Midahalo ya wagombea Urais :- CHADEMA ni wakati wenu kujenga ustaarabu mpya Nchini

Phillemon Mikael

Platinum Member
Nov 5, 2006
10,534
8,619
Kwenye nchi zenye demokrasia iliyostawi , harakati za kuomba kuteuliwa kuwa Rais huanzia ndani ya Chama , ambako wagombea wote wanaotaka kupeperusha bendera huwa na midahalo ya wazi juu ya masuala mbali mbali , na hurushwa LIVE , huu ni ustaarabu mzuri kwakua mgombea atakayepita anakua amepimwa na wanachi hasa wanachama wa chama husika. Midahalo huwa zaidi ya mmoja na inaweza kufanyika kwenye kanda mbali mbali mfano Pwani,Kati,Nyanda za juu etc

Katika ushindani hufikia mahali baadhi ya wagombea wakajitoa na kuamua kumuunga mkono mgombea mmoja , na kufikia mkutano mkuu wa chama husika kila mmoja anakuwa anajua kwa hakika nani atakua mgombe .

Pakiwa na uwazi wa namna hiyo ndani ya chama husika ni rahisi sana na vyama vingine kuiga ustaarbu wa namna hiyo ....pia itapelekea kuwa na mdahalo wa wagombea urais uchaguzi mkuu, Mdahalo ni jambo jema kwani mwaka 1995 Mkapa amekiri hadharani kuwa ule mdahalo ndio uliomsaidia sana kuweza kushinda kwani kabla ya mdahalo akakiri uugwaji wake mkono ulikuwa mdogo hasa dhidi ya Mrema., alijieleza vizuri watu wakamkubali ...huku Mrema aliyekua tishio akishindwa kabisa kuelezea sera zake

Pascal Mayalla kaka yetu anakumbuka sana mambo ya midahalo na kipindi chake cha KITIMOTO pale bilcanas chini ya MASAI STUDIOS

Kwakua tayari Chadema wameonyesha uwazi kwenye utamaduni mzuri wa kutangaza nia tunaomba waende mbele zaidi wafanye midahalo ....na iwe LIVE .

Tunawatakia wagombea wa vyama vyote heri na fanaka kwenye harakati za 2020
 
Ni wazo zuri kama wafanyavyo wana REPUBLICAN au DEMOCRATIC kule Marekani. Kwa hapa kwetu bado mikusanyiko ya KISIASA si iko LOCKED DOWN? Wagombea wote wangeweza kuzungukia kanda zote kuelezea sera zao kwa wanachama wao lakini hiyo ruhusa haipo na wale kwenye taratibu za ndani ya chama (vyama) haupo
 
Ni wazo zuri kama wafanyavyo wana REPUBLICAN au DEMOCRATIC kule Marekani. Kwa hapa kwetu bado mikusanyiko ya KISIASA si iko LOCKED DOWN? Wagombea wote wangeweza kuzungukia kanda zote kuelezea sera zao kwa wanachama wao lakini hiyo ruhusa haipo na wale kwenye taratibu za ndani ya chama (vyama) haupo

Nadhani Technology zinahusika ....wanaweza kuwa Live kwenye Tv Na wakapokea maswali kwa njia za skype ,twitter au simu.
 
Kwenye nchi zenye demokrasia iliyostawi , harakati za kuomba kuteuliwa kuwa Rais huanzia ndani ya Chama , ambako wagombea wote wanaotaka kupeperusha bendera huwa na midahalo ya wazi juu ya masuala mbali mbali , na hurushwa LIVE , huu ni ustaarabu mzuri kwakua mgombea atakayepita anakua amepimwa na wanachi hasa wanachama wa chama husika. Midahalo huwa zaidi ya mmoja na inaweza kufanyika kwenye kanda mbali mbali mfano Pwani,Kati,Nyanda za juu etc

Katika ushindani hufikia mahali baadhi ya wagombea wakajitoa na kuamua kumuunga mkono mgombea mmoja , na kufikia mkutano mkuu wa chama husika kila mmoja anakuwa anajua kwa hakika nani atakua mgombe .

Pakiwa na uwazi wa namna hiyo ndani ya chama husika ni rahisi sana na vyama vingine kuiga ustaarbu wa namna hiyo ....pia itapelekea kuwa na mdahalo wa wagombea urais uchaguzi mkuu, Mdahalo ni jambo jema kwani mwaka 1995 Mkapa amekiri hadharani kuwa ule mdahalo ndio uliomsaidia sana kuweza kushinda kwani kabla ya mdahalo akakiri uugwaji wake mkono ulikuwa mdogo hasa dhidi ya Mrema., alijieleza vizuri watu wakamkubali ...huku Mrema aliyekua tishio akishindwa kabisa kuelezea sera zake

Pascal Mayalla kaka yetu anakumbuka sana mambo ya midahalo na kipindi chake cha KITIMOTO pale bilcanas chini ya MASAI STUDIOS

Kwakua tayari Chadema wameonyesha uwazi kwenye utamaduni mzuri wa kutangaza nia tunaomba waende mbele zaidi wafanye midahalo ....na iwe LIVE .

Tunawatakia wagombea wa vyama vyote heri na fanaka kwenye harakati za 2020
Naunga mkono hoja
P
 
Hili la mdahalo naona limepata baraka zote za wanacdm, na wananchi wengi kwa ujumla. Hili la midahalo litasababisha watu wenye uwezo wa mashaka, na makandokando mengine kukaa mbali.
 
Yes, hii mara zote hufanyika baada ya mchujo ndani ya chama kufanyika na kubaki na "the top best 2 or 3"....

Kisha hawa wa3 ama wa2 ndiyo wanafanya debate mbili ama tatu kabla kumteua mmoja kusimama kwa ajili ya chama.....

Hili ni jema sana na litasaidia watu kuwajua wagombea hawa uwezo wa ufahamu wao ktk nyanja zote za kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia na kijamii kwa ujumla wake....

Si hivyo tu bali pia wananchi tutapata nafasi kuwaelewa namna wanavyo challenge udhaifu wa KIUTENDAJI na KISERA za Rais aliyepo madarakani na namna ambavyo kila mmoja was hawa wagombea wapya watafanya tofauti kwa manufaa ya nchi na wananchi....

Hii ni njema sana. Lakini muda siyo rafiki ni mfupi, hautoshi. Tunashauri utaratibu ufanyike haraka kuwezesha hili kutendeka. Na lazima liwe live kwenye digital platforms zote i.e TV, FB, Twitter, YouTube, radios nk

Hii ikifanyika, nawahakikishia itawaweka CCM na mgombea wao pabaya sana. Maana hii ndiyo hofu yao kuu. Rais wao kutopenda SERA na UTENDAJI wake kukosolewa au mapungufu yake kuanikwa hadharani....

Kwa hiyo, kama mpango huu ukaiva na ukafanyika tusishangae ukakutana na vikwazo mbalimbali toka Tume ya Uchaguzi (NEC) ama Msajili wa Vyama vya siasa kwa kisingizio cha kwamba, ".....pazia la kampeni halijafunguliwa....!!"
 
Hio midahalo yote ni mbwembwe tu tutapoteza bando zeti za kuunga na hata midahalo ifanyike 24/7 bado ni upuuzi tu.

Wote mnajua tatizo liko sehemu moja tu NEC lkn wote tunazunguka mbuyu na kutafuta simple solution/Soft Spot/kujilisha upepo/mind musterbation.
 
Kwenye nchi zenye demokrasia iliyostawi , harakati za kuomba kuteuliwa kuwa Rais huanzia ndani ya Chama , ambako wagombea wote wanaotaka kupeperusha bendera huwa na midahalo ya wazi juu ya masuala mbali mbali , na hurushwa LIVE , huu ni ustaarabu mzuri kwakua mgombea atakayepita anakua amepimwa na wanachi hasa wanachama wa chama husika. Midahalo huwa zaidi ya mmoja na inaweza kufanyika kwenye kanda mbali mbali mfano Pwani,Kati,Nyanda za juu etc

Katika ushindani hufikia mahali baadhi ya wagombea wakajitoa na kuamua kumuunga mkono mgombea mmoja , na kufikia mkutano mkuu wa chama husika kila mmoja anakuwa anajua kwa hakika nani atakua mgombe .

Pakiwa na uwazi wa namna hiyo ndani ya chama husika ni rahisi sana na vyama vingine kuiga ustaarbu wa namna hiyo ....pia itapelekea kuwa na mdahalo wa wagombea urais uchaguzi mkuu, Mdahalo ni jambo jema kwani mwaka 1995 Mkapa amekiri hadharani kuwa ule mdahalo ndio uliomsaidia sana kuweza kushinda kwani kabla ya mdahalo akakiri uugwaji wake mkono ulikuwa mdogo hasa dhidi ya Mrema., alijieleza vizuri watu wakamkubali ...huku Mrema aliyekua tishio akishindwa kabisa kuelezea sera zake

Pascal Mayalla kaka yetu anakumbuka sana mambo ya midahalo na kipindi chake cha KITIMOTO pale bilcanas chini ya MASAI STUDIOS

Kwakua tayari Chadema wameonyesha uwazi kwenye utamaduni mzuri wa kutangaza nia tunaomba waende mbele zaidi wafanye midahalo ....na iwe LIVE .

Tunawatakia wagombea wa vyama vyote heri na fanaka kwenye harakati za 2020
CHADEMA Akili kubwa siku zote, utaona na yale mataahira yatafuata!
 
Naunga mkono mdahalo ndani ya CDM, njua of-course jiwe hawezi kamwe kukubali kuaibika katika mjadala kati yake na Lissu au Nyalandu.
 
Back
Top Bottom