

Habari zenu wanajamvi!kabla ya yote napenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa manajamvi kwa michango ya mawazo mbalimbali ambayo inatusaidia wengi wetu.
wana jf wamekua sio wachoyo wa mawazo na ama kwa hakika wa tz wote tungekua tunapeana michango na mawazo kama ivi,tungefika mbali sana.
Mimi ni mfanyakazi serikalini,mshahara ninaopata si mkubwa sana,nilikua nafkiria kujishughulisha na mradi ambao utanisaidia kidogo kusogeza ili gurudumu la maisha.Swali langu ni kwamba,nina 3 mil naweza nkafanya biashara gani?
Naomba mnisaidie mawazo yenu wakuu!

Hizo mil.3 umekopa au unazo mkononi?
 
Karibu Mama Derick,
Niliziona pale Guangzhou(China) last year,incubator zenye capacity ya mayai 500 ilikuwa ni us$ 200~us$ 300.Ukiagiza kutoka China unatakiwa uongeze umakini,utafute suppliers wa uhakika,ukinunua vibandani tu utalamba feki.
Mashine ya kuchekia mayai sikuwahi kuulizia bei.

Kila la kheir Mama Derick

Mama Derick; kuhusu incubator sifikiri kama kuna haja ya kuagia toka China, nenda SIDO watakuunganisha na watengenezaji wa incubator wa hapa nchini. Nimekuwa nikiziona katika maonyesho ya biashara (sabasaba) na hata kwenye nanenane. Nitajaribu kutafuta contact zao kwani nilichukua vipeperushi.
 
Kwakuwa uko serikalini na asilimia kubwa wanakipato kidogo si haba ukawatangazia kuwa unakopesha fedha kwa riba ya asilimia 10 kwa mwezi na kiwango kisizidi laki mbili kwa mtu so unazikopesha mwanzo wa mwezi kwenye msahahara wanakurudishia nadhani itakulipa zaidi kuliko we fikiria kwa kila mwezi unafaida ya Tsh 300,000/= kwa miezi kumi 3m unayo ni biashara gani utafanya kwa mtaji huo upate faida kama hii achana na mawazo mgando mara fuga kuku,kitimoto,karanga,nwea pombe nk nk
 
biashara ya pikipiki ina mambo mengi sana yanaweza kuku-discourage kuna mtu hapo juu ametoa mchanganuo wa kipato bila kupiga hesabu ya gharama za uendeshaji kama services, vifaa kuharibika n.k na pia pikipiki (za kichina) zina life span fupi sana kabla ya kuanza kusumbua. Naongea kwa uzoefu maana mke wangu ana hiyo biashara na ana pikipiki 4 na ile yenye kubeba mizigo moja ila hicho kizunguzungu cha uendeshaje wake ni balaa na pia unatakiwa kuiuza mara moja inapoleta matatizo na watu uwa wanalalia sana wakati wa kuzinunua zikiwa used. Unaweza kufanya hiyo biashara ila ni ngumu sana na unatakiwa kuwa una-save hela yote ili uendelee ila kama mapato yake ndio unayategemea kuendeshea maisha achana nayo kabisa

Pikipiki ikikaa miezi 6 inakuwa imechoka tayari kwa hiyo unaiangalia kama bado inaingiza kipato vizuri au inakugharimu zaidi ukiona gharama ni kubwa au faida ni kidogo uza nunua nyingine na mshauri alisema kuwa inaweza kaa mwaka 1 na nusu hiyo ni ngumu maana ikifika mwaka tu inakuwa imechoka sana

Sikushauri kununua pikipiki ni biashara ngumu sana na ushindani ni mkubwa saba pia ajali ni nyingi mno unaweza kukuta zimegongwa au kuanguka ikawa right off na huyo dereva akakugharimu kumtibu mie naijua hiyo biashara A to Z na mke wangu ameifanya zaidi ya miaka miwili sasa mwanzo zilikuwa zinalipa wakati ziko chache ila kwa sasa anataka kuacha maana imekuwa biashara kichaa
 
Ungekuwa unaweza ungekuja huku kanda ya ziwa, kwani kuna opportunities nyingi tuu (ila zinatafunwa na wajanja kutoka kenya, uganda rwanda, china etc) kama vile biashara ya kununua na kuuza dhahabu, almasi, silver etc yaani unanunua wewe mwenyewe kwa wachimbaji wadogo wadogo alafu unasafirisha Dar, Nairobi, Kampala au hata abroad (kama mtaji ukikua) kwa kweli biashara hii imewatoa vijana wengi sana! tena wengi wao walianza na mtaji mdogo tuu, ila inahitaji your full involvement, kujishusha na umakini wa hali ya juu
vile vile kuna uvuvi wa samaki ( sato & sangara) especial ukiwa na boti mbili tatu hivii, kwani kuna viwanda vinanunua kwa kilo (up to 2$ per Kg depend on fish qualities), biashara ya mifugo ( mbuzi, kondoo, ng'ombe etc), Asali, nta, etc
 
Wakuu tusisahau kwamba mtoa Mada ana 3M (Milioni Tatu Tu)..., tukitoa ushauri tuzingatie hilo.
 
Mama Derick; kuhusu incubator sifikiri kama kuna haja ya kuagia toka China, nenda SIDO watakuunganisha na watengenezaji wa incubator wa hapa nchini. Nimekuwa nikiziona katika maonyesho ya biashara (sabasaba) na hata kwenye nanenane. Nitajaribu kutafuta contact zao kwani nilichukua vipeperushi.

nashkuru sana mgombezi,bs naomba untumie contact zao kama ukipata ivo vipeperushi
 
Habari zenu wanajamvi!kabla ya yote napenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa manajamvi kwa michango ya mawazo mbalimbali ambayo inatusaidia wengi wetu.
wana jf wamekua sio wachoyo wa mawazo na ama kwa hakika wa tz wote tungekua tunapeana michango na mawazo kama ivi,tungefika mbali sana.
Mimi ni mfanyakazi serikalini,mshahara ninaopata si mkubwa sana,nilikua nafkiria kujishughulisha na mradi ambao utanisaidia kidogo kusogeza ili gurudumu la maisha.Swali langu ni kwamba,nina 3 mil naweza nkafanya biashara gani?
Naomba mnisaidie mawazo yenu wakuu!

Mama ushauri wangu bora uzingize kwenye kilimo huko iringa kuna mazingira mazuri ya kilimo hebu fanya utafiti wa kilimo kilimo kinatoa watu unaweza kulima vitungu vinasoko unaweza angalia mazao yoyte kulingana na Aridhi iliyopo sehem unayoishi
 
Mama ushauri wangu bora uzingize kwenye kilimo huko iringa kuna mazingira mazuri ya kilimo hebu fanya utafiti wa kilimo kilimo kinatoa watu unaweza kulima vitungu vinasoko unaweza angalia mazao yoyte kulingana na Aridhi iliyopo sehem unayoishi

nashkuru kwa mawazo yako mkuu
 
biashara ya pikipiki ina mambo mengi sana yanaweza kuku-discourage kuna mtu hapo juu ametoa mchanganuo wa kipato bila kupiga hesabu ya gharama za uendeshaji kama services, vifaa kuharibika n.k na pia pikipiki (za kichina) zina life span fupi sana kabla ya kuanza kusumbua. Naongea kwa uzoefu maana mke wangu ana hiyo biashara na ana pikipiki 4 na ile yenye kubeba mizigo moja ila hicho kizunguzungu cha uendeshaje wake ni balaa na pia unatakiwa kuiuza mara moja inapoleta matatizo na watu uwa wanalalia sana wakati wa kuzinunua zikiwa used. Unaweza kufanya hiyo biashara ila ni ngumu sana na unatakiwa kuwa una-save hela yote ili uendelee ila kama mapato yake ndio unayategemea kuendeshea maisha achana nayo kabisa

