Mikopo HESLB sio Siasa, Waliokopa walipe

Mikopo HESLB sio Siasa, Waliokopa walipe

Bibi Mikopo

Senior Member
Joined
May 15, 2015
Posts
180
Reaction score
35
Wadau,
Tangu HESLB watoe majina ya wadaiwa ambao walikopeshwa na hawajaanza kulipa kumekua na kelele nyingi -- nyingi kutoka wale waliokopa na hawajawahi kulipa hata senti moja. Hatuwezi kuendelea hivi. Kelele nyingine hazina hoja kabisa, kwa mfano:

1. Mbona hatujaambiwa tunadaiwa shilingi ngapi? Wametoa majina tu. -- Uliyekopa ni wewe, ulikua na wajibu wa kwanza wa kulipa. Umeutekeleza? Umewahi kuchukua jitihada zozote za kujua unadaiwa shilingi ngapi na kwa sababu gani?

2. Eti, ninalipa kodi kwa hiyo siwezi kulipa deni hilo. -- Huu nao ni uchovu wa zama zilizopita. Kukopa harusi, kulipa matanga. Sio zama hizi. Wajibu wea msingi wa mkopaji na kulipa -- popote duniani. HESLB wawape haya majina TRA, Uhamiaji, Mifuko ya Hifadhi za Jamii, Chama cha Waajiri, professional bodies n.k -- wakose pa kutokea. Tuachane na siasa, mikopo irejeshwe na wengine wanufaike.

3. Eti, niliuliza deni langu mwaka juzi nikaambiwa Shs 4milioni, mwaka huu naambiwa shs 5milioni. Siwezi kulipa. -- Ulivyoambiwa ni shs 4 milioni ulifanya nini? Kama hukuanza kurejesha imekula kwako. Kuna penalti na tozo nyingine -- na hizi sio mpya -- muhimu ni kuwa pata deni lako, anza kulipa na hakikisha unapata uthibitisho kuwa umemaliza kulipa kutoka HESLB.

4. Eti, salary slips zangu zinaonyesha nilimaliza kukatwa zamani -- sasa inakuwaje naambiwa mimi mdaiwa sugu? -- Hii nayo ni siasa. Mkopaji ni wewe. Unayekatwa ni wewe. Mwajiri ni 'agent' tu. Tunawajua waajiri wetu. Ni vema kujiridhisha kuwa makato yako yanafika HESLB, NSSF, PSPF, LAPF n.k Waulizeni UDASA au wahadhiri wa SAUTI Mtwara!

5. Mimi nilishamaliza zamani, inakuwaje wananidai tena! -- Ukimaliza kulipa, HESLB wanatoa Clearance Certificate -- wewe unayo? Wadai kwa nguvu!

Mwisho, ukweli ni kwamba wabongo tulizoea business as usual kwa miaka 10 iliyopita. Ngoja twende sawa.
 
Ongezea na hoja kwamba hakuajiriwa ndio maana ameshindwa kurejesha mkopo. Hii ni hoja ya Boniface Jacob, Meya wq Manispaa ya Ubungo. Kwani ukikopa si wajibu wako kurejesha? Na kama hoja ni kwamba hukuwahi kuajiriwa, ulichukua hatua gani kuihabarisha Bodi? By the way, fedha za kampeni ulipata wapi ukashindwa kupata fedha za kurejesha mkopo?
 
1. Mbona hatujaambiwa tunadaiwa shilingi ngapi? Wametoa majina tu. -- Uliyekopa ni wewe, ulikua na wajibu wa kwanza wa kulipa. Umeutekeleza? Umewahi kuchukua jitihada zozote za kujua unadaiwa shilingi ngapi na kwa sababu gani?
Ni nani kabla ya 2004 alikuwa anaingia chuoni huku akijua kwamba anakopeshwa? Kuanzia 2003 kurudi nyuma HAKUNA aliyekopeshwa isipokuwa baada ya kuwa wameshamaliza ndipo wakaambiwa ni mkopo kwa wale wote from 1991! Na kama ilikuwa ni mkopo, serikali itoe hadharani form za mikopo zilizosainiwa na beneficiaries kwa hicho kipindi!
 
Ishu ya mikopo imeshaisha utamu habari kubwa mda huu ni million tano za shisha.
 
Wadau,
Tangu HESLB watoe majina ya wadaiwa ambao walikopeshwa na hawajaanza kulipa kumekua na kelele nyingi -- nyingi kutoka wale waliokopa na hawajawahi kulipa hata senti moja. Hatuwezi kuendelea hivi. Kelele nyingine hazina hoja kabisa, kwa mfano:

1. Mbona hatujaambiwa tunadaiwa shilingi ngapi? Wametoa majina tu. -- Uliyekopa ni wewe, ulikua na wajibu wa kwanza wa kulipa. Umeutekeleza? Umewahi kuchukua jitihada zozote za kujua unadaiwa shilingi ngapi na kwa sababu gani?

2. Eti, ninalipa kodi kwa hiyo siwezi kulipa deni hilo. -- Huu nao ni uchovu wa zama zilizopita. Kukopa harusi, kulipa matanga. Sio zama hizi. Wajibu wea msingi wa mkopaji na kulipa -- popote duniani. HESLB wawape haya majina TRA, Uhamiaji, Mifuko ya Hifadhi za Jamii, Chama cha Waajiri, professional bodies n.k -- wakose pa kutokea. Tuachane na siasa, mikopo irejeshwe na wengine wanufaike.

3. Eti, niliuliza deni langu mwaka juzi nikaambiwa Shs 4milioni, mwaka huu naambiwa shs 5milioni. Siwezi kulipa. -- Ulivyoambiwa ni shs 4 milioni ulifanya nini? Kama hukuanza kurejesha imekula kwako. Kuna penalti na tozo nyingine -- na hizi sio mpya -- muhimu ni kuwa pata deni lako, anza kulipa na hakikisha unapata uthibitisho kuwa umemaliza kulipa kutoka HESLB.

4. Eti, salary slips zangu zinaonyesha nilimaliza kukatwa zamani -- sasa inakuwaje naambiwa mimi mdaiwa sugu? -- Hii nayo ni siasa. Mkopaji ni wewe. Unayekatwa ni wewe. Mwajiri ni 'agent' tu. Tunawajua waajiri wetu. Ni vema kujiridhisha kuwa makato yako yanafika HESLB, NSSF, PSPF, LAPF n.k Waulizeni UDASA au wahadhiri wa SAUTI Mtwara!

5. Mimi nilishamaliza zamani, inakuwaje wananidai tena! -- Ukimaliza kulipa, HESLB wanatoa Clearance Certificate -- wewe unayo? Wadai kwa nguvu!

Mwisho, ukweli ni kwamba wabongo tulizoea business as usual kwa miaka 10 iliyopita. Ngoja twende sawa.
una wivu kwa kuwa hukuwa na uwezo wa kufika elimu ya juu ndo maana unaharisha kama bata
 
Back
Top Bottom