Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Zomboko aponda utaratibu wa tuzo


na Shehe Semtawa


amka2.gif
Mchambuzi maarufu wa muziki wa dansi nchini, Rajabu Zomboko, amesema haridhishwi na utaratibu wa kupiga kura ili kuwapata washindi wa tuzo za ‘Kili awards'.
Zomboko aliiambia Tanzania Daima kuwa mtindo huo wa kupiga kura kwa kutumia ujumbe mfupi kwa njia ya simu umekuwa ukitoa ushindi kwa watu ambao hawana uwezo kimuziki.
Alisema kinachofanyika pale ni kudanganyana kutokana na kwamba baadhi ya washiriki wana uwezo kifedha hivyo hutumia ushawishi wao kwa kuwaongezea pesa jamaa zao kwenye simu zao ili watume ujumbe mra nyingi.
Aidha, Zomboko alibainisha kuwa wale wenye uwezo wa kuimba wamekuwa wakikosa tuzo kutokana kwamba hawana uwezo wa kuwaingizia fedha jamaa zao kwenye simu zao ili wawapigie kura kwa wingi.
Zomboko alisema kwa upande mwingine utaratibu uanaotumika umekuwa ukiwanufaisha zaidi makampuni ya simu kadiri ujumbe unavyotumwa kwa wingi huku washindi wakipata fungu dogo.
"Unajua ile ni biashara ya wajanja wachache ambao wanajinufaisha wenyewe kwani ujumbe unaotumwa ni mwingi sana ingawa sina uhakika ujumbe ni kiasi gani," alisema Zomboko.
Zomboko alisema mwanamuziki wa kweli hapatikani kwa kupigiwa kura bali wanapambanishwa jukwaani na kuonyesha vitendo kama enzi za nyuma zilivyokuwa zinapambanishwa bendi mbalimbali za muziki wa dansi.
 
Warembo shindano la Kisura watambiana


na Dina Ismail


amka2.gif
WAREMBO wanaowania taji la Kisura wa Tanzania 2010/11, kila mmoja amejinadi kuibuka kidedea katika shindano hilo linalotarajiwa kufanyika kesho katika ukumbi wa Hoteli ya Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa warembo hao, Lethina Christopher, alisema kuwa ingawa miongoni mwao kila mtu anaonekana kuwa mshindi, lakini hakuna wa kumzidi na kwamba yeye ndiye atakayeibuka kidedea.
"Nawaomba Watanzania waendelee kunipigia kura namba 20 kuniwezesha kunipa ushindi," alisema huku Mshiriki mwingine, Flaviana Makungwa alisema kuwa amejiandaa vizuri na anajiamini kuwa anao uwezo wa kushinda na kuielimisha jamii sambamba na kuendelea kulitangaza shindano hilo.
Kwa upande wake, Lilian Bussa, alisema amejiandaa vizuri kwa sababu kambini amepewa mafunzo mbalimbali na pia ana vigezo vitakavyomuwezesha kuwabwaga wenzake.
Mshindi wa shindano hilo anayemaliza muda wake, Diana Ibrahim, aliwataka washiriki hao kukubali matokeo, kwani wale ambao hawatashinda, wajijue kuwa ni washindi, wadumishe nidhamu kwa muda wote wanapokuwapo kambini na hata baada ya shindano hilo ili wawe mfano wa kuigwa katika jamii.
"Mashindano haya humsaidia mshiriki kujifunza vitu vingi vya jamii na wakitoka hapa, wanaweza kujitegemea kwa kujiongoza kimaisha," alisema Diana.
Kwa upande wake, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Mradi wa Kisura wa Tanzania, Juliana Urio, amewataka visura wote wazidi kumuomba Mungu kuelekea shindano hilo la kesho na hata wanaporudi katika makazi yao.
Pia, amewataka wazazi kuzidi kuwaruhusu watoto wao kushiriki mashindano hayo kwa kuwa yana utofauti na mashindano mengine yote ya urembo na uanamitindo kwa ujumla hapa nchini.
"Nawaomba wazazi wawaruhusu watoto kushiriki katika shindano hili kwa mwaka unaokuja kwa kuwa mashindano yetu yanamjenga msichana kuweza kujitambua zaidi katika jamii yake na kuacha utegemezi wa mtu," alisema Urio.
Kisura wa Tanzania 2011 imeandaliwa na BTA na mdhamini mkuu wa shindano hilo ambalo linafanyika kwa mara ya tatu sasa ni Family Health International (FHI),TBL kupitia kinywaji chake cha REDDS, TBC1, Kiromo View Resort, TanFoam (Arusha), SBC Limited, Flare Magazine, Hugo Domingo, BASATA, GRM Production, Clouds FM, ATCL, MJ Records, I-View Media, PURE Hair and Beauty Spa na PURE Academy of Aesthetics.
 
Mabondia wa Madola watemwa taifa ngumi Send to a friend Wednesday, 16 March 2011 21:06

Imani Makongoro
MABONDIA waliokuwa timu ya taifa na wawakilishi wa Tanzania kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola mwaka jana iliyofanyika nchini India wametemwa katika kikosi cha timu hiyo.

Mabondia hao wameachwa katika mchujo uliofanywa na jopo la makocha walioteuliwa na Shirikisho la mchezo huo Tanzania (BFT) wakiongozwa na kocha mkuu Pimentel Hurtado raia wa Cuba.

Kati ya mabondia waliochaguliwa na kocha huyo Mcuba ni bondia mmoja tu ambaye alishiriki Michezo hiyo ya Madola 2010 Selemain Kidunda ndiye aliyeitwa kuendelea kuitumikia timu hiyo ya taifa.

Hurtado aliiiambia Mwananchi kuwa nidhamu mbaya ya ulingoni ndiyo sababu kubwa iliyowaondoa mabondia waliokuwa timu ya taifa mwaka jana katika kikosi cha mwaka huu ambacho chenye kibarua cha michuano ya Afrika mjini Maputo Msumbiji mapema mwezi Septemba.

"Tangu nimekuja Tanzania kufundisha ngumi Septemba 2009 na kukaa na mabondia hawa kwa zaidi ya mwaka mmoja nimewaona na kugundua kuwa baadhi yao hawana nidhamu na katika mchujo wa safari hii nidhamu ilizingatiwa hivyo moja ya sababu ambazo zimewaondoa mabondia hawa kwenye timu ya taifa ni nidhamu," alisema Hurtado.

Mabondia watakaounda timu hiyo na klabu zao kwenye mabano ni John Christian na Yahaya Malik, (Polisi) Mussa Dogo ( Ilala), Abdallah Kassim (Ngome) wote wanazichapa katika uzani wa fly.

Wengine ni Nassor Ally (Pwani), Boniface, Godfrey Timoth (Morogoro) uzani wa bantam, wakati katika uzani wa light ni Ismail Izak, Omary Mrisho (Ngome) na Wambura Amir wa Temeke.

Aliwataja mabondia waliochaguliwa katika uzani wa light welter kuwa ni Bakari Paschal, Elius Mkoma (Rukwa) na Iddy Pialali, wakati katika uzani wa welter ni Victor Nyaiti (Magereza), Godfrey James (Ngome) Mohamed Chimbumbuli, Prosper (Polisi) na Greyson Choga wa Pwani.

Uzani wa middle ni Kidunda, Abdallah Rashid (Kinondoni), Juma Ally (Tabora) Ibrahim Shababi (Kinondoni) Juma Falhan (Tabora) na Kimanga Issa wa Ruvuma, huku uzani wa heavy ni Shaban Yusuph (Temeke) Amos Godwin (Magereza) na katika super heavy ni Maximilian Patrick.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
 
Simba yazidi kuimarika Arusha


na Makuburi Ally


amka2.gif
KIUNGO wa kimataifa wa klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Mganda Hillary Echessa, aliyekuwa majeruhi hivi sasa amerejea uwanjani huku akiendelea vema na akionyesha matumaini makubwa ya kucheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), unaotarajiwa kuchezwa Machi 20 mjini Lubumbashi nchini humo.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Simba, Clifford Ndimbo, alisema kuwa kutokana na jinsi nyota huyo anavyoendelea vema, Kocha Mkuu, Mzambia Patrick Phiri, anatarajia kumchezesha katika mchezo huo wa kwanza.
Licha ya marejeo hayo ya Echessa, Ndimbo alisema kuwa, bado klabu hiyo ina majeruhi kadhaa kwa sasa akiwamo beki mahiri raia wa Uganda, Joseph Owino na kiungo mshambuliaji, Uhuru Suleiman, ambao watakuwa nje ya uwanja hadi msimu wa ligi utakapomalizika Aprili 10.
Aidha, Ndimbo alisema kiungo Abdulhalim Humoud ambaye atakuwa nje ya dimba kwa wiki mbili, anatarajia kurejea dimbani hivi karibuni, ikiwa tayari kakaa nje kwa wiki moja sasa.
Kuhusu mchezo na TP Mazembe, Ndimbo alisema hakuna kisichowezekana, hivyo kuwataka benchi la ufundi, wachezaji, viongozi, wanachama na mashabiki wasikate tamaa.
"Sisi tunajiandaa kucheza na timu yoyote ngumu, ikiwamo TP Mazembe, huwezi kufika fainali au kuchukua kombe bila kuzifunga timu ngumu kama Mazembe na Al Ahly, ambazo zinatisha barani Afrika katika medani ya soka," alisema Ndimbo.
Simba ambayo iko kambini jijini Arusha inatarajiwa kurejea jijini Jumamosi kabla ya kuunganisha Lubumbashi kwa ajili ya mtanange huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka ndani na nje ya Bara la Afrika.
 
Mabondia waliogoma watoswa timu ya taifa
• Yumo Nahodha Joseph Martin, Nasser Mafuru

na Samia Mussa


amka2.gif
KATIKA kile kinachoonekana Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), kuwashughulikia mabondia wa timu ya taifa walioshiriki mgomo wa mashindano ya Mabingwa wa Mabingwa Ukanda wa Afrika Mashariki mwishoni mwa mwaka jana, limetangaza kikosi kipya huku mabondia mahiri na wa siku nyingi wakitemwa.
Katika tukio ambalo liliacha historia chafu katika medani ya michezo hapa nchini, ni pale mabondia hao chini ya Nahodha wao Joseph Martin, waligomea mashindano hayo ya mabingwa wa mabingwa yaliyokuwa yanafanyika ukumbi wa DDC Mlimani Park, Mwenge jijini Dar es Salaam huku wao wakiwa wenyeji kwa madai ya kunyimwa kifungua kinywa huku timu ngeni kutoka Uganda, Kenya na Mauritius zenyewe zikipata huduma hizo.
Akitangaza jijini Dar es Salaam jana, kikosi hicho kipya cha taifa ambacho kinatarajiwa kushiriki mashindano mbalimbali ya kimataifa ikiwamo ya majiji huko Kampala, Uganda na All Africa Games, Maputo Msumbiji, Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, alisema uteuzi huo umezingatia mambo mengi, likiwamo suala la umri, kiwango kizuri alichokionyesha bondia katika mashindano ya taifa na nidhamu, ambapo kamati ya utendaji ya BFT, imepitia majina ya mabondia wote na kujiridhisha kuwa wanastahili kuitwa timu ya taifa ambayo itakuwa chini ya kocha mkuu, Mcuba Hurtado Primenter.
"Tunawaomba mabondia ambao nitawatangaza muda mchache ujao, watangulize uzalendo pamoja na nidhamu wanapokuwa katika na wanapochaguliwa kushiriki mashindano ya kimataifa," alisema Mashaga, kauli inayoonyesha wazi kukemea tukio lililofanywa na mabondia wa timu ya taifa mwaka jana la kugomea mashindano na kuitia aibu nchi kimataifa.
Alisema, pamoja na kutangaza kikosi hicho, hadi hivi sasa hakuna vifaa vinavyoweza kutumiwa na mabondia wala fedha za kuiweka kambini, lakini uongozi wa BFT, bado unaendelea kufanya jitihada ili kikosi hicho kiweze kuingia kambini haraka iwezekanavyo.
Katika kikosi hicho kipya, mabondi wa muda mrefu katika timu ya taifa akiwamo nahodha, Joseph Martin wa JKT, Leonard Machichi wa Ngome, Nasser Mafuru wa Magereza na wengineo wametemwa.
Mashaga alitaja majina ya wanaounda kikosi hicho kipya kuwa ni John Christian (Kinondoni), Yahaya Maliki (Polisi), Dogo Mussa (Ilala), Abdallah Kassim, Boniface Mlingwa, Omary Mrisho (Ngome), Nassoro Ally, Ismail Isack (Pwani), Godfrey Timothy (Morogoro) na Wambura Amiry (Temeke).
Wengine ni Bosco Bakari (Mwanza), Elius Nkome (Rukwa), Idd Pialali (Kinondoni), Victor Njaiti (Magereza), Godfrey James Ngome), na Museven Gasper (Polisi).
Pia wamo Mohamed Chimbulimbuli (Polisi), Method Choga (Pwani), Suleimani Kidunda (Ngome), Abdallah Rashid, Abdallah Shabani (Kinondoni), Juma Ally, Juma Farahani (Tabora), Issa Kimanga (Ruvuma), Shabani Yusuph (Temeke), Amosi Godwin (Magereza), na Maxmilian Patrick (JKT).
Mashaga alisema kuwa kocha mkuu wa timu hiyo atakuwa Mcuba, Hurtado akisaidiwa na kocha mkuu mzawa, Benjamin Mwangata, Makoye Isangula na Edward Emmanuel, kutoka Klabu ya Sifa, huku aliyekuwa kocha msaidizi, Remmy Ngabo akiachwa.
Wakati huo huo, kamati ya utendaji ya BFT, imempa adhabu bondia Renatus Mpandangazi wa Polisi, kutocheza mashindano mawili yanayoandaliwa na BFT, baada ya kuomba radhi kwa barua na kukiri kosa ili asamehewe, baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu wakati wa mashindano ya taifa.
Aliongeza kuwa BFT inaendelea kupitia taarifa za baadhi ya mabondia na makocha ambao walionyesha utovu wa nidhamu katika mashindano hayo, ili kujiridhisha kama wanastahili kuadhibiwa, ambapo uchunguzi ukikamilika, watatoa taarifa.
 
Mgosi: Iko siku Poulsen atanikubali Send to a friend Wednesday, 16 March 2011 20:55

Vicky Kimaro
MSHAMBULIAJI wa Simba Mussa Hassan 'Mgosi' amesema iko siku kocha wa Taifa Stars, Jan Poulsen atamkubali na atamuita kwenye kikosi chake cha timu ya taifa.Wakati akitangaza majina ya wachezaji wa Taifa Stars Jumanne iliyopita, Paulsen aliwaacha baadhi ya wachezaji akiwemo Mgosi. Stars inajiandaa na mpambano dhidi ya Afrika ya Kati Jumamosi ijayo.

Mgosi alisema kuwa kocha huyo ni wazi hamkubali lakini anaamini kuwa anaweza na ni mkali kwani tangu atue nchini amekuwa akimuacha mara kwa mara kwenye kikosi chake kitu ambacho ameadai kuwa ipo siku atamkubali.

"Unajua kila kocha na falsafa zake, tangu amekuja Poulsen hanikubali lakini naamini ipo siku atanikubali mimi nina kiwango kizuri na kikubwa ipo siku." alisema Mgosi.Wakati akitangaza kikosi cha Chalenji mwishoni mwa mwaka jana, mshambuliaji wa timu hiyo, Jerry Tegete alitoa kauli ya kumshangaa kocha huyo kumwacha na kumchukua Gaudence Mwaikimba.

"Uwezo wangu ni wa kucheza Ligi Kuu na si kuchezea timu ya taifa, najiamini nina kiwango cha hali ya juu ila kocha hajanikubali kwa sababu zake mwenyewe," alisema.

Wachezaji waliotemwa mbali na Mgosi ni Jerry Tegete, Kelvin Yondani, Mohamed Ally 'Shibori' na Salum Machaku.
Hata hivyo wakati Mgosi akisema hayo, mchezaji wa Yanga, Jerry Tegete alisema "Sijisikii vibaya kuachwa kwa sababu kuna wachezaji wengi wazuri wanachipukia, ni wakati wa wao kupata nafasi ya kutumikia timu ya taifa,"alisema Tegete

Tegete alipoulizwa haoni kiwango chake kimeshuka ndio maana Mdenmark huyo amekuwa akimuacha mara kwa mara alisema: "Mimi kiwango changu hakijashuka, bado kipo juu na kinazidi kupanda, kocha mwenyewe ndio mwenye maamuzi, huwezi kumlazimisha akuchague ipo siku ataniita," alisema.
 
Timbe kurejea Jangwani leo


na Juma Kasesa


amka2.gif
KOCHA Mkuu wa timu ya Yanga, Mganda Sam Timbe, anatarajiwa kutua jijini Dar es Salaam leo tayari kwa kukipa makali mapya kikosi chake kinachojiwinda na mechi tatu muhimu za Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kumalizika Aprili 10 mwaka huu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Louis Sendeu alisema Timbe anatarajiwa kutua, akiwa na mbinu mpya za kuwapa wachezaji wa timu hiyo, ili waweze kufanya vema katika mechi zilizosalia ili kusaka ubingwa wa ligi hiyo unaoshikiliwa na ‘Wekundu wa Msimbazi' Simba.
Yanga imezidi kujiweka katika mazingira magumu ya vita ya kuwania ubingwa wa Ligi hiyo, baada ya wiki iliyopita kulazimishwa sare ya bila kufungana na maafande wa JKT Ruvu, huku mahasimu wao wa jadi Simba, ikizidi kuchanja mbuga baada ya kuwatandika mabao 2-0, vibonde wa ligi hiyo AFC ya Arusha.
Sendeu alisema, kikosi cha timu hiyo kinatarajiwa kuanza mazoezi rasmi kesho Uwanja wa Kaunda chini ya Timbe, kujiandaa na mechi ngumu iliyo mbele yao dhidi ‘Watengeneza Lambalamba' Azam FC Machi 30 mwaka huu, kabla ya kuvaana na African Lyon na Toto Africa ya Mwanza.


h.sep3.gif
 
Miyeyusho kuzipiga Philippines


na Makuburi Ally


amka2.gif
BONDIA Francis Miyeyusho wa Tanzania Machi 19 anatarajia kupanda ulingoni kuzipiga na Aj Banal wa Philippines ikiwa ni pambano lisilo la ubingwa.
Akizungumza na Tanzania Daima kutoka Philippines jana, Rais wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) Emmanuel Mlundwa ambaye yuko na Miyeyusho nchini humo alisema pambano hilo litakuwa la raundi 10.
Mlundwa alisema pambano hilo ni kwa ajili ya kumweka sawa Miyeyusho ambaye ni mojawapo ya mabondia bora Tanzania ambaye wanamuandaa na mapambano ya kimataifa.
"Tumemtafutia pambano hilo," Mlundwa alisema baada ya pambano hilo wanatarajia kurejea nchini ambako siku chache baada ya pambano hilo watarejea kutoka nchini humo.
"Tumeamua kumtafutia Miyeyusho pambano nje ya nchi kwa sababu ya ubora wake katika medani ya ngumi hapa Tanzania," alisema Mlundwa.
 
AT wamchanganya kocha wa riadha Send to a friend Wednesday, 16 March 2011 20:52

Moses Mashalla, Arusha
KOCHA wa timu ya riadha taifa, Andro Baro ameishangaa serikali na makampuni binafsi hapa nchini kujali soka na kuipa kisogo riadha.Mbali na hayo, alisema hakuna kinachofanyika kuanza maandalizi ya michezo ya Afrika iliyopangwa kufanyika kwenye mji wa Maputo nchini Msumbiji baadaye Septemba.

Baro alitoa kauli hiyo juzi wakati akihojiwa na gazeti hili ndani ya uwanja wa Sheikh Amri Abeid wakati akisimamia mazoezi ya wachezaji mbalimbali wa riadha kutoka klabu binafsi na zile za taasisi za serikali.

Alisema kuwa anashangaa serikali na makampuni binafsi kukazania kujikita katika kufadhili soka na kuitupa riadha huku akidai kwamba bila kuwekeza nguvu katika mchezo huo kamwe Watanzania wasitarajie medali yoyote.

ìMi nashangaa naona serikali na makampuni kama Vodacom wakifadhili soka tu lakini kwenye riadha sisikii, nimesikia hizi Fun Run za Kili Maradhon ambazo si za ushindani hasa...sijui ni kwa sababu ya fedha, lakini hata huku kwenye riadha kuna fedha pia watu hawajui tu,î alisema Baro
Alisema kuwa yeye kama kocha wa timu ya taifa ya riadha alipaswa kukusanyiwa wachezaji na Chama cha Riadha Tanzania, AT, kwa lengo la kuwachuja lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea.

"Binafsi nashangaa sijapatiwa wachezaji ihali kuna mashindano makubwa mbeleni, kuna Michezo ya Afrika baadaye Septemba.Hata hivyo, alisema kuwa anashangazwa na kitendo cha serikali kukazania mashindano ya mbio ndefu badala ya fupi na kusema kuwa nchini kuna wakimbiaji wazuri wa mbio fupi.

ìSerikali inaaangalia fedha tu kwa mbio ndefu hata hizi fupi kuna hela kwa mfano mimi tangu nimefika hapa nimesaidia wakimbiaji wa mbio fupi kama 10 na wameshinda vizuri tuî alisisitiza Baro

Akizungumzia maandalizi ya timu ya taifa ya riadha kwa ajili ya mashindano ya All Africa Games yanayotaraji kufanyika nchini Msumbiji mwezi septemba mwaka huu kocha huyo alisema kuwa ni lazima timu yake ipate maandalizi ya kutosha kwa muda wa miezi mitatu kabla ya kushiriki mashindano hayo.
 
Liverpool, Ajax vitani Europa Ligi Send to a friend Wednesday, 16 March 2011 20:48

BERNE,Switzerland
TIMU za Liverpool na Ajax Amsterdam leo zinakabailiwa na mechi za marudiano za mashindano ya Europa Ligi ili kutafuta kufuzu kuingia hatua ya robo fainali ya mashindano hayo.Ajax yenyewe itakuwa ikicheza na Spartak Moscow, ambapo katika mechi ya ya kwanza Ajax ilifungwa bao 1-0, pia Liverpool itakuwa ikicheza na Braga, katika mechi ya kwanza Braga ilishinda bao 1-0.

Katika mechi ya leo, timu ya Liverpool itamkosa mshambuliaji wake Luis Suarez.Akimzungumzia mshambuliaji huyo, kocha wa Liverpool, Kenny Dalglish alisema,"tungependa kumchezesha mchezahji huyo, lakini haiwezekani."

Suarez alinunuliwa na Liverpool akitokea Ajax mwezi Januari, ambapo wakati yupo katika klabu ya Ajax, Suarez alifunga mabao 81 katika misimu minne aliyochezea timu hiyo.

Pia leo kutakuwa na mechi mechi za mashindano hayo ambapo, mjini Paris,Paris Saint-Germain itapambana na Benfica. Katika mechi ya kwanza Benfica ilishinda mabao 2-1.

Huko mjini Manchester, England, Manchester City itaumana na Dynamo Kiev, ambapo katika mechi ya kwanza Dynamo Kiev lead ilishinda mabao 2-0.

Mjini St Petersburg, Russia, Zenit St-Petersburg,itacheza na FC Twente, matokeo katika mechi ya kwanza ni Twente ilishinda mabao 3-0. FC Porto itaikaribisha CSKA Moscow, ambapo katika mechi ya kwanza Porto ilishinda bao 1-0.

Nayo Rangers itacheza dhidi ya PSV Eindhoven, lakini timu hizi katika mechi ya kwanza zilitoka sare ya 0-0.

Villarreal yenyewe itaikaribisha Bayer Leverkusen, ambapo katika mechi ya kwanza Villarreal ilishinda 3-2.
 
Mwaitege athibitisha kushiriki tamasha Send to a friend Wednesday, 16 March 2011 21:01

Vicky Kimaro
MWIMBAJI wa nyimbo za injili, Bonny Mwaitege, amethibitisha kushiriki Tamsha la Pasaka litakalofanyika Aprili 24, kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema kuwa walikuwa katika mazungumzo ya mwisho kabla ya kukubaliana kushiriki tamasha hilo. Pia atakuwa kwenye msafara wa Dodoma na Shinyanga.

Msama alisema kuwa kwa sasa mwimbaji huyo yuko kambini mkoani Mbeya akiwa kambini kujiandaa na tamasha hilo ambalo Rais Kikwete atakuwa mgeni rasmi siku hiyo.

Mwaitege anakuwa mwimbaji wa tatu wa injili kuthibitisha, wengine ni Rose Mhando na Upendo Nkone. Mwingine ni Anastazia Mukubwa kutoka Kenya ambaye atawasili na kundi la wasanii wanane.

Msama alisema kuwa wanaendelea na mazungumzo na wasanii wengine wa muziki wa injili wakiwemo chipukizi na wakongwe kwa ajili ya tamasha hilo ambalo fedha zake zitatumika kusaidia jamii mbalimbali.

"Tunakamilisha mazungumzo na waimbaji wengine kwa mmoja mmoja na vikundi vya kwaya, naamini mambo yatakamilika...Pia tuko katika mazungumzo na Kwaya Upendo ya Mwananyamala," alisema.

Tamasha hilo mwaka jana pia lilishirikisha waimbaji wa nyimbo za injili akiwemo Flora Mbasha, Christina Shusho, Jennifer Mgendi na wengine ambao walitikisha mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Mara.

Msama alisema kuwa baada ya onyehso la Dar es Salaam, siku inayofuata watakuwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma na baadaye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
 
Machaku, Yondani chali, Dihile, Kazimoto waula Send to a friend Tuesday, 15 March 2011 21:13

kocha%20poulsen21.jpg
Sosthenes Nyoni
KOCHA wa timu ya taifa,Taifa Stars, Jan Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kitakachojiandaa kwa mchezo dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati na kuwaacha Salum Machaku na Kelvin Yondani.

Mbali ya kuwaacha nyota hao Poulsen amewaita kwa mara ya kwanza nyota wa JKT Ruvu kiungo Mwinyi Kazimoto na kipa Shaaban Dihile waliokuwa nje ya kikosi hicho kwa zaidi ya miezi 8 tangu kuoondoka Mbrazil Marcio Maximo.

Akitangaza kikosi hicho kwenye ofisi za Shirikisho la Soka nchini TFF, Poulsen alitetea uamuzi wake wa kumuita mshambuliaji mkongwe Athuman Machupa kwa kusema uzoefu wake una umuhimu katika kujenga ari ya kikosi kwa kuwa anajua nini anachokifanya.

"Tunahitaji kuchanganya wachezaji ili kuwapa uzoefu wale chipukizi ili waweze kujifunza kwa wale wachezaji wazoefu,"alisema Poulsen.

Mdenmark huyo amemwacha beki wa Simba, Kelvin Yondan, kipa wa Majimaji, Said Mohamed na mshambuaji wa Mtibwa Sugar, Salum Machaku aliyekuwa moja ya nguzo muhimu kwenye kikosi cha Kilimanjaro Stars kilichotwaa ubingwa wa Kombe la Chalenji mwishoni mwaka jana.

Pia, amewachagua Shaban Kado na Mbwana Samata katika kikosi chake ili hali anajua wazi wachezaji hao wamo katika kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23, Ngorongoro Heroes kinachojiandaa na mechi dhidi ya Cameroon.Poulsen alisema kuwa timu zote hizo ni muhimu, lakini duniani kote timu ya taifa ya wakubwa ni muhimu zaidi.

Kwa mara ya kwanza Mdenmark huyo amewaita Kazimato na Dihile ambao waliwahi kuichezea Taifa Stars ilipokuwa ikinolewa na Marcio Maximo.Akizungumzia uamuzi wa Poulsen, kocha wa JKT Ruvu, Charles Kilinda alisema amefurahishwa na uteuzi wa wachezaji wake wawili Dihile na Kazimoto na kumtaka kuongeza idadi ya wachezaji kutoka kikosi cha maafande hao.

"Nimefurahi, kwanza nasema alikuwa hatutendei haki, alichelewa sana kuwaita, lakini Poulsen aangalie uwezekano wa kuongeza wengine kwani nina wachezaji wengi mahiri,"alisema Kilinda.

Naye Dihile aliyeiongoza Stars kucheza hatua ya mtoano ya michuano ya CHAN mwaka 2009 alisema; "Nimefurahi kwa sababu mwalimu ameona nafaa na mimi naahidi sitamuangusha nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kwa kushirikiana na wenzangu kuhakikisha tunaisaidia timu ifikie malengo yake.''

''Kwa sababu Mungu ndiye muweza wa yote na kila kitu ni juu yake hata hilo suala zima la ushindani wa makipa katika timu ya taifa yeye mwenyewe ndiye atafanikisha,''alieleza Dhile.Akizungumzia mchezo wa Machi 26, Poulsen alisema ni dhahiri utakuwa mgumu ukizingatia uzuri wa wapinzani wao Jamhuri ya Afrika ya Kati ambao wanaongoza kundi hilo na walipata ushindi ugenini dhidi ya Algeria.

"Tunahitaji pointi nne ili tujiweke katika nafasi nzuri ya kufuzu,tunafahamu wazi kwamba Jamhuri ya Afrika ya Kati si timu rahisi, waliifunga Algeria kwao, lakini na sisi tunataka ushindi pia, hivyo tutahakikisha tunashinda mechi hiyo,"alisema Poulsen.

Kikosi kamili kilichotangazwa jana mbele wa Wanahabari ni makipa Shaaban Kado, Juma Kaseja na Shaaban Dihile wakati mabeki ni Shadrack Nsajingwa, Aggrey Morris, Nadir Haroub'Canavaro', Stephano Mwasika,Haruna Shamte, Juma Nyoso na Idrisa Rashid.

Viungo ni Nurdin Bakari, Shaaban Nditi, Jabir Aziz, Henry Joseph, Abdi Kassim na Mwinyi Kazimoto huku washambuliaji ni Dan Mrwanda, Nizar Khalfan, Mrisho Ngassa, Mohamed Banka, Athumam Machupa, John Boko na Mbwana Samata.

Wakati huo huo; Salome Millinga anaripoti kuwa timu ya soka ya vijana U-23, Ngorongoro Heros leo itashuka dimbani uwanja wa Uhuru kucheza mechi yake ya kirafiki dhidi ya Azam FC kabla ya kuifuata Mtibwa Sugar, Machi 18 mjini Morogoro.

Akizungumza na Mwananchi, kocha Ngorongoro Heroes, Jamhuri Kihwelu alisema anategemea mechi hizo mbili zitamsaidia kujua mapungufu ya kikosi chake kabla ya safari ya Cameroon."Pia, tunasubiri majibu kutoka Shirikisho la soka Uganda kama timu yao itakuja huku kwa ajili ya mechi ya kirafiki au tutaenda kwao kucheza na timu ya U23 ya kwao," alisema Kihwelu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom