Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Airtel Flava yazinduliwa Dar


na Shehe Semtawa


amka2.gif
KAMPUNI ya simu za mikononi ya Airtel jana ilizindua huduma ya ‘Airtel Flava', ambayo ni ya kwanza kutolewa hapa nchini na ya kipekee katika burudani kwa njia ya simu.
Meneja Masoko wa Kampuni hiyo, Kelvin Twissa, alisema wakati wa hafla ya uzinduzi jijini Dar es Salaam jana kuwa, huduma hiyo ya ziada katika simu ni ya kisasa zaidi, ambayo inamwezesha mteja wa Airtel kupata miziki mbalimbali katika simu yake na kuweza kumiliki, kuitumia na hata kuwatumia wengine vile apendavyo.
"Kwa kuwa na ‘Airtel Flava' wateja sasa wanaweza kujichagulia miziki waipendayo na kusikiliza kupitia simu zao za Airtel, wakati wowote kwa kupiga namba 15565 na kuchagua muziki husika," alisema Twissa.
Pia aliongeza kwamba, ikiwa imeambatana na aina kadha wa kadha, Airtel Flava inatoa fursa kwa msikilizaji kuchagua muziki wa kusikiliza, kulingana na hisia zake.
"Bila ya kujali aina ya muziki unaopenda kuchangamka nao, iwe wa kisasa au wa kizamani, kwa hakika kila mtu atapata kile akipendacho, Bongo Flava, Hip Hop, Rhumba, Taarab, Injili pamoja na zilipendwa," alisema Twissa.
Naye Meneja wa Huduma za Ziada wa kampuni hiyo, Frank Semaganga, alisema, ujio wa Airtel Flava, wateja wataweza kuchagua miziki na kuituma kwenye namba nyingine za ndugu, jamaa na marafiki, hata kuweza kuchagua muda na siku ya muziki aliochagua kumfikia mhusika.
Alisema, huduma hiyo inatolewa bure katika mwezi wa kwanza kwa kujiunga na kuwa, huduma ya Airtel Flava inatarajia kuleta mirindimo motomoto, hasa kwa wote wenye kupenda kupata burudani wakati wakiendelea kujishughulisha na kazi nyingine au wakiwa mapumzikoni.
 
Simba, Yanga zawindana


na Dina Ismail


amka2.gif
HOMA ya pambano la watani wa jadi katika soka hapa nchini, Simba na Yanga imeanza kupanda ambapo kamati za utendaji za timu hizo zikijipanga kukutana kwa ajili ya kuweka mikakati ya kuibuka na pointi tatu muhimu.
Wakati Yanga ikitarajiwa kukutana keshokutwa Jumapili, Simba inatarajiwa kukutana wakati wowote kuanzia sasa.
Vigogo hao wanatarajiwa kumenyana Machi 5, katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom itakayopigwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Timu hizo, zinaendelea kujifua kwa ajili ya mechi nyingine za ligi hiyo, ambako wachezaji wa Simba waliingia kambini juzi, huku Yanga wakifanya mazoezi ya kwenda na kurudi.
Ofisa habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema jana kwamba, kamati ya utendaji itakutana Jumapili kujadili masuala mbalimbali ya timu hiyo, hususani mwenendo wake katika ligi hiyo.
"Pamoja na hilo, pia watajadili mustakabali wa timu katika harakati za kuwania ubingwa," alisema.
Sendeu alisema, wachezaji wote wako katika hali nzuri, huku kiungo wake aliyekuwa majeruhi Shamte Ally akianza mazoezi magumu na wenzake.
Kwa upande wa Simba, wachezaji wake wote wameingia kambini hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam, huku wachezaji wote waliokuwa majeruhi wakipona isipokuwa Uhuru Seleman.
Katika hatua nyingine, kituo cha televisheni cha Super Sports cha Afrika Kusini, jana kilirekodi mazoezi ya timu ya Yanga yaliyokuwa yakifanyika uwanja wa Kaunda.
Aidha, kituo hicho kilifanya mahojiano na kocha mkuu Sam Timbe, nahodha Shadrack Nsajigwa ‘Fusso' na kipa Ivan Knezevic.
 
TASWA yampongeza Tenga


na Dina Ismail


amka2.gif
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kimempongeza Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga, kwa kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF).
Tenga alichaguliwa katika nafasi hiyo katika uchaguzi uliofanyika juzi huko Khartoum, Sudan, baada ya kumshinda Celestine Musabiyima wa Rwanda aliyekuwa akitetea nafasi hiyo.
"Taswa inaungana na wadau wa soka pamoja na wapenda michezo wengine wote Tanzania, kumtakia kila la kheri Tenga, ambaye pia ni Rais wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), katika wadhifa wake huo mpya, huku tukiamini utakuwa na manufaa kwa soka letu na ukanda huu kwa ujumla," ilisema taarifa ya TASWA iliyotolewa na Katibu Mkuu, Amir Mhando.
"Licha ya kumpongeza, lakini tunampa changamoto aelewe kwamba kutekeleza na kutelekeza ni maneno mawili yanayoshabihiana katika kuyatamka na usipokuwa makini, yanaweza kukuchanganya na kukupoteza kabisa," alisema Mhando.
Mhando aliongeza, "Haya ni maneno yenye maana tofauti, ambazo moja ni kama chanya na lingine hasi. Neno kutekeleza maana yake kwa tafsiri rahisi ni kufanya, wakati kutelekeza maana yake ni kutofanya, kuacha au kupuuzia."
Alisema TASWA inaamini Tenga atatekeleza mambo mbalimbali ambayo yalimsukuma kuwania wadhifa huo na hatayatelekeza na kama ataona kuna mambo magumu asiwe mvivu wa kuomba ushauri kwa Mtanzania mwingine aliyepata kushika wadhifa huo, Said Hamad El Maamry mwanzoni mwa miaka ya 80 kwa vipindi viwili mfululizo.
 
Mburahati yaichafua Real Tanzanite


na Ruhazi Ruhazi


amka2.gif
TIMU ya Mburahati Queens juzi iliichapa Real Tanzanite ya Magomeni, kwa mabao 3-0 katika mechi ya Ligi ya Soka Wanawake Mkoa wa Dar es Salaam.
Katika mechi hiyo iliyopigwa kwenye dimba la Karume, washindi walijipatia bao la kuongoza mapema dakika ya pili, mfungaji akiwa Irine Matowo.
Kabla Tanzanite hawajazinduka, Mwanahamisi Omari ‘Gaucho' akaipigia timu yake bao la pili dakika ya 11 na Sheila Juma akakandamiza la tatu dakika ya 21, hivyo kwenda mapumziko wakiwa kifua mbele.
Kipindi cha pili, kila timu ilifanya mabadiliko ambayo hayakuleta manufaa yoyote, hivyo hadi mwamuzi wa mchezo huo Nuru Mushi anapuliza filimbi ya mwisho, Mburahati 3, Tanzanite 0.
Ligi hiyo, inatarajiwa kuendelea tena leo saa 10:00 jioni kwenye uwanja huo kwa mechi kati ya majirani Evergreen Queens ya Tandika na Temeke Queens.
Aidha, kesho Jumamosi kutakuwa na mechi mbili, Mndela Queens dhidi ya EMIMA na baadaye Simba Queens watawavaa Mlimani Queens
 
Angola, Tunisa fainali ya CHAN leo Send to a friend Thursday, 24 February 2011 20:39

KHARTOUM, Sudan
MASHABIKI wa soka wa Angola wamewasili kwenye mji wa Khartoum nchini Sudan kuishangilia timu yao, Palancas Negras iliyoingia fainali ya CHAN, inayoshirikisha wachezaji wa Ligi za Ndani.

Angola itapambana na Tunisia katika mechi ya fainali leo kwenye Uwanja wa Merriekh mjini Kahertoum.

Mashabiki hao zaidi ya 100 walisafiri kwenda huko kuishangilia timu yao wakiamini watatwaa ubingwa. Angola iliingia fainali baada ya kuwafunga wenyeji Sudan kwa mikwaju ya penalti 4-2 baada ya mechi kumalizika kwa sare ya 1-1 baada ya dakika 120 mjini Omdurman.

Hata hivyo, mchezo huo ulimalizika kwa mashabiki wa soka kukasirishwa na timu yao na kuanza kurusha chupa na vitu vingine uwanjani.

Mashabiki zaidi ya 42,000 wanatarajiwa kufurika kwenye Uwanja wa Al Merreikh nchini kushuhudia mchezo huo.

Wakati timu hizo zikiingia fainali, wenyeji Sudan watacheza na Algeria katika mechi ya kutafuta mshindi wa tatu na nne.
 
