Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
4 Maoni:

blank.gif

Anonymous said... Dewji anaiburuza team ya Simba. Mpatie nafasi yake Phiri na kazi itaonekana. Tusitumie uwezo wetu kifedha kutwala. kinachohitajika ni ujuzi na busara, baadaye hela na kujituma. Simba kuna maneno mengi kuliko matendo. Pamoja na hayo, Wachezaji wa simba waeathirika kisaikolojia na wanahitaji ushauri wa kisaikolojia. I think Phiri will look into that.
April 10, 2011 9:27 PM
blank.gif

Anonymous said... Hivi hawa tff walijuaje kama yanga itachukua ubingwa na kuandaa kombe uwanjani!mi sipati jibu hapo ila naona giza tuuuuuuuuuuuu
April 11, 2011 2:02 AM
blank.gif

Anonymous said... makombe yalikuwa mawili yameandaliwa moja mechi ya simba na majimaji na lingine mechi ya yanga na toto... so walifanya kitu kilichokwenda shule.... umeshaela sasa!1
YANGA OYEE! CCM OYEE! DAR OYEE!!! JANGWANI OYEEE!! ILALA OYEEE!!TANZANIA OYEEE.... BENDERA YA CCM OYEEE!! SAM TIMBE OYEEE! jamani yanaga mmenipa raha ya kuongea leo
April 11, 2011 4:00 AM
blank.gif

Anonymous said... CCM oyee nini? wana nini cha ziada kama si tu wizi wao! nawe pia jizi nini?
April 11, 2011 5:18 AM
 
Bayern wamtimua kocha Van Gaal


MUNICH, Ujerumani

KLABU ya Bayern Munich imemtimua kocha wake, Louis van Gaal mara moja kwa mujibu wa taarifa zilitoka Ujerumani jana.Van Gaal mkataba wake ulikuwa
unaisha mwishoni mwa msimu huu, lakini bodi ya Bayern imeamua kumtimua kocha huyo wa kidachi mwenye umri wa miaka 59, huku zikiwa zimesalia mechi tano kabla ya msimu kuisha.

Klabu hiyo tayari ilikuwa imetangaza kuwa Van Gaal nafasi yake itachukuliwa na kocha wa Bayer Leverkusen, Jupp Heynckes mwishoni mwa msimu, lakini matokeo ya bao 1-1 ugenini dhidi ya Nurnberg Jumamosi yamefanya timu hiyo kuharakisha kumtimua.

Sare hiyo imeifanya Bayern kuwa katika nafasi ya tatu na inataka kufuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya, wako nafasi ya nne nyuma ya Hannover katika msimamo wa ligi ya Bundesliga huku zikiwa zimesalia mechi tano.

Van Gaal aliiongoza Bayern katika ligi hiyo na kutwaa makombe mawili msimu uliopita, lakini mabingwa hao wa Ujerumeni mara 22 kwa sasa wako nafasi ya nne katika Bundesliga, pointi 14 nyuma ya vinara Borussia Dortmund.

Magazeti ya Bild na Kicker yote yalisema kuwa Bayern imemtimua Van Gaal, kutokana na matokeo ya sare ya bao 1-1, Msaidizi wake Andries Jonker anatarajia kukabidhiwa mikoba kwa kipindi kilichobakia.

Wajumbe wa bodi Karl-Heinz Rummenigge, Uli Hoeness na Karl Hopfner wanaamini walikutana na Mkurugenzi wa Michezo, Christian Nerlingerna kuchukua uamuzi Jumamosi usiku.

Klabu hiyo imefanya vibaya katika mashindano ya ndani msimu huu na na iko katika hatari ya kukosa mashindano ya Ulaya msimu ujao ambayo fainali yake itachezwa Munich.

katika mechi ijayo Bayern, itacheza dhidi ya Leverkusen ikiwa na maana kuwa Heynckes ataiongoza timu hiyo kupigania nafasi ya kuwemo katika mashindano ya Ulaya.
 
Hughes aitabiria ubingwa Man United


LONDON, Uingereza

MARK Hughes juzi alishuhudia timu yake ikifungwa dhidi ya Manchester United na kisha akatabiri kuwa miamba hiyo, inaweza kutwaa makombe matatu msimu
huu.

Mabao mawili ya Dimitar Berbatov na Antonio Valencia, yaliifanya United kuzidi kuendelea kuwa kinara wa Ligi Kuu wakiongoza kwa tofauti ya pointi 10.

Na kocha wa Fulham, Hughes alisema kuwa klabu yake ya zamani inaweza kufikia rekodi yake ya mwaka 1999, kwa kutwaa makombe ya Ligi ya Mabingwa na FA.

Hughes alisema: "Wanaweza kutwaa kila kitu.

Alisema wamekuwa wakishinda mechi, kitu ambacho ni muhimu katika kipindi hiki cha msimu, wanajua ni kitu gani wanataka.

Kocha huyo alisema ni ngumu sana kufanya kitu kama hicho, lakini timu ya Sir Alex imekuwa ikifanya hivyo.

"Lakini nina amini mimi ni kitu ambacho watajaribu na kufanikiwa. Kila la kheri kwao."

Ila wakati Hughes akiipongeza United, kocha wa Old Trafford, Alex Ferguson aliwalaumu wachezaji wake kwa kutocheza vizuri pamoja na kupata mabao mawili katika muda wa dakika 32.

Alisema: "Ilikuwa ni matokeo lakini siwezi kusema ilikuwa ni kazi iliyofanywa vizuri.

"Kipaindi cha kwanza tulicheza soka nzuri sana na tungeweza kufunga magoli mengine zaidi."lakini tulipoteza umiliki wa mpira katika kipindi cha pili na tungeweza kupata matatizo kwa hilo."

Mcheazaji wa Chelsea anayecheza kwa mkopo Fulham, Gael Kakuta alianza kucheza kwa mara kwa kwanza akiwa chini ya Hughes.

Alimjaribu kipa mbamba mbili wa United, Tomasz Kuszczak ambaye alicheza badala ya Edwin van de Sar.Nani alicheza vizuri na kusaidia kupatikana kwa mabao yote mawili ya United.

United ingeweza kupata panalti, lakini mwamuzi Michael Jones hakutoa baada ya Nemanja Vidic kumnawisha mpira Dickson Etuhu.

Moussa Dembele wa Fulham naye alimjaribu kipa, Kuszczak mwishoni mwa mchezo ambaye alipangua shuti lake na kisha Bobby Zamora naye alipaisha mpira alipokuwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga.
 
Tanzania U-23 yalambishwa milioni 20/
• Kocha Cameroon aitabiria makubwa

na Juma Kasesa


amka2.gif
WACHEZAJI wa timu ya taifa ya Vijana wa Tanzania chini ya miaka 23, ‘U-23', wamezawadiwa kitita cha sh milioni 20 kufuatia ushindi wao wa penalti 4-3 walioupata juzi dhidi ya vijana wenzao wa Cameroon, katika mechi ya kusaka tiketi ya kufuzu kucheza Olimpiki mwakani jijini London, Uingereza.
Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, aliyekuwa mfadhili wa klabu ya Simba, Azim Dewji, alisema, amefurahishwa na ushindi huo ambao umeindosha Cameroon katika kinyang'anyiro hicho cha kusaka tiketi ya kufuzu, ambako kampuni yake imetoa sh milioni 10, huku Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), likitoa kiasi kama hicho ikiwa ni pongezi kwa ushindi huo.
Alisema, ushindi huo, ni faraja kwa Watanzania wapenda maendeleo ya soka hivyo wanapaswa kuiunga mkono timu hiyo kwa hali na mali ili iweze kusonga mbele zaidi na kupeperusha bendera ya taifa vyema.
"Huu ni ushindi wetu sote tunapaswa kuwaunga mkono vijana wetu waweze kusonga mbele, kwani tumechoka kuwa wasindikizaji katika michuano ya kimataifa," alisema Dewji.
Aidha, Dewji alisema, mara baada ya mchezo huo kumalizika kwa dakika 120, alilazimika kukutana na viongozi wa NSSF, kutoa motisha kwa wachezaji katika ngwe ya mikwaju ya penalti ambapo walimuahidi kipa Shabani Kado iwapo atapangua penalti atajinyakulia kitita cha shilingi milioni moja kwa kila penalti.
Kutokana na ahadi hiyo, Kado amejinyakulia kitita cha sh milioni moja , baada ya kufanikiwa kupangua penalti ya Mouangue Otele, ambayo iliisadia Tanzania kuiondosha katika mashindano timu hiyo.
Katika hatua nyingine, Serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imeipongeza timu hiyo kwa ushindi iliyoupata dhidi ya Cameroon.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi kwa niaba ya Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi, Mkurugenzi wa Michezo katika wizara hiyo, Leornad Thadeo, alisema serikali imefurahishwa na ushindi huo na kuahidi itazidi kuwa bega kwa bega na vijana hao ili waweze kufuzu kucheza fainali hizo.
Wakati huo huo, Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya vijana ya Cameroon chini ya U-23, Nke Jean, amesema timu ya taifa ya Tanzania kwa umri huo ‘Manyara Stars' ina nafasi ya kufuzu kucheza fainali za Olimpiki mwakani zitakazofanyika England kutokana na kucheza kwa jihadi na kujiamini.
Kauli ya kocha huyo imekuja saa chache baada ya Manyara Stars inayonolewa na Kocha mzalendo Jamhuri Kihwelo ‘Julio', juzi kuifurusha Cameroon katika mashindano kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Alisema kikosi cha Manyara kilicheza kwa jihadi kubwa ndiyo maana kilifanikiwa kuibuka na ushindi huo licha ya vijana wake nao kupigana kufa na kupona ili kushinda mchezo huo, hivyo kuipa nafasi Tanzania ya kupenya kucheza fainali hizo iwapo wataendelea na jihadi hiyo.
Jean alisema kutolewa kwa vijana wake baada ya kucheza dakika 120 kabla ya kuingia katika hatua ya mikwaju ya penalti ni ishara ya kuwa walipigana kufa na kupona lakini bahati haikuwa yao.
Akizungumzia kukosekana kwa mshambuliaji wake, Mrisho Ngassa, katika mchezo wa juzi, Julio alisema mchezaji huyo alikuwa anakabiliwa na malaria na hakushindwa kumchezesha kwa uvumi kuwa ana umri mkubwa.
 
Ndassa aifunda Simba


na Juma Kasesa


amka2.gif
MBUNGE wa Jimbo la Sumve, Richard Ndassa, amelipa changamoto benchi la ufundi la Simba kujipanga upya kuongeza wachezaji wengine wenye kiwango kwa ajili ya kuimarisha safu ya ulinzi na ushambuliaji ikiwa ni maandaalizi kwa mashindano mengine ya kimataifa mwakani.
Ndassa alitoa changamoto hiyo ikiwa ni wiki kadhaa baada ya Simba kuondoshwa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika na TP Mazembe kwa jumla ya mabao 6-3 mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Alisema licha ya Simba kuinyesha soka safi lakini makosa yaliyofanywa na safu ya ulinzi ya timu hiyo ndiyo yaliyosababisha washambuliaji wa Mazembe kufanikiwa kufunga mabao yote matatu na timu hiyo kuondoshwa katika mashindano.
"Simba walicheza vizuri lakini makosa ya mabeki yalikuwa na gharama kubwa kwa timu yao, ni wakati wa Kocha Mkuu wa timu hiyo Patrick Phiri, na benchi lake la ufundi kuanza kusaka wachezaji ambao wataongeza nguvu katika ulinzi ili kuisadia Simba katika michuano ya kimataifa ya mwakani," alisema Ndassa.
Katika mchezo huo Mazembe waliibuka na ushindi wa mabao 3-2, ikiwa ni wiki kadhaa baada ya kuvuna ushindi mwingine wa mabao 3-1, mchezo uliopigwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mjini Lubumbashi.
Aidha, mbunge huyo aliigeukia safu ya ushambuliaji ya timu hiyo kuwa nayo inatakiwa kunolewa sana ili kuipa makali ya kucheka na nyavu, kwani mabao waliyokosa katika mechi na Mazembe kipindi cha kwanza yangeweza kuisaidia Simba kuwavuruga Wacongo hao na hatimaye timu hiyo kupenya katika hatua hiyo.
"Kimsingi washambuliaji wetu walikosa magoli ya wazi mengi ambayo iwapo wangeyapata yangewasaidia, wenzetu ilikuwa ni faraja kwao, na mpira wa miguu ni mchezo wa makosa, ndiyo maana walipopata nafasi za kufunga walizitumia vizuri na kufanikiwa kuvuka hatua hiyo," alisema Ndassa.
 
Tunawapongeza vijana wa ‘Julio’

ban_tahariri.jpg

amka2.gif
TIMU ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 23, mwishoni mwa wiki waliwapa faraja wapenzi, mashabiki wa soka na Watanzania kwa ujumla.
Ni faraja iliyokuja baada ya vijana hao kufanikiwa kupiga hatua moja mbele katika mbio za kuwania tiketi ya kucheza fainali za Olimpiki zitakazofanyika mwakani mjini London, Uingereza.
Tanzania imesonga hatua moja mbele baada ya kuwafurusha katika kampeni hiyo vijana wenzao wa Cameroon kwa penalti 4-3.
Katika mechi hiyo ya juzi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, timu hizo zilipigiana penalti baada ya kumaliza dakika 120, zikiwa zimefungana jumla ya mabao 3-3.
Kiasi hicho cha mabao kilitokana na Tanzania kufungwa mabao 2-1 katika mechi ya kwanza iliyokuwa imechezwa wiki mbili zilizopita mjini Younde, Cameroon.
Wakiwa nyuma, juzi vijana wa Tanzania chini ya Kocha wao, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, walicheza kwa juhudi kubwa na kufanikiwa kushinda 2-1.
Licha ya timu hizo kuingia kwenye muda wa nyongeza wa dakika 30, bado zikashindwa kutoa mshindi baina yao, hivyo kuingia kwenye mikwaju.
Katika hatua hiyo, ndipo vijana wa Tanzania, wakafanikiwa kupata mikwaju 4-3, hivyo safari ya Cameroon katika kampeni hizo kuishia hapo.
Kwetu Tanzania Daima, tunachukua fursa hii kuwapongeza wachezaji wote wa timu hiyo kwa maana ya waliocheza na wale ambao hawakupangwa katika mechi hiyo ya marudiano.
Tunaamini hakuna kingine kilichowasukuma kujituma kwa juhudi hadi kuvuna ushindi huo licha ya kuwa nyuma, isipokuwa kiu ya mafanikio ikisukumwa na uzalendo.
Kitendo cha kuwa nyuma, lakini vijana wakafanikiwa kupambana vilivyo na kusawazisha na kushinda, ni cha kishujaa kinachopaswa kuwa mfano wa kuigwa.
Mbali ya wachezaji, pia benchi la ufundi chini ya Kocha wake Julio, nalo linahitaji pongezi kubwa kwa kuwaandaa vizuri vijana kuelekea mechi ya marudiano.
Maandalizi tunayomaanisha hapa, si yale ya kuwafundisha mbinu za uchezaji tu, pia kuwajenga vijana kisaikolojia kwamba, kama Cameroon walishinda kwao, wao walikuwa na uwezo wa kushinda mechi ya marudiano.
Kweli, vijana wakazingatia maelekezo yote ya kiufundi na mbinu, huku wakijengwa kisaikolojia na kufanikiwa kuwang’oa Cameroon.
Hata hivyo ni wajibu wa kila mchezaji kuona fahari kubwa kwa kuiwezesha nchi yake kusonga mbele kwenye kampeni hizo, lakini kamwe mwanzo huo wa mafanikio, usiwavimbishe vichwa.
Kitu muhimu kwa kila mchezaji ni kuyachukulia mafanikio hayo kama changamoto kwake ya kusaka mafanikio zaidi, hivyo kujipanga zaidi kwa maana ya kuongeza juhudi katika mazoezi.
Aidha, kwa benchi la ufundi la timu hiyo chini ya Julio ambalo pia linastahili pongezi kubwa kwa kazi nzuri na kubwa waliyofanya, wanapaswa kujipanga zaidi.
Kujipanga ambako tunanaamisha hapa, ni kufanyia kazi dosari zote zilizojitokeza katika mechi zote mbili zilizopita ili kujisahihisha kabla ya kuanza kwa ngwe nyingine.
Kwa upande wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), nalo lizidi kuipatia matunzo bora timu hiyo kwa kuiandalia mechi nyingi za kirafiki ili kuwaimarisha zaidi wachezaji.
Tunamaliza maoni haya huku tukiwapongeza wachezaji wote wa timu ya vijana wa chini ya miaka 23 na makocha wao, lakini ushindi dhidi ya Cameroon, uwe mwanzo wa kujipanga zaidi.
 
Wawakilishi wetu sasa waanze kujipanga kimataifa
ban.mtazamo.jpg


Makuburi Ally​

amka2.gif
LIGI Kuu Tanzania Bara msimu wa 2010/11 umekamilika jana huku Yanga ya Dar es Salaam wakiwa mabingwa, wakiwanyang'anya ubingwa mahasimu wao Simba.
Mechi za mwisho zilichezwa viwanja vinne tofauti hapa nchini, lakini michezo ya jijini Mwanza kwa Yanga walipomenyana na Toto Africans wakati katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Simba walimenyana na Majimaji ya Songea ndizo zilizokuwa gumzo kutokana na matokeo yake kutoa bingwa wa Ligi Kuu Bara.
Katika michezo hiyo ambayo mahasimu hao kila mmoja alikuwa akiwania nafasi muhimu ya kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara iliyoanza kutimua vumbi Agosti 21 mwaka jana.
Ligi Kuu Tanzania bara iliyomalizika jana ilishirikisha timu 12 ambazo ni pamoja na
Yanga, Simba, Azam FC, Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, JKT Ruvu, African Lyon, Toto African, Ruvu Shooting, Polisi Dodoma, Majimaji FC na AFC Arusha.
Kwa mujibu wa utaratibu mpya wa Ligi Kuu Tanzania bara, timu mbili za mwisho ambazo ni AFC na Majimaji ya Songea na nafasi zao zinachukuliwa na timu nne zilizopanda daraja kutoka la kwanza msimu uliopita.
Timu zitakazoshiriki Ligi Kuu msimu ujao ni pamoja na Villa Squad, JKT Oljoro, Coastal Union na Moro United ambako msimu ujao wa Ligi Kuu utakuwa na timu 14 badala ya 12 za msimu uliomalizika.
Ongezeko la timu hizo, iwe chachu ya kushindana ipasavyo na ligi kuwa na ushindani mkubwa ambao utatoa bingwa stahili ambaye atatwaa ubingwa kutokana na wingi wa timu.
Msimu uliopita baada ya Simba kunyakua ubingwa ilipata nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa barani Afrika ambako wiki chache zilizopita walitolewa na mabingwa wa Afrika TP Mazembe kwa vipigo vya nyumbani na ugenini, baada ya kuiadhibu Elan ya Comoro kwa michezo miwli ya nyumbani na ugenini.
Wakati mahasimu wao Yanga walipata nafasi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambako walishiriki Kombe la Shirikisho ambayo nayo iliishia hatua ya kwanza ya michuano hiyo baada ya kutolewa na Dedebit ya Ethiopia kwa michezo yake miwili ya nyumbani na ugenini.
Kwa Mtazamo wangu napendekeza kwa Simba na Yanga ambazo msimu ujao zitashiriki mashindano ya kimataifa kujipanga ipasavyo na kuacha ubabaishaji ambao umekuwa ndio mtindo kwa soka yetu, jambo ambalo halitufikishi popote.
Wakati huu wa mapumziko uwe ni kusaka namna ya kupiga hatua katika maendeleo ya soka letu ambalo inatakiwa tuondokane na kuwa kichwa cha mwendawazimu.
Mara nyingi hatufanyi masuala ya msingi ambayo yatafanikisha timu kuonyesha mambo makubwa ambayo yanaonyeshwa na wenye nia ya kufanya makubwa katika maendeleo hasa ukizingatia sasa hivi soka na kiwanda.
Sababu ya kuanza kupayuka mapema zinatokana na sababu kwamba tumeona Simba ambao walionyesha wana uwezo wa mashindano ya kimataifa lakini vitu vidogo vimewaangusha.
Naeleza kwamba wameangushwa na vitu vidogo kwa sababu, mchezo wa kwanza uliochezwa katika uwanja wa De Stade de Kenya, jijini Lubumbashi, Simba walifungwa mabao 3-1, mabao ambayo yalitokana na uzembe wa kushngaa shangaa.
Hata mchezo wa pili Simba walifungwa kwa staili kama mchezo wa kwanza, sasa tusirejeee yaliyopita, tugange yajayo na pia suala la kusajili wachezaji wenye uwezo wa mashindano ya kimataifa.
Inatakiwa pia timu zetu kuzingatia pendekezo la Whitesands Declaration, mkutano uliofanyika Februari mwaka huu ulioongozwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ambako katika mkutano huo yalitokea mapendekezo kama usajili wa wachezaji wa kigeni wasizidi watatu kwa sababu za msingi zilizowasilishwa na washiriki ambao ni klabu za Ligi Kuu.
Pamoja na mapendekezo mengine pia mkutano huo wa wiki moja ulizungumzia maazimio ya Bagamoyo yaliyofanyika mwaka 2007 yakiwa na lengo la kukuza na kuendeleza soka la Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Chonde Chonde Simba, Yanga na klabu nyingine za Ligi Kuu Tanzania Bara kutofanya maandalizi bora ambayo yatasaidia kufanya vizuri katika michuano ya Ligi Kuu na ile ya Kimataifa na kuachana na ujanja ujanja wa kuleta wachezaji ambao wanatangazwa kwa mbwembwe lakini hamna kitu.
Ni wakati wa viongozi kuketi chini na kusaka namna ya kupiga hatua kuliko kusubiri wiki chache kabla ya Ligi Kuu kuanza msimu ujao ambayo inatarajia kuanza Agosti mwaka huu.
Tusitarajie ligi mbaya na ushiriki mbovu wa mashindano ya kimataifa kutoka kwa Yanga na Simba ambayo yatatoa visingizio vingi visivyokuwa na msingi.
 
Wawakilishi wetu sasa waanze kujipanga kimataifa
ban.mtazamo.jpg


Makuburi Ally​

amka2.gif
LIGI Kuu Tanzania Bara msimu wa 2010/11 umekamilika jana huku Yanga ya Dar es Salaam wakiwa mabingwa, wakiwanyang’anya ubingwa mahasimu wao Simba.
Mechi za mwisho zilichezwa viwanja vinne tofauti hapa nchini, lakini michezo ya jijini Mwanza kwa Yanga walipomenyana na Toto Africans wakati katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Simba walimenyana na Majimaji ya Songea ndizo zilizokuwa gumzo kutokana na matokeo yake kutoa bingwa wa Ligi Kuu Bara.
Katika michezo hiyo ambayo mahasimu hao kila mmoja alikuwa akiwania nafasi muhimu ya kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara iliyoanza kutimua vumbi Agosti 21 mwaka jana.
Ligi Kuu Tanzania bara iliyomalizika jana ilishirikisha timu 12 ambazo ni pamoja na
Yanga, Simba, Azam FC, Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, JKT Ruvu, African Lyon, Toto African, Ruvu Shooting, Polisi Dodoma, Majimaji FC na AFC Arusha.
Kwa mujibu wa utaratibu mpya wa Ligi Kuu Tanzania bara, timu mbili za mwisho ambazo ni AFC na Majimaji ya Songea na nafasi zao zinachukuliwa na timu nne zilizopanda daraja kutoka la kwanza msimu uliopita.
Timu zitakazoshiriki Ligi Kuu msimu ujao ni pamoja na Villa Squad, JKT Oljoro, Coastal Union na Moro United ambako msimu ujao wa Ligi Kuu utakuwa na timu 14 badala ya 12 za msimu uliomalizika.
Ongezeko la timu hizo, iwe chachu ya kushindana ipasavyo na ligi kuwa na ushindani mkubwa ambao utatoa bingwa stahili ambaye atatwaa ubingwa kutokana na wingi wa timu.
Msimu uliopita baada ya Simba kunyakua ubingwa ilipata nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa barani Afrika ambako wiki chache zilizopita walitolewa na mabingwa wa Afrika TP Mazembe kwa vipigo vya nyumbani na ugenini, baada ya kuiadhibu Elan ya Comoro kwa michezo miwli ya nyumbani na ugenini.
Wakati mahasimu wao Yanga walipata nafasi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambako walishiriki Kombe la Shirikisho ambayo nayo iliishia hatua ya kwanza ya michuano hiyo baada ya kutolewa na Dedebit ya Ethiopia kwa michezo yake miwili ya nyumbani na ugenini.
Kwa Mtazamo wangu napendekeza kwa Simba na Yanga ambazo msimu ujao zitashiriki mashindano ya kimataifa kujipanga ipasavyo na kuacha ubabaishaji ambao umekuwa ndio mtindo kwa soka yetu, jambo ambalo halitufikishi popote.
Wakati huu wa mapumziko uwe ni kusaka namna ya kupiga hatua katika maendeleo ya soka letu ambalo inatakiwa tuondokane na kuwa kichwa cha mwendawazimu.
Mara nyingi hatufanyi masuala ya msingi ambayo yatafanikisha timu kuonyesha mambo makubwa ambayo yanaonyeshwa na wenye nia ya kufanya makubwa katika maendeleo hasa ukizingatia sasa hivi soka na kiwanda.
Sababu ya kuanza kupayuka mapema zinatokana na sababu kwamba tumeona Simba ambao walionyesha wana uwezo wa mashindano ya kimataifa lakini vitu vidogo vimewaangusha.
Naeleza kwamba wameangushwa na vitu vidogo kwa sababu, mchezo wa kwanza uliochezwa katika uwanja wa De Stade de Kenya, jijini Lubumbashi, Simba walifungwa mabao 3-1, mabao ambayo yalitokana na uzembe wa kushngaa shangaa.
Hata mchezo wa pili Simba walifungwa kwa staili kama mchezo wa kwanza, sasa tusirejeee yaliyopita, tugange yajayo na pia suala la kusajili wachezaji wenye uwezo wa mashindano ya kimataifa.
Inatakiwa pia timu zetu kuzingatia pendekezo la Whitesands Declaration, mkutano uliofanyika Februari mwaka huu ulioongozwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ambako katika mkutano huo yalitokea mapendekezo kama usajili wa wachezaji wa kigeni wasizidi watatu kwa sababu za msingi zilizowasilishwa na washiriki ambao ni klabu za Ligi Kuu.
Pamoja na mapendekezo mengine pia mkutano huo wa wiki moja ulizungumzia maazimio ya Bagamoyo yaliyofanyika mwaka 2007 yakiwa na lengo la kukuza na kuendeleza soka la Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Chonde Chonde Simba, Yanga na klabu nyingine za Ligi Kuu Tanzania Bara kutofanya maandalizi bora ambayo yatasaidia kufanya vizuri katika michuano ya Ligi Kuu na ile ya Kimataifa na kuachana na ujanja ujanja wa kuleta wachezaji ambao wanatangazwa kwa mbwembwe lakini hamna kitu.
Ni wakati wa viongozi kuketi chini na kusaka namna ya kupiga hatua kuliko kusubiri wiki chache kabla ya Ligi Kuu kuanza msimu ujao ambayo inatarajia kuanza Agosti mwaka huu.
Tusitarajie ligi mbaya na ushiriki mbovu wa mashindano ya kimataifa kutoka kwa Yanga na Simba ambayo yatatoa visingizio vingi visivyokuwa na msingi.
 
HENRY ALFRED AMEDE: Mlinzi wa kati alieibukia ulaya
ban.blank.jpg


Andrew Chale​

amka2.gif
HENRY Alfred Amede ni jina geni miongoni mwa mashabiki wa soka nchini Tanzania hasa wanaofuatilia Ligi Kuu Tanzania Bara lakini si geni kwa waliokuwa wanafuatilia maandalizi ya timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 (U-23) Manyara Stars dhidi ya Cameroun ambapo timu hiyo ya vijana iliweka kambi katika Hoteli ya Bamba Beach Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Katika mchezo wake wa juzi, Manyara Stars iliibuka na ushindi baada ya kuiadhibu Cameroon kwa mikwaju ya penalti 4-3, baada ya kumalizika kwa dakika 120 kwa Stars kuwa mbele kwa mabao 2-1, matokeo yaliyofanana na mchezo wa kwanza uliochezwa wiki mbili zilizopita jijini Younde, Cameroon, ambapo Stars ilikubali kipigo cha mabao 2-1.
Mwandishi wa makala hii alifanya mahojiano na Amede ambaye katika kikosi cha timu hiyo wachezaji wenzake walimwita ‘Mrashia', wakimaanisha Mrusi, kutokana na kuishi kwake huko kwa muda wake wote akisakata soka.
"Mimi ni mtoto wa tatu kati ya watoto sita wa mzee Henry Amede na mama Annastazia James, ambapo nilizaliwa miaka 18 iliyopita katika Kijiji cha Nyampulukano wilayani Sengerema jijini Mwanza," Henry alianza kwa kujitambulisha.
Anaendelea kujitambulisha kwamba katika familia yao yeye pekee ndiye mwenye kipaji cha kucheza soka wakati wenzake si wanamichezo.
Anasema alianza kucheza soka tangu akiwa Shule ya Msingi Sengerema, kipindi hicho alikuwa akicheza chandimu na wanafunzi wenzake na huku akiwakumbuka walimu waliomsaidia kipindi hicho cha miaka ya 1990 akiwamo mwalimu wake aliyemtaja kwa jina la Dennis na Mwalimu Mtani, ambao kila mara walikuwa wakimsaidia katika kumuelekeza cha kufanya pindi awapo uwanjani.
Anasema katika pilikapilika na harakati zake za michezo alibahatika kukutana na Francis Michael ambaye alikuwa akichezea timu ya SEDCO iliyokuwa chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema iliyokuwa ikishiriki Ligi Daraja la Tatu ngazi ya Mkoa wa Mwanza.
Anasema alipata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa nahodha wa timu hiyo aliyemkumbuka kwa jina moja la Mbembe, ambapo aliweza kuendesha soka yake hadi alipomaliza shule ya msingi, na mwaka 2005 alibahatika kwenda nchini Urusi na kujiunga na timu moja iliyokuwa inaendeshwa kama kituo cha Sports Academy cha Urusi kinacholea na kusaka vipaji.
Amede anasema nchini Urusi aliishi kwa miaka sita akiwa hana timu zaidi ya kufanya mazoezi katika kituo na baadaye alifanikiwa kujiunga na timu ya Sakhalini FC ya Daraja la Nne nchini humo.
"Baada ya kupanda daraja timu hiyo mwaka 2010, sikuweza kuendelea nayo kwa kuwa daraja la 3 kisheria wasio raia wa Urusi hawaruhusiwi kucheza hivyo nikarejea tena katika kituo nilichokuwepo awali," alisema.
Kuonekana kwake U- 23 ya Tanzania
Anasema kuwa ni bahati pekee kuonekana kwake na kuitwa katka timu ya taifa ya vijana ya chini ya umri wa miaka 23 ‘Manyara Stars' iliyokuwa chini ya Meneja Mohamed Adolph na Kocha Mkuu, Jamhuri Kiwhelo ‘Julio' sambamba na Kocha Msaidizi Mohamed Ayoub.
Anasema katika kikosi hicho aliitwa kujiandaa na mchezo dhidi ya Cameroun, lakini kutokana na maumivu ya nyama za paja yaliyomkabili hakuweza kuendelea na kambi na kurejea Urusi katika kituo anacholelewa.
"Niliweza kukaa na kuwa pamoja na wenzangu ndani ya kikosi na kuonyesha kiwango cha hali ya juu lakini bahati mbaya majeraha yalinisababisha kupunguza mazoezi hali iliyonifanya kurudi Urusi, lakini kwa upande mwingine hali ya hewa ilichangia kupata maumivu ya mwili," alisema.
Anede bado ana imani na ana hamu ya kurudi kuichezea nchi yake katika michuano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa mara atakapopona maumivu yanayomsumbua.
"Nipo huru, hivyo sitaiacha nchi yangu katika kuitumikia kwenye soka hivyo nipo tayari muda wowote kuichezea timu yangu ya taifa, iwe Manyara Stars au Taifa Stars nikiwa ni mzalendo mwenye moyo safi," alisema.
Matarajio yake
Henry anasema kuwa mara zote matarajio yake ni kuona anacheza katika timu mahiri Ulaya na kuwa tegemeo la taifa lake hasa katika mashindano ya kimataifa.
"Kila mchezaji anatarajia kucheza soka ya kulipwa Ulaya lakini kwa kweli soka ya Ulaya ni ngumu inayohitaji kuwa sawa, hali itakayoendana na nao na hilo ndilo linalonifanya nitamani kuendelea kuishi huko ili kuizoea soka yao zaidi ili siku nafasi ikipatikana niwe tayari nimeishazoea aina ya soka ya huko," alisema.
Anaendelea kueleza kuwa suala la msingi hapa ni kuendeleza juhudi katika mazoezi ili kubahatika kupata nafasi hiyo, hasa katika timu za Urusi, nchi ambayo anaishi kwa muda mrefu.
Ushauri Kwa TFF
Ushauri wake kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ni kuendelea kuhamasisha zaidi soka ya Tanzania, hasa kwa wadau ambao ni wenye soka yao.
Anasema TFF inapaswa kuwa na idara inayoshughulikia wachezaji walio nje ya Tanzania ili waweze kuwafuatilia na kujua maendeleo yao na hata ikibidi kuwatembelea katika timu zao kama wanavyofanya wenzetu wa nchi zilizoendelea katika michezo na hii itamfanya hata Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen, kuwa na chaguo bora katika mashindano ya kimataifa.
Amede anasema kuna Watanzania wengi walioko nje ya Tanzania na wanacheza soka, si katika ligi kubwa ama timu kubwa lakini wanaweza kuwa msaada wa timu ya taifa, kwa mfano golikipa wa Togo aliyejeruhiwa kule Angola alikuwa anacheza daraja la 4 Ufaransa na hapo utajiuliza wamemjuaje.
Akielezea juu ya kitengo hicho kama TFF watakianzisha, kitakuwa kinahakikisha wachezaji walio nje wanapewa taarifa za kujiunga na timu ya taifa mapema na pia kutoa taarifa kwa uongozi wa klabu zao mapema ili kuepuka mkanganyiko, ambapo mfano hai wa hivi karibuni ni uliotokea kwa wachezaji Danny Mrwanda na Abdi Kassim Babi wanaokipiga nchini Vietnam, walioshindwa kuja Tanzania kwa ajili ya mchezo dhidi ya Afrika ya Kati uliochezwa Machi 26 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Ushauri kwa wenzake

Amede anasema soka ina miiko yake na lazima mchezaji aifuate ikiwa ni pamoja na kuchunga kiwango chake kisishuke huku mlinzi wa kiwango chake ni yeye mwenyewe.
Anasema kinachosababisha kushuka kwa viwango vya wachezaji ni pamoja na soka ya mchangani ‘ndondo' kwa sababu mchezaji hana muda wa kupumzika ikiwa anatakiwa apate muda wa kupumzika.
Nafasi yetu kucheza Ulaya
Soko la mchezaji kutoka Tanzania kwenda kucheza soka nje ya Tanzania bado ni kazi ngumu ukilinganisha na wachezaji kutoka magharibi mwa Afrika na hii inatokana na kiwango cha timu ya taifa kuwa kidogo na pia kutoshiriki michuano mikubwa Afrika na Kombe la Dunia.
Anasema kwa hali hii hata kama mchezaji ni mzuri bado wanakuwa hawakuamini kama ambavyo wanawaamini haraka wachezaji kutoka nchi za Cameroon, Ivory Coast, Ghana na Nigeria. "Hivyo kwa wenzangu wanaopata nafasi ya kuwakilisha taifa, basi wakumbuke kuwa wao ndio wanatutangaza," anasema.
Shukrani zake
Henry anasema mara zote familia yake imekuwa ikimpa sapoti ili apige hatua katika mpangilio wa mafanikio yake ya soka na maisha yake kwa ujumla.
Mbali na familia yake pia ni ndugu na jamaa, msaada mkubwa ameupata kutoka kwa wakala Damas Ndumbaro na Kocha Mohamed Adolph bila kumsahau Jamhuri Kihwelo ‘Julio' ambao kwa pamoja wamefanikisha kuendelea kuwa katika hali ya kujiamini na kuendelea katika soka.



h.sep3.gif

Maoni: chalefamily@yahoo.com
 
Kusubiri timu ishinde tuwatuze wachezaji
ban.blank.jpg


Mwandishi wetu​

amka2.gif
WADAU wa soka nchini juzi walijawa na furaha baada ya timu yao ya vijana chini ya miaka 23 kuing'oa timu ya vijana ya Cameroon, katika kinyang'anyiro cha kusaka tiketi ya michezo ya Olimpiki 2012.
Michezo hiyo ya Olimpiki 2012 inatarajiwa kufanyika mwakani jijini London, nchini England.
Timu hiyo ambayo iliteuliwa kwa kushtukizwa na Kocha, Jamhuri Kihwelo ‘Julio' ilianza kwa kupigwa mwereka wa mabao 2-1 katika mechi ya kwanza iliyopigwa ugenini nchini Cameroon.
Hata hivyo, vijana hao wakiongozwa na nahodha wao Shaban Kado, walijuiliza na juzi wakawatoa kimasomaso Watanzania kwa kuwanyuka Wacameroon kwa mabao 2-1 katika mechi iliyopigwa kwenye dimba la taifa jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo ulisababisha timu hizo kufungana kwa kila kitu, hivyo ili apatikane mshindi ikabidi ziongewezwe dakika 30, ambapo timu hizo zilishindwa kubadili matokeo hivyo kuingia kwenye mikwaju ya penalti tano tano.
Vijana wa Tanzania wakatia nyavuni penalti nne na kupoteza moja wakati Wacameroon walipoteza mbili moja ikipanguliwa na Kado, hivyo Tanzania kusonga.
Ushindi huo ulipokewa kwa nderemo na mashabiki wa soka, si tu wale waliojitokeza kuwashangilia vijana wetu kwenye Uwanja wa Taifa lakini mashabiki wote wa soka nchini.
Kwa ushindi huo vijana wa Tanzania wanasubiri ipangwe ratiba ili kujua tutacheza na nchi gani katika hatua inayofuata, mechi ambazo zitapigwa Juni mwaka huu.
Kama nilivyodokeza awali timu hii ya vijana iliitwa zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kushiriki mechi dhidi ya Cameroon, hivyo haikujiandaa vya kutosha.
Kwa maana hiyo wakati tukisubiri kupangwa kwa ratiba timu inapaswa iingie kambini kujifua vilivyo ili angalau mwaka huu tuweze kuandika historia ya kujikatia tiketi ya kushiriki mashindano ya Olimpiki mjini London.
Ni ukweli usiopingika kuwa kambi ya maandalizi ina gharama kubwa, hivyo kuiachia TFF peke yake haitakuwa jambo la busara ni wajibu serikali na wadau wote wa soka tujitokeze kusaidia maandalizi ya vijana hawa.
Utakuwa ujinga tukisubiri timu hii ishinde kwa bahati halafu ndipo tujitokeza kwa wingi kuwatuza wachezaji kwa mafanikio.
Huu ndio wakati muafaka mwenye chochote kile achangie kuwafanya vijana hawa wajifue kwa nguvu na bidii ili mwisho wa siku watufurahishe kwa kuzifunga kila timu watakazokutana nazo.
Tuache mtindo wa kuvizia timu ikishinda ndipo tujitokeze badala yake tujitokeze mapema ili tuwe sehemu ya mafanikio hayo yatakayopatikana.
Ni muda muafaka kwa mawaziri, wabunge na viongozi wengine wa kitaifa na wale wa vyama vya siasa, mashirika na taasisi kujitokeza kutoa michango ya hali na mali kuiwezesha timu hii kuingia kambini kujifua.
Kinyume cha hivyo ni kuifanya Tanzania iendelee kuwa kichwa cha Mwendawazimu ambacho hata kichaa anajisifia kwa kukinyoa.
Vijana wetu wametudhihirishia kuwa wakiandaliwa vya kutosha wanaweza kushindana badala ya kushiriki na kuwa wasindikizaji, kama ilivyozoeleka hivyo tusisite kujitokeza na kusaidia kuwaandaa.
Sitaki kusikia wala kuona waheshimiwa wabunge wakisubiri hadi timu yetu ishinde ndipo wajitokeze na kupeleka katuni za juisi na maji au kuwazawadia fedha taslimu.
Ni kweli zawadi washindi wanastahili kutuzwa, lakini kusubiri kwetu washinde ndiko kunakotufanya tuishie kuwa wasindikizaji wa mashindano mbalimbali kila mwaka.
Hii ni kutokana na timu zetu kutolewa mapema kwa sababu ya kukosa maandalizi ya kutosha, jambo ambalo nasema kama tutaendelea kulifumbia macho hatutafika.
Tumuunge mkono Kocha Julio, ili kwa kugharamia kambi ya uhakika na tuwape wapambanaji wetu hawa posho za kujikimu ili wauone mpira kama Lulu na kuucheza kwa mapenzi wakiiona ni ajira na si burudani kama inavyochukuliwa na wengi.
Hakuna kinachoshindikana penye dhamira na vijana hawa wametuthibitishia hilo kwa kuwatoa Cameroon, timu yenye nyota wanaolelewa vema kisoka ikiwa hata na vijana wanaokipiga Ulaya.
Chonde Watanzania tushikamane kuichangia kambi ya vijana wetu hawa ambao tukiwaandaa vyema tutakuwa na furaha isiyokoma katika medani ya soka ya kimataifa, kinyume cha hivyo tutaishia kulaumiana na kulumbana.
 
Wajue mabingwa wa Bara tangu 1965
ban.blank.jpg


Ruhazi Ruhazi​

amka2.gif
KINYANG'ANYIRO cha kusaka ubingwa wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara ‘Vodacom Premier League' (VPL), msimu wa 2010/2011 kilifikia tamati jana kwa mechi kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti.
Mabingwa watetezi Simba walikuwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kupigana kutetea taji hilo.
Historia ya michuano hiyo iliyoanza mwaka 1965 inaonyesha kuwa Simba ndiyo ilikuwa timu ya kwanza kulinyakua kombe hilo ilipolitwaa mwaka huo, lakini wakati huo ilikuwa ikiitwa Sunderland na ikaweza tena kulitetea mwaka uliofuata 1966.
Timu nyingine iliyokuwa ikitamba katika Jiji la Dar es Salaam ya Cosmo Politan, ilijipanga vema na kuweza kulitwaa taji hilo mwaka 1967.
Kutokana na kulikosa taji hilo kwa miaka mitatu ya kwanza, kuliwafanya watoto wa Jangwani, Dar es Salaam Young African ‘Yanga', kujiuliza sana na mwisho wakapata ufumbuzi wa kile wanachopaswa kukifanya.
Yanga waliweza kukitengeneza kikosi chao vema, ambacho kiliweza kulitwaa taji hilo kwa mara ya kwanza mwaka 1968, lakini ubora wa kikosi chao ukawafanya waweze kulitetea 1969.
Utamu wa kuwa na taji, uliwafanya Yanga walirejeshe tena makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani mwaka 1970, na wakalitwaa tena mwaka 1971 na kama hiyo haitoshi 1972, Yanga wakalitwaa tena.
1973, watani wao Simba wakayarekebisha makosa yao hivyo kuwapokonya, lakini nao walikaa nalo mwaka mmoja tu kwani 1974, Yanga wakalitwaa tena.
Kwa mara ya kwanza taji la Ligi kuu likaondoka jijini Dar es Salaam, baada ya kutwaliwa na timu ya Mseto ya Morogoro mwaka 1975.
Hata hivyo Mseto hawakuwa na ubavu wa kulibakisha tena taji hilo Mji Kasoro bahari, kwani mwaka uliofuata, yaani 1976 taji hilo likatwaliwa na ‘Mnyama', Simba.
Wekundu hao wa Msimbazi waliendelea kulimiliki taji hilo baada ya kulitetea kwa miaka ya 1977, 1978, 1979 na mwaka 1980.
Baada ya kulikosa kwa muda, Watoto wa Jangwani, wakazichanganya vema karata zao na kuwapokonya taji hilo watani zao mwaka 1981.
Mwaka 1982 timu iliyozaliwa kutoka ubavuni mwa Yanga, yaani Pan African nao wakachomoza makucha yao kwa kulitwaa taji hilo.
Mwaka 1983 taji hilo likarudi tena Jangwani kwa Yanga kuwapokonya taji hilo, ingawa nao walikaa nalo mwaka mmoja tu wakapokonywa na Simba 1984.
Mchezo wa kunyang'anyana taji kati ya Simba na Yanga ukaendelea, kwani mwaka 1985, Yanga wakawapoka Simba taji hilo lakini 1986 vigogo hivyo vyote vikatoka kapa baada ya timu ngeni kabisa katika medani ya soka Tanzania, Tukuyu Stars ya Mbeya kulitwaa taji hilo.
Hata hivyo, timu hiyo kama ilivyokuwa kwa Cosmo na Mseto, Tukuyu nayo haikuwa na ubavu wa kushindana na wakongwe Yanga na Simba, kwani mwaka 1987 taji hilo likarejeshwa tena jijini Dar es Salaam likitua Jangwani kwa – Yanga.
Mwaka 1988 kwa mara nyingine taji hilo likaondoka Bandari ya Salama likaenda bandari ya Tanga, likitwaliwa na Coastal Union ya Tanga.
Kama zilivyo timu nyingine za mikoani, Coastal Union nayo haikweza kulitetea taji hilo, bali kuruhusu lirejeshwe Dar es Saalam, ambako lilitua mikononi mwa Yanga, ambayo iliweza kulitetea tena 1989.
Mwaka 1990, Simba iliyokuwa kimya kwa muda, ikafanikiwa kulipeleka kombe Mtaa wa Msimbazi, lakini haikuweza kulishikilia tena mwaka uliofuatia.
Taji hilo likapokwa na Yanga 1991, na kulitetea tena mwaka 1992 na vijana hao wa Jangwani wakadhihirisha ubabe wao kwa kuendelea kulibeba mwaka 1993.
Vijana wa Msimbazi nao hawakukubali unyonge, kwani mwaka 1994 wakalitwaa taji hilo na wakajikakamua na kulitetea mwaka 1995.
Hata hivyo hawakuwa na jeuri ya kuwazuia Yanga wasiwapokonye mwaka 1996, ambao waliweza kukaa nalo kwa miaka mitatu mfululizo, kwani walilitwaa tena miaka 1997 na 1998.
Mkoa wa Morogoro ukajitutumua tena na kulitwaa taji hilo mwaka 1999 lilipokwenda kwa wakata miwa wa Manungu, Mtibwa Sugar, ambayo iliweza kuandika historia ya kuwa timu ya kwanza kutoka nje ya Dar es Saalam kufanikiwa kulitetea taji hilo walipolitwaa pia mwaka
2000.
Mnyama akawapokonya Mtibwa mwaka 2001 na kukaa na taji hilo kwa mwaka mmoja kisha akampisha mtani wake, Yanga aliyelitwaa 2002.
Simba wakalipoka tena taji hilo na kulifungia kwenye makabati yao ya Msimbazi mwaka 2003 na wakaweza kulitetea 2004.
Yanga wakajibu mapigo kwa kulitwaa taji hilo mwaka 2005 na 2006, kabla ya TFF kutangaza mabadiliko ya mfumo wa kuanza kwa Ligi za Tanzania.
Uamuzi huo wa kuzifanya ligi kuanza Agosti badala ya Januari, ulilazimisha kufanyika kwa ligi ndogo ili kupata wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kimataifa ngazi ya klabu, ambako Simba ndio waliofanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi ndogo 2007.
Hivyo ligi ya msimu wa 2007/2008 Yanga wakawahi na kulitwaa taji hilo, kisha wakafanikiwa kulitetea tena katika msimu wa 2008/ 2009, lakini wakachemka 2009/ 2010 walipopokonywa na mtani wao Simba.
Katika kuonyesha kuwa sasa vigogo hivyo vya soka havitaki utani, msimu wa 2010/2011 timu hizo zimejikuta zikibakisha mchezo mmoja zikiwa na pointi sawa, 46 baada ya kucheza mechi 21, hivyo kusubiri mechi za mwisho zilizopigwa jana kumpata bingwa wa msimu wa 2010/2011.
VIONJO
TIMBE - Kocha wa bahati?
Endapo Yanga itafanikiwa kutwaa taji, basi Kocha huyo raia wa Uganda, atazidi kudhihirisha ni kocha wa bahati na mataji, na kuzidi kuiboresha rekodi yake katika klabu mbalimbali alizowahi kuzifundisha kwa mafanikio, ikiwamo Polisi Uganda, Atletico ya Rwanda na mwaka huu alipoipokea Yanga ikiwa imeachwa takriban pointi tano na mtani wake Simba.
PHIRI - Nuksi Msimbazi?
Kocha huyo raia wa Zambia ana rekodi nzuri ndani ya klabu ya Simba, ukiacha vitendo vyake vya mara kadha wa kadha kuicha timu timu hiyo na kurejea kwao kutokana na sababu mbalimbali.
Msimu uliopita aliiwezesha timu hiyo kutwaa taji na kuiongoza vema kwa muda mrefu msimu huu, lakini dakika za majeruhi zinaweza kumtia nuksi na kuchafua mustakabali wake ndani ya klabu hiyo endapo watalikosa taji, hasa ukizingatia kabla ya mechi tatu kumalizika kwa ligi ilikuwa ikiongoza kwa tofauti ya pointi tano, kabla ya kuja kuboronga katika mechi mbili za mwisho na kumpa mwanya mtani wake Yanga kuwapiku.
 
Wajue mabingwa wa Bara tangu 1965
ban.blank.jpg


Ruhazi Ruhazi​

amka2.gif
KINYANG’ANYIRO cha kusaka ubingwa wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara ‘Vodacom Premier League’ (VPL), msimu wa 2010/2011 kilifikia tamati jana kwa mechi kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti.
Mabingwa watetezi Simba walikuwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kupigana kutetea taji hilo.
Historia ya michuano hiyo iliyoanza mwaka 1965 inaonyesha kuwa Simba ndiyo ilikuwa timu ya kwanza kulinyakua kombe hilo ilipolitwaa mwaka huo, lakini wakati huo ilikuwa ikiitwa Sunderland na ikaweza tena kulitetea mwaka uliofuata 1966.
Timu nyingine iliyokuwa ikitamba katika Jiji la Dar es Salaam ya Cosmo Politan, ilijipanga vema na kuweza kulitwaa taji hilo mwaka 1967.
Kutokana na kulikosa taji hilo kwa miaka mitatu ya kwanza, kuliwafanya watoto wa Jangwani, Dar es Salaam Young African ‘Yanga’, kujiuliza sana na mwisho wakapata ufumbuzi wa kile wanachopaswa kukifanya.
Yanga waliweza kukitengeneza kikosi chao vema, ambacho kiliweza kulitwaa taji hilo kwa mara ya kwanza mwaka 1968, lakini ubora wa kikosi chao ukawafanya waweze kulitetea 1969.
Utamu wa kuwa na taji, uliwafanya Yanga walirejeshe tena makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani mwaka 1970, na wakalitwaa tena mwaka 1971 na kama hiyo haitoshi 1972, Yanga wakalitwaa tena.
1973, watani wao Simba wakayarekebisha makosa yao hivyo kuwapokonya, lakini nao walikaa nalo mwaka mmoja tu kwani 1974, Yanga wakalitwaa tena.
Kwa mara ya kwanza taji la Ligi kuu likaondoka jijini Dar es Salaam, baada ya kutwaliwa na timu ya Mseto ya Morogoro mwaka 1975.
Hata hivyo Mseto hawakuwa na ubavu wa kulibakisha tena taji hilo Mji Kasoro bahari, kwani mwaka uliofuata, yaani 1976 taji hilo likatwaliwa na ‘Mnyama’, Simba.
Wekundu hao wa Msimbazi waliendelea kulimiliki taji hilo baada ya kulitetea kwa miaka ya 1977, 1978, 1979 na mwaka 1980.
Baada ya kulikosa kwa muda, Watoto wa Jangwani, wakazichanganya vema karata zao na kuwapokonya taji hilo watani zao mwaka 1981.
Mwaka 1982 timu iliyozaliwa kutoka ubavuni mwa Yanga, yaani Pan African nao wakachomoza makucha yao kwa kulitwaa taji hilo.
Mwaka 1983 taji hilo likarudi tena Jangwani kwa Yanga kuwapokonya taji hilo, ingawa nao walikaa nalo mwaka mmoja tu wakapokonywa na Simba 1984.
Mchezo wa kunyang’anyana taji kati ya Simba na Yanga ukaendelea, kwani mwaka 1985, Yanga wakawapoka Simba taji hilo lakini 1986 vigogo hivyo vyote vikatoka kapa baada ya timu ngeni kabisa katika medani ya soka Tanzania, Tukuyu Stars ya Mbeya kulitwaa taji hilo.
Hata hivyo, timu hiyo kama ilivyokuwa kwa Cosmo na Mseto, Tukuyu nayo haikuwa na ubavu wa kushindana na wakongwe Yanga na Simba, kwani mwaka 1987 taji hilo likarejeshwa tena jijini Dar es Salaam likitua Jangwani kwa – Yanga.
Mwaka 1988 kwa mara nyingine taji hilo likaondoka Bandari ya Salama likaenda bandari ya Tanga, likitwaliwa na Coastal Union ya Tanga.
Kama zilivyo timu nyingine za mikoani, Coastal Union nayo haikweza kulitetea taji hilo, bali kuruhusu lirejeshwe Dar es Saalam, ambako lilitua mikononi mwa Yanga, ambayo iliweza kulitetea tena 1989.
Mwaka 1990, Simba iliyokuwa kimya kwa muda, ikafanikiwa kulipeleka kombe Mtaa wa Msimbazi, lakini haikuweza kulishikilia tena mwaka uliofuatia.
Taji hilo likapokwa na Yanga 1991, na kulitetea tena mwaka 1992 na vijana hao wa Jangwani wakadhihirisha ubabe wao kwa kuendelea kulibeba mwaka 1993.
Vijana wa Msimbazi nao hawakukubali unyonge, kwani mwaka 1994 wakalitwaa taji hilo na wakajikakamua na kulitetea mwaka 1995.
Hata hivyo hawakuwa na jeuri ya kuwazuia Yanga wasiwapokonye mwaka 1996, ambao waliweza kukaa nalo kwa miaka mitatu mfululizo, kwani walilitwaa tena miaka 1997 na 1998.
Mkoa wa Morogoro ukajitutumua tena na kulitwaa taji hilo mwaka 1999 lilipokwenda kwa wakata miwa wa Manungu, Mtibwa Sugar, ambayo iliweza kuandika historia ya kuwa timu ya kwanza kutoka nje ya Dar es Saalam kufanikiwa kulitetea taji hilo walipolitwaa pia mwaka
2000.
Mnyama akawapokonya Mtibwa mwaka 2001 na kukaa na taji hilo kwa mwaka mmoja kisha akampisha mtani wake, Yanga aliyelitwaa 2002.
Simba wakalipoka tena taji hilo na kulifungia kwenye makabati yao ya Msimbazi mwaka 2003 na wakaweza kulitetea 2004.
Yanga wakajibu mapigo kwa kulitwaa taji hilo mwaka 2005 na 2006, kabla ya TFF kutangaza mabadiliko ya mfumo wa kuanza kwa Ligi za Tanzania.
Uamuzi huo wa kuzifanya ligi kuanza Agosti badala ya Januari, ulilazimisha kufanyika kwa ligi ndogo ili kupata wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kimataifa ngazi ya klabu, ambako Simba ndio waliofanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi ndogo 2007.
Hivyo ligi ya msimu wa 2007/2008 Yanga wakawahi na kulitwaa taji hilo, kisha wakafanikiwa kulitetea tena katika msimu wa 2008/ 2009, lakini wakachemka 2009/ 2010 walipopokonywa na mtani wao Simba.
Katika kuonyesha kuwa sasa vigogo hivyo vya soka havitaki utani, msimu wa 2010/2011 timu hizo zimejikuta zikibakisha mchezo mmoja zikiwa na pointi sawa, 46 baada ya kucheza mechi 21, hivyo kusubiri mechi za mwisho zilizopigwa jana kumpata bingwa wa msimu wa 2010/2011.
VIONJO
TIMBE - Kocha wa bahati?
Endapo Yanga itafanikiwa kutwaa taji, basi Kocha huyo raia wa Uganda, atazidi kudhihirisha ni kocha wa bahati na mataji, na kuzidi kuiboresha rekodi yake katika klabu mbalimbali alizowahi kuzifundisha kwa mafanikio, ikiwamo Polisi Uganda, Atletico ya Rwanda na mwaka huu alipoipokea Yanga ikiwa imeachwa takriban pointi tano na mtani wake Simba.
PHIRI - Nuksi Msimbazi?
Kocha huyo raia wa Zambia ana rekodi nzuri ndani ya klabu ya Simba, ukiacha vitendo vyake vya mara kadha wa kadha kuicha timu timu hiyo na kurejea kwao kutokana na sababu mbalimbali.
Msimu uliopita aliiwezesha timu hiyo kutwaa taji na kuiongoza vema kwa muda mrefu msimu huu, lakini dakika za majeruhi zinaweza kumtia nuksi na kuchafua mustakabali wake ndani ya klabu hiyo endapo watalikosa taji, hasa ukizingatia kabla ya mechi tatu kumalizika kwa ligi ilikuwa ikiongoza kwa tofauti ya pointi tano, kabla ya kuja kuboronga katika mechi mbili za mwisho na kumpa mwanya mtani wake Yanga kuwapiku.
 
Hekaheka za waimbaji Tamasha la Pasaka 2011
ban.blank.jpg


Makuburi Ally​

amka2.gif
SIKU 13 kabla ya kufanyika kwa tamasha la kimataifa la muziki wa Injili kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam, CCM Kirumba, Mwanza na Jamhuri Dodoma, maandalizi kwa waimbaji yameshika kasi.
Hili ni tamasha la Pasaka litakaloanzia Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam Aprili 24 na siku itakayofuata, litahamia Jamhuri Dodoma.
Aidha, baada ya waimbaji mahiri wa ndani na nje ya Tanzania kutikisa Dar es Salaam na Dodoma, Aprili 26, itakuwa zamu ya CCM Kirumba, Mwanza.
Kwa mujibu wa kamati ya maandalizi chini ya Mwenyekiti wake, Alex Msama, ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, anasema maandalizi yanakwenda vizuri.
"Maandalizi yanakwenda vizuri, kilichobaki ni kuzidi kuwaombea wote wanaotamani kushuhudia tamasha hili ambalo mgeni rasmi ni Rais wetu mpendwa Jakaya Kikwete," anasema Msama.
Kuhusu waimbaji, Msama anasema tayari wapo kwenye maandalizi ya nguvu kuhakikisha siku hiyo wanatoa burudani ya kiwango cha hali ya juu ili kila atakayefika katika Diamond Jubilee, Jamhuri-Dodoma na Kirumba, asijutie muda wake.
"Kamati yangu imejitahidi kufanya kila iwezalo kuhakikisha tamasha hili linakuwa lenye kiwango cha ubora wa hali ya juu," anasema Msama.
Wakati Msama anayasema hayo, waimbaji nao kwa nyakati tofauti, wamezungumza kwa njia ya simu na kila mmoja ameahidi kufanya vitu vya uhakika katika matamasha yote matatu.
Rose Muhando, malkia wa muziki wa injili wa mwaka 2009, akizungumza kutoka mkoani Dodoma, anasema hawezi kuahidi mengi, isipokuwa wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili, wafike kwa wingi Diamond Jubilee, Jamhuri, Kirumba.
"Unajua, binadamu unaweza ukapanga hivi, lakini Mwenyezi Mungu akapanga vinginevyo…. niseme tu tuombe Mungu alie hai atujalie sote uzima na afya siku hiyo ili tuweze kuifurahia Pasaka kwa namna yake pale Diamond Jubilee.
Muhando ambaye alishirikishwa na Annastazia Mukabwa wa Kenya katika albamu ya ‘Kiatu,' inayotamba vilivyo kwa sasa, anasema Tamasha la Pasaka kwake ni kitu cha kipekee.
Rose aliyetamba na kung'ara na vibao mbalimbali katika anga ya muziki wa injili kikiwemo cha ‘Jipange Sawaswa', anasema ana sababu mbili zinazolifanya tamasha la injili kuwa la kipekee kwake.
Sababu ya kwanza, anasema Pasaka ni alama ya ushindi wa Yesu Kristo dhidi ya dhambi kwa niaba ya wanadamu, hivyo ni fumbo lenye maana kubwa kwa maisha ya kiroho.
Rose anaongeza kuwa, kwa vile Pasaka huadhimishwa mara moja tu kwa mwaka, hivyo uwepo wake katika jukwaa la Diamond Jubilee siku hiyo ni njia mojawapo ya kuisindikiza Pasaka.
"Sababu ya pili inayofanya Pasaka iwe ya kipekee kwangu ni kwamba siku hiyo nitakuwa nikishambulia jukwaa huku nikikumbuka siku ya ubatizo wangu" anasema Rose.
Mwimbaji mwingine aliyezungumzia tamasha hilo ni Mukabwa ambaye kwa sasa anatamba na albamu ya ‘Vua Kiatu' aliyomshirikisha Rose Muhando.
Akizungumza kwa simu kutoka Nairobi, Kenya, Mukabwa amesema tayari alishaanza mazoezi kwa lengo la kutoa burudani ya uhakika siku hiyo mbele ya mkuu wa nchi, Rais Jakaya Kikwete.
Mbali ya kibao cha Kiatu kilichobeba jina la albamu, vibao vingine vilivyomo kwenye albamu hiyo ni ‘Ee Mungu', ‘Tabu zangu', ‘Usiwe Manamba', ‘Nzizilela', ‘Nishike Mkono Bwana' na ‘Wanaokudharau' na Mfalme.
"Naomba Mungu anijalie uzima na afya siku hiyo, mimi binafasi, ninaitamani sana siku hiyo kwa sababu ni heshima ya aina yake kuimba mbele ya mkuu wa nchi, pia kukutana na waimbaji wengine kama dada yangu Rose," anasema Mukabwa.
Kuhusu tamasha, Mukabwa anasema ingawa itakuwa mara ya kwanza kwake kushiriki, anaamini litakuwa lenye mvuto wa aina yake kutokana na uzoefu wa Msama na Kamati yake.
Msama na kamati yake, ndio imechangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa muziki wa injili kupitia matamasha mbalimbali ya Pasaka, Krismasi au uzinduzi wa albamu kadha wa kadha tangu mwaka 2000.
Mwimbaji mwingine aliyezungumzia tamasha hilo na maandalizi yake, ni Solomon Mukubwa, mwimbaji raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo anayeishi nchini Kenya.
Mukubwa ambaye si mara ya kwanza kwake kutumbuiza kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, anasema yupo fiti licha ya kubaki na mkono wake mmoja wa kulia kwani huohuo unatosha kufanya vitu vya kumtukuza Mungu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.
Mukabwa anayetamba na wimbo wa 'Mfalme wa Amani', anasema hiyo ni nafasi muhimu kwake kushirikiana na wengine kushambulia Jukwaa la Diamond Jubilee mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
"Pamoja na kubaki na mkono mmoja, haunizuii kumuimbia Mungu, hivyo wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili waje washuhudie na kupata baraka za Mungu kupitia uimbaji," anasema.
Mukabwa anayekiri kwamba kwenda kwake nchini Kenya ilikuwa ni kumfuata mwimbaji wa nyimbo za Injili Angela Chibalonza ambaye kwa sasa ni marehemu, anaamini kila atakayekuja kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, ataondoka na baraka za Mungu.
Mbali ya Mukabwa aliyetokea familia ya watoto tisa (saba wa kiume), waimbaji wengine watakaopamba tamasha hilo la kimataifa, ni Boniface Mwaitege na Pamela Wanderwa.
Mukabwa aliyemwoa Betty Japheth tangu Machi mwaka jana, ni kati ya waimbaji mahiri wa muziki wa injili katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati wenye mapenzi makubwa na Tanzania.
Mwaitege ambaye kwa sasa aliyewahi kutamba na vibao mbalimbali kama ‘Mke Mwema' na ‘Utamtambuaje' kwa sasa anatesa na albamu yake ya Mama ni Mama iliyojaa vibao vyenye ujumbe wa kuvutia.
Akizungumzia tamasha hilo, Mwaitege amesema hana mengi ya kuzungumza isipokuwa amewataka wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili, kufika Ukumbi wa Diamond Jubilee kusikia ujumbe wa neno la Mungu kupitia vipawa vya uimbaji kutoka kwa waimbaji watakaohudumu siku hiyo.
"Nashukuru kupata nafasi hii ya kuimba kwenye Tamasha kubwa la Pasaka, ni nafasi ya kipekee kwangu kujumuika na waimbaji wengine kufurahia ushindi wa Yesu Kristo pale Msalabani," alisema Mwaitege kwa njia ya simu.
Kuhusu maandalizi, Mwaitege amesema tayari ameshaanza kujipanga kwa ajili ya tamasha hilo kwa lengo la kutoa burudani ya kutosha kwa kadri Mungu atakavyomjalia.
Naye Upendo Nkone ambaye ni kati ya waimbaji watakaopamba jukwaa la Diamond Jubilee mbele ya Rais Kikwete, anasema ni furaha kubwa kwake kujumuika na waimbaji wengine kwenye tukio hilo la aina yake.
Anasema, Pasaka ni alama ya ushindi wa Yesu Kristo dhidi ya dhambi baada ya kuteswa, kufa na kufufuka kwa ajili ya kuwakomboa wanadamu kutoka katika vifungo vya dhambi, hivyo kujumuika na wengine siku hiyo, kwake ni siku ya kipekee.
"Nashukuru sana kupata nafasi hii ya kujumuika pamoja na waimbaji wengine na wananchi kwa ujumla bila kujali kama ni mkristo au vinginevyo kwa sababu sote tu wana wa Mungu," anasema Nkone.
Anasema, anamwomba Mungu amjalie uzima na afya ili siku hiyo aende Diamond kuchota baraka za Mungu kwa sababu wakusanyikapo wawili watatu kwa jina la Mungu, naye huwepo mahali hapo, hivyo Mungu atakuwepo Diamondi Jubilee.
Anasema pamoja na malengo mengine ya uwepo wa tamasha hilo kwa mfano sehemu ya kile kitakachopatikana kuwafariji yatima, wajane na wengine wenye shida, anatoa wito pia kwa kila atakayefika Diamond Jubilee, autumie nafasi hiyo kusamehe wengine.
"Natoa wito kwa wote watakaofika Diamond Jubilee kuwa na furaha pamoja na ufufuko wa Yesgu Kristo kwa kungua mioyo yao kwa kuwasamehe hata wale waliowakosea badala ya kuhama kiti kimoja hadi kingine kumkimbia mwenzako," anasema Nkone.
Christina Shusho kwa upande wake, hakuna na mengi ya kusema isipokuwa amewataka wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili wasikose kwenda Ukumbi wa Diamond Jubilee siku ya Aprili 24 kupata baraka za Mungu kupitia uimbaji.
Amedokeza kuwa, ni furaha kubwa watu kujumuika pamoja wakipata burudani ya nyimbo za kumsifu na kumwinua Mungu kwa matendo yake makuu ya kumleta mwanaye Yesu Kristo kuzifia dhambi msalabani ili wanadamu wapate ukombozi.
Hizi ni kauli za waimbaji waliopo kwenye maandalizi makali ya kufanya mashambulizi kwenye matamasha matatu; kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam; Jamhuri, Dodoma na CCM Kirumba, Mwanza.
Je, viongozi wa kiroho wanayaonaje matamasha haya?
Kwa mujibu wa Askofu wa Kanisa la Mungu mkoani Dodoma, Donald Mhango, anasema matamasha hayo yanaonekana kuwagusa wengi kwani mbali ya kueneza ujumbe wa neno la Mungu kwa njia ya uimbaji, pia sehemu ya mapato kusaidia wenye shida.
Anasema, kusaidia wenye shida kama vile yatima, wajane na waathirika wa mabomu ya Gongo la Mboto, ni jambo jema linalopaswa kuungwa mkono na kuwataka wapenzi na mashabiki wa nyimbo za injili na Watanzania kwa ujumla, kujitokeza kwa wingi.
"Nawasihi wapenzi na mashabiki wote wa muziki wa injili na wananchi kwa ujumla, tujitokeze kwa wingi kushiriki tamasha kama hili la Jamhuri, kwa lengo la kusaidia wenye mahitaji," anasema Askofu Mhango.
Kiongozi mwingine wa kiroho aliyezungumzia matamasha hayo matatu ni Mchungaji wa Kanisa la KKKT mkoani Dodoma, Timothy Holela, aliyetoa pongezi kwa waratibu kuandaa kitu kizuri kama hicho na kuwataka kujitokeza kwa wingi.
Mchungaji Holela anasema anaamini kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Jamhuri, Kirumba na Diamond, kutawafanya waandaaji wa tamasha hilo kufikiria kuendelea na jambo hilo jema na maana kubwa.
Anasema kitendo cha sehemu ya mapato kusaidia wajane, yatima na waathirika wa Gongo la Mboto, ni jambo jema mbele za wanadamu na Mungu.
Zaidi ya hapo, ametoa wito pia kwa Kampuni ya Msama Promotions kufanya matamasha hayo kila mwaka ili kufikisha ujumbe wa neno la Mungu kupitia uimbaji na kusaidia wenye matatizo ambao ni wengi nchini.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi wa matamasha hayo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, Alex Msama, amewashukuru viongozi wa kiroho kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwake.
"Najisikia faraja kubwa kusikia viongozi wa kiroho wakitoa sapoti katika harakati hizi za kamati yangu katika kuandaa matamasha haya ambayo mbali ya kufikisha ujumbe wa neno la Mungu kupitia uimbaji, pia kile kitakachopatikana kwenda kwa wenye makundi maalumu," anasema Msama.
Kuhusu wito wa matamasha hayo kuwa endelevu kwa maana ya kufanyika kila mwaka, Msama anasema lengo ni kufanya kila mwaka, ingawa wakati mwingine wanafanya hivyo katika mazingira magumu kutokana na kuhitaji gharama kubwa.
Anasema unapotumia gharama kubwa kwa maandalizi ikiwamo kuwaalika waimbaji kutoka nje, gharama huwa ni kubwa na ili walau urudishe gharama, unaweza kufikiria kiiingilio kiwe kikubwa, lakini kwa kufanya hivyo, ni wachache watakaomudu.
Waimbaji wa Tanzania ambao wamethibitisha hadi sasa ni Rose Mhando, Upendo Nkone, Bony Mwaitege na Christina Shusho.
Kutoka nje, ni Ephraem Sekeleti wa Zambia, Annastazia Mukabwa, Solomoni Mukubwa na Pamela Wanderwa, wote kutoka Kenya.
Baada ya waimbaji hao kutikisa Diamond Jubilee, siku inayofuata yaani Aprili 25, wote watahamia Uwanja wa Jamhuri, Dodoma kisha kuruka hadi mwanza kwa ajili ya mashambulizi ya nguvu ya hapo Aprili 26, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.
Msama anasema kiingilio cha Diamond ambapo Rais Jakaya Kikwete atakuwa mgeni rasmi, kitakuwa sh 4,000 kwa viti vya kawaida; viti vya maalumu (B) sh 10,000 na viti maalumu (A) sh 20,000.
Kwa tiketi za viti maalumu vya VIP A zitakazokuwa kama meza za familia, watakaohitaji watalazimika kupiga simu selula 0713 383838, 0786 383838 na 0786 373737 kwa ufafanuzi zaidi.
Kwa upande wa matamasha yatakayofanyika Jamhuri na Kirumba, kiingilio kitakuwa cha aina moja ambacho ni sh 3,000 kwa lengo la kuwawezesha wengi kuingia kupata baraka za Mungu kupitia uimbaji na kuwaona ‘live' waimbaji mahiri.
 
Uwanja wa Taifa, wizara inataka hadi JK aseme?
ban.nachonga.jpg


Tullo Chambo​

amka2.gif
KARIBUNI wadau wa safu hii ya Uwanja wa Kuchonga, iwajiayo kila siku kama ya leo, lengo kuu likiwa ni kupeana changamoto za kimichezo kwa ajili ya kuzidisha ufanisi.
Bila shaka mu- wazima wa afya na mnaendelea vema na majukumu ya ujenzi wa taifa, kwa wale ambao kwa namna moja ama nyingine hali si shwari tunawaombea nafuu.
Kabla hatujasonga mbele, haitakuwa haki na uungwana kama hatuwapa pongezi wale wote waliofanikisha ushindi wa timu ya taifa ya soka Tanzania chini ya miaka 23 ‘U-23’ kwa kuanza vema kampeni ya kwenda kwenye Olimpiki huko Uingereza baada ya kuiondosha Cameroon kwa jumla ya mabao 7-6. Hakika juhudi hizi zinapaswa kuenziwa na hata kuongezwa ili kuweza kuandika historia kwa kushiriki kwa mara ya kwanza katika michezo hiyo maarufu duniani.
Wiki iliyopita, nilielezea matuamaini hafifu juu ya maandalizi ya Tanzania kuelekea michezo ya Afrika ‘All Africa Games’ itakayopigwa Septemba nchini Msumbiji, hasa nikiweka bayana kuwa, vyama vingi kama si vyote vinavyotarajiwa kutuwakilisha katika michezo hiyo havina maandalizi, na kama yapo ni ya tia maji tia maji.
Kwa muda uliobaki, ni wazi ilikuwa tayari tunawajua watakaotuwakilisha, wanafanya nini na wanaendelea kufanya nini kuelekea Maputo, Septemba, lakini jambo hilo halipo, bali tunasubiri kuuudanya umma wa Watanzania medali, siku ya kuwaaga wawakilishi wetu watakapokuwa wakielekea huko, kama ambavyo umekuwa utamaduni wetu hivi sasa.
Basi hiyo ndiyo ilikuwa mada yetu ya wiki iliyopita, hivyo ni matuamaini yetu changamoto zimefika kwa wahusika.
Tukijikita katika mada yetu ya leo, Tanzania hivi licha ya mikoa mingi kuwa na matatizo ya miundombinu ya michezo hususan viwanja, lakini serikali ya Awamu ya Tatu, itakumbukwa na wengi, hasa wadau wa michezo, baada ya kuwezesha kujengwa kwa uwanja wa kimataifa wa kisasa jijini Dar es Salaam.
Hiyo ilikuwa ni ahadi ya Rais wa awamu hiyo, Benjamin William Mkapa, ambaye hadharani aliwaambia Watanzania kuwa licha ya kuwa yeye si mnazi wa michezo, lakini atawaachia ukumbusho wanazi wa michezo, nao ni kuwaachia uwanja wa kisasa wa michezo. Na kweli kwa ushirikiano na Watu wa China leo tuna kitu kinaitwa Uwanja wa Taifa.
Bila shaka, nia ya Rais Mkapa wakati huo ilikuwa ni kutaka kuona Watanzania wananufaika na uwanja katika nyanja ya michezo, lakini tangu uwanja huo ukamilike na a kukabidhiwa rasmi kwa serikali Juni 15, 2009, nadiriki na ninaendelea kudiriki kusema kuwa, bado uwanja huo ni mali ya Wachina ambao tumeshirikiana nao katika kuujenga.
Ni wazi uwanja huo hadi sasa unasimamiwa na ndugu zetu hao, huku serikali hivi sasa ikiwa na kitu kinachoitwa msimamizi, ambaye imemteua - ofisa mmoja kutoka wizara yenye dhamana na michezo.
Lakini kimsingi, msimamizi huyo yuko kinadharia sana, wadau wengi wa michezo wanapata taabu sambamba na kudhalilika katika kuutumia uwanja huo, kisa ndugu zetu hao ambao wameamua kabisa hivi sasa kuweka kambi uwanjani hapo.
Katika mada zetu uwanjani, tumewahi kuhoji Uwanja wa Taifa ni mali ya nani? Tumewahi kuonya jinsi ndugu zetu hao wa Kichina wanavyowadhalilisha wadau wetu wa michezo na kuitaka serikali kuchukua hatua au kueleza bayana uwazi na mantiki ya uwanja huo, lakini hakuna kauli ya msingi iliyowahi kutolewa na wahusika.
Imewahi kutokea, wakati mashindano ya riadha ya kitaifa na kimataifa yalipofanyika uwanjani hapo, wataalamu hao wa Kichina kugoma kufungua milango, kutoa vifaa na hata kufikia kuzima taa wakati shughuli zikiwa bado zinaendelea. Hakika kama ukiwahi kushuhudia matendo haya, ni ya kusikitisha na kuhuzunisha.
Kutokana na hali hiyo, wadau wa riadha waliwahi kwa nyakati tofauti kutoa vilio vyao, lakini kwa sababu fulani au kutoonekana msukumo wa umma, hakuna hatua wala matamko maalumu yaliyowahi kutolewa na wahusika.
Lakini wakati ‘kiburi’ cha wahusika wetu kikiwa bado kinaendelea, labda kutokana na kuwa watendwa wanatokea mchezo wa riadha, urasimu huo ukaja kutuumbua mbele ya mkuu wa n chi na hata aibu kusambaa nje ya mipaka yetu.
Wakati Rais Jakaya Kikwete akiwa mgeni rasmi katika mechi ya soka, mchezo pendwa hapa nchini, matatizo yakaanza kwa mitambo ya uwanja huo kushindwa kupiga nyimbo za taifa katika mechi ya Stars na Brazil.
Hilo likapita kwa kufunikwa funikwa, lakini kutokana na kiburi ama sijui tukitafsiri vipi, ufumbuzi wa kudumu hakupatikana na ubabaishaji wa usimamizi na uendeshaji wa uwanja huo ukaendelea, likaja la kutokea tena mbele ya Rais Kikwete, ambapo kwa mara nyingine tena nyimbo za taifa zikagoma katika mechi ya Stars dhidi ya Morocco. Hapo aibu ikawa kubwa na kuwashukia wahusika.
Hapo shughuli ikaanzia, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), wakaanza kushikana uchawi na kuwajibishana, ili kutoa nafasi kwa tume maalumu kuchunguza ili kubaini chanzo cha tatizo na kutoa ushauri ili yasije kutokea tena.
Tunashukuru kamati hiyo ikamaliza kazi yake na kubainisha matokeo, sipendi kuzama ndani katika watendaji wa TFF, lakini ilibainishwa sehemu moja ambayo nadhani ni nyeti kuliko mbeba CD anayetakiwa kuziwasilisha uwanjani hapo, nacho ni chumba cha mitambo, ambako ilielezwa kuna mtaalamu ambaye yeye anajua Kichina tu na ndiye pekee anayeimudu mitambo hiyo! Sijui hapa kama wahusika walipatafakari kwa undani.
Lakini wakati hilo bado likionekana halina maana, hivi karibuni nimepigwa na butwaa kusikia kuwa hata vifaa vya michezo mingine kwenye uwanja huo, hususan vya riadha, hakuna mtaalamu anayeweza kuvisimamia isipokuwa Mchina, ambaye kwa wakati huu yuko nje ya nchi.
Hivyo mchezo wa riadha endapo watataka kutumia vifaa hivyo, itabidi wamsubiri mtaalamu huyo hadi arejee. Hakika inashangaza, tangu Juni 2009 tulipokabidhiwa uwanja huo, hadi leo tunautafuta mwaka tatu, hatuna wataalamu wakuendesha vifaa vya uwanja huo na wizara ipo imetulia. Tusubiri aibu zaidi kama hali yenyewe ndo hii na tusitafutane ‘sisimizi’ wa kumuangushia jumba bovu.
Ni aibu kwa nchi hii ambayo ina wasomi na wataalamu wa nyanja mbalimbali kushindwa kuwa na wataalamu wa kuendesha mitambo ya umeme ya Uwanja wa Taifa au vifaa vya michezo mbalimbali hadi tumsubiri Mchina mmoja atoke anakotoka na ikitokea bahati mbaya akaugua au kusafiri ndiyo basi shughuli imeingia ruba.
Kutokana na mauza uza haya na kutotaka kusubiri la kusubiri kama ilivyokuwa kwenye nyimbo za taifa, ndiko kumenisukuma kutamka tusubiri aibu nyingine Uwanja wa Taifa, kwani naona wahusika hawana uchungu katika haya, sijui hadi waisikie sauti ya Rais Kikwete ikitoa amri kama ilivyokuwa kwenye uvamizi wa viwanja vya Jangwani? Jamani watendaji serikalini, rais amekwisha kusema, kachoka kusema kila siku nyie ni watu wazima.
Kila la heri, tukutane wiki ijayo, wenye masikio na wasikie.
 
Dk. Licky Abdallah, wapenzi wanakulilia
ban.blank.jpg


Kenny Mwaisabula​

amka2.gif
MAKALA yangu ya wiki iliyopita, nilihoji yuko wapi Dk. Licky Abdallah? Maana kimya kimekuwa kikubwa.
Nilitegemea hayo mawazo yalikuwa ni ya kwangu binafsi, kama mtu niliyekuwa nampenda kupita maelezo mtaalamu huyu na kikubwa nilichokuwa namkubali, ni uwezo wake mkubwa wa kuchambua soka na mambo mengi yahusuyo mchezo huo kwa ujumla, lakini nilipata taabu baada ya makala ile kutoka Jumatatu iliyopita.
Simu yangu ilikuwa na wakati mgumu mno, tangu Jumatatu hadi Jumatano, baada ya wapenzi wa soka takriban kutoka sehemu mbalimbali kuisoma makala ile.
Simu na ujumbe, zilikuwa ni nyingi kupita maelezo, kila mtu alikuwa ameshikwa na kigugumizi na kutaka kujua, kweli huyu mtu yuko wapi, mbona kimya mno na wengi wao walikuwa wakinitaka nifanye kila aina ya mbinu, nionane naye na nimwonyeshe hii makala, labda angalau watu wamwone katika makala akiandika.
Kilichonisukuma kuiandika tena makala hii, ni pamoja kufanya kila aina ya jitihada kumtafuta mtu huyu bila mafanikio, pamoja na wadau kunipa namba yake ya simu, lakini nilipiga haikupokelewa asilani na hivyo nikaona ni vema niandike ujumbe tena kwa kuandika ‘sms' zote nilizotumiwa na baadhi ya wapenzi wake, ingawa walionipigia ni wengi kuliko waliotuma ujumbe.
Wa kwanza alikuwa ni mwenye namba 0713 216 056 Edes Kinunda, yeye aliandika; ‘Mzazi mimi ni mpenzi mkubwa sana wa Simba Sports Club, ilifika wakati tulitaka Dk. Licky awe kocha wetu, kwa kweli mwili wote unanisisimka kila nilipokuwa naisoma ile makala yako ya Licky, hivi kweli hata TFF imeshindwa kumtumia mtu huyo? Mzazi we ni kiboko katika makala zako, unatukumbusha mengi,"
Wa pili ni mchezaji wangu wa zamani wa Yanga African, Deo Lucas mwenye namba 0715 274 343; "Shikamoo Mzazi! Nimeisoma makala yako na Dk. Licky, naonana naye ingawa sijamwona kwa sasa mitaa ya City Centre, lakini ntamtafuta nimpe hii makala asome ili arudi tumwone tena ana mambo matamu sana kayafanya, ndiye mwasisi wa wachambuzi wote nchini."
Mwingine wa Songea Mjini mwenye namba 0713 723 684 aliyesema; "Nimeikubali makala yako ya Licky Abdallah, ilipaswa awe mshauri wa soka nchini, anajua sana soka, tafuta namba zake Watanzania tumwombe atoe mchango kwa Taifa, naitwa Sajadi wa Songea."
"Kaka Shikamoo, asante sana makala yako nzuri sana, kwani mimi binafsi nililazimika kununua ‘dishi' mwaka 2005 ili nipate Channel Ten kwa ajili ya Licky tu na si soka lenyewe, Licky alikuwa ni balaa Mzazi, huyu mtu ni hatari mno, ni mimi John Kaswende 0658 877 431 wa Moshi."
Mwenye namba 0712 453 944 Goodluck Justine wa Ubungo River Side, anasema; "Mzazi makala zako zinanitia mshawawasha kila kukicha, lakini hii ya wiki hii ya Dk. ndio imenitia simanzi kuliko maelezo, hivi ni kweli huyu jamaa yuko wapi? Huyu mtu alikuwa ni kichaa wa soka na soka alikuwa analijua, mbona yuko kimya mno? Watanzania tuna muhitaji mno mzazi, tutafutie tumwone."
Mwenye namba 0715 262 308, Kenny,anasema; Unajua umefanya mengi makubwa katika medani ya soka katika miaka yote uliyokuwa mwalimu wa mpira wa miguu, leo umeongeza kitu cha ziada, umetaka wenye vipaji wasife navyo. Dk. Licky Abdallah asifanye hivyo, atumike mpaka pumzi ya mwisho, kona hii yako ikibadilika iitwe kona ya uchambuzi wa michezo na wewe uwe mratibu.
Mwingine 0712 363 522, Habari! Bwana Mwaisabula! Yaani kama ulikuwa kichwani mwangu, wiki nzima iliyopita nimekuwa nikimwazia Dk. Licky kupotea kwake, wengi kunatunyima raha, tatizo hatuna pa kusemea au kuuliza. Hebu waulize Channel Ten au ITV wamekosa nini kuonyesha mipira? maana TBC kaondoka Mhando basi tena. Kadewele.
Naitwa Godwin Masingwa, 0714 102 363 niko Singida ni mpenzi mkubwa sana wa mpira, ulichokiongea bwana Mwaisabula, ndicho Watanzania wengi wapenda mpira tumekikosa muda mrefu kutoka kwa Dk. Licky, tunaomba kama kuna mtu anamfahamu, amwambie Watanzania bado tunahitaji mchango wake kwa udi na uvumba, asikae kimya namna hiyo.
0712 453 944; Hongera sana Mr. Mwaisabula kwa makala yako tamu sana juu ya Dk. Licky, umetugusa wadau wengi sana, nakutakia afya njema na umpate huyo mtaalamu wetu, ambaye wengi tunamhusudu.
Naitwa Aminiel wa Arusha, 0715 797 063, kaka Mwaisabula nashukuru sana kwa kutukumbusha Dk. Licky Abdallah, ukweli huyu bwana hana mpinzani katika uchambuzi wa soka, ni furaha kwetu kama utampa nafasi atukumbushe mengi kwa kupitia makala.
0715 388 517 Big up brother kwa makala yako ya kumuulizia Dk. Licky, mimi binafsi nasononeka kimoyomoyo, niliwahi kuambiwa anapatikana mara kwa mara katika hoteli fulani kule Kariakoo, nikaenda nikaambiwa alikuwa amekwenda Dubai, nikakata tamaa ya kumwona, kweli Dk. Licky ni kama wa Loliondo wa soka, tunamkubali sana.
Mwingine ni swahiba wangu, mwana makala mwenzangu, Markus Mpangala; ‘Mzazi heshima yako, yaani kichwa cha makala yako kimenikumbusha jinsi mwaka jana nilivyomlilia sana mzee huyo, yupo kimya mno na sote tulikuwa tunamkubali.
Naitwa Bakari Fungo wa Morogoro, 0715 388 143, Coach Mwaisabula hakika umenena juu ya Dk. Licky Abdallah, familia ya soka tunamhitaji sasa kuliko hapo mwanzo, atafutwe popote pale alipo tunamuhitaji mno.
Joseph John wa Vingunguti, 0713 242 499, Dk. Licky tuna mengi ya kujifunza na kujua toka kwako, iwe kwa njia ya radio au tv au kwa mawasiliano yeyote ya kwako, hasa kwa sisi walalahoi, tunaomba ujitokeze mashabiki wako bado tuna kuhitaji mno.
Naitwa Apollo Ndali, 0713 378 068 kiongozi wa chama cha mpira wa miguu Tabora, naungana na wewe kuwa, Dk. Licky arudi kwenye Tv atupe raha na pia TFF Taifa wamshirikishe hata kwenye kamati ya ligi kuu mwaka ujao ni mtu muhimu sana, jamii bado inamhitaji.
Namalizia kwa mtu anayeitwa Burton Mbajo, yeye aliniandikia kupitia barua pepe yangu, alianza kwa kusema; Makala yako ya Jumatatu Aprili 4, 2011 kwenye gazeti la Tanzania Daima, imenifanya nikuandikie japo nikupongeze kwa mtazamo wako wa kimichezo zaidi, hasa kumkumbuka mchambuzi huyo Dk. Licky.
Ni nadra sana kwa mchambuzi wa masuala fulani kumkubali mwenzie wa fani hiyo hiyo, na ikibidi kumwachia nafasi yako katika gazeti hilo ni jambo la kiungwana sana na hilo ndilo litakalotufanya makala zako tupende zaidi kuzisoma.
Hapa suala si kumpisha Licky, bali ni kuomba vyombo vya habari kumpa nafasi aweze kutupatia kile anachokijua katika michezo, hususan mpira wa miguu, ningependa kukuomba kuwa, ukiweza tafuta anuani yake ya barua pepe, umwandikie moja kwa moja, kwani yawezekana gazeti asisome hizi makala unazoziandika, binafsi nikiipata nitakutumia ili uwasiliane naye, nadhani kwako ni vizuri zaidi kuliko nikimwandikia mimi au wa kariba yangu.
Sielewi kwa nini vituo vya runinga kama Star TV au TBC hawapendi kumualika kuchambua kwenye michezo, hivi hawahisi kuwa wapenzi tunamhitaji mno Dk Licky kwa uchambuzi wake.
Nakubaliana na wewe kwamba, wengi wanamkubali na hata wasiomwamini hupenda kumsikiliza na kwenda kuthibitisha uongo wake kwenye vyanzo mbalimbali vya habari na kwa kufanya hivyo, wanaongeza hazina ya ufahamu vichwani mwao.
Namalizia kwa kukupongeza bwana Mwaisabula na kukutakia kila la heri katika shughuli zako za kila siku.
Dk. Licky Abdallah, Watanzania wanakuhitaji mno, katika kuwaelimisha mambo yahusuyo soka.


h.sep3.gif

Mwandishi wa makala hii ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Kitengo cha Uhandisi. Anapatikana kwa simu: 0652 875 794, email: kennymwaisabula@yahoo.com.
 
Makinda awavunja mbavu wabunge

Imeandikwa na Basil Msongo, Dodoma; Tarehe: 11th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 260; Jumla ya maoni: 0








SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, leo amwavunja mbavu wabunge wakati anawatangaza viongozi wa klabu ya michezo ya wabunge waliyochaguliwa Jumamosi mjini Dodoma.

Kamati ya Ufundi ya klabu hiyo ndiyo iliyoanza kuwavunja mbavu wabunge kwa kuwa wajumbe wake wanatoka katika maeneo yanayoaminika kuwa yamekithiri vitendo vya ushirikina.

Wabunge waliangua vicheko wakati Makinda akianza kuwataja wajumbe hao akiwemo Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu kwa jina la Profesa Majimarefu, kutoka Tanga, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa kutoka Bagamoyo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), Hawa Ghasia anayetoka mkoani Mtwara.

Wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Mbunge wa Sumbawanga Mjini, Khalfan Hilal Aeshi, Mbunge wa Wete, Khalifa Khalifa kutoka Pemba, Mbunge wa Viti Maalum, Maria Hewa kutoka Mwanza na Mtutura Mtutura kutoka Tunduru.

Kwa mujibu wa Spika wa Bunge, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutoka Sumbawanga mkoani Rukwa ndiye Mlezi wa Kamati ya Ufundi na timu ya wabunge.

Kwa mujibu wa Makinda, wanachama wa klabu hiyo, wamemchagua Mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan kuwa Mwenyekiti wao, Mbunge wa Mvomero, Amos Makalla amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti.

Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mnyaa amechaguliwa kuwa Msimamizi Mkuu wa Mazoezi, na Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Kassim Majawaliwa amechaguliwa kuwa Kocha wa timu ya mpira wa miguu.

Wanachama wa klabu hiyo pia wamewachagua wajumbe wa Kamati ya Utendaji akiwemo waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Mnyaa, Mkiwa Kimwaga, Mwanahamisi Said na Betty Machangu.
 
Yanga raha mustarehe

Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 11th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 159; Jumla ya maoni: 0








MABINGWA wapya wa soka Tanzania Bara timu ya Yanga waliwasili Dar es Salaam Jumatatu wakitokea Mwanza walipoutwaa ubingwa huo Jumapili, baada ya kuifunga Toto Africans mabao 3-0, huku Kocha Mkuu Sam Timbe akisema mawazo yake ni ubingwa wa Afrika mwakani.

Msafara wa wachezaji wa timu hiyo uliwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
saa saba mchana ambapo ulikwenda moja kwa moja makao makuu ya klabu hiyo, mtaa wa
Twiga na Jangwani.

Akizungumza baada ya kufika klabuni hapo ambako walikuta umati wa mashabiki wa Yanga
ukiwasubiri, nahodha wa timu hiyo Shadrack Nsajigwa alisema ligi ilikuwa ngumu, lakini
wamepigana mpaka dakika ya mwisho na kutwaa ubingwa.

"Tunashukuru tumetwaa ubingwa, ligi ilikuwa ngumu sana, sasa kilichobaki ni kujipanga kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa kwani Yanga hatuna rekodi nzuri,"alisema.

Alisema kingine wanachokifanyia kazi kwa sasa ni kuhakikisha wanabakisha kombe msimu
ujao na kurejesha heshima ya Yan-ga ambayo imepotea kwa muda mrefu.

"Tutalifanyia kazi hilo, tunataka kubakisha kombe mwakani ili kurudisha heshima ya Yanga maana ilikuwa imepotea," alisema.

Naye Mwenyekiti wa Yanga, Llyod Nchunga alisema ubingwa uliopatikana ni wa Wanayanga wote hivyo kila mmoja ana haki ya kuusherehekea.

"Sisi kama uongozi tunaanza kufanya maandalizi ya usajili mapema, ili tupate kikosi bora kitakachoweza kutetea ubingwa msimu ujao," alisema.

Kwa ujumla mapokezi hayo yalilakiwa na maelfu ya mashabiki na wanachama wa timu hiyo ambao walionekana wenye furaha wakiimba na kucheza wimbo wa mwanamuziki gwiji wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Hayati Kabasele Yampanya (Pepe Kalle) wa Young
Africans.

Yanga ilitwaa ubingwa huo kwa tofauti ya bao 1 dhidi ya mtani wake Simba iliyokuwa bingwa mtetezi ambayo katika mechi yake ya mwisho dhidi ya Majimaji iliibuka na ushindi wa mabao 4-1.

Lakini ilishindwa kutetea taji kwani ilikuwa na faida ya mabao 24 huku Yanga ikiwa na faida ya mabao 25, zote zikiwa na pointi 49.

Naye David Azaria anaripoti kutoka Mwanza kuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Sam Timbe amesema baada ya kikosi chake kutwaa ubingwa na sasa anafanya mkakati kuhakikisha klabu hiyo inatwaa mataji mengine, ikiwemo lile la klabu bingwa Afrika ambalo itacheza mwakani.

Akizungumza Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza mara baada ya mchezo na Toto Jumapili, Timbe alisema kuutwaa ubingwa huo ni jambo moja, lakini la pili ni kuhakikisha anaisuka Yanga ili kutwaa mataji mengine ikiwemo ubingwa wa Afrika.

Alisema mashindano ya msimu huu yalikuwa magumu na ndiyo maana hata wao wameuchukuwa ubingwa kwa tofauti ya idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa na kuwa Simba haikuwa imejipanga kuuchukua ubingwa.

"Wakati naichukua timu hii, Simba walikuwa kwenye nafasi nzuri sana ya kuuchukua ubingwa, lakini kadri muda ulivyokuwa ukienda walikuwa wanajichanganya na kuzidi kutupatia nafasi, na sisi pia tulitumia hesabu kali kuhakikisha tunautwaa huu ubingwa, tunashukuru Mungu ametusaidia ," alisema.
 
Nyota 15 kufukuzwa Simba

Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 11th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 259; Jumla ya maoni: 0








BAADAya kupoteza ubingwa wa soka Tanzania Bara, sasa Simba hali si shwari tena.

Habari za kuaminika zilizopatikana Dar es Salaam Jumatatu kutoka kwa mmoja wa viongozi wa juu wa timu hiyo, zinasema kuwa uongozi umeamua kulifumua benchi lote la ufundi ikiwa ni pamoja na kuwapiga panga wachezaji 15.

Kiongozi huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema uongozi umeona bora kufanya hivyo ili kuinusuru timu ambayo ilikuwa na kila dalili ya kutetea ubingwa wake lakini ikashindwa kufanya hivyo katika mechi mbili za mwisho.

Simba imekosa ubingwa kwa tofauti ya bao moja dhidi ya Yanga ambapo zote zilifungana pointi kwa kufikisha pointi 49 lakini Yanga ikiwa na faida ya mabao 25 na Simba 24.

"Kuna vitu vingi sana uongozi umevigundua, kwa baadhi ya wachezaji kujiamini na kufanya kila wanalotaka wao kwa faida yao... na baada ya kuangalia kwa kina wameona ni bora wawaache watafute timu nyingine za kucheza," alisema.

"Uongozi umegundua kuwa kuna watu wapo kwa ajili ya maslahi yao na si ya timu hiyo, basi ni bora tuwaache wafanye mambo yao na kwenda kucheza timu wanazotaka wao," alisema.

Alisema kuna baadhi ya wachezaji wamekuwa wakifanya vitu tofauti na mikataba yao bila kujali na kutambua kwamba mpira ndio unaendesha maisha yao ya kila siku.

"Tutawaacha wachezaji 15, bado tutakuwa na vikao vya hapa na pale kidogo lakini lazima
tuwaache… si kwa wale ambao mikataba yao imekwisha, hata ambao hawajamaliza mikataba tutaivunja," alisema kiongozi huyo kwa hasira.

"Tutavunja mikataba ya wachezaji wanne ambao walikuwa bado wamebakiza mwaka mmoja ili tuweke timu sawa na kuondoa kirusi kilichopo ndani ya timu, inaelekea kila msimu tutaendelea kufanya hivi hivi kama tutaendelea kuwa nao,"alisema.

Kiongozi huyo hakuwa tayari kuwaweka hadharani wachezaji hao lakini habari zinadai
kuwa baadhi ya watakaotupiwa virago ni Mussa Hassan Mgosi, Kelvin Yondani na Mohamed Banka.
 
Kaseja, Mwasika waenguliwa Stars

Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 11th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 120; Jumla ya maoni: 0








KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars Jan Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji watakaocheza mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Msumbiji huku akimuacha kipa namba moja wa Simba Juma Kaseja pamoja na Stephano Mwasika wa Yanga.

Lakini kocha huyo amemwita tena Kaseja kwenye kikosi kitakachocheza na Afrika ya Kati Juni 4 katika mechi ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika mwaka 2012.

Hata hivyo kocha Poulsen hakusema sababu za kumuacha Kaseja safari hiyo ya Msumbiji ila alimzungumzia Mwasika kwamba anaonekana hayuko sawa kwa sasa nay eye kama kocha anayo nafasi ya kuchagua mchezaji mwingine.

Aidha, mbali na mechi dhidi ya Msumbiji itakayochezwa Maputo Aprili 23, Stars pia itacheza mechi ya kirafiki na timu ya soka ya taifa ya Afrika Kusini 'Bafana Bafana' Mei 14 kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Taifa Stars inatarajia kwenda ugenini kuivaa Msumbiji kwa mualiko maalumu kutoka nchini humo kwa ajili ya ufunguzi wa uwanja mpya wa kisasa uliokamilika kujengwa hivi karibuni.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kocha Poulsen alisema, mechi zote hizo mbili zinachezwa kwa ajili ya kuiandaa timu yake na mchezo wa marudiano dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati unaotarajiwa kuchezwa Juni 4.

Poulsen alisema, katika kujiandaa na mechi dhidi ya Msumbiji, wachezaji 18 aliowaita bila ya nyota wanaocheza soka ya kulipwa wataingia kambini Ijumaa baada ya kupata mapumziko ya siku nne baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara juzi.

Alisema kuwa baada ya kutoka Msumbiji, Taifa Stars itaingia tena kambini Mei 2 ili kujiwinda na mechi dhidi ya Bafana Bafana.

"Pia tunatarajia kucheza mechi nyingine mbili za kirafiki za kimataifa kati ya Mei 22 na 28, ratiba inaonyesha Taifa Stars itakuwa inaingia kambini mara kwa mara kwa ajili ya kuwaweka imara wachezaji kwa sababu muda huu hawatakuwa na mechi za ligi," alisema kocha huyo.

Aidha alisema, wachezaji katika timu hiyo watakuwa wanabadilika kutokana na uwezo na upatikanaji wao hasa wale wanaocheza nje ya nchi kufuatia ratiba zao zitakavyokuwa.

Aliwataja wachezaji watakaoivaa Msumbiji kuwa ni Makipa Shabani Kado na Shabani Dihile; mabeki ni Shadrack Nsajigwa, Aggrey Morris, Nadir Haroub 'Cannavaro', Amir Maftah, Juma Nyosso, Kigi Makasi; viungo ni Nurdin Bakari, Shabani Nditi, Jabir Aziz, Ramadhani Chombo,' Redondo' na Mwinyi Kazimoto.

Wengine ni washambuliaji Salum Machaku, Mrisho Ngassa, Mohammed Banka, John Bocco na Mbwana Samatta. Aliongeza kuwa wachezaji wanaocheza nje ambao wataungana na wenzao kuivaa Jamhuri ya Kati hapo Juni, mbali na Juma Kaseja, ni Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya),
Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Abdi Kassim, Danny Mrwanda DT Long An, Vietnam), Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada) na Athumani Machuppa (Vasalund IF, Sweden).
 
Fabiani Joseph, Mary Naali wang'ara Ngorongoro

Imeandikwa na Na John Mhala, Karatu; Tarehe: 11th April 2011 @ 13:10 Imesomwa na watu: 63; Jumla ya maoni: 0



Habari Zaidi: Makinda awavunja mbavu wabunge
Yanga raha mustarehe
Nyota 15 kufukuzwa Simba
Kaseja, Mwasika waenguliwa Stars
Fabiani Joseph, Mary Naali wang'ara Ngorongoro
Odour, Ntaboba kukamua Pasaka
Yanga bingwa 2010/11
Wadau waitwa Tamasha la Utamaduni Moro
Wasanii kuimba wimbo kuhamasisha amani
Diamond, Tundaman kupagawisha Mzumbe
Extra Bongo wapata ajali
Ni hofu Simba, Yanga
Vijana Stars yaingia 16 Bora Olimpiki
Simba, Yanga zaonywa
Wachezaji 26 waitwa kuunda Twiga Stars
Vijana Stars kibaruani Jumamosi
Kombe la Andengenye kuanza Arusha Jumamosi
Sekeleti, Mukubwa kutua Dar es Salaam wiki ijayo
Utata umiliki wa studio aliyoitoa JK wafika bungeni
Wachezaji Simba wadaiwa kuhujumu

Habari zinazosomwa zaidi: Balaa lingine kwa Chenge
Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
‘Housigeli' anataka kuniharibia ndoa
Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
Vatican yamvua jimbo Askofu
Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
MWANARIADHA Fabiani Joseph (24) wa klabu ya riadha ya mjni Arusha ya (WSAC) juzi alijinyakulia zawadi ya Sh 500,000 baada ya kushika nafasi ya kwanza katika mbio za Nusu
Marathon zijulikanazo kwa jina la ‘Ngorongoro Run zilizofanyika katika mji wa Karatu mkoani Arusha.

Joseph alishinda mbio hizo baada ya kutumia muda wa saa 1: 04.36 na nafasi ya pili ilinyakuliwa na mwanariadha Samsoni Ramadhani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ambaye alitumia muda wa saa 1;05;31 na kujinyakulia zawadi ya shilingi 300,000.

Ramadhani mwaka 2010 alishika nafasi ya kwanza katika mbio hizo. Nafasi ya tatu ilinyakuliwa na Faustine Mussa wa JWTZ ambaye alitumia muda wa saa 1: 05.58 na kujinyakulia zawadi ya Sh 150,000.

Kwa upande wa wanawake nafasi ya kwanza ilinyakuliwa na Mary Naali wa klabu ya Skytel ya
mjini Arusha aliyetumia muda wa saa 1:16;37 na kujinyakulia zawadi ya Sh 300,000.

Nafasi ya pili ilinyakuliwa na Siata Ramanus wa JWTZ ambaye alitumia muda wa saa 1;29;06 na kupewa Sh 150,000 na nafasi ya tatu ilinyakuliwa na Anastazia Msandawe aliyetumia muda wa saa 1:20;12 na kupata zawadi ya Sh 100,000.

Kwa upande wa watoto walioshiriki mbio za kilometa tano, nafasi ya kwanza alikuwa Edsward
Leopard ambaye alipata Sh 50,000 nafasi ya pili ilinyakuliwa na Emanuel Gabriel aliyepata Sh 20,000 na nafasi ya tatu ilishikwa na Yohani Elisante aliyepata Sh 10,000.

Mratibu wa mashindano hayo mwanariadha wa zamani, Filbert Bayi aliwashukuru wadhamini wa mbio hizo kwa kushiriki kikamilifu kufanikisha mbio hizo mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi, mgeni rasmi katika mbio hizo Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige aliwataka waratibu wa mbio hizo kuiboresha zaidi zawadi ili mbio ziwe za ushindani zaidi.

Mbali ya hilo pia Waziri Maige alilitaka Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kujitokeza mwakani kudhamini mashindano hayo na kuboresha zawadi zaidi kwa washindi.

Waziri huyo aliwasifu waratibu wa mbio hizo kwa kuwa na kauli mbiu ya kupiga vita malaria kwani ugonjwa huo unaua mamia ya watu kwa sasa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom