chanaga
JF-Expert Member
- Jan 30, 2013
- 344
- 190
Leo nilikua naangalia ITV kumbukumbu ya vita vya Kagera,na wakati vita hivi vikipiganwa nilikua nimeshazaliwa ila maji nilikua naita mmaah wakati huo,nimekua nikiadithiwa kuwa wakati wa vita migambo walitangulizwa mbele kama chambo kwa jeshi la Idd Amin na wengi wao waliuliwa,wanaojua naomba mnieleweshe je wale migambo ambao walirudi salama baada ya vita walichukuliwa jeshini au walirudi vijijini kukumbiza wananchi wakisaka kodi ya kichwa?