Mikosi na Laana kwenye fedha/mali za dili, wizi na dhuluma

Kinaeleweka

Senior Member
Nov 10, 2014
145
104
Habarini wapendwa,

Naomba niende moja kwa moja kwenye maada husika kwa kutumia uzoefu kutoka kwangu mwenyewe lakini na baadhi ya watu wa karibu wanaonizunguka.

Katika mihangaiko yetu ya kimaisha tunapitia mambo mengi tukiwa makazini katika biashara ,ujasiriamali na hustle nyingine.Kuna mengine yanatupelekea kuwa na ukwasi wa kutaka kujilimbikizia mali nyingi na hasa pasipo njia halali.Mie mwenyewe nimeshawahi kuajiliwa shirika fulani na nikajaribu kutengeneza myanya ya kupiga hela kama Tsh.35m.Hizo niliwekeza kwenye mashamba ya miti heka 30 huko Iringa na nyingne nikaanzisha kilimo cha vitunguu maji nikiamini vyote au kimojawapo kitanitoa.

Nilijitahdi sana kufuatilia kwa ukaribu hiyo miradi yote miwili,kwa maana ya kuhudumia miti kwa palizi na kuwekà mipaka ya kuzuia majanga ya moto lakini hasa kilimo cha vitunguu ambacho kilihtaji kuhudumiwa kwa karibu zaidi kwa maana ya umwagiliaji,palizi,madawa,mafuta ya diesel ya kuwashia pump ya kumwagilia na kadhalika na kilikuwa kinaendelea vizuri sana.

Kufupisha tu,miti ilipofika miaka 10 nikapata majanga ya moto ambao uliunguza karibu shamba lote.Moto unasemekana ulitokea shamba la jirani na kurukia shambani kwangu.Nilikatishwa sana tamaa na hasa nikizingatia gharama na muda niliopoteza katika kuwekeza hiyo miti.Pia shamba la vitunguu sikuwahi kupata faida licha ya kutumia gharama kubwa sana za uendeshaji.Mfano kuna kipindi nilitumia million 8 gharama zote nikaja kupata mil.1.5.Nikaja nikatumia mil.5 nikapata laki 6 nakuendelea.

Isitoshe,kuna mazingira mengine unapiga hela ya dili,lakini mikosi unayokutana nayo.Unakuta mara umepata ajari.Hiyo fedha unakuta inashia kwenye hiyo ajari.

Lakini kuna ushuhuda kwa watu wengine pia,jamaa mmoja alipiga deal hela ya maana akajenga apartments na kuweka wapangaji ila unakuta wapangaji hawalipi kodi,na akiwatimua na kuweka wengine unakuta hali inajirudia.Aliwekeza kwenye viwanja pia lakini kuna migogoro ilitokea ambayo ilimfanya apoteze hela nyingi mahakamani kwa kuweka mawakili.Lakini bado mgogoro haujaisha.

Hitimisho,nimekuja kugundua kuwa vitu visivyo halali havina baraka mbele ya mwenyezi Mungu.Utakosa amani binafsi lakini pia mradi hautakuletea faida utayotegemea baadae.Hapo nakumbuka mafundisho ya Yesu kwa mitume wake,kuwa tusisumbukie maisha ya kuwa tutakula nn au tutavaa nn,kwani Mwenyezi Mungu anajua shida zetu tayari.Tazama ndege wa angani hawalimi wala kuvuna lakini wanaishi vizuri.Je,sisi si zaidi ya hao ndege.

Baraka kamili za Mungu zinapatikana kwa kushika amri zake na hasa kupitia Malaki 3:8-10. Ahsante
 
Habarini wapendwa,

Naomba niende moja kwa moja kwenye maada husika kwa kutumia uzoefu kutoka kwangu mwenyewe lakini na baadhi ya watu wa karibu wanaonizunguka.

Katika mihangaiko yetu ya kimaisha tunapitia mambo mengi tukiwa makazini katika biashara ,ujasiriamali na hustle nyingine.Kuna mengine yanatupelekea kuwa na ukwasi wa kutaka kujilimbikizia mali nyingi na hasa pasipo njia halali.Mie mwenyewe nimeshawahi kuajiliwa shirika fulani na nikajaribu kutengeneza myanya ya kupiga hela kama Tsh.35m.Hizo niliwekeza kwenye mashamba ya miti heka 30 huko Iringa na nyingne nikaanzisha kilimo cha vitunguu maji nikiamini vyote au kimojawapo kitanitoa.

Nilijitahdi sana kufuatilia kwa ukaribu hiyo miradi yote miwili,kwa maana ya kuhudumia miti kwa palizi na kuwekà mipaka ya kuzuia majanga ya moto lakini hasa kilimo cha vitunguu ambacho kilihtaji kuhudumiwa kwa karibu zaidi kwa maana ya umwagiliaji,palizi,madawa,mafuta ya diesel ya kuwashia pump ya kumwagilia na kadhalika na kilikuwa kinaendelea vizuri sana.

Kufupisha tu,miti ilipofika miaka 10 nikapata majanga ya moto ambao uliunguza karibu shamba lote.Moto unasemekana ulitokea shamba la jirani na kurukia shambani kwangu.Nilikatishwa sana tamaa na hasa nikizingatia gharama na muda niliopoteza katika kuwekeza hiyo miti.Pia shamba la vitunguu sikuwahi kupata faida licha ya kutumia gharama kubwa sana za uendeshaji.Mfano kuna kipindi nilitumia million 8 gharama zote nikaja kupata mil.1.5.Nikaja nikatumia mil.5 nikapata laki 6 nakuendelea.

Isitoshe,kuna mazingira mengine unapiga hela ya dili,lakini mikosi unayokutana nayo.Unakuta mara umepata ajari.Hiyo fedha unakuta inashia kwenye hiyo ajari.

Lakini kuna ushuhuda kwa watu wengine pia,jamaa mmoja alipiga deal hela ya maana akajenga apartments na kuweka wapangaji ila unakuta wapangaji hawalipi kodi,na akiwatimua na kuweka wengine unakuta hali inajirudia.Aliwekeza kwenye viwanja pia lakini kuna migogoro ilitokea ambayo ilimfanya apoteze hela nyingi mahakamani kwa kuweka mawakili.Lakini bado mgogoro haujaisha.

Hitimisho,nimekuja kugundua kuwa vitu visivyo halali havina baraka mbele ya mwenyezi Mungu.Utakosa amani binafsi lakini pia mradi hautakuletea faida utayotegemea baadae.Hapo nakumbuka mafundisho ya Yesu kwa mitume wake,kuwa tusisumbukie maisha ya kuwa tutakula nn au tutavaa nn,kwani Mwenyezi Mungu anajua shida zetu tayari.Tazama ndege wa angani hawalimi wala kuvuna lakini wanaishi vizuri.Je,sisi si zaidi ya hao ndege.

Baraka kamili za Mungu zinapatikana kwa kushika amri zake na hasa kupitia Malaki 3:8-10. Ahsante
Hitimisho,nimekuja kugundua kuwa vitu visivyo halali havina baraka mbele ya mwenyezi Mungu.Utakosa amani binafsi lakini pia mradi hautakuletea faida utayotegemea baadae.Hapo nakumbuka mafundisho ya Yesu kwa mitume wake,kuwa tusisumbukie maisha ya kuwa tutakula nn au tutavaa nn,kwani Mwenyezi Mungu anajua shida zetu tayari.Tazama ndege wa angani hawalimi wala kuvuna lakini wanaishi vizuri.Je,sisi si zaidi ya hao ndege.
 
Hapo inawezekana kabisa wala sio sababu kwakuwa hii dunia pesa ya halali ni almost kama hakuna
Kama ni dili za kawaida mbona una survive fresh tuu ila ni LAZIMA uiwekee ulinzi kwa kutoa zaka na kusaidia wenye uhitaji mbalimbali.. Kumbuka ni kwa kutoa ndio tunapokea

Pesa yenye laana na mikosi ni hii hapa
Kama uliipata kwa kudhulumu uhai wa mtu
Kama kuipata kwake kulichangia wengine kufukuzwa kazi
Kama kuipata kwako kulichangia wenye mahitaji ya lazima kukosa huduma
Kama kuipata kwako kulichangia wengine kupata kesi na kufungwa
Kama kuipata kwako kulichangia madhila mengine yoyote kwa wengine nknk

Katika maisha cheza na vyote lakini sio ardhi na uhai! Maana hivi ni tunu ya Mwenyezi Mungu kwa uumbaji wake!

Sometimes tunapata pesa ama mali yoyote lakini haituletei baraka wala mafanikio yoyote basi tambua haikumaanishwa kuwa yetu ama kwa kupotea au kuharibika kwake tunakuea tumeepushiwa kitu kibaya mno, ambacho badala ya kukudhuru wewe kikaenda kupiga huko
Ndio maana tunaaswa kushukuru kwa kila jambo
 
IMG_5401.jpg

Yeremia 17:11
 
Kumbukumbu la Torati 24:14-15

[14]“Msiwadhulumu watumishi walioajiriwa walio maskini na maskini, iwe ni Waisraeli wenzetu au wageni wanaoishi katika mojawapo ya miji yako.

[15]Kila siku kabla ya jua kutua, wape malipo ya kazi ya siku hiyo; wanahitaji pesa na wamehesabu kuzipata. Usipowalipa, watamlilia BWANA juu yako, nawe utakuwa na hatia.
 
Pesa yoyote inayopatikana kwa nguvu zako au akili yako pasi na kumdhuru mtu kimwili, kiakili au kihisia hiyo ni pesa halal na ina baraka ndani yake, kinyume na hapo hata kama hujaua ila umetumia janja ambayo itawaaffect wengine hiyo pesa lazima ikutese au haitozalisha chochote cha maana na hautokuwa na furaha wala amani kamwe, japo wengi hawajui furaha na amani nini hiyo hujipumbaza na starehe na mali wakidhani ndio furaha lakini dakika chache kabla ya mwili kuacha roho ndo huwa wanajua kwa hawajui
 
Hakuna ridhki yenye nataka Kama ridhiki ya biashara halali.....lakini sijui dili ukiipata pesa haikai mpaka mshahara nao wa kupewa ima serikalini au kampuni nao haukai mi nasemaga Kama zinarudi kulekule mwezi ujao unalipwa ileile ndio maana wafanyakazi wengi wameamua kuwekeza katika miradi.
 
Kazi ya zaka ni kulinda mali zako zisipotee. Ila shetani kaingiza mawazo kwa watu wasitoe zaka na sadaka eti zinaenda kupigwa na wachungaji maana anajua nguvu ya zaka na sadaka. Lakini kwake watumishi wake ni lazima watoe zaka na sadaka tena kwa shetani unatoa 60% 40 ndio yako unatumia na wanatoa kwa uaminifu kabisa, lakini Mungu anataka 10 % tu zikalishe watumishi wa MUNGU. Mtumishi wa Mungu atakiwi kufanya Kazi ya kipato bali Kazi ya kuhudumia watu 24hrs kwa siku kama mwanadamu anayo mahitaji. Hivi mtumishi wa Mungu akapige vibarua ndio ale Saa ngapi atawachunga watu huko huko kwenye kutafuta kipato ni rahisi kupotelea huko akatekwa na dunia. Inatakiwa awaze Kazi moja tu ya kuhudumia watu kiroho. Toa zaka na sadaka mali zako zitalindwa.
 
Back
Top Bottom