Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Ruud van Nistelrooy out for season after muscle tear in Hamburg draw

• Ruud van Nistelrooy injured in home draw with Hannover
• Dutch striker out of contract at end of the current campaign




  • Associated Press
  • guardian.co.uk, Sunday 17 April 2011 15.06 BST <li class="history">Article history
    Ruud-van-Nistelrooy-007.jpg
    Hamburg's Ruud van Nistelrooy admitted he was 'sure to be out some time' after injuring a calf muscle. Photograph: Fabian Bimmer/AFP/Getty Images

    Hamburg have said their striker Ruud van Nistelrooy has been ruled out for the rest of the season.
    The Dutch forward tore a muscle in his left calf during Saturday's 0-0 draw at home to Hannover in the Bundesliga.
    Van Nistelrooy told Hamburg's website on Sunday that "it happened toward the end. The pain got worse after the game". He added: "I'm sure to be out for some time."
    The former Manchester United and Real Madrid striker's contract with the club runs out at the end of the season.

 
Mazembe yazidi kuibomoa Simba Send to a friend Sunday, 17 April 2011 20:58

samathasimba.jpg
Mbwana Samatha

Clara Alphonce
MABINGWA wa Afrika, TP Mazembe wameendelea kuisambaratisha Simba baada ya kumnasa Mbwana Samata kwa Shs 150m, sasa wamemgeukia kiungo wa klabu hiyo Patrick Ochan anayetarajia kuondoka wiki ijayo kwenda DR Congo kwa majaribio.

Hata hivyo habari zilizopatika jana kutoka Lumbushashi zimeeleza kuwa kiungo huyo wa kimataifa wa Uganda tayari ameshaanza majaribio na Mazembe.

Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyanga 'Kaburu' alisema baada ya tajili wa TP Mazembe, Moize Katumbi kumsajili, Samatta sasa wanamtaka Ochan wiki ijayo atakuwa kwenye majaribio huko.

Alisema wao kama Simba hawana tatizo kama Ochan akifaulu majaribio yake watakaa kwenye meza na Mazembe kujadiliana kuhusu bei ya mchezaji huyo.

''Kweli tumepata taarifa kutoka kwa Mazembe na mchezaji mwenyewe kuwa anatakiwa kwenda kwenye majaribio hivyo kwa kuwa mchezaji huyo yupo likizo tunafanya utaratibu iliaweze kwenda huko kwani sisi kama viongozi hatuna pingamizi lolote'' alisema Kaburu.

Alisema kwa upande wao bado wanazidi kuwa karibisha watu wanaowataka wachezaji wao kwani wanajua wachezaji hao mpira ndio maisha yaona kama wanapata sehemu nzuri zaidi ya Simba awana budi kuwaruhusu kwenda kutafuta maisha.

Alisema kuhusu suala la usajili katika timu yao mpya ya msimu ujao bado wanaendelea nayo japo kamati inatakiwa ipewe muda wa kutosha kuakikisha wanatafuta wachezaji wazuri na wenye kushindana.

"Suala la Samata kwao limemalizika hivyo mchezaji huyo sasa anatakiwa wiki ijayo kwenda TP Mazembe na kusaini mkataba wake na kuangalia ni suala lake la mshahara.

Simba tayari imeshawauza nyota wake kadhaa sehemu mbalimbali duniani kama kiungo Henry Joseph (Kongsvinger, Norway), Danny Mrwanda (DT Long An, Vietnam) na Haruna Moshi (Gefle IF, Sweden).
 
Kickboxing yamponza Kaseba Send to a friend Sunday, 17 April 2011 20:52

Clara Alphonce
BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini Japhet Kaseba jana alitangaza rasmi kustaafu kucheza mgumi na kickboxing baada ya kupokea kipigo kutoka kwa Mada Maugo hadi kuokolewa na mwamuzi wa pambano hilo Bakari Champion katika raundi ya saba.

Mwamuzi huyo alivunja pambano hilo raundi ya saba ya mchezo baada ya Kaseba kumkata mtama Maugo na kudondoka chini na mashabiki wa Kaseba kupanda jukwaani na kuanzisha fujo.

Tukio hilo lililofanywa na mashabiki hao lilisababisha fujo kubwa ndani ya jukwaa ndipo polisi walipoingilia kati na kutuliza fujo hilo ambazo zilichukua kama dakika 15.

Baada ya fujo kutulia kutulia Kaseba alikataa kuendelea na pambano hilo na kuvua grovus zake mikono kuashiria kuwa hachezi tena pambano hilo ndio muamuzi wa pambano hilo alipomtangaza Mada Maugo kuwa mshindi.

''Kwa mujibu wa sheria za ngumi dunia mcheza wa ngumu kama atavua grovus wakati pambano halijaisha ina maana amejitoa katika pambano hivyo na mtangaza Maugo kuwa ndio mshindi katika pambano hilo,'' alisema Champion.

Kwa upande wake Kaseba alisema kuwa ameamua kutangaza kuacha ngumi rasmi ilikutimiza azma yake kwani alishatangaza kuacha ngumi baada ya pambano hilo.

Alisema wakati ametoka kwenye kickboxing kuja kwenye ngumi za kawaida alitaka kuja kuinua ngumi na kutoa hamasa kwa watu wazidi kuisaidia mchezo huo, lakini matokeo yake amekuta vitu vingine.

Alisema kuwa mchezaji wa pambano la juzi alikuwa anataka Maugo ashinde kwani yeye alimdodosha mpinzani wake mara tatu, lakini mwamuzi hakutoa maamuzi yoyote hivyo ameona ni bora hajitoe ili watu wasimjaji tofauti kuwa ameenda kuaribu ngumi tofauti na alivyokuwa akitaka yeye.
 
Zanzibar Heroes yakabiziwa Shs16m Send to a friend Sunday, 17 April 2011 20:50

Zabron Joseph
SHIRIKA la Bandari Zanzibar (ZPC) imetimiza ahadi yake iliyoitoa wakati wa hafla ya kuichangia timu ya soka ya Zanzibar ëZanzibar Heroesí kwa kutoa hundi ya Shs 16milioni katika hafla iliyofanyika mjini Zanzibar mwishoni mwa wiki.

Akikabidhi hundi hiyo ya shs milioni 16 kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Future Century, Hellene Masanja waratibu wa kampuni hiyo ya kuisaidia Heroes, Mkurugenzi Mtendaji wa ZPC Mustafa Jumbe, alisema wana furaha kubwa kutimiza ahadi hiyo.

ìSisi kama Shirika la Bandari Zanzibar tunafuraha kwa kutimiza ahadi yetu kwani bila shaka kitendo hiki pia kitasaidia kuharakisha maendeleo ya timu yetu na soka la Zanzibar kwa ujumla.î

Alisema wametiwa moyo sana na kampuni ya Future Century kwa juhudi zake zinazostahili kupongezwa za kujitutumua kwa ajili ya maendeleo ya mchezo wa soka visiwani humo.

Sisi kama bandari tunawapongeza Century na tunatoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kuungana mkono na wadhamini waliojitokeza ili kwa pamoja tuweze kuipaisha Zanzibar katika medani ya sokaî, alisema.

Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Helene Masanja mbali ya kuishukuru TPC kwa kutimiza ahadi yake akatoa wito kwa wadhamibni wengine, wakiwemo watu binafsi, mashirika, makampuni na wadau wa soka la Zanzibar kwa ujumla kuiga mfano wa Shirika la Bandari Zanzibar ili kuiinua timu hiyo na soka la visiwa hivyo kwa ujumla.

ìKutoa ahadi ni kitu kimoja na kutimiza ahadi ni kitu kingine hivyo kitendo cha TPC ni cha kuigwa na wadau wengine kitakachasaidia kuharakisha maendeleo ya Herous.î

Hafla ya kuichangia Zanzibar Heroes iliyofanyika mjini Zanzibar, Machi 26 mgeni rasmini alikuwa Rais Dk Ali Mohamed Shein kulisanya jumla ya zaidi ya shs 86m ikiwa ni ahadi na fedha taslimu.
 
TP Mazembe yazidi kuvuna Simba


*Ochan naye atua Lubumbashi

Na Zahoro Mlanzi

KIUNGO wa timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes' na Simba, Parick Ochan amemfuata mchezaji mwenzake, Mbwana Samatta kwa mabingwa wa Afrika, TP Mazembe
kwa mkataba wa miaka mitano.

Ochan atakuwa mchezaji wa pili kunyakuliwa na mabingwa hao wa Afrika baada ya Samatta, wiki iliyopita kusajiliwa na klabu hiyo kwa ada ya uhamisho wa sh. milioni 100.

Kwa mujibu wa taarifa ya Klabu ya TP Mazembe, ilieleza kwamba wachezaji hao wote kwa pamoja walisainiwa tangu Alhamisi iliyopita katika hoteli ya Movenpick Royal Palm jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo ilieleza kwamba TP Mazembe walikuja Dar es Salaam zaidi ya mara mbili kuzungumza na viongozi wa Simba, huku wakiongozwa na Rais wa timu hiyo, Moses Katumbi na Meneja Frederick Kitenge Kinkumba, ambapo baada ya kukamilisha suala hilo walifungua mvinyo na kusherehekea.

"Chaguo la kwanza lilikuwa ni kwa Mganda Patrick Ochan, ambaye walipoumana na timu hiyo ya Simba alipokuwa amevaa jezi namba 10 waliridhishwa na kiwango chake ndipo walipotuma wakala wao aanze kumfuatilia," ilieleza sehemu ya taarifa ya klabu hiyo.

Taarifa hiyo ilieleza zaidi kwamba, Ochan tayari alishakwenda Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), na alikaa kwa siku nne ambapo alionana na Kocha Mkuu wa timu hiyo, Lamine N'Diaye.

Chaguo la pili lilikuwa kwa mshambuliaji Samatta ambaye wakati wa kusaini mkataba Movenpick, alikuwepo na kaka yake, Ali Samatta na baba yake Mzee Samatta wakisherehekea kusaini mkataba huo.

Samatta na familia yake wanatarajiwa kutua Lubumbashi keshokutwa, akiambatana na Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' kwa kukamilisha makubaliano ya mwisho.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi, licha ya wachezaji hao kusaini mkataba wa miaka mitano, lakini ada ya uhamisho bado haijawekwa wazi mpaka sasa na itawekwa wazi baada ya kukamilisha kila kitu keshokutwa.

Alipotafutwa Kaburu kuzungumzia suala hilo, alikiri kweli Ochan kutakiwa na TP Mazembe na kwamba wiki ijayo atakwenda nchini humo kufanya majaribio.
 
Kaseba atangaza kuacha ngumi


Na Amina Athumani

BINGWA wa Dunia wa kickboxing, Japhet Kaseba ametangaza kuachana na mchezo wa ngumi na kujikita zaidi katika kuendeleza vipaji vya kickboxing kwa vijana.Kaseba
amefikia hatua hiyo baada ya kubondwa na Mada Maugo katika pambano lililofanyika juzi katika Ukumbi wa PTA, Dar es Salaam.

Maugo alishinda pambano hilo la uzito wa kg. 72 mara baada ya Kaseba kuingia ulingoni akiwa amevua glovs katika raundi ya saba ya pambano hilo, ikiwa imepaki raundi moja mchezo kumalizika ambapo mwamuzi John Chagu akamtangaza Maugo kuwa mshindi wa pambano hilo.

Akizungumza na mwandishi wetu Dar es Salaam jana, Kaseba alisema endapo ataendelea kucheza mchezo huo lawama zitakuwa haziishi na kwamba ni bora awe nje ya ulingo, ili aweze kuendeleza vipaji vya vijana zaidi.

"Mchezo ulikuwa mzuri, ila tatizo ni kwamba viongozi wa ngumi hapa nchini si mzuri wamekaa zaidi kichuki na kickboxing na ndiyo maana wamekuwa wakiweka jitihada za kuhakikisha ushindi unakwenda kwenye ngumi.

"Nilipokuwa nikimwangusha Maugo, nilikuwa sihesabiwi pointi lakini mimi nilipocheza faulo moja 'kumkata mtama' badala ya kunionya wananipa adhabu hii ni hatari na kamwe hatutafika kama itaendelea kuwa hivi," alisema Kaseba.

Katika pambano hilo ambalo pia kulikuwepo na mapambano mengine ya utangulizi, ikiwa ni pamoja na kumtafuta bingwa wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania(TPBO) ambapo, Yohana Robart alitangazwa bingwa wa mkanda huo baada ya kumtwanga Saidi Zungu kwa KO raundi ya nne.
 
Kihwelo alia na waamuzi Uganda

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 18th April 2011 @ 08:15 Imesomwa na watu: 467; Jumla ya maoni: 0


04_11_0bj919.jpg

Kikosi cha Vijana Stars





KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 23 &#8216;Vijana Stars', Jamhuri Kihwelo &#8216;Julio' amelalamikia waamuzi wa mchezo wao na Uganda akisema hawakuwa wakiitendea haki timu yake.

Akizungumza na kituo kimoja cha redio kutoka Kampala, Uganda, Julio alisema waamuzi walikuwa wakiwabeba wenyeji na walichangia kwa kiasi kikubwa kipigo hicho.

Kocha huyo ambaye hivi karibuni aliiongoza Vijana Stars kuiondoa Cameroon katika michuano ya kuwania kufuzu michezo ya Olimpiki itakayofanyika Uingereza mwakani, alieleza kuwa kwa kiasi kikubwa waamuzi walichangia matokeo hayo.

Vijana Stars ilikubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Uganda &#8216;The Kobs' katika mchezo wa kwanza kuwania kufuzu michezo ya Afrika itakayofanyika baadaye mwaka huu nchini Msumbiji.

Mabao ya Uganda yalifungwa na Moses Olaya dakika ya nne baada ya shuti lililopigwa na mshambuliaji Owen Kasule kumtoka kipa Shaabani Kado.

Kiiza Hamis alifunga la pili dakika ya 23 akiunganisha mpira wa krosi, ambapo bao la Tanzania lilifungwa dakika ya 46 kwa shuti la mbali na Kigi Makasi.

Julio pia alisema atajipanga kwa mechi ya marudiano kwa kuufanyia kazi upungufu wote uliojitokeza katika pambano hilo, ingawa pia alikiri Uganda ni wazuri na anatambua kuwa watajipanga vizuri zaidi kwa mechi ya marudiano.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura timu hiyo itarejea Dar es Salaam leo mchana.
 
Kaseba ampiga ngwala Maugo, adundwa

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 18th April 2011 @ 08:09 Imesomwa na watu: 207; Jumla ya maoni: 0


04_11_kh4vgj.jpg

Mwamuzi John Chagu (kushoto) akimuonya bondia Japhet Kaseba baada ya kumchapa ngwala mpinzani wake Maada Maugo kwenye raundi ya saba wakati wa pambano lao lisilo la ubingwa kwenye ukumbi wa PTA Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam. (Na Mpigapicha Maalumu).





BONDIA Maada Maugo Aprili 16 alikuwa mwenye furaha kupita kiasi baada ya kutangazwa mshindi katika pambano la masumbwi uzani wa kati lisilo la ubingwa dhidi ya Japhet Kaseba.

Kutokana na matokeo hayo, Kaseba naye ametangaza kustaafu mchezo wa masumbwi pamoja na ule unaohusisha ngumi na mateke &#8216;kickboxing' ili kutimiza ahadi yake aliyoiweka kwamba endapo angepoteza mchezo wake na Maugo angestaafu.

Katika pambano hilo lililofanyika ukumbi wa PTA kwenye Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam, lilionekana kuwa na ushindani mkali tangu mwanzo, lakini lilikuja kubadilika raundi za mwisho na kusababisha vurugu kwa baadhi ya mashabiki.

Mwamuzi wa pambano hilo, John Chagu alilazimika kumtangaza Maugo mshindi kwenye raundi ya saba, ambayo haikumalizika kutokana na kutokea vurugu na mashabiki wa pande zote mbili kuvamia juu ya ulingo.

Hatua hiyo ilitokana na Kaseba kumpiga ngwala mpinzani wake, jambo ambalo haliruhusiwi katika masumbwi, hivyo mashabiki wa Maugo kupanda ulingoni kwa hasira na wale wa Kaseba nao kupanda ulingoni wakidai Maugo alimchezea faulo bondia wao na ndiyo maana alipanda hasira na kumpiga teke.

Vurugu hizo za mashabiki na wapambe wa mabondia wote zilichukua karibu nusu saa, huku polisi waliokuwepo kwenye ukumbi huo wakifanya kazi ya ziada kuweka hali ya ukumbi kuwa wa amani.

Lakini wakati mashabiki kadhaa wakiwa juu ulingoni Kaseba alivua gloves zake na kutaka kushuka, lakini baadhi ya wapambe wake wakimsihi aendelee kupigana, kwani ilikuwa imebaki raundi moja na wengine wakimtaka ashuke.

Pambano lilikuwa la raundi nane. Hata hivyo bondia huyo aliendelea kubaki ulingoni, huku Maugo naye akiwa ulingoni kila mmoja akiwa amezingirwa na wapambe wake na wengine walikuwa wakibishana kuhusiana na tukio la Kaseba kupiga ngwala.

Lakini baada ya muda, polisi walifanikiwa kuwashusha wote waliokuwa juu ulingoni, kisha mwamuzi akawataka mabondia wote waondoke kwenye kona zao na waende kwenye kona huru.

Baada ya mabondia wote kuitikia wito huo, Chagu ambaye ni mwamuzi wa kimataifa wa Tanzania, alichukua kipaza sauti na kusema pambano lilikuwa likiendelea, lakini bondia mmoja tayari alishavua gloves na hakuwa nazo, hivyo kulingana na sheria za masumbwi hakuwa na sifa za kuendelea kupigana.

Kutokana na hali hiyo, Chagu alimtangaza Maugo kuwa mshindi wa pambano hilo na kuamsha shangwe kubwa kwa mashabiki wake waliokuwa wamejazana ukumbini hapo, huku wale wa Kaseba wakionekana kunyongea.

Akizungumza baada ya tukio hilo, Kaseba ambaye amepata kuwa bingwa wa dunia wa kickboxing alisema ameamua kustaafu ngumi pamoja na kickboxing kwani aliweka ahadi hiyo kabla ya mchezo wa juzi kwamba kama akipoteza ataacha.

Hata hivyo alielezea kusikitishwa na namna Maugo alivyokuwa akimchezea faulo, hivyo naye kuamua kulipiza kwa namna nyingine, kwa vile yeye pia alifanyiwa faulo.

Katika pambano hilo lililokuwa linasimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), chini ya Rais wa oganaizesheni hiyo, Yassin Abdallah lilichangamka zaidi kadri muda ulivyokuwa unaenda.

Maugo alianza pambano raundi ya kwanza na ya pili kwa kupiga ngumi za jab, lakini Kaseba hakuogopa, alisonga mbele akijibu mashambulizi na kuachia ngumi iliyomkamata Maugo na kumpa mshituko.

Raundi hizo za mwanzo walikuwa wanasogeleana na kujibizana mashambulizi ya ana kwa ana.

Mambo yalianza kubadilika raundi ya tatu, ambapo Maugo alikutana na left hook ya Kaseba na kujikuta akianguka chini, ambapo alihesabiwa na kuendelea na mchezo.

Maugo alijaribu katika raundi ya tatu na nne kumweka mbali mpinzani wake, lakini Kaseba
hakutaka kumwachia hivyo kulazimisha ngumi za piga nikupige zitumike.

Raundi ya sita Maugo aliianza kwa kusukuma jab nyingi mwilini mwa, kisha aliachia left hook na right hook fupi na zilizomkamata Kaseba na kumyumbisha, kiasi cha kuonekana kama
mambo yalianza kumgeuka Kaseba, lakini alitulia na raundi ilimalizika salama.

Mchezo ulibadilika raundi ya saba, ambayo iligeuka kuwa ya faulo nyingi kwa mabondia wote, ambapo Maugo alianza kwa kumchezea mwenzake faulo ambayo ni ya kimchezo kabla ya Kaseba kujibu kwa staili iliyosababisha kelele kwa mashabiki.
 
Van der Sar: Tulijiua wenyewe


LONDON, England

MLINDA mlango wa Manchester United, Edwin van der Sar amekiri kuwa walijiua wenyewe kwa kucheza chini ya kiwango na kisha wakakubali kufungwa na Manchester City
katika mechi ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la FA.

Mholanzi huyo anaamini kuwa mashetani hao wekundu hawakuwa kwenye kiwango kizuri na akasema timu yao ilichoka kwa kiasi fulani dakika za mwisho.

"Tulianza mpambano taratibu mno, lakini tukapata nafasi mbili za kuweza kushinda kwa haraka," alikiambia kituo cha televisheni cha MUTV. "Endapo moja ya nafasi ingeweza kuingia nyavuni mechi ingekuwa tofauti na ingebidi waanze kutufukuza," aliongeza.

Alisema kipindi cha pili wapinzani wao walifanikiwa kufunga bao, huku wao wakiwa wamebaki wachezaji 10 hivyo ilikuwa vigumu kwao kuwafukuza na kujaribu kusawazisha.

Mlinda mlango huyo alisema kuwa kuna wakati walikuwa almanusura kupata bao, ama kupata uwezekano wa kuingia ndani ya eneo la hatari lakini hakuna kilichotokea na hivyo wakabaki na matumani ya kupata bao dakika za majeruhi, lakini bahati haikuwa yao.

"Mara zote inakuwa vizuri unapokuwa wa kwanza kufunga bao, lakini haikutokea na nafasi tulizozipata zilitoweka," alisema na kuongeza kuwa hata hivyo hakuna mchezaji wa kumlaumu kwa maana wote walikuwa uwanjani na anadhani hakuna hata mmoja, aliyecheza kwa kiwango chake hivyo akawashauri kukaza buti kesho.
 
TFF yachimba mkwara Kili Taifa Cup

Imeandikwa na Betram Lengama; Tarehe: 18th April 2011 @ 07:43 Imesomwa na watu: 77; Jumla ya maoni: 0








SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema litakuwa kali na litasimamia vilivyo sheria na kanuni za michuano ya Kili Taifa Cup ambayo itaanza kutimua vumbi mwezi ujao katika vituo sita.

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alibainisha hayo kwenye semina ya waandishi wa habari kwa ajili ya michuano hiyo iliyoandaliwa na waratibu wa masuala ya habari katika michuano hiyo Kampuni ya Executive Solutions na wadhamini wake Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.

Osiah alisema hayo wakati akijibu maswali yaliyoelekezwa katika shirikisho hilo kuhusiana na udhibiti na kufuatwa kwa sheria na kanuni za michuano hiyo kutokana na mashindano ya mwaka uliopita kugubikwa na ukiukwaji wa kanuni hasa suala la usajili wa wachezaji.

"Baada ya kuwepo na ukiukwaji wa baadhi ya sheria na kanuni katika michuano iliyopita, safari hii TFF ina dhamiria na inasisitiza itafuata sheria na kanuni za michuano hiyo, ambayo ni mojawapo ya vyanzo vizuri na vikubwa vya kuibua vipaji vya soka hapa nchini," alisema Osiah.

Alisema TFF haitakuwa na masihara kuhakikisha hilo linafanyika na kuzitaka timu za mikoa yote itakayoshiriki kwenye michuano hiyo kuhakikisha wanazijua na kuzitekeleza kwa ufasaha sheria na kanuni za michuano hiyo.

"Kwa kuanzia tunataka wafanye usajili wa wachezaji watakaochezea timu za zao kwa umakini na kwa wakati, kwani mkoa utakaofanya kinyume na hapo utakabiliwa na adhabu kwa mujibu wa kanuni," alisema.

Michuano hiyo itafanyika katika vituo sita, ambavyo vitakuwa na timu nne kila kimoja vituo hivyo ni Kilimanjaro , Mwanza, Mbeya, Tabora , Morogoro na Lindi Jumla ya Sh bilioni 1.3 zitatumika katika michuano hiyo ambayo bingwa mbali ya kutwaa kombe atazawadiwa Sh milioni 40 , wa pili Sh milioni 20 na wa tatu Sh milioni 10, mfungaji bora Sh milioni 2.5, kocha, mwamuzi, kipa na mchezaji bora wa michuano hiyo kila mmoja atazadiwa Sh milioni mbili.
 
Wasanii kutua Dar es salaam Jumatano

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 18th April 2011 @ 07:43 Imesomwa na watu: 50; Jumla ya maoni: 0








WASANII kutoka nje ya Tanzania ambao watashiriki Tamasha la Pasaka mwaka huu wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam Jumatano wiki hii.

Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ilieleza kuwa maandalizi yote yamekamilikakwa tamasha hilo litakalofanyika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam Jumapili.

Tamasha hilo baada ya kufanyika jijini Dar es Salaam pia litafanyika mjini Dodoma Aprili 25 na baadaye Mwanza Aprili 26.

"Wasanii wote wa nje ya Tanzania watafika Jumatano, ambao ni Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo anayeishi Kenya, Ephraim Sekeleti wa Zambia, Anastazia Mukabwa na Pamela Wanderwa kutoka Kenya," alisema Msama.

Wakati huo huo, Msama alisema kwaya ya Kinondoni Revival nayo imethibitisha kushiriki kwenye tamasha hilo.

Baadhi ya waimbaji wengine watakaoshiriki kwenye tamasha hilo ni Rose Muhando, Boniface Mwaitege, Christina Shusho, Upendo Nkone, Faraja Ntatoba kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Geraldine Odour kutoka Kenya.
 
&#8216;Nitasambaza mafunzo ya masumbwi mikoa yote'

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 18th April 2011 @ 07:35 Imesomwa na watu: 25; Jumla ya maoni: 0








BONDIA wa zamani hapa nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amesema atasambaza mafunzo ya mchezo huo mikoa yote Tanzania Bara.

Akizungumza na gazeti hili Aprili 16 Super D alisema dhamira yake ni kuhakikisha vijana wanaopenda mchezo huo wanatimiza malengo yao bila matatizo.

Alisema aliamua kujikita kwenye klabu ya ngumi ya Ashanti kuwafua vijana na kupata mafanikio makubwa na sasa ameamua kutoa CD na DVD zenye mafunzo ya mchezo huo.

"Najua itakuwa vigumu kumfikia kila mtu, lakini kupitia nia hii ya CD na DVD ambazo zina
mapambano yangu wakati nacheza na pia zina mafunzo mbalimbali ya ngumi zitasaidia sana jamii.

"Dhamira yangu ni kuhakikisha mchezo wa masumbwi unapata mafanikio makubwa kama ilivyokuwa zamani," alisema bondia huyo ambaye kwa sasa amestaafu.
 
Bingwa Kili Taifa Cup kulamba 40m Send to a friend Sunday, 17 April 2011 20:51

Imani Makongoro
VINARA wa michuano ya Kili Taifa Cup watajinyakulia zawadi za kitita cha zaidi ya shilingi 40milioni kutoka kwa wadhamini wakuu wa michuano hiyo Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro.

Mashindano hayo yanatarajia kuanza kutimua vumbi Mei 6 na kushirikisha timu 24 za mikoa ya Tanzania bara katika hatua ya makundi huku hatua ya robo fainali, nusu fainali na fainali ikitarajia kufanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kwa mara ya kwanza.

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alizitaja zawadi kwa washindi kuwa bingwa atajinyakulia kitita cha shilingi 40 milioni huku mshindi wa pili akiondoka na Shs20m wakati mshindi wa tatu atajinyakulia Shs10m.

Alisema kuwa kocha bora, refa bora, mchezaji bora na kipa bora wa michuano hiyo watajinyakulia shilingi 2m kila mmoja wakati timu bora wa michuano hiyo ikiondoka na kitita cha sh 2.5m.

"Tunatarajia pia kila mchezaji bora wa kila mechi kujinyakulia kitita cha shilingi laki moja ili kuleta ushindani kwa wachezaji hao na hatimaye taifa kupata timu bora za ligi na hatimaye kuleta mapinduzi katika soka la Tanzania," alisema Kavishe.

"Mbali na hilo TBL itatumia shilingi 1.3 Bilioni kwa ajili ya kufanikisha mashindano hayo ambapo pesa hizo zitatumika kwa ajili ya chakula, usafiri, malazi na zawadi kwa washindi.

"Zawadi ya mshindi wa kwanza inatofauti ya shilingi 20 m na ile ya mshindi wa pili, tumeamua kuboresha zaidi zawadi hiyo ili kuleta ushindani katika kila timu na ili timu itakayojinyakulia kitita hicho cha mshindi wa kwanza iwe imepata kihalali."

Katika hatua za makundi Mwanza itaumana na Kagera, Shinyanga na Musoma, wakati Arusha itakuwa na Kilimanjaro, Tanga na timu ya vijana chini ya miaka 23 huku Tabora itavaana na Kigoma, Singida na Dodoma, Rukwa itachuana na Mbeya, Iringa na Temeke, Mtwara itatunishiana msuli na Ruvuma, Kinondoni na Lindi, huku Pwani ikicheza na Manyara, Ilala na Morogoro.
 
JKT Mlale yafagiliwa kuibuka kidedea

Imeandikwa na Juma Nyumayo, Songea; Tarehe: 18th April 2011 @ 07:35 Imesomwa na watu: 25; Jumla ya maoni: 0








MKUU wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Samuel Kitundu ameipongeza timu ya mpira wa miguu ya JKT Mlale kutwaa ubingwa taifa ngazi ya mkoa wa Ruvuma na kuongeza idadi ya timu bingwa zinazotokana na JKT hapa nchini.

Salamu hizo zilizosomwa katika sherehe zilizoandaliwa kuwapongeza mabingwa hao, mbele ya
mashabiki wa soka wa wa mji wa Songea wakiongozwa na mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Vijijini, Anna Mbogo kikosini hapo.

Pongezi hizo zilisindikizwa na ahadi ya mkuu wa kikosi hicho, Meja Ahmed Abbas, ambaye alisema aliwekeza kuijenga timu katika nyanja zote, ikiwa ni pamoja na nidhamu ya michezo na ari ya kupata ushindi.

"Niliwaambia nguvu tulizotumia ni nyingi na zingelipotea bila kuleta kombe hili ningeliwapokea pale lango kuu, tabasamu hili lisingelionekana," alisema.

Timu ya JKT Mlale imetwaa ubingwa huo, wakati timu ya Majimaji ya Songea iliyokuwa Ligi Kuu Tanzania Bara ikishuka daraja.

Kwa upande wake Mbogo, aliishauri timu hiyo kuendelea kuijenga nidhamu ya michezo na kuwaheshimu viongozi wao ili washinde michezo yote inayofuata ligi ya taifa daraja la kwanza ngazi ya kanda hadi taifa ili washuhudie tena Ligi Kuu Tanzania Bara.
 
Bunge yaizima LAPF

Imeandikwa na Jasmin Shamwepu, Dodoma; Tarehe: 18th April 2011 @ 07:35 Imesomwa na watu: 16; Jumla ya maoni: 0








TIMU ya soka ya wabunge &#8216;Bunge FC' juzi iliibuka kidedea baada ya kuichapa timu ya Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF) kwa mabao 3-0 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini hapa.

Mechi hiyo ilifanyika baada ya wabunge hao kuahirisha vikao vya Bunge, ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athuman Mfutakamba.

Akizungumza kabla ya mechi hiyo, Naibu Waziri aliwataka wachezaji hao kuwa makini wawapo uwanjani ili wasiumizane na kushindwa kwenda ofisini.

Alisema michezo si ugomvi bali ni urafiki, afya na ajira kwa hiyo wanatakiwa kuwa watulivu na kucheza kwa utulivu na wala si kugombana.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwa dakika 60, Bunge ilianza kupata bao la kwanza dakika ya pili mfungaji akiwa Mark Tanda.

Bao la pili lilipatikana dakika ya 9, ambapo Tanda aliwatoka mabeki wa LAPF na kupiga shuti lililomshinda kipa, Nimrod Marcel.

Timu hizo ziliendelea kushambuliana kwa zamu, lakini umaliziaji haukuwa mzuri. Tanda alifunga bao la tatu kutokana na pasi ya Amos Makala.

Kwa upande wa netiboli timu ya Bunge iliibuka na ushindi wa mabao 28-4 dhidi ya LAPF.
 
Mambo yaiva Tuzo za Wanamichezo Bora

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 18th April 2011 @ 07:35 Imesomwa na watu: 19; Jumla ya maoni: 0








KAMATI ya Kusimamia Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa) imekamilisha kazi ya kuandaa vigezo kwa ajili ya tuzo hizo.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na kusainiwa na Katibu Mkuu wa Taswa ambaye pia ni Katibu wa kamati hiyo, Amir Mhando, ilieleza kuwa mambo yanaenda vizuri na kamati imedhamiria tuzo ya mwaka huu itakayofanyika Mei 6, iwe ya aina yake.

Alisema kamati yake yenye wajumbe 18 imeshakutana mara mbili chini ya Mwenyekiti Masoud Sanani na mshauri wa kamati, Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Michezo, Juliana Yassoda, ambaye ni mshauri wa kamati hiyo.

"Kamati ilikubaliana kuweka vigezo maalumu kwa ajili ya kuwapata wanamichezo hao, ambavyo vitakuwa mwongozo mzuri kwa shughuli hiyo, jambo ambalo tayari limekamilika na vitatangazwa wakati wowote kuanzia sasa.

"Tayari kamati inayo majina ya wanamichezo kutoka vyama mbalimbali vya michezo, ambayo ni matatu ya wanaume na matatu ya wanawake kwa michezo ambayo jinsia zote mbili zinacheza.

Na ile ambayo inachezwa na jinsia moja tu basi majina matatu kamati inayo.

"Hata hivyo kamati inasikitishwa na baadhi ya vyama ambavyo bado havijawasilisha majina ya wanamichezo wake licha ya kupewa barua kuhusiana na jambo hilo kwa muda mrefu.

Tunaviomba vyama hivyo vijitahidi kuwasilisha majina kabla ya Jumanne (kesho) ili yafanyiwe kazi kama ambavyo ya vyama vingine yameshafanyiwa," alisema.

Alitaja majina ambayo kamati inayo ni ya michezo ya riadha, wavu, netiboli, kuogelea, soka, tenisi, karate, kikapu, ngumi za kulipwa, ngumi za ridhaa, gofu, mpira wa mikono, kriketi na paralimpiki.

Pia alisema leo Kampuni ya MultiChoice Tanzania itafanya mkutano na waandishi wa habari kutangaza udhamini wake kwenye tuzo hizo.

Wadhamini wengine wa tuzo hizo mpaka sasa ni Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambao ni wadhamini wakuu, Hoteli ya Movenpick na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Wakati huo huo, Mhando alisema Kamati ya Utendaji ya Taswa iliyokutana Aprili 9, mwaka huu Dar es Salaam ilijadili mambo mbalimbali ikiwemo kuimarisha vyanzo vya mapato kwa chama na kushiriki kwenye masuala ya kuchangia jamii.

Alisema kutokana na hali hiyo wameteua Kamati Maalumu kuandaa michezo mbalimbali ambayo fedha zitakazopatikana kiasi zitatumika kwa masuala ya kijamii kadri itakavyokuwa imeonekana na nyingine zitabaki kuimarisha chama, lengo likiwa ni kukifanya chama kijitegemee kimapato.

Aliwataja Walioteuliwa kuingia kwenye kamati hiyo na vyombo vyao kwenye mabano ni Majuto Omary (The Citizens), ambaye atakuwa Mwenyekiti wa Kamati na Katibu wa Kamati atakuwa George John ambaye ni Katibu Msaidizi wa Taswa.

"Wajumbe wa Kamati ni Sultani Sikilo (Mhazini Taswa), Somoe Ng'itu (Nipashe), Asha Kigundula (JamboLeo),Angela Msangi (TBC1), Onesmo Kapinga, Grace Hoka, Elius Kambili na Zena Chande (Wajumbe Taswa), Mwani Nyangassa (The African), Frank Balile, Dina Ismail (Tanzania Daima), Athanas Kazige (Burudani), Clara Alphonce (Mwananchi) na Peter Mwenda (Majira).

"Moja ya mechi ambazo kamati itashughulikia ni ile ya mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa mwaka 2010/2011 na wachezaji bora wa ligi hiyo wa msimu wa mwaka 2010/2011, ambayo kikao cha Taswa ilishauri ifanyike Juni mwaka huu," ilisema taarifa hiyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom