Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,508
- 911,249
- Thread starter
- #13,281
Mukubwa: Mkono mmoja haunizuii kufunika Pasaka
na Mwandishi wetu
KATIKA tamasha la Pasaka mwaka 2010 lililopambwa kwa muziki wa Injili kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, nyoyo za mashabiki zilikongwa na waimbaji kochokocho waliotumbuiza.
Hata hivyo, kivutio kikubwa walikuwa ni mwimbaji wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo anayeishi Kenya, Solomon Siaka Mukubwa na Rose Muhando, ambao mara kwa mara kelele za mashabiki zilisikika wakitaka kila mmoja aendelee kuwapa burudani.
Mbali ya Rose Muhando ambaye wimbo wake wa Nibebe uliteuliwa kuwa Wimbo Bora wa Mwaka 2009 kupitia televisheni ya Taifa, TBC1 na Mukubwa, wasanii wengine walioshiriki ni Flora Mbasha na Upendo Nkone.
Waimbaji wengine ni Bahati Bukuku, Jennifer Mgendi, Geraldine Oduor, Enock Jonas na kundi la muziki wa Injili la Upendo la Kijitonyama, Dar es Salaam.
Mukubwa na Rose ndio waliokuwa kivutio zaidi kutokana na kushangiliwa kwa nguvu.
Mukubwa alisema hamasa aliyoipata mwaka jana ndiyo inampa msukumo zaidi wa kuendelea kukonga nyoyo za mashabiki katika tamasha la mwaka huu.
Tamasha la mwaka huu litafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Aprili 24 mwaka huu, kisha litarindima kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 25 na kisha kutibwirika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza Aprili 26 ambayo itakuwa Sikukuu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema kwa vile tamasha la mwaka jana lilikuwa la mafanikio makubwa, anaamini hata mwaka huu watavuka malengo ya kukusanya fedha kwa ajili ya watoto yatima, kuwasaidia mitaji ya biashara wajane wasiojiweza na waathirika wa mabomu yaliyotokea kambi ya JWTZ Gongo la Mboto, Dar es Salaam, Februari 16.
Mukubwa ni mlemavu wa mkono wa kushoto ambapo kwa mujibu wa maelezo yake, ulitokana na kufanyiwa vitendo vya kishirikina.
Anasema akiwa na miaka 12 alipata matatizo hayo kwa kutokea uvimbe wa ajabu na hakuna aliyejua tatizo lililomsumbua.
Kwa mantiki hiyo, alifikia uamuzi wa kukatwa mkono kwa vile ulikuwa umeharibika.
Mukubwa ametoa albamu mbili ambazo ni ‘Sijaona Rafiki' na ‘Mungu Mwenye Nguvu'.
Alisema mkono huo aliokatwa haumzuii kumuimbia Mungu.
Mbali ya Mukubwa, wengine watakaoshiriki tamasha la Pasaka mwaka huu, ni mwimbaji wa muziki wa Injili kutoka Zambia, Ephraim Sekeleti. Mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Kiingilio katika tamasha hilo kitakuwa sh 4,000 kwa viti vya kawaida, viti maalumu (B) sh 10,000 na viti maalumu (A) sh 20,000. Tiketi za kategoria hiyo hazitauzwa mlangoni.
Wasanii wengine wa nyimbo za injili watakaopamba tamasha hilo
ni Rose Muhando, Upendo Nkone, Bony Mwaitege na wanamuziki kutoka Kenya, Anastazia Mukabwa na Pamela Wanderwa.
Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi sita ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Afrika Kusini na Zambia. Pia kutakuwa na kwaya mbili kutoka katika nchi
hizo.
na Mwandishi wetu
Hata hivyo, kivutio kikubwa walikuwa ni mwimbaji wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo anayeishi Kenya, Solomon Siaka Mukubwa na Rose Muhando, ambao mara kwa mara kelele za mashabiki zilisikika wakitaka kila mmoja aendelee kuwapa burudani.
Mbali ya Rose Muhando ambaye wimbo wake wa Nibebe uliteuliwa kuwa Wimbo Bora wa Mwaka 2009 kupitia televisheni ya Taifa, TBC1 na Mukubwa, wasanii wengine walioshiriki ni Flora Mbasha na Upendo Nkone.
Waimbaji wengine ni Bahati Bukuku, Jennifer Mgendi, Geraldine Oduor, Enock Jonas na kundi la muziki wa Injili la Upendo la Kijitonyama, Dar es Salaam.
Mukubwa na Rose ndio waliokuwa kivutio zaidi kutokana na kushangiliwa kwa nguvu.
Mukubwa alisema hamasa aliyoipata mwaka jana ndiyo inampa msukumo zaidi wa kuendelea kukonga nyoyo za mashabiki katika tamasha la mwaka huu.
Tamasha la mwaka huu litafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Aprili 24 mwaka huu, kisha litarindima kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 25 na kisha kutibwirika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza Aprili 26 ambayo itakuwa Sikukuu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema kwa vile tamasha la mwaka jana lilikuwa la mafanikio makubwa, anaamini hata mwaka huu watavuka malengo ya kukusanya fedha kwa ajili ya watoto yatima, kuwasaidia mitaji ya biashara wajane wasiojiweza na waathirika wa mabomu yaliyotokea kambi ya JWTZ Gongo la Mboto, Dar es Salaam, Februari 16.
Mukubwa ni mlemavu wa mkono wa kushoto ambapo kwa mujibu wa maelezo yake, ulitokana na kufanyiwa vitendo vya kishirikina.
Anasema akiwa na miaka 12 alipata matatizo hayo kwa kutokea uvimbe wa ajabu na hakuna aliyejua tatizo lililomsumbua.
Kwa mantiki hiyo, alifikia uamuzi wa kukatwa mkono kwa vile ulikuwa umeharibika.
Mukubwa ametoa albamu mbili ambazo ni ‘Sijaona Rafiki' na ‘Mungu Mwenye Nguvu'.
Alisema mkono huo aliokatwa haumzuii kumuimbia Mungu.
Mbali ya Mukubwa, wengine watakaoshiriki tamasha la Pasaka mwaka huu, ni mwimbaji wa muziki wa Injili kutoka Zambia, Ephraim Sekeleti. Mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Kiingilio katika tamasha hilo kitakuwa sh 4,000 kwa viti vya kawaida, viti maalumu (B) sh 10,000 na viti maalumu (A) sh 20,000. Tiketi za kategoria hiyo hazitauzwa mlangoni.
Wasanii wengine wa nyimbo za injili watakaopamba tamasha hilo
ni Rose Muhando, Upendo Nkone, Bony Mwaitege na wanamuziki kutoka Kenya, Anastazia Mukabwa na Pamela Wanderwa.
Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi sita ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Afrika Kusini na Zambia. Pia kutakuwa na kwaya mbili kutoka katika nchi
hizo.
PRINT