Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Timu 22 kuvaana gofu Gymkhana

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 11th March 2011 @ 23:00 Imesomwa na watu: 20; Jumla ya maoni: 0








TIMU 22 zimethibitisha kushiriki mashindano ya gofu yatakayofanyika kwenye viwanja vya Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam leo.

Mashindano hayo ya pili ya timu ambazo zinaundwa na wachezaji wawili wawili yamepangwa kufanyika katika mtindo wa ‘four ball better ball' katika viwanja 18.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Katibu mpya wa kusimamia viwango vya wachezaji Vikas Varma, timu hizo zitapambana katika makundi 11.

Ratiba hiyo inaonesha kuwa kundi litakaloanza kuchuana ni kati ya P.N. Kamani/Joseph Masawe ambao watavaana na Iddi Mzaki atakayeshirikiana na Tayana William.

Geoffrey Kilenga/P. Waweru wataoneshana kazi na Elia Mwaibanje/Michael Makala, Pele Svarvar/Joyce Svarvar dhidi ya Joseph Tairo/E. Maseke, wakati Shazi Myombe na Mwanaidi Ibrahim watachuana na timu ya Pembe Kondo na Salvatory Rwabizi katika mpambano unaotarajia kuwa mkali.

Mpambano mwingine utawapambanisha Katibu wa gofu Lawrance Pangani/C. Simatyaba dhidi ya Hamis Ally na Fatma Makame, Anil Chopra/N. Kanabar dhidi ya Mohamed Dewji/Ally Dewji.

Timu inayoundwa na M. Rahim/M. Jacksi itachuana na C. Sumbwe/H. Kabwe, Gautam Chavda/A. Patel wanaoneshana kazi na Balozi Salehe Tambwe anayeshirikiana na Katibu wa Klabu ya Gymkhana, Adam Ngamilo.

Bupesh Aima/M.Bharwani watavaana na nahodha wa gofu Joseph Tango anayeshirikiana na Mwenyekiti wa Chama cha Gofu Tanzania (TGU) Dioniz Malinzi, wakati H. Rahim/A. Nazarali watapambana na timu ya Foti Gwebe na Idd Mzaki.
 
Simba bingwa-Phiri

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro; Tarehe: 10th March 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 705; Jumla ya maoni: 0


03_11_xx5gub.jpg

Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri.
Habari Zaidi: Simba, Yanga majaribuni leo
Afrika ya Kati yaja kamili kuivaa Stars
Tamasha la wanahabari sasa kufanyika Cine Club
Miriam Mauki akamilisha video yake
Mshindi Kisura kuzawadiwa Sh mil. 5
Wasanii, Moro Veteran kuvaana leo
Timu 22 kuvaana gofu Gymkhana
Simba bingwa-Phiri
Rais Kikwete awapa Bajaj Survival Sisters
Nchimbi kubariki bonanza la wanahabari kesho
Wasanii Injili kuwania tuzo Jumapili
‘Tamasha letu linakubalika Afrika'
Michuano ya gofu ridhaa yapigwa jeki
Aliyeimba 'Vua kiatu' kunogesha tamasha la Pasaka
Katibu wa soka Tabora apigwa stop
Simba mambo safi
Wazenji wamkuna Julio
Ulimwengu huyooo TP Mazembe
Simba karata muhimu leo
Tanzania yaalikwa skwashi vijana Nairobi

Habari zinazosomwa zaidi: Balaa lingine kwa Chenge
Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
‘Housigeli' anataka kuniharibia ndoa
Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
Vatican yamvua jimbo Askofu
Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Patrick Phiri amejipa matumaini ya kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara nyingine baada ya kushinda mchezo dhidi ya Ruvu Shooting na kushika usukani wa Ligi Kuu Bara.

Kutokana na ushindi huo, amesema mkakati alionao ni kuhakikisha ushindi mnono unapatikana katika mchezo wao na AFC Arusha kesho na kwamba ingawa kimahesabu bado, lakini ameanza kuona dalili ya Simba kutetea ubingwa wake.

Akizungumza mjini hapa, baada ya timu yake kuifunga Ruvu Shooting bao 1-0 mchezo uliofanyika juzi kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini hapa, alisema haikuwa rahisi timu yake kuibuka na ushindi kutokana na ugumu wa mchezo huo.

" Nimefurahi kupata ushindi muhimu ambao unatutanguliza mbele na sasa nguvu zetu zote zipo kwenye mchezo dhidi ya AFC Arusha wiki hii na nina imani tutaendeleza wimbi la ushindi," alisema.

Phiri katika mchezo huo alikaa eneo la mashabiki baada ya kutolewa nje kwenye mchezo dhidi ya Yanga Jumamosi iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambao ulimalizika kwa timu hizo kufungana bao 1-1.

" Tunahakikisha pointi tatu kwenye mchezo wetu na AFC tutazipata na hapo ndipo tunaweza kusema ubingwa upo mikononi mwetu, " alisema.

Akizungumzia mchezo kati ya Simba na Ruvu Shooting, aliisifu timu hiyo kuwa ina wachezaji vijana na chipukuzi wenye uwezo mkubwa, kitendo kilichowafanya wachezaji wake kushindwa kupata bao kirahisi.

Naye Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Rage, akizungumza baada ya kumalizika mchezo huo, aliwapongeza wachezaji wake kwa kazi nzuri waliyoifanya kuwezesha kupatikana kwa ushindi muhimu uliokuwa ukitafutwa.

Simba inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 41, huku Yanga ikifuatia ikiwa na pointi 39 na Azam ni ya tatu ina pointi 36. Zote zimecheza mechi 18 na zimebakisha mechi nne.

Wakati huohuo, Kocha Mkuu wa Ruvu Shooting Charles Boniface, alisema timu yake ina nafasi ngumu katika kuhakikisha inabaki Ligi Kuu msimu ujao.

Akizungumza mjini hapa, Boniface alisema kinachohitajika kwa sasa ni kushinda michezo yote iliyobakia, ili iweze kubaki kwenye ligi hiyo.

Ruvu Shooting inashika nafasi ya tatu kutoka chini ikiwa na pointi 15, wakati AFC inashika nafasi ya mwisho ikiwa na pointi 11 na Majimaji inashika nafasi ya pili kutoka chini ikiwa na pointi 12. Timu mbili za chini ndizo zitashuka daraja.

"Tunahitaji tushinde michezo iliyobakia ambayo yote ni migumu, tumebakia kucheza na JKT Ruvu, Mtibwa Sugar, Majimaji na Azam, " alisema Boniface.

Alisema pamoja na wachezaji wake kucheza vuzuri katika michezo yao, bado wanakabiliwa na changamoto ya kukosa uzoefu mkubwa wa kiuchezaji, jambo linalosababisha kupoteza michezo yao hasa wanapocheza na timu zenye wachezaji wenye uzoefu wa ligi na mashindano ya kimataifa.

Akizungumzia mchezo wao na Simba, alisema wachezaji walijituma vilivyo na kuutawala kwa kipindi kirefu, lakini makosa madogo yaliyotokea ndiyo yaliyowezesha wachezaji wa Simba kuyatumia.
 
Simba bingwa-Phiri

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro; Tarehe: 10th March 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 705; Jumla ya maoni: 0


03_11_xx5gub.jpg

Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri.
Habari Zaidi: Simba, Yanga majaribuni leo
Afrika ya Kati yaja kamili kuivaa Stars
Tamasha la wanahabari sasa kufanyika Cine Club
Miriam Mauki akamilisha video yake
Mshindi Kisura kuzawadiwa Sh mil. 5
Wasanii, Moro Veteran kuvaana leo
Timu 22 kuvaana gofu Gymkhana
Simba bingwa-Phiri
Rais Kikwete awapa Bajaj Survival Sisters
Nchimbi kubariki bonanza la wanahabari kesho
Wasanii Injili kuwania tuzo Jumapili
‘Tamasha letu linakubalika Afrika’
Michuano ya gofu ridhaa yapigwa jeki
Aliyeimba 'Vua kiatu' kunogesha tamasha la Pasaka
Katibu wa soka Tabora apigwa stop
Simba mambo safi
Wazenji wamkuna Julio
Ulimwengu huyooo TP Mazembe
Simba karata muhimu leo
Tanzania yaalikwa skwashi vijana Nairobi

Habari zinazosomwa zaidi: Balaa lingine kwa Chenge
Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
‘Housigeli’ anataka kuniharibia ndoa
Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
Vatican yamvua jimbo Askofu
Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Patrick Phiri amejipa matumaini ya kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara nyingine baada ya kushinda mchezo dhidi ya Ruvu Shooting na kushika usukani wa Ligi Kuu Bara.

Kutokana na ushindi huo, amesema mkakati alionao ni kuhakikisha ushindi mnono unapatikana katika mchezo wao na AFC Arusha kesho na kwamba ingawa kimahesabu bado, lakini ameanza kuona dalili ya Simba kutetea ubingwa wake.

Akizungumza mjini hapa, baada ya timu yake kuifunga Ruvu Shooting bao 1-0 mchezo uliofanyika juzi kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini hapa, alisema haikuwa rahisi timu yake kuibuka na ushindi kutokana na ugumu wa mchezo huo.

“ Nimefurahi kupata ushindi muhimu ambao unatutanguliza mbele na sasa nguvu zetu zote zipo kwenye mchezo dhidi ya AFC Arusha wiki hii na nina imani tutaendeleza wimbi la ushindi,” alisema.

Phiri katika mchezo huo alikaa eneo la mashabiki baada ya kutolewa nje kwenye mchezo dhidi ya Yanga Jumamosi iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambao ulimalizika kwa timu hizo kufungana bao 1-1.

“ Tunahakikisha pointi tatu kwenye mchezo wetu na AFC tutazipata na hapo ndipo tunaweza kusema ubingwa upo mikononi mwetu, “ alisema.

Akizungumzia mchezo kati ya Simba na Ruvu Shooting, aliisifu timu hiyo kuwa ina wachezaji vijana na chipukuzi wenye uwezo mkubwa, kitendo kilichowafanya wachezaji wake kushindwa kupata bao kirahisi.

Naye Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Rage, akizungumza baada ya kumalizika mchezo huo, aliwapongeza wachezaji wake kwa kazi nzuri waliyoifanya kuwezesha kupatikana kwa ushindi muhimu uliokuwa ukitafutwa.

Simba inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 41, huku Yanga ikifuatia ikiwa na pointi 39 na Azam ni ya tatu ina pointi 36. Zote zimecheza mechi 18 na zimebakisha mechi nne.

Wakati huohuo, Kocha Mkuu wa Ruvu Shooting Charles Boniface, alisema timu yake ina nafasi ngumu katika kuhakikisha inabaki Ligi Kuu msimu ujao.

Akizungumza mjini hapa, Boniface alisema kinachohitajika kwa sasa ni kushinda michezo yote iliyobakia, ili iweze kubaki kwenye ligi hiyo.

Ruvu Shooting inashika nafasi ya tatu kutoka chini ikiwa na pointi 15, wakati AFC inashika nafasi ya mwisho ikiwa na pointi 11 na Majimaji inashika nafasi ya pili kutoka chini ikiwa na pointi 12. Timu mbili za chini ndizo zitashuka daraja.

“Tunahitaji tushinde michezo iliyobakia ambayo yote ni migumu, tumebakia kucheza na JKT Ruvu, Mtibwa Sugar, Majimaji na Azam, ” alisema Boniface.

Alisema pamoja na wachezaji wake kucheza vuzuri katika michezo yao, bado wanakabiliwa na changamoto ya kukosa uzoefu mkubwa wa kiuchezaji, jambo linalosababisha kupoteza michezo yao hasa wanapocheza na timu zenye wachezaji wenye uzoefu wa ligi na mashindano ya kimataifa.

Akizungumzia mchezo wao na Simba, alisema wachezaji walijituma vilivyo na kuutawala kwa kipindi kirefu, lakini makosa madogo yaliyotokea ndiyo yaliyowezesha wachezaji wa Simba kuyatumia.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom