Mila za mababu zetu zinavyofanya kazi sometimes siyo vitu vya kupuuzwa hivi

Koffi Annan

JF-Expert Member
Dec 23, 2018
1,235
3,194
Kwenye jamii ya leo kumekua na mila mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanywa na wazee wetu ila ujio wa dini umefanya tuzisahau. Je, mambo kama haya yapo au umeshawahi kushuhudia?

Nitaweka hapa visa vichache ambavyo nimeshawahi kusimuliwa na kushuhudia jinsi mila zinavyofanya kazi hata sasa katika familia zetu.

Kisa cha kwanza kuna ndugu yangu yeye alioa mwanamke na yule mwanamke alikua kila akipata ujauzito unatoka au mtoto kufariki wakati wa kuzaliwa mimba tatu mfululizo, wazee wakasema kuwa huyo mwanaume ana kaka yake aliyefariki tokea akiwa mdogo hivyo anatakiwa amkabidhi huyo mke kwa kaka yake ndipo atapata mtoto, jamaa akaenda akafanya mila na kunena tu maneno kwamba fulani(akataja jina la huyo kaka yake aliyefariki) nimekukabidhi huyu mke ni wako. Tokea hapo akawa anapata uzazi kama kawaida.

Kisa cha pili ni kuhusu Bibi mmoja wa jirani na home, huyu bibi alikua anataka kumpa mtoto wake wa kike shamba ila mume wake akakataa, akawapa tu watoto wa kiume, yule mume wake alipofariki bibi alikua na shamba lilibaki hivyo akataka kumpa huyo mtoto wa kike napo watoto wa kiume wakakataa.

Yule bibi akaenda kulaani kwenye lile shamba akasema hamna mtu atavuna kitu hapa na atakayekula chochote hapa atakufa, kesho yake akaenda kukata ndizi kwenye lile shamba alilolaani akapika akala, asubuhi tu alivoamka akatoka kibarazani akaanguka akafa hapo hapo wazee wakasema ile laana yake ndo imemchukua maana alisema mtu akila kitu hapo shambani afe.

Kisa kingine kule Uchagani kuna utaratibu wa kufanya sherehe ya kumbukumbu ya marehemu baada ya muda fulani tokea kifo cha marehemu wenyewe wanaita matanga, basi unaambiwa baadhi ya marehemu wasipofanyiwa matanga huwatokea ndugu zao au wanaukoo, kuna huyo alikuwa anamtokea mdogo wake wa kiume usiku anamchapa fimbo mpaka siku alipofanyiwa matanga ndo hiyo kitu ikakoma.

Wazee wanakwambia kuna vitu unaweza kufanya usifanikiwe kumbe kuna roho zipo nyuma yako may be zinateseka hivyo ukifanya kitu fulani zile roho za wale watu zinapata amani na wewe utaishi kwa amani.
 
Juzi Njombe kuna Dada alikua amejifungua pale Zahanati ya Igagala, na mtoto hakua riziki! Basi tukaenda kumchukua, nikawa napewa story kuwa kila akibeba mimba akijifungua Mtoto anakufa.

Wenyeji wakaniambia hio inasababishwa na kwamba huyo Dada ni mke wa mtu spiritually, alishawahi kupendwa au kuwa kwenye mahusiano na hakuolewa na huyo mtu, kwahiyo inabidi wakafanye matambiko.
 
Juzi Njombe kuna Dada alikua amejifungua pale Zahanati ya Igagala, na mtoto hakua riziki! Basi tukaenda kumchukua, nikawa napewa story kuwa kila akibeba mimba akijifungua Mtoto anakufa...
Na hapo mpaka wakafanye tambiko unless otherwise ata mimba kumi wanakwambia siyo riziki.
 
Yani ukiwa muafrika tabu sana maana pamoja na maisha magumu tunayopitia huku duniani bado ukifa unatakiwa uwe mzimu utatue shida za ukoo..😂😂

Nipo hapa kusoma visa na Mikasa..😅
 
kuna stori mingi sana kuhusu hizi mambo lakini kiundani ukianza kuchambua kujua ukweli wake hakuna uthibitisho wowote kuonesha kweli kua nguvu ya supernatural iliyosababisha

kuna siku mtaani kulizuka habari kua marehemu amekataa kuzikwa eti walimlaza kitandani baada ya dakika kadhaa wakakuta mkushi amekaa

Unaambiwa limeletwa jeneza watu wako nje wanasubiri maiti ipakiwe kwenye jeneza wakazike kumbe huko ndani shughuli imeambatana na mvua wafiwa kwa wazee na baadhi ya watu wa dini wanakazi ya kumbembeleza marehemu azikwe afu naye marehemu nyodo zikamjaa eti hataki kuzikwa.

watu karibia wote waliokuwepo lile eneo walianza kuamini kuwa kweli marehemu kasusa kuzikwa mpaka ikafikia hatua ukimuambia mtu kuwa hiyo ni scripts imeundwa kwa kusudi maalumu anachukia.

Mwisho wa siku ikaja kutubu familia ya marehemu kuwa marehemu kabla hajafa alikua na ugomvi na jirani yake hivyo aliamini kuwa hata ugonjwa wake alioumwa alilogwa na huyo mhasimu wake.

Kwahiyo endapo atakufa alipendekeza huyo mhasimu wake asiuzulie akiamini kua kuudhuria kwake msibani kunaweza kusababisha matatizo kwa wana familia wake walio bakia.

kwahiyo wana ndugu walikua waoga nao waliamini kuwa mwenzao kalogwa na njia pekee ya wao kuepushwa na hiyo series ya kulogwa ni kutengeneza drama jamaa aondolewe pale msibani
 
kuna stori mingi sana kuhusu hizi mambo lakini kiundani ukianza kuchambua kujua ukweli wake hakuna uthibitisho wowote kuonesha kweli kua nguvu ya supernatural iliyosababisha

kuna siku mtaani kulizuka habari kua marehemu amekataa kuzikwa eti walimlaza kitandani baada ya dakika kadhaa wakakuta mkushi amekaa...
Sasa unasema hazina ukweli wakati umethibitisha mwenyewe kaka mkubwa
 
Safi kabisa.na mimi natoa kisa cha rafiki yangu wa karibu. alikua ana maisha magumu sana japo kuwa anaelimu nzuri ya kumfanya apate ajira,hata sisi rafiki zake tulianza kumuona mzigo na tukaanza kumkataa.

sasa wazazi wake kwa muda mrefu walimbembeleza arudi kwao kijijini wakamfanyie matambiko lkn jamaa hataki.

mjomba wake alimfata kwa nguvu akampeleka kwao na akafanyiwa matambiko,akaa huko kwa muda akarudi mjini.
kapata ajira aliyoitamani kwenye maisha yake na maisha yake yamefunguka kwa kasi ya Covid-19.
mimi binafsi naamini mizimu japokuwa sijapata muda hasa wa kuanza kudili nayo.
 
Safi kabisa.na mimi natoa kisa cha rafiki yangu wa karibu. alikua ana maisha magumu sana japo kuwa anaelimu nzuri ya kumfanya apate ajira,hata sisi rafiki zake tulianza kumuona mzigo na tukaanza kumkataa.
sasa wazazi wake kwa muda mrefu walimbembeleza arudi kwao kijijini wakamfanyie matambiko lkn jamaa hataki..
Unaona jamaa angeendelea kusota mjini bila mchongo wowote
 
Mila zipo ila kuna jinsi ambavyo zinafanyika zinafanyika katika mazingira yasiyo ya kisasa ndio maana watu wanazikataa,Kule Moshi kuna wazee wanausoma utumbo wa mbuzi na kujua jambo lolote zuri/ Baya linaloendelea katika Boma/ukoo fulani na ni kweli.
Wapo hawa ata ukitaka wakusomee wako wanakusomea vizuri tu
 
kuna stori mingi sana kuhusu hizi mambo lakini kiundani ukianza kuchambua kujua ukweli wake hakuna uthibitisho wowote kuonesha kweli kua nguvu ya supernatural iliyosababisha

kuna siku mtaani kulizuka habari kua marehemu amekataa kuzikwa eti walimlaza kitandani baada ya dakika kadhaa wakakuta mkushi amekaa...
Eti marehemu analeta nyodo duuuh
 
Back
Top Bottom