Pikipiki ikikaa miezi 6 inakuwa imechoka tayari kwa hiyo unaiangalia kama bado inaingiza kipato vizuri au inakugharimu zaidi ukiona gharama ni kubwa au faida ni kidogo uza nunua nyingine na mshauri alisema kuwa inaweza kaa mwaka 1 na nusu hiyo ni ngumu maana ikifika mwaka tu inakuwa imechoka sana

Sikushauri kununua pikipiki ni biashara ngumu sana na ushindani ni mkubwa saba pia ajali ni nyingi mno unaweza kukuta zimegongwa au kuanguka ikawa right off na huyo dereva akakugharimu kumtibu mie naijua hiyo biashara A to Z na mke wangu ameifanya zaidi ya miaka miwili sasa mwanzo zilikuwa zinalipa wakati ziko chache ila kwa sasa anataka kuacha maana imekuwa biashara kichaa

thanx funzadume kwa mfano wako hai.bora nimejua mapema..thanx
 
please ni PM with the details za hii machine,na inapatikana wapi in China
mama derick... je songea juices za concentrates kama zinazokua packed kwenye cups kama za METL zinapatikana.... kuna machine ndogo (semi automatic sealing machine) yaku seal juice kwenye cups kama hizo za METL ....zinapatikana china kwa bei ndogo sana...halafu utanunua juice concentrates with different flavour from anywhere pamoja na cups and seal film zitatoka china... ukapack na ku seal na kuuza katika mji mzima wa songea... ukaipa brand name ya derick juices.... budget yako ni nzuri kwa mradi huu... ni PM nikutumie more details pamoja na photos na machine particulars uamue kusuka au kunyoa bure kabisa


View attachment 21901


something like this
 
biashara ya boda boda,bima yenu inachukua muda gani kucompesate pikipiki iliyoibiwa?
Kama haupendi biashara ya mboga mboga na boda boda, basi nunua mshine ya juice pale university of Dar es salaam, inauzwa milioni moja na nusu. Nenda sido lipa laki mbili na nusu soma wiki 2 jinsi ya kutengeneza juice. Mashine inatengeneza lita mia moja kwa saa. Uwiano kama ukitengeneza maembe ya shilingi elfu mbili na mia tano, utauza na utapata shilingi elfu kumi na tano kwa kuuza kila glass au robo lita shs mia tano. Kama una mtoto wa kiume au wa kike ambaye si mlevi, mtume akanunue alizeti magunia mia moja. Kila gunia moja litakupatia faida ya shilingi elfu ishirini. 20,000 x 100 = 2,000,000/= Magunia mia utayapata kwa shilingi milioni mbili. Nimekwisha kufanyia hesabu nyingine kama vile usafiri, kukamua mafuta kwa mashine ya mtu. Kusafirisha mafuta sokoni na mwisho wa siku kwa siku 60 utakuwa na faida shilingi milioni 2, akiba yako ingelikuwa laki 4 na mtaji wako utakuwa umebaki pale pale milioni 3. Utakuwa umekwishajilipa mshahara pia hata kama umeajiriwa. Kwa mawazo zaidi, 0718 19 4606. Mwalimu wa ujasiriamali. Nitakuchaji shilingi elfu kumi ushauri kwani wewe ni mwana JF. Usisahau kukata bima kama utaamua kufanya biashara ya boda boda. Ukinitumia mimi nitakuuzia pikipiki na utakata bima shs 72,000 majambazi wakikunyanganya au ikipata ajali tunakupa pikipiki nyingine. Jamaa alioandika biashara ya mboga mboga na pikipiki nao pia ushauri ni mzuri sana. Uchukue wowote
 
Back
Top Bottom