Jamaa_Mbishi
JF-Expert Member
- Jun 15, 2013
- 10,185
- 7,377
natazama sherehe za ufunguzi wa michezo ya jumuiya ya madola, ninashuhudia kila taifa limekua likijitambulisha kwa mavazi pamoja na miondoko yao ya kiasili, ila aibu ilitokea lilipotajwa jina la tanzana, wakaingia watu wamevaa masuti na manguo yasio kua hata na rangi za kuutambulisha utaifa wetu, tunatia aibu yaani tumeshindwa hata kutambulisha vazio lolote ambalo ni common kama vile kanga na kanzu, kweli nchi yetu haina utamaduni wa kujitambulisha nje?aibu ilioje eti kuna wizara ya utamaduni, usanii mtupu.
We mpuuzi kweli. Nani kakuambia kanzu ni vazi la taifa la Tanzania au Khanga? Wewe unaweza kwenda kwenye interview ya kazi umevaa khanga au kanzu? Khanga ni vazi japo linavaliwa na kila mwanamke (karibia kila mwanamke) ila si vazi la kuitambulisha nchi yetu. Huku kwenye kanzu bora nisije kabisa maana nitasomewa albadiri bure,maana najiuliza nikisema kanzu ni asili yetu sijuwi waarab nao kule Uarabuni wanatesemaje kuhusu hili.