Milio ya risasi Arusha

Milio ya risasi Arusha

Sodium 23

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2013
Posts
484
Reaction score
492
Habari wanajukwaa!

Hivi karibun kumekua na milio ya risasi jijini Arusha mida ya saa tatu usiku.
Hii ni takribani Mara ya tatu kwa milio hii ya silaha za kivita kusikika.

Kutokana na milio hiyo kuna kitu viwili aidha mazoezi ya wanajeshi vikosini hali inayopelekea sauti ya risasi kusikika town kwa kua hali ya anga usiku inakua imetulia.

Au kuna uwezekano yakawa in majibizano ya risasi kati ya vikosi vyetu na wahalifu.
Hadi sasa hakuna taarifa yoyote kuhusu milio hiyo ambayo inatufanya tulale tukiwa tumekumbatia rozari na Biblia.

Nadhan jeshi la polisi litatolea ufafanuzi jambo hilo ili kusije kutengenezwa taarifa za uongo zitakazohatarisha soko la utalii hapa town.

Mfano mzuri ni siku ya jana tarehe 7 novemba 2018 ambapo milio hiyo imechukua takribani masaa mawili.
Nawasilisha
 
Hivi ukikumbatia rozari na bibilia risasi haitakupata kumbe ? Mimi najua kuwa neno la Mungu linapaswa likae ndani yako kwa kusoma bibilia na kutenda kama mungu anyotutaka katika neno lake. Kukumbatia bibilia ni bure bila kusoma na kuelewa kilichoandikwa humo ndani
 
Habari wanajukwaa!
Hivi karibun kumekua na milio ya risasi jijini Arusha mida ya saa tatu usiku.
Hii ni takribani Mara ya tatu kwa milio hii ya silaha za kivita kusikika.
Kutokana na milio hiyo kuna kitu viwili aidha mazoezi ya wanajeshi vikosini hali inayopelekea sauti ya risasi kusikika town kwa kua hali ya anga usiku inakua imetulia.
Au kuna uwezekano yakawa in majibizano ya risasi kati ya vikosi vyetu na wahalifu.
Hadi sasa hakuna taarifa yoyote kuhusu milio hiyo ambayo inatufanya tulale tukiwa tumekumbatia rozari na Biblia.
Nadhan jeshi la polisi litatolea ufafanuzi jambo hilo ili kusije kutengenezwa taarifa za uongo zitakazohatarisha soko la utalii hapa town.
Mfano mzuri ni siku ya jana tarehe 7 novemba 2018 ambapo milio hiyo imechukua takribani masaa mawili.
Nawasilisha

FATAKI ZA WAHINDI HIZO, HII NDO SHIDA YA KUAMIA ARUSHA KUTOKA BIHARAMULO
 
FATAKI ZA WAHINDI HIZO, HII NDO SHIDA YA KUAMIA ARUSHA KUTOKA BIHARAMULO
I was born in Arusha bro, Sina undugu na wahindi...mambo ya biharamulo yanatoka wapi mkuu?
 
nyie si ndio mabilionea? wewe ukisikia hivyo zama uibuke na ya kwako kutoka uliko ificha kisha ikoki na uilelekeze mlamgoni au dirishani tayari kwa kufumua kiumbe chochote utakacho kitilia shaka. Achana na rozali
 
Hivi ukikumbatia rozari na bibilia risasi haitakupata kumbe ? Mimi najua kuwa neno la Mungu linapaswa likae ndani yako kwa kusoma bibilia na kutenda kama mungu anyotutaka katika neno lake. Kukumbatia bibilia ni bure bila kusoma na kuelewa kilichoandikwa humo ndani
Ulichosema ni sahihi sana lakini sometimes tunasahau kuwa Mungu anabaki kuwa Mungu. Unaweza kuwa na huo uelewa na bingwa wa kuomba na kukemea lakini janga likakupata vile vile na yule ambaye hana ufahamu wa kiwango hicho lakini kwa imani akabeba rozali na kukumbatia biblia Mungu akuvutwa na kiwango cha imani cha mtu huyo kwake na kumuokoa.

Yule aliyeponywa kuvuja damu miaka mingi aligusa tu upinde wa nguo ya Yesu, mwingine kwa ufupi wake akaamua apande juu ya dari ili amuone Yesu akabahatika kutembelewa kabisa nyumbani kwake ingawa walikuwepo waliofuatana na Yesu kila mahali na kuwa karibu nae zaidi.

Tukumbuke hata Yesu alipotoa mfano wa kupokea ufalme wa Mungu kama watoto wadogo unaweza kuelewa nini Mungu anataka kwetu. Mungu atabaki kuwa Mungu tusimuweke kwenye ukomo wa uelewa wetu.

Ni vyema kuwa na maarifa ya kutosha kama anavyosema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa lakini tusisahau kila mmoja ukomo wake wa maarifa unapokoma lakini anamtegemea Mungu wa kweli ndipo Mungu anapoanzia kusimama nae.
 
Back
Top Bottom