Mifuko ya Kuhifadhia Mazao Pasipotumika Dawa/Sumu

Styvo254

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
246
226
Hamjambo WanaJamii
Kero kubwa kwa mkulima hasa pale anapokua akihesabu 'vifaranga', ni wadudu wanaokula mazao yanapohifadhiwa. Swala hili limekera tangu binadamu wa kwanza kugundua kuhifadhi chakula kwa matumizi ya baadae. Ni swala ambalo liko kati kwa kumfilisi au kumhujumu mkulima wa Afrika. Mbinu zinazotumika sasa kupambana na swala hili sana sana ni madawa au sumu za kuwaua wale viumbe. Dawa/Sumu hizi hutumika kwenye mazao na basi ni hatarishi kwa matumizi ya binadamu.
Sasa kuna mbinu mbadala isiyotumia sumu, endelevu na sio hatarishi kwa binadamu. Mbini hii inatumia mifuko aina mbili kwa kuhifadhia mazao. Kuna mifuko MIWILI ya polythene/nailoni ndani ya kiloba/gunia, huja pia na kamba mbili za kufungia ile mifuko ya ndani.
Matumizi sahihi ya mfumo huu ndio siri ya urembo. Unapokua ukiweka mazao, mifuko lazima iwe imesimama wima ili kupata ujazo wote wa mfumo kwa sababu muhimu na ya msingi katika matumizi haya; KUJAZA KABISA MAZAO ILI KUTOA HEWA YOTE MLE!! Hii ndio njia ya kuhakikisha wale wadudu, hapo wakiwa mayai, hawata komaa na kuanzia kula mazao. Kuhakikisha hakuna hewa yeyote itakayo weza kuingia mle, mfumo wa pili pia lazima ufungwe vizuri pale juu, kuufinikia wa kwanza ndani; mwisho kuishona ile gunia na kuhifadhi vizuri.
Njia hii upunguza uharibifu wa wanyama wengine kama panya wanaokua pia wanashambulia mazao. Vipi utauliza? Mnyama yule utegemea harufu au hutumia pua kutafuta chakula, kwa vile mazao haya yamewekwa ndani ya mifuko MIWILI ya nailoni/polythene, hakuna harufu inayotoka na kuwavutia wale wanyama. Ila hakukosi mmoja wawili mtundu anayeangukia, kwa hivyo basi ni muhimi kuwashughulikia wengine kama hawa kwa kuiweka ile mifuko sehemu iliandaliwa vizuri dhiidi yao.
Bila hewa, au mzunguko wake hakuna kiumbe hai chochote kinachoweza kuishi. Mimea pia ni viumbe hai na mazao, ambayo hua ni mbegu au sehemu zingine za mmea - hasaa za uzazi, hayawezi ota yakaendelea na Mzunguko wa Maisha kwa vile hakuna hewa au mvuke/maji mle ya kuotesha. Mazao yale hubaki vile vile kwa mda mrefu - kuna repoti ya kuufungua mfuko baada ya miezi saba na kuyapata mazao safi kabisa. Wale wadudu kwa kuna hata hawakupita ngazi(stage) ya mayai hawatakua issue tena.
Tulivyo ona hapo juu, ni muhimu sana ile mifuko ya polythene iwe MIWILI ili kuzuia kabisa upenyaji wa hewa. Kutotii kwa maagizo ya matumizi kama sala, pia hudhuru utendakazi wa mifuko.
Mifuko hii ilibuniwa na Purdue University ya America.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iko poa sana. Je nikaweka gunia zangu 100 halafu zikaharibika itakuwaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna hatua zake za kuweka mahindi, kama yameharibika basi mfuko umeufunga vibaya au mahindi uliyohifadhi hayaja kauka vizuri na kusababisha hewa kuingia, hiyo hewa inafanya wadudu kuendelea kuishi na kuzaliana.
 
Inapatikana Tshs 4000 mpaka 5000 kwa mfuko mmoja, kwenye duka lolote la pembejeo za kilimo. Inaitwa PICS
Mingi inayopatikana kwa bei hizi ni ya hali ya chini. Ujazo mdogo, mfuko mmoja tu wa nailoni na pia uzito wake (kiloba na nailoni) ni hafifu ukilinganisha na inayotoka nje ya nchi.
Kwa ufupi, iliyochakachuliwa ndio ya hiyo bei hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mingi inayopatikana kwa bei hizi ni ya hali ya chini. Ujazo mdogo, mfuko mmoja tu wa nailoni na pia uzito wake (kiloba na nailoni) ni hafifu ukilinganisha na inayotoka nje ya nchi.
Kwa ufupi, iliyochakachuliwa ndio ya hiyo being hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuna tasisi moja ya kimataifa inashughulika na mambo ya kilimo ndo niliudhulia mafunzo yao, wao wanasupply hiyo mifuko yenye layer 3 kati ya hizo 2 ni nylon
 
Kwa sisi wakulima hili liko Poa. Polepole kaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kulingana na uchunguzi uliofanywa hasa kwa wakulima wa kimo cha chini, gharama ya kuhifadhi mazao; hii ni kujumlisha gharama za dawa, mifuko ya kubadilishia, mda na -muhimu sana- upweke wa mkulima anapofikiria kuhusu adhari za wale wadudu na kwa hivyo kuuza mazao yale kwa bei ya chini ili kuepuka hasara; iko juu kuliko kuwekeza kwa hii mifuko ambayo ni suluhu endelevu na pia inaongeza dhamani ya mazao. Ndugu zetu huko ng'ambo wanuza mazao yasio na dawa -organic, kwa bei ya juu zaidi kuliko mazao yaliyowekwa madwa.
Kuna mengi ya kuchangia ni mda tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kuna tasisi moja ya kimataifa inashughulika na mambo ya kilimo ndo niliudhulia mafunzo yao, wao wanasupply hiyo mifuko yenye layer 3 kati ya hizo 2 ni nylon
Tunayo ya ubora wa juu - uzito wa ile nailoni(polythene) gm/in³ na pia ujazo mkubwa 105kg. Hapo labda ndipo bei zinatofautiana.
Thanks for clarification.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona siku hiI tu tunafanya maisha kuwa magumu..mababu walitengeneza vihenge na wakapaka mavi ya ng'ombe na mazao yakawa salama...kwanini wasomi hawafanya tafiti juu ya hili? Tunaazima technolojia kubwaa wakati tunayo ya kwetu tena ni rahisi
 
Vihenge vya mavi ya ng'ombe sio suluhu kwa wakati na mida tunayoishi. Jiulize wewe kama utatumia mazao hayo yanayohifadhiwa hivyo. Kwa mkulima wa mamia ya mahekta, ilo kweli ni suluhu?; si mavi ya ng'ombe yatakua ni madini flani - au dawa!
Bara la Afrika liko nyuma kwa kilimo kwa sababu moja ndogo lakini ya muhimu sana; HATUTUMII TEKNOLOJIA KWENYE KILIMO. Teknolojia sio mashine na viwanda tu, ila mifumo, njia na mipangilio. Kw. mfn.; mmea wa Mexican Merrigold ni tatizo shambani, lakini unaweza kutumika kuzuia na kudhibiti wadudu flani kutoharibu mimea! Mfumo wa zero-grazing umewezesha wengi kufanya mambo ya ajabu kwa eneo ndogo kama robo acre hivi; bio-gas > umeme, gesi jikoni, mbolea, n.k. Na bado hatuja hesabu mda walio okoa kwa kutoenda tafuta kuni, kasi ya mambo pale nyumbani na mengine mengi.
Engine ya diesel ya haice yaweza 'boreshwa' ikatumia ile gesi ya ng'ombe na hapo basi kuzalisha umeme pale nyumbani. Kenya kuna wakulima wanaotumia gesi hiyo kuendesha jenereta ndogo za nyumbani!
Tafakari hayo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom