Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Simanzi, majonzi vyatawala mazishi Five Stars


Na Addolph Bruno

SIMANZI, vilio na majonzi ziliendelea tena jana kwa mashabiki wa taarabu katika jiji la Dar es Salaam wakati wa maziko ya wasanii wa Kundi la taarabu la
Five Stars waliopata ajali na 13 kufariki Dunia ambao baadhi yao walizikwa juzi usiku na wengine jana mchana.

Baadhi ya wasanii hao ambao walifariki katika ajali iliyotokea katika eneo la Duma ndani ya Hifadhi ya Mikumi, wakitokea Songea walizikwa kwa nyakati tofuati kutokana na miili yao kuharibika vibaya ambao wengine walizikwa Dar es Salaam na wengine katika Mkoa wa Pwani.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kiongozi wa bendi hiyo anayefahamika kwa jina la Ally Juma 'Ally J' alisema miili ya wasanii wawili iliyohalibika vibaya katika ajali hiyo, Issa Kijoti na Omary Hashim walizikwa usiku wa kuamkia jana ambapo Kijoti alizikwa nyumbani kwao Mtoni kwa Azizi Ally, Dar es Salaam na Omary alizikwa nyumbani kwao Kibaha mkoani Pwani.

Kiongozi huyo ambaye ni baadhi ya sehemu ya wasanii walionusurika katika ajali hiyo alisema mazishi ya wasanii hao yaliendelea kufanyika jana ambapo miili ya wasanii wengine watatu, ilizikwa kwa nyakati tofauti Jijini Dar es Salaa na Pwani.

Alisema wasanii waliozikwa katika mkoa wa Pwani ni aliyekuwa mpiga kinanda wa kundi hilo, Tizo Mgunda na mwimbaji Hamisa Omary ambao walizikwa jana asubuhi vijiji viwili tofauti mkoani Pwani ambako ni nyumbani kwa wasanii hao.

Ally J alisema Mgunda alizikwa katika kijiji cha Mkamba huku Hamisa yeye alizikwa katika Msongola vilivyomo katika Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.

"Baada ya kutoka Pwani, kulikuwa na mazishi ya msanii mwingine Juma seba, naye amezikwa leo (jana) katika makaburi ya Madoto Mburahati hapa Dar es Salaam ambapo viongozi mbalimbali wa bendi tulijumuika katika mazishi hayo na sasa bado tunaangalia taratibu za wengine baada ya familia kupanga," alisema kiongozi huyo.

Msanii mwingine wa kundi hilo, Hammer Q alizungumzia kwa uchungu ajali hiyo iliyotokea baada ya yeye kuachwa njiani akisafiri kwa basi kwa kusema vifo vya wasanii hao ni pengo kubwa katika bendi hiyo na kwamba itachukua muda kusahaulika.

Mjomba wa marehemu Kijoti, Lugendo Somo alisema familia yao ipo katika kipindi kigumu baada ya kuondokewa na msanii huyo ambaye alikuwa tegemeo katika familia yao na kwamba watafanya hitima kesho asubuhi na kufuatiwa na sadaka nyumbanii kwao Mtoni kwa Azizi.

Alisema kutokana kifo hicho kilichosababishwa na ajali ya ghafla, familia yao imekaa na kuamua kufanya mapema hitima kumaliza shughuli za msiba huo baada ya hitima ya wasanii wote iliyoandaliwa na Baraza la wasanii iliyopangwa kusomwa leo.

Naye Dada wa marehemu Tizo Mgunda, aliyejitambulisha kwa jina la Halima Mgunda alisema familia yao imepokea kwa masikitiko kifo cha msanii huyo kutokana na kwamba alikuwa tegemeo katika familia yao na kuongeza kuwa amewaacha watoto wawili mmoja wa kike na mmoja wa kiume.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa bendi ya muziki wa dansi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Asha Baraka, alisema katika tasnia ya muziki wa taarabu wamepata pengo kubwa ambapo kuliziba itachukua muda mrefu.

Alisema wamepoteza watu maarufu katika muziki huo hivyo ni vigumu kupata watu wanaofanana na wale waliopata ajali kwa ajili ya kuziba nafasi zao.

Alisema kuwa kupeteza maisha kwa wasanii hao kutafanya muziki huo kutokuwa na ladha kutokana na ushindani uliokuwepo kati ya Five Stars na Jahazi.

´´Tumepoteza watu muhimu katika muziki wa taarabu na pengo lao halitazibika mapema na ushindani katika muziki huo utakuwa mdogo sana kutokana na kupeteza wasanii wengi kwa wakati mmoja, tunaomba tutoe ushirikiano wa kutosha kwa ajili ya kuwapa moyo na kuwafariji ndugu wa marehemu,´´ alisema Asha.
 
Wanachama Yanga waendelea kuvutana


Na Elizabeth Mayemba

MKUTANO wa viongozi wa matawi wa Yanga, uliokuwa ufanyike juzi makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya Twiga na Jangwani, ulishindwa kufanyika baada ya
kutokea mvutano baina ya wanachama hao ambao wengine walitaka ufanyika lakini wengine walikataa na hivyo ukavunjika.

Awali Katibu wa tawi la Uhuru, Dar es Salaam Edwin Kaisi alisema mkutano huo ajenda yake kubwa ilikuwa ni kumjadili Mwenyekiti wa matawi Mkoa wa Dar es Salaam, Mohammed Msumi juu ya utendaji wake ikiwemo na kukaa madarakani kwa muda mrefu.

Habari zilizopatikana Dar es Salaam jana kutoka kwa mmoja wa viongozi wa Yanga, zinadai kuwa mkutano huo ulivunjika baada ya kutokea mabishano baina ya wanachama hao, kwa madai kwamba ulilenga kuleta vurugu ndani ya klabu yao.

"Kabla ya kuanza kwa mkutano kuliiibuka mabishano, ambapo baadhi ya wanachama walidai kwamba hawatakubali kuona mkutano huo unafanyika kwani ulilenga kuhatarisha amani ndani ya klabu hiyo, hasa kipindi hiki ambacho timu yao inakabiliwa na mechi tatu za Ligi Kuu ya Bara mzunguko wa lala salama," alisema kiongozi huyo ambaye aliomba kuhifadhiwa jina lake kwa kuwa si msemaji wa viongozi wa matawi.

Alisema baada ya mabishano hayo, mkutano huo ukavunjika na kila mwanachama akatawanyika.

Kwa upande wake Kaisi ambaye ndiye aliitisha mkutano huo, alisema kwamba walishindwa kufanya mkutano huo baada ya Kamati ya Utendaji ya matawi kuingia mitini.

Alisema kamati hiyo ya matawi, ina wajumbe watano lakini wanne waliingia mitini ambapo alibakia katibu peke yake, hivyo kuifanya kolam kushindwa kutimia ndiyo maana wakaamua kuahirisha mkutano huo.

"Mwenyekiti Msumi pamoja na wajumbe wengine wanne wa Kamati ya Utendaji ya Matawi waliingia mitini, hivyo tukaamua kuahirisha mkutano huo mpaka siku utakapopangwa kufanyika tena," alisema Kaisi.
 
Silaha nne za Afrika ya Kati zafikishwa Stars Send to a friend Wednesday, 23 March 2011 20:28

osiah.jpg
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah

Sweetbert Lukonge na Jessca NangaweWAKATI Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likiwataka wapenzi na mashabiki wa soka nchini kuacha tabia ya kuwabagua wachezaji wa timu ya taifa, Taifa Stars kwa sababu ya klabu watokako katika mchezo wa Jumamosi, timu hiyo (Stars) imepewa majina ya wachezaji hatari wanne wa wapinzani wao, Jamhuri ya Afrika ya Kati na kutakiwa kuwachunga.

Kulingana na taarifa za mitandao na vyombo vya habari vya Jamhuri ya Afrika ya Kati, timu hiyo ambayo inaongoza Kundi D linaloundwa pia na Algeria na Morocco ikiwa na pointi nne, licha ya kushiriki mara chache michuano mikubwa ya Afrika, inaundwa na wachezaji wenye damu mchanganyiko ambao Stars haina budi kuwachunga.

Nyota hao chini ya kocha Jules Acorsi, raia wa Ufaransa wametajwa kuwa ni kiungo mshambuliaji Foxi Kethevoama (24) ambaye ndiye mfungaji wao tegemeo ambaye pia huichezea klabu ya Kecskeméti TE ya Hungary anayetajwa kuwa atasumbua mabeki wa Stars Jumamosi.

Wengine ni, Hilaire Momi, anayechezea Cotonsport ya Cameroon, viungo Romaric Linganzi wa US Bitam ya Gabon na Marcelin Tamboulas aliyekuwa katika benchi la akiba la TP Mazembe katika mechi dhidi ya Simba Jumapili.

Kwa kuangalia wastani wa umri wa wachezaji wa timu inao vijana wa umri wa kuanzia miaka 19 hadi mkongwe zaidi mwenye umri wa miaka 32, wote wakicheza soka katika nchi yao na nyingine Afrika na Ulaya. Wastani wa umri wao si zaidi ya miaka 24, jambo ambalo kwa soka la kisasa litawawasaidia.

Awali, akizungumza uzalendo kuelekea mechi hiyo , Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema kuwa Watanzania wote wapenda soka wanatakiwa kushikamana na kuiunga mkono Stars katika mechi zake zote inazoshiriki bila kuangalia aina ya klabu wanakotoka wachezaji wanaounda kikosi hicho.

Stars itashuka uwanjani, Jumamosi Machi 26 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kupambana na Jamhuri ya Afrika ya Kati kuwania nafasi ya kufuzu kushiriki fainali za Afrika mwakani.

"Nawaomba Watanzania wenzangu tushikamane na kuiunga mkono timu yetu ya taifa katika mchezo wake wa Jumamosi dhidi ya Afrika ya Kati.

"Umefika wakati wa kutanguliza kwanza utaifa na kuachana na tabia ya ubaguzi na kuwazomea wachezaji wetu kwa sababu tu kwamba kikosi kimeundwa na wachezaji kutoka klabu wasiyoshabikia," alisema Osiah.

Katika hatua nyingine kocha mkuu wa timu hiyo Jan Poulsen alisema kuwa maandalizi kwa ajili ya mechi hiyo yanaendelea vizuri na kikosi chake kipo tayari kwa ajili ya kuhakikisha kinashinda mchezo huo.

Alisema mbali na hilo pia ana matumaini makubwa na wachezaji waliopo kwa sasa katika kikosi chake hata kama kiungo mshambuliaji wa Vancouver Whitecaps ya Canada, Nizar Khalfan asipotokea licha ya mchango wake kuhitajika kwenye kikosi hicho waliopo wataziba pengo lake.

Kumekuwepo na tetesi kuwa Nizar huwenda asijiunge na Stars kutokana na timu yake kuwa katika mikikimiki ya Ligi Kuu ya Marekani (MLS ), jambo ambalo Ofisa habari wa TFF, Boniface Wambura alisema kuwa taarifa hizo hazina ukweli na mchezaji huyo aanatarajia kutua nchi leo tayari kwa kuungana na wenzake kwa mechi hiyo ya Jumamosi dhidi ya Afrika ya Kati.

Kuhusu hilo, shirikisho hilo limesema endapo uongozi wa klabu hiyo ya Canada hautamruhusu Nizar Khalfan kwa ajili ya kushiriki mchezo wa kimataifa dhidi ya Afrika ya kati Jumamosi, klabu hiyo itashtakiwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).

Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Angetile Osiah alisema jana kuwa wao walitumia utaratibu na kumwombea ruhusa mapema mchezaji huyo ili aweze kuja kuungana na wenzake kwa ajili ya mchezo huo lakini inashangaza klabu hiyo kujibu kuwa hawana taarifa za mchezo huo na hadi sasa kushindwa kutoa jibu la kumruhusu mchezaji huyo.

"Sisi tulifuata taratibu na kutuma maombi kwa Whitecaps ili wamruhusu Nizar aje nchini kuungana na wenzake, lakini cha kushangaza wametuambia hawana taarifa za mchezo wetu wa kimataifa ndio maana mpaka sasa hajafika, lakini bado kuna muda anaweza kuwasili kesho (leo), kinyume na hapo tutaiarifu Fifa ili sheria na kanuni zichukue mkondo wake kwani Fifa wanatambua umuhimu wa mchezaji kuchezea timu ya taifa la nchi yake,"alisema Angetile.

Alisema kwa upande wa maandalizi yao yanakwenda vizuri na wapinzani wao, Afrika ya Kati tayari wamewasili nchini tangu juzi kwa ajili ya mchezo huo ambao mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi.

Kwa upande mwingine, Osiah alisema kufuatia na kubanwa katika michezo ya Ligi Kuu na ile ya kimataifa kwa timu za Simba na Yanga, walishindwa kucheza mechi za kimataifa za kirafiki ingawa tayari walipata mialiko katika nchi za Afrika Kusini na Afrika ya Magharibi.
 
ZFA kupendekeza Msemaji, Katibu


Na Mwajuma Juma, Zanzibar

CHAMA cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), kimesema kinatarajia kupendekeza nafasi ya Msemaji wa chama hicho na Katibu Msaidizi Unguja, ili
ziwemo katika katiba ya chama chao.

Akizungumza mjini hapa jana Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya ZFA, Mussa Soraga alisema kwamba mwambia mapendekezo hayo yatatolewa katika Mkutano Mkuu wa dharura utakaofanyika wakati wowote kuanzia sasa.

"Nafasi hizi hazimo katika katiba ya chama, lakini katika mkutano huo tunatarajia kupendekeza na kama zitapitishwa zitaingizwa katika katiba yetu," alisema Soraga.

Alisema mbali na pendekezo hilo, pia wanatarajia kupendekeza kufanyiwa marekebisho kwa Kamati ya Usimamizi ya Uchaguzi, ili iweze kutumika wakati wa uchaguzi pekee na baadaye kuvunjwa.

Mjumbe huyo alisema kwamba Kamati ya Uchaguzi inayotumika hivi sasa imekuwa ikikaa kwa muda mrefu bila ya kufanya kazi, hasa ikizingatiwa kwamba uchaguzi wake hufanyika kila baada ya miaka minne.

"Sasa hivi katiba hiyo inakaa kwa muda wa miaka minne, jambo ambalo imeonekana kuwa inakaa muda mwingi huku uchaguzi ukiwa unafanyika kila baada ya miaka mine," alisema.

Hata hivyo Mjumbe huyo hakuweza kutaja ni lini mkutano huo utafanyika, lakini alisema kuwa kati ya ajenda watakazozizungumza katika mkutano huo na nafasi hizo nazo zitakuwa miongoni mwa ajenda zao.
 
Wadau wazidi kuwalilia Five Stars


na Mwandishi wetu


amka2.gif
WADAU na wapenzi wa muziki wa taarabi nchini, wamehuzunishwa na vifo vya wasanii 13 wa kundi la muziki la Five Stars Modern vilivyotokea juzi usiku kwa ajali ya gari maeneo ya Mikumi mkoani Morogoro.
Wasanii hao waliokuwa kwenye Coaster wakitokea mikoa ya Mbeya na Iringa, walipata ajali baada ya gari lao lilipogonga lori la mbao lililokuwa limeegeshwa pembeni mwa barabara wakati wakielekea Dar es Salaam.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam jana, wadau na wapenzi hao walisema, vifo hivyo wamevipokea kwa mshituko mkubwa, kwa kuwa ni kitu ambacho hakikutarajiwa na walio wengi.
Salma Abdallah, mdau wa taarabu na mkazi wa Mabibo, alisema: "Niliposikia katika vyombo vya habari msiba huo … nilipata shinikizo la damu, lakini hatuna jinsi, tunatakiwa kuwaombea kwa Mungu ili awalaze mahali pema peponi."
Naye Mahamoud Juma, mkazi wa Manzese alisema, msiba huo ni pigo kwa tasnia ya taarabu, kwani waliofariki, walikuwa ni wasanii hodari wa kutegemewa.
Pamoja na wadau na wapenzi wa muziki huo, serikali nayo kupitia Rais Jakaya Kikwete juzi alituma salamu za rambirambi kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi, kufuatia vifo vya wasanii hao.
"Binafsi nimeguswa mno na msiba huu, kwa vile umetupotezea wasanii ambao walikuwa na mchango mkubwa katika kukuza na kuendeleza sanaa ya muziki wa taarabu nchini kwetu," alisema rais katika salamu zake kwa Waziri Nchimbi.
Alisema hilo ni pigo kubwa siyo kwa usanii wa taarabu tu, bali kwa taifa zima la Tanzania na kumtaka Waziri Nchimbi afikishe salamu zake kwa ndugu wa wafiwa.
 
Sikinde wahaha kumrejesha Benno


na Mwandishi wetu


amka2.gif
BENDI ya muziki wa dansi ya Mlimani Park ‘Sikinde Ngoma ya Ukae', inafanya kila liwezekanalo kumrejesha kundini mwimbaji wake wa zamani Bennovila Anthony ‘Benno'.
Sikinde, ambayo hivi karibuni ilipata pigo baada ya kuondokewa na mwimbaji mkongwe na alama ya bendi hiyo, Shaaban Dede, tayari imefanikiwa kumrejesha kundini mwimbaji mwingine, Hussein Jumbe ‘Mzee wa Nachechemea'.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Habari wa Mlimani Park, Jimmy Chika, alisema mazungumzo kati ya Maseneta wa bendi hiyo na mwanamuziki huyo yamefikia mahali pazuri.
"Kwa sasa, Maseneta wa Sikinde wapo kwenye mazungumzo ya mwisho mwisho ya kumrejesha kundini mwimbaji wetu wa zamani Bennovila Anthony," alisema Chika.
Alisema kutokana na hilo, wanaamini Benno atarejea kundini na kwamba kurejea kwa mwimbaji huyo kutaifanya safu yao ya uimbaji kukamilika, ambapo waimbaji hao wapya wataungana na Hassan Rehan Bitchuka, Hassan Kunyata na Abdallah Hemba.


h.sep3.gif
 
FM yajipanga kwa albamu mpya


na Happiness Katabazi


amka2.gif
BENDI ya mahiri ya muziki wa dansi nchini, FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma' imeanza maandalizi ya albamu yao ya mwaka 2012.
Akizungumza kwa njia ya simu jana, Rais wa bendi hiyo, Nyoshi El Sadat alisema, tayari wameishaanza mazoezi ya maandalizi ya albamu hiyo ambayo yanafanyika mara mbili kwa wiki katika ukumbi wa New Msasani Club.
Nyoshi alisema albamu hiyo itajulikana kwa jina la ‘Chuki ya Nini', ambapo alisema jina hilo linatokana na wimbo wa chuki ya nini ambao umetungwa na yeye mwenyewe Nyoshi.
"Kama ulivyosikia ni kweli bendi yetu imeanza maandalizi ya albamu hiyo ambayo itabeba jumla ya nyimbo 12, ambapo karibu kila mwanamuziki ametunga wimbo wake hivyo tunawaambia mashabiki wetu wakae mkao wa kula, kwani tupo jikoni tayari kwa ajili ya kuipika albamu hiyo ambayo itakuwa ni kabambe ...ila wakati tunaendelea na maandalizi hayo tunaomba waendelee kuifurahia albamu ya vuta ni kuvute," alisema Nyoshi El Sadati
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom