Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,502
- 911,254
- Thread starter
- #16,581
Mashindano ya Judo yaota mbawa Send to a friend Sunday, 17 April 2011 20:49
Imani Makongoro
MASHINDANO ya Taifa ya Judo yaliyopangwa kufanyika jana kwenye Uwanja wa ndani wa taifa jijini Dar es Salaam, yameota mbawa kufuatia Chama cha mchezo huo hapa nchini (Jata) kukabiliwa na ukata.
Mashindano hayo yaliyokuwa na lengo la kupata wachezaji wa timu ya taifa ya mchezo huo kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Kanda ya Tano Afrika Mashariki yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam mapema mwezi ujao na yale ya Afrika yatakayofanyika mapema Septemba nchini Msumbiji.
Katibu Mkuu wa Jata, Kashinde Shaban, aliiambia Mwananchi kuwa kutokana na mipangilio ya pesa mashindano hayo yamesogezwa mbele hadi mwishoni mwa mwezi Mei.
"Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika jijini Dar es Salaam na kushirikisha timu za Bara na Visiwani ili kupata timu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya mashindano ya kimataifa.
"Aprili 14 wenzetu wa Zanzibar walitutumia barua ya kuomba mashindano yafanyike visiwani siku ya Aprili 16, tulishindwa kutokana na mipangilio ya kifedha ingawa timu ya bara ilikuwa tayari na hadi leo hii inaendelea na mazoezi.
"Tuliamua wao wafanye mashindano ya kwao huko ambayo yamefanyika jana kwa ajili ya kupata wachezaji wazuri ambao watachuana na hawa wa Bara mwezi Mei kwa ajili ya kupata timu ya taifa ya Judo," alisema Shaban.
Imani Makongoro
MASHINDANO ya Taifa ya Judo yaliyopangwa kufanyika jana kwenye Uwanja wa ndani wa taifa jijini Dar es Salaam, yameota mbawa kufuatia Chama cha mchezo huo hapa nchini (Jata) kukabiliwa na ukata.
Mashindano hayo yaliyokuwa na lengo la kupata wachezaji wa timu ya taifa ya mchezo huo kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Kanda ya Tano Afrika Mashariki yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam mapema mwezi ujao na yale ya Afrika yatakayofanyika mapema Septemba nchini Msumbiji.
Katibu Mkuu wa Jata, Kashinde Shaban, aliiambia Mwananchi kuwa kutokana na mipangilio ya pesa mashindano hayo yamesogezwa mbele hadi mwishoni mwa mwezi Mei.
"Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika jijini Dar es Salaam na kushirikisha timu za Bara na Visiwani ili kupata timu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya mashindano ya kimataifa.
"Aprili 14 wenzetu wa Zanzibar walitutumia barua ya kuomba mashindano yafanyike visiwani siku ya Aprili 16, tulishindwa kutokana na mipangilio ya kifedha ingawa timu ya bara ilikuwa tayari na hadi leo hii inaendelea na mazoezi.
"Tuliamua wao wafanye mashindano ya kwao huko ambayo yamefanyika jana kwa ajili ya kupata wachezaji wazuri ambao watachuana na hawa wa Bara mwezi Mei kwa ajili ya kupata timu ya taifa ya Judo," alisema Shaban.