Mkutano Mkuu Yanga waiva


Na Elizabeth Mayemba

KAMATI ya Utendaji ya Yanga, itakutana keshokutwa kupanga tarehe ya Mkutano Mkuu ulioombwa na Wanachama wa klabu hiyo.Akizungumza Dar es Salaam
jana Msemaji wa Yanga, Louis Sendeu alisema kamati hiyo imeamua kukutana keshokutwa baada ya Jumanne kushindikana kwa sababu baadhi ya viongozi hawakuwepo.

"Keshokutwa Kamati ya Utendaji itakutana kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali na ajenda kubwa itakuwa ni ile ya kupanga tarehe ya Mkutano Mkuu wa Wanachama," alisema Sendeu.

Alisema Jumanne walishindwa kukutana kwa sababu Mwenyekiti, Lloyd Nchunga na Makamu wake Davis Mosha, walikuwa safarini pamoja na baadhi ya wajumbe wengine, hivyo mpaka kufikia keshokutwa endapo kolamu ya wajumbe itatimia watafanya kikao hicho.

Hivi karibuni baadhi ya wanachama wa klabu hiyo, waliuomba uongozi wa Yanga kuitisha haraka Mkutano Mkuu wa dharura kwa lengo la kujadili mambo mbalimbali lokiwemo la kutoelewana baina viongozi.

Katika hatua nyingine, Sendeu alisema timu yake inaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Kaunda uliopo makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam chini ya kocha wake Mganda Sam Timbe.

Sendeu alisema wanajindaa na mchezo wao wa Jumatatu, dhidi ya Ruvu Shooting utakaochezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
 
Kaseba amdhihaki Francis Cheka


Na Amina Athumani

BINGWA wa Dunia wa mchezo wa ngumi na mateke (Kicboxing), Japheth Kaseba amemdhihaki Francis Cheka kwamba hamtishi kwa kuwa hana kiwango cha
kutisha, kwani anaitwa bingwa kwa sababu majaji waliamua hivyo.

Kaseba anatarajia kupanda ulingoni machi 16, mwaka huu dhidi ya Mada Maugo ambapo mshindi kati yao ataandaliwa pambano maalumu dhidi ya Cheka ambaye ni bingwa wa uzito wa kati nchini baadaye mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kaseba alisema hapigani na Maugo kwa ajili ya kuzichapa na Cheka, isipokuwa anacheza kama sehemu ya mchezo kuwapa raha mashabiki wake.

"Cheka anastahili kuitwa bingwa kutokana na maamuzi ya majaji tu, kwa sababu siku zote majaji wanaubeba mchezo, lakini ukiangalia kiwango na uwezo wake ni ule ule sioni kama kuna sababu ya kumwogopa namchukulia kama mabondia wengine," alisema Kaseba.

Akizungumzia pambano la awali dhidi ya Cheka lililopigwa mwaka jana, Kaseba alisema kilichomwangusha ni kukosa maandalizi, lakini kwa sasa anajianda vya kutosha.

Kuhusu pambano dhidi ya Maugo, alisema litakuwa rahisi kwake kwa kile alichodai kuwa anamfahamu vizuri mpinzani wake na kwamba hiyo ni sehemu ya maandalizi tu ya micheyo mingine.
 
Sheikh Yahaya atabiri vifo wanamichezo, waandishi Send to a friend Thursday, 24 February 2011 20:38

Sadick Mtulya
MTABIRI maarufu, Sheikh Yahya Hussein katika utabiri wake kwa mwaka 2011, amesema kutakuwa na vifo vya wanamichezo, wasanii na waandishi habari maarufu.

Vilevile amesema wanamichezo wengi watapata umaarufu na mafanikio na kwamba kutakuwapo na habari nyingi na nzuri za michezo

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam jana, Sheikh Yahya alisema hayo yatatokea kutokana na mwaka huu, kutawaliwa na sayari ya Saturn na Uranus ambazo zote zinaashiria matatizo na misukosuko.

"Kuanzia Januari 23, mwaka huu sayari ya Jupiter imeingia katika nyota ya Punda, kinyota mtasikia habari nyingi kuhusiana na masuala ya michezo, wanamichezo wengi kupata umaarufu na mafanikio.

"Vilevile mtasikia habari za vifo vya wanamichezo, wasanii na waandishi wa habari maarufu,'' alisisitiza Sheikh Yahya.

Alisema kutokana na mpangilio wa kinyota, kutakuwa na matukio ambayo yatabadilisha mwenendo mzima wa dunia na kuathiri maisha kwa ujumla na kwamba madhara yatakayoletwa na Sayari ya Uranus yatachukua miaka saba na inawakilisha mambo kadhaa yenye nguvu zaidi kila baada miaka 84.

Mtabiri huyo ambaye alijitapa kutabiri na matukio kuwa ya kweli ikiwamo ya chama cha CUF kuungana na CCM visiwani Zanzibar, ameonya watu walio katika sehemu za kutoa haki kwa wananchi wahakikishe wanafanya hivyo bila kupindisha na kwamba kinyume na hivyo watapata matatizo makubwa
 
BMT, TASWA wampongeza Tenga Send to a friend Thursday, 24 February 2011 20:38

Mwandishi Wetu
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kimetuma salaam za pongezi kwa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF baada ya Rais wake, Leodegar Tenga kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka afrika, CAF.
Tenga alimshinda Celestine Musabiyima wa Rwanda baada ya kupata kura 34 kati ya 53 zilizopigwa katika uchaguzi uliofanyika Khartoum, Sudan. Musabiyima alikuwa akitetea nafasi yake.

Mbali na Taswa, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limetoa pongezi kwa Tenga kuibuka kidedea katika kiny'anganyiro hicho cha ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya CAF. Tenga pia ni Rais wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati, CECAFA.

Mwenyekiti wa BMT, Iddi Kipingu alisema nafasi aliyoipata Tenga ni sifa kwa Tanzania na anatakiwa aitumie ipasavyo kwani kwa kufanya hivyo atailetea Tanzania sifa

Naye Katibu Mkuu wa Taswa, Amir Mhando alisema kuwa chama hicho kinaungana na wadau wa soka pamoja na wapenda michezo wengine wote Tanzania kumtakia kila la kheri Tenga katika wadhifa wake huo mpya, huku tukiamini utakuwa na manufaa kwa soka yetu na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Alisema kuwa licha ya kumpongeza, lakini wanampa changamoto aelewe kwamba kutekeleza na kutelekeza ni maneno mawili yanayoshabihiana katika kuyatamka na usipokuwa makini yanaweza kukuchanganya na kukupoteza kabisa.

ìHaya ni maneno yenye maana tofauti, ambazo moja ni kama chanya na nyingine hasi. Neno kutekeleza maana yake kwa tafsiri rahisi ni kufanya, wakati kutelekeza maana yake ni kutofanya, kuacha au kupuuzia."
 
Suluhu yakera wachezaji Man. United Send to a friend Thursday, 24 February 2011 20:36 0diggsdigg

LYON, Ufaransa
KIUNGO wa Manchester United, Michael Carrick amesema yeye na wachezaji wenzake, wamekerwa na suluhu dhidi ya Marseille ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 lakini akasema anaamini Red Devils itashinda mchezo wa marudiano.
Katika mchezo huo, kila upande ulishindwa kutumia nafasi ilizopata, na Darren Fletcher ndiye pekee aliyepata nafasi nzuri ya kumtungua kipa wa Marseille, Steve Mandanda lakini akashindwa kufunga.

Kikosi cha Sir Alex Ferguson kilichokuwa Stade Velodrome kina nafasi ya kutumia uwanja wa nyumbani licha ya kuelezwa kuwa si kigezo sahihi cha timu kushinda, na Carrick alisisitiza kusema, walicheza ovyo.

Aliiambia ITV Sport: "Tumesikitika kushindwa kufunga, lakini bado tuna nafasi ya kufanya vizuri nyumbani, lakini hiyo si kitu sana, kinachotakiwa ni kucheza vizuri zaidi ya mchezo wa kwanza.

"Mechi za ugenini ni ngumu hasa Ulaya, lakini tulichofanya hakifanani na sisi, tulistahiki kushinda.

"Tunaamini marudiano tutafanya kweli kwenye Uwanja wetu wa Old Trafford.
"Haikuwa kama vile tunataka, hatukucheza vizuri, hatukuwa makini kwa k ila tulichokifanya.

Naye kocha wa Manchester United, Ferguson alisema: ìMechi ilikuwa mbaya.
Wenzetu walihakikisha hatufungi. 0-0 ni matokeo mabaya, lakini sasa tunajiamini kwa kuwa tutakuwa nyumbaniî aliongeza Ferguson ambaye naye anaamini mambo yote yatakuwa Old Trafford wiki tatu zijazo.

ìSi matokeo mabaya sana, uzuri ni kwamba hatukuruhusu bao,î alisema kocha wa Marseille, Didier Deschamps. ìIlikuwa mechi ngumu dhidi ya timu ngumu yenye wachezaji wazuri.î

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge amekiri kuwa vijana wake wa Bavarian walikuwa na bahati hata kushinda bao 1-0 tena ugenini dhidi ya Inter katika mchezo wa kwanza wa raundi ya 16 ya Ligi ya Ulaya.

Rummenigge alisema kila upande ulipata nafasi ya kufunga, lakini vijana wake wa Bavarians walikuwa washindi mwisho wa siku.

"Kila timu zilipata nafasi nyingi na nzuri za kufunga, lakini wachezaji walishindwa kuzitumia," aliiambia Sky Sport baada ya mechi. "Ilikuwa mechi ya kufurahisha kuangalia.

"Tulikuwa na bahati na tunashukuru tumeshinda. Lakini hatuwezi kufikiria kuwa tayari tumeshafuzu. Lazima kujipanga vizuri zaidi tuweze kufika mbali," alisema.

Naye Rais wa Inter, Massimo Moratti amesema pamoja na vijana wake wa Nerazzurri kupoteza mchezo kwa kufungwa 1-0 na Bayern Munich kwenye Uwanja wa Giuseppe Meazza, bado wana imani kubwa kufuzu.

Mlezi huyo aliwapongeza wachezaji wake, kwa kucheza vizuri na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga kitu kinachompa matumaini kwa mchezo wa marudiano.

"Hatukuwa na bahati kwa jinsi mchezo ulivyokuwa," Moratti aliiambia Sky Sport baada ya mchezo. "[Kocha] Leonardo alifanya kazi nzuri, katika timu ilivyocheza, kwa kutengeneza mipira mingi, pasi na mashambulizi.

"Tunatakiwa kujipanga na kuicheza mechi vizuri, tunaweza hata kushinda 1-0 huko kwao Munich kwa jinsi tulivyocheza mchezo wa kwanza."

Moratti alisikitishwa kuumia kwa Andrea Ranocchia. Mchezaji huyo aliumia kifundo cha mguu na kushindwa kuendelea na mchezo. Kuumia kwa Ranocchia kweli kumetumaliza," alimaliza. Mechi za marudiano zitachezwa Machi 15.
 
Hayatou: Soka ya Afrika iko juu Send to a friend Thursday, 24 February 2011 20:35 0diggsdigg

KHARTOUM, Sudan
RAIS wa Shirikisho la Soka Afrika, CAF, Issa Hayatou ameuambia Mkutano Mkuu wa 33 wa CAF kuwa mwaka 2010 ulikuwa wa majonzi na furaha kwa Afrika.

Akiuelezea zaidi mwaka 2010 kuwa ni mwaka wa kipekee, Hayatou alisema Fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza zilifanyika katika ardhi ya Afrika . ìKwa mara ya kwanza, Afrika ilipewa heshima ya kuwa mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia, ikiwa ni miaka 53 tangu kuundwa kwa CAF.

Hapo kabla Afrika haikuwahi kupata heshima hiyo. Ilikuwa ikifahamika kama Bara la migogoro, majanga, magonjwa na lisilokuwa na maendeleo," alisema Hayatou.

Rais huyo wa CAF alisema,î Afrika ilipeleka salamu tosha kila eneo la dunia akiwemo Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki, IOC, Jacques Rogge kuwa Afrika nayo inaweza kuwandaa Michezo ya Olimpiki.

Hayatou alimpongeza Rais wa FIFA, Joseph Blatter kwa kuwa ndiye aliyesimama kidete kuhakikisha Fainali za Kombe la Dunia zinafanyika Afrika. ìBlatter...Waafrika, hawana maneno ya kumwambia zaidi ya asante ì alisema Hayatou.

Hayatou alisema kuwa ni heshima kwa Sudan ambaye ni mwananchama mwanzilishi wa CAF kuwa mwenyeji wa michuano ya CHAN mwaka huu na wameandaa kwa mafanikio makubwa.

Alisema CHAN ni moja ya michuano inayotumiwa na kwa ajili ya makocha kupata uzoefu na timu 15 kati ya timu 16 zilikuwa na makocha wazawa.

Timu ya wanawake ya Nigeria ya U-20 itakayoshiriki Kombe la Dunia na TP Mazembe ya DR Congo ni kati ya klabu zilizokuwa na mafanikio Afrika kwa mwaka 2010.

Rais wa FIFA aliwapongeza viongozi wa soka Afrika kwa kufanikisha Fainali za Kombe la Dunia 2010 na kusema waliokuwa wakiidharau Afrika, wameumbuka.

Blatter alisema kuwa habari njema ni kwamba Fainali za 2010, FIFA wamevuna dola 1. 2 bilioni ikilinganisha na dola 600 million za Fainali za 2006 nchini Ujerumani. ìVyama vya soka na mashirikisho Afrika vitapata mgawo waoî alisema Blatter aliyeipongeza CAF kwa kuanzisha michuano ya CHAN.
 
Liverpool beats Sparta 1-0 to make last 16


storypage_APlogo_01.png




PRINT RSS



Updated Feb 24, 2011 6:26 PM ET
Dirk Kuyt headed in a late winner as Liverpool beat Sparta Prague 1-0 in the second leg of their Europa League last-32 match to squeeze through by the same score on aggregate on Thursday.
The Netherlands forward glanced home an inswinging corner from Raul Meireles in the 86th minute, sparing the three-time competition winners the need for extra time at Anfield.

abacus_20100819181442_0_0.GIF
EL Scores | Tables | Fixtures

"It took us a while to score but 1-0 is enough to go through so we're happy with that," Kuyt said. "It was a hard game and we should have finished it off earlier, but at the end of the day a win is all that counts."
Liverpool, which will play Lech Poznan or Braga in the second knockout round, dominated the second leg but could not find a way past goalkeeper Jaromir Blazek until Kuyt's late goal.
Sotirios Krygiakos had a header tipped round the post, Meireles volleyed over from Martin Kelly's cross, and lone striker David Ngog had a shot parried away by Blazek as Liverpool, missing captain Steven Gerrard, laid siege on Sparta's goal in the first half.
The visiting Czech side played its part in an entertaining match but failed to create the kind of chances its opponents did, with Blazek denying Ngog and Kuyt early in the second half.
Kuyt, who worked tirelessly down the right wing, got the goal he deserved when he drifted away from his marker and buried a header into the corner from five yards.
"I think we deserved it," Liverpool manager Kenny Dalglish said. "We had a lot of chances and didn't take them, but the boys deserve a lot of credit.
"They hung in really well and showed the determination and effort to get a result."
The Europa League represents the Reds' last chance of silverware this season. They have been knocked out of both domestic cup competitions and sit sixth in the Premier League.
 
Thursday, February 24, 2011​
Round of 32​

Anfield
Expand

6140.gif

Liverpool​
1 : 0
Final


Sparta Prague​
6323.gif


Match Stats | Match Trax
goal.gif
(85') Dirk Kuyt
Goals
yellow-card.gif
(30') Martin Kelly
yellow-card.gif
(35') Christian Bager Poulsen
yellow-card.gif
(59') Jamie Carragher
yellow-card.gif
(90') Lucas Leiva
Cards Manuel Pamic (32')
yellow-card.gif

Marek Matejovsky (40')
yellow-card.gif

Leonard Kweuke (64')
yellow-card.gif

greenArrow.gif
(46') Jamie Carragher
redArrow.gif
Martin Kelly

greenArrow.gif
(65') Jay Spearing
redArrow.gif
Christian Bager Poulsen

greenArrow.gif
(85') Martin Skrtel
redArrow.gif
Daniel Agger

Substitutions Jakub Podany (74')
greenArrow.gif

Libor Sionko
redArrow.gif


Tomas Pekhart (78')
greenArrow.gif

Martin Achille Abena Biholong
redArrow.gif


Andrej Keric (90')
greenArrow.gif

Manuel Pamic
redArrow.gif



Jose Alvalde
Expand

6451.gif

Sporting Lisbon​
2 : 2
Final


Rangers​
6208.gif


Match Stats | Match Trax
goal.gif
(42') Pedro Mendes
goal.gif
(83') Yannick Djalo
Goals El Hadji Diouf (20')
goal.gif

Maurice Edu (90')
goal.gif

yellow-card.gif
(10') Alberto Zapater
Cards Maurice Edu (58')
yellow-card.gif

greenArrow.gif
(81') Saleiro
redArrow.gif
Pedro Mendes

greenArrow.gif
(87') Andre Santos
redArrow.gif
Hélder Postiga

greenArrow.gif
(90') Nuno Coelho
redArrow.gif
Matías Fernández

Substitutions Kyle Lafferty (71')
greenArrow.gif

David Weir
redArrow.gif


Vladimir Weiss (71')
greenArrow.gif

John Fleck
redArrow.gif


David Healy (82')
greenArrow.gif

El Hadji Diouf
redArrow.gif



BayArena
Expand

6133.gif

Bayer Leverkusen​
2 : 0
Final


FC Metalist Kharkiv​
10418.gif


Match Stats | Match Trax
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom