Mijadala: Kama mtu hujui ni bora kukaa kimya

Mijadala: Kama mtu hujui ni bora kukaa kimya

JAMHURI

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
449
Reaction score
60
Wengi wenye busara wanashauri watanzania kama sio wapana juu ya mijadala mbalimbali inayohusu maslahi ya nchi ama maendeleo yoyote bora mtu akakaa kimya kusikiliza wenzake wana maoni gani, kufanya hiyo haina maana kuwa huna akili bali ni Busara.

Ushauri huu ni wa bure kabisha, kwani nimeshuhudia mtu anajaribu kupotosha mambo ya msingi kukosoa anachozungumza msomi wakati hana uwezo wa japo kuchangia kinachozungumzwa, na hapo utaona mtu anaishia kutukana au kuponda.

Sio vyema tukaendelea kuvumilia hali hiyo, tufuate ushauri huu.
 
Wasomi wa siku hz si wa kuamini sana mkuu, so unapoona msomi anapondwa usishangae ndo hali ilivyo kwa sasa..pia usimuamini sana msomi na kumbka kuchanganya na za kwako.
 
Wasomi wapi unawaongelea? hawa wa JAMHURI YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR? Hapana, japo niliishia la7 nina kila sababu ya kuwapinga.
 
Anafuata mku.... kama jina lake lilivyo.....
 
tatizo sasa hv kuna vyuo vingi ila ubora uko chini kila anayepata nafasi anajiona msomi ukichanganya na rushwa za ngono na pesa.msomi anajionyesha kwa matendo wala sio vyeti wasomi wengi wa sasa ni majanga
 
Wengi wenye busara wanashauri watanzania kama sio wapana juu ya mijadala mbalimbali inayohusu maslahi ya nchi ama maendeleo yoyote bora mtu akakaa kimya kusikiliza wenzake wana maoni gani, kufanya hiyo haina maana kuwa huna akili bali ni Busara.

Ushauri huu ni wa bure kabisha, kwani nimeshuhudia mtu anajaribu kupotosha mambo ya msingi kukosoa anachozungumza msomi wakati hana uwezo wa japo kuchangia kinachozungumzwa, na hapo utaona mtu anaishia kutukana au kuponda.

Sio vyema tukaendelea kuvumilia hali hiyo, tufuate ushauri huu.


bora ungekaa kimya!
 
Back
Top Bottom