Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Angola, Tunisia fainali CHAN Send to a friend Wednesday, 23 February 2011 19:59

KHARTOUM, Sudan
TIMU ya Angola imewachapa wenyeji Sudan kwa penati 4-2 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika dakika za kawaida na kupata tiketi ya kucheza fainali ya fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani ya bara la Afrika.

Pia timu ya Tunisia na yenyewe imepata tiketi ya kucheza fainali baada ya kuifunga Algeria kwa penati 5-3 baada ya kutoka sare ya 1-1 katika dakika za kawaida.

Kwa matokeo hayo Angola na Tunisia zitacheza mechi ya fainali Februari 25, huku wenyeji Sudan waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa kombe hilo wakicheza mechi ya kuwania mshindi wa tatu dhidi ya Algeria kabla mechi ya fainali haijachezwa.

Katika mechi kati ya Angola dhidi ya wenyeji Sudan, mashabiki wa soka wa Sudan wapatao 42,000 walijitokeza kushuhudia mechi hiyo ya nusu fainali na kuujaza uwanja wa Al-Merreikh uliopo huko Omdurman, lakini ndoto za mashabiki hao kushuhudia timu yao ikiingia fainali ziliyeyuka baada ya Mohamed Tahir na Mudathir Eltaib kukosa penati.

Angola wenyewe walifunga penati nne huku Masunguna 'Dani' Afonso akifunga penati ya mwisho ambayo iliipeleka Angola fainali.

Katika mechi hiyo, Sudan walikitawala kipindi cha kwanza, ambapo mshambuliaji wa Sudan, Saifeldin Ali Idris aliipatia timu yake bao la kwanza, mbele ya raisi wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA, Sepp Blatter, raisi wa Shirikisho la Soka Barani Ulaya, Michel Platini na raisi wa Shirikisho la Soka Asia AFC,Mohamed Bin Hammam.

Viongozi hao wa mashinrikisho hayio makubwa wapo Afrika kwa ajili ya kushiriki mkutano mkuu wa Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF.

Hata hivyo katika dakika ya 71, Angola walisawazisha bao hilo ambalo lilifungwa na Arsenio 'Love' Cabungula aliyeunganisha faulo iliyopigwa na Osorio Carvalho.

Baada ya kusawazishwa bao hilo baadhi ya mashabiki wa Sudan walianza kurusha mawe uwanjani, pia mashabiki hao walifanya hivyo katika dakika majeri baada ya kipa wa Angola, Luis 'Lama' Joao kupoteza muda.

Baada ya kusawazishwa bao hilo pia hasira zilionyeshwa hadi kwa wachezaji uwanjani, ambapo kipa wa Sudan, Baha Eldin alichezea faulo ya wazi mchezaji hatari wa Angola, Regio 'Mingo Bille' Zalata.

Pia beki wa Sudan, Haitham Mostafa katika dakika ya 23 ya dakika za nyongeza alipewa kadi nyekundu baada ya kumpiga kiwiko mchezaji wa Angola, ambapo refa kutoka Angola alimuona na kumpa kadi nyekundu.

Katika mechi ya Tunisia dhidi ya Algeria, timu ya Tunisia ilifunga penati zote tano katika mechi nyingine ya nusu fainali iliyochezwa kwenye Uwanja wa Khartoum, huku Khaled Korbi akifunga penati ya mwisho baada ya Hocine Metref kukosa penati kwa upande wa Algeria.

Katika mechi hiyo, Tunisia ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao baada ya Slama Gasdaoui kuipatia bao timu hiyo katika dakika ya 18, ambapo alipiga mpira uliokwenda upande wa kushoto wa kipa Mohamed Zemmamouche.

Katika kipindi cha pili Algeria ilifanya mabadilipo ilimuingiza Hadj Aissa aliyesaidia kuongeza mashambulizi katika safu ya ushambuliaji na hivyo Abdelmoumene Djabou alipiga shuti la mbali na kuipatia timu yake bao la kusawazisha.

Timu hizo zilikwenda katika muda wa ziada baada ya muda wa wakawaida kumalizika huku wachezaji wakiona wamechoka baadaya kutumia knguvu nyingi katika dakika 90 za kawaida.

Mashindano hayo ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi kuu za ndani ya bara la Afrika yalianza Februari nne na yanatarajiwa kumalizika Februari 25 kwenye Uwanja wa Merreikh nchini Sudan.
 
TFF yaitaka ZFA kuunda Vijana Stars


Na Zahoro Mlanzi

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limekiandikia Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), kuteua Kocha Msaidizi wa timu ya taifa ya
vijana chini ya umri wa miaka 23 (Vijana Stars) kwa ajili ya michuano ya Olimpiki.

Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Julai 27, mwakani na kumalizika Agosti 12 katika jiji la London nchini Uingereza ambapo michezo mbalimbali itakuwepo kwenye michuano hiyo.

Kwa mujibu wa ratiba ya michuano hiyo, Vijana Stars itaanza kampeni zake za kuwania kucheza michuano hiyo Machi 26, mwaka huu kwa kuumana na Kameroon ugenini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na kusainiwa na Ofisa Habari wa shirikisho hilo, Boniface Wambura ilieleza kwamba kocha atakayeteuliwa na ZFA, atapaswa kuchagua wachezaji kati ya 10 mpaka 15.

"Baada ya kufanya uteuzi huo, wachezaji hao watajiunga moja kwa moja na wenzao 25, ambao wameanza mazoezi leo (jana) chini ya makocha Addolph Richard na Jamhuri Kihwelo," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Alisema baada ya wachezaji hao kutoka Zanzibar kuungana na wenzao kwa ajili ya mazoezi, benchi la ufundi litafanya mchujo ili kubaki na kikosi cha mwisho cha wachezaji 25, ambacho ndicho kitakachoikabili Kameroon.

Aliongeza kwamba Vijana Stars inatarajia kucheza mechi mbili za kirafiki kati ya Machi 12 au 13 na 19 au 20 mwaka huu. Safari ya Yaounde kwa timu hiyo inatarajiwa kufanyika Machi 22 mwaka huu.
 
Phiri apata matumaini ya Echessa, Uhuru Send to a friend Wednesday, 23 February 2011 20:03

Sosthenes Nyoni na Jesca Nangawe
KOCHA wa Simba Patric Phiri huenda sasa atambea kifua mbele baada ya Kiungo wake Hilary Echesa aliyekuwa majeruhi kurejea kikosini huku Uhuru Suleiman akianza mazoezi mepesi.

Echesa ambaye alikuwa katika mapumziko ya wiki mbili nyumbani kwao nchini Kenya akiuguza nyama za paja alirejea nchini juzi na jana jioni alitarajia kuanza mazoezi kwenye ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam.

Afisa habari wa Simba, Cliford Ndimbo aliliambia Mwananchi jana kuwa kurejea kwa Echessa kumefanya kikosi hicho kutokuwa na majeruhi baada ya Uhuru Suleiman naye kupona.

Alisema pia kuwa mlinda mlango namba mbili wa Simba Ally Mustapha 'Barthezi' ambaye alikuwa anasumbuliwa na Malaria kwa sasa yuko fiti na anaendelea na majukumu yake ya kuitumikia klabu hiyo.

Naye Selemani anatarajia kuanza mazoezi mepesi ya gym mara baada ya kumaliza wiki tisa alizopewa huku akidai hana haraka ya kurudi uwanjani hadi hapo mguu wake utakapopona kabisa.
Uhuru ambaye hivi karibuni alifanyiwa upasuaji wa goti nchini India kwa sasa anaendelea na matibabu yake na kwa mujibu wa daktari wake anatakiwa kuanza mazoezi mara baada ya kumaliza muda aliopewa wa kupumzika.

Akizungumza na Mwananchi Uhuru alisema anamshukuru Mungu kwani hali yake inazidi kumarika na ataendelea na mazoezi ya kuendesha baiskeli katika gym iliyopo maeneo ya Veta jijini Dar es salaam.
 
Madrid yashikwa lyon, Chelsea Yatesa Copenhagen Send to a friend Wednesday, 23 February 2011 20:01

LONDON, England
TIMU ya Real Madrid ilishindwa kuitambia Lyon baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 huku timu ya Chelsea ikiichapa bao 2-0 FC Copenhagen na kukaribia kuingia hatua ya robo fainali.

Alikuwa mshambuliaji wa Lyon, Bafetembi Gomis aliyeondoa furaha ya Real Madrid baada ya kuisawazishia timu yake bao katika dakika ya 83 wakati Real Madrid ilikuwa ikiongoza kwa bao 1-0 lililokuwa limefungwa na Karim Benzema.

Benzema alifunga bao hilo baada ya kuwatoka mabeki watatu wa Lyon katika eneo la penati na kumchambua kipa wa Lyon, Hugo Lloris.

Kwa matokeo hayo, klabu ya Lyon imeendeleza rekodi yake ya kutofungwa na Real Madrid katika mashindano hayo ya Klabu Bingwa barani Ulaya katika mechi saba walizowahi kukutana.

"Wanao wachezaji wazuri, kocha mzuri na mwenye uzoefu barani Ulaya, hivyo mechi ya pili itakuwa ngumu zaidi, nadhani nimechangia Real kufanya vizuri katika mechi hii kwa sababu ilikuwa ni mechi ngumu iliyokuwa na mpambano wa kweli na zilitengenezwa nafasi chache,