Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,775
- 699,200
Kuzimu hakushibi wafu... Kila jambo lina nyakati na majira yake... Kuzimu nako kuna majira... Majira ya uhitaji wa wafu... Kwasababu ya mahitaji na matendo ya binadamu... Binadamu wanaoipa haki kisogo, utu wema, tafakuri na upendo.... Matendo yake ya ubinafsi huzaa chuki, udhalimu, kisasi, rohombaya na mauaji ya wasio hatia... Ni miito na mialiko ya kuzimu......
Majira yake ndio haya... Nyakati zake ndio hizi... Nyakati za harakati za kukutana ndugu jamaa na marafiki... Wavizia uhai, wapenda kafara na wale wa mazindiko... Mumiani wa damu za watu wanatega sasa.....! Makinika
Wanatega sasa... Wametega hata kitambo... Njia panda, barabara kuu, mtoni, kwenye kilima, mteremko na kilindoni... Hukuwa na safari ya kutoka, hukuwa na mpango wa kusafiri na wala hujisikii kufanya hivyo lakini ghafla unabadili mawazo... Nguvu kubwa isiyojulikana inakushawishi, inakuvuta inakutaka utoke... Uende! Mwishoni unakubaliana nayo unatoka, unaenda unasafiri... Kumbe wanakusubiri...
Nyakati za majira ya matukio makubwa, matukio ya mwaka, matukio ya kijamii na kifamilia, ya furaha na ya huzuni... Miito na mialiko ya kuzimu huwa si haba
Ni vipindi vya nyakati kama hizi roho yako inaposita kufanya jambo usilazimishe... Isikilize kwakuwa inaona zaidi ya kuona... Lakini pia kama wewe ni mtu wa ibada fanya ibada, fanya sala kabla hujatoa mguu wako nje, kabla hujadanda kipandwa...
Fanya dua, ombea safari.. Ombea kipandwa.. Ombea dereva... Ombea njia.. Ombea na wasafiri wote wasafirio angani nchi kavu na baharini... Kwa rehema za mwenyezi Mungu tuumalize mwaka kwa amani na furaha...
Aaamen... Kukichwa kutambazuka lakini kabla jua halijachomoza kiza huwa totoro... Barikiwa wewe utakayebahatika kusoma ujumbe huu... Nakuombea miito na mialiko ya kuzimu ikupitie mbali wewe na familia yako, jamaa zako marafiki na wote wenye mapenzi mema!
Imendikwa leo
Jumamosi asubuhi
Tarehe 15.12.2018
Saa 08: 45 asubuhi
Kilingeni Msata
Mkoa wa pwani
Jr
...!
Majira yake ndio haya... Nyakati zake ndio hizi... Nyakati za harakati za kukutana ndugu jamaa na marafiki... Wavizia uhai, wapenda kafara na wale wa mazindiko... Mumiani wa damu za watu wanatega sasa.....! Makinika
Wanatega sasa... Wametega hata kitambo... Njia panda, barabara kuu, mtoni, kwenye kilima, mteremko na kilindoni... Hukuwa na safari ya kutoka, hukuwa na mpango wa kusafiri na wala hujisikii kufanya hivyo lakini ghafla unabadili mawazo... Nguvu kubwa isiyojulikana inakushawishi, inakuvuta inakutaka utoke... Uende! Mwishoni unakubaliana nayo unatoka, unaenda unasafiri... Kumbe wanakusubiri...
Nyakati za majira ya matukio makubwa, matukio ya mwaka, matukio ya kijamii na kifamilia, ya furaha na ya huzuni... Miito na mialiko ya kuzimu huwa si haba
Ni vipindi vya nyakati kama hizi roho yako inaposita kufanya jambo usilazimishe... Isikilize kwakuwa inaona zaidi ya kuona... Lakini pia kama wewe ni mtu wa ibada fanya ibada, fanya sala kabla hujatoa mguu wako nje, kabla hujadanda kipandwa...
Fanya dua, ombea safari.. Ombea kipandwa.. Ombea dereva... Ombea njia.. Ombea na wasafiri wote wasafirio angani nchi kavu na baharini... Kwa rehema za mwenyezi Mungu tuumalize mwaka kwa amani na furaha...
Aaamen... Kukichwa kutambazuka lakini kabla jua halijachomoza kiza huwa totoro... Barikiwa wewe utakayebahatika kusoma ujumbe huu... Nakuombea miito na mialiko ya kuzimu ikupitie mbali wewe na familia yako, jamaa zako marafiki na wote wenye mapenzi mema!
Imendikwa leo
Jumamosi asubuhi
Tarehe 15.12.2018
Saa 08: 45 asubuhi
Kilingeni Msata
Mkoa wa pwani
Jr
![](http://emoji.tapatalk-cdn.com/emoji769.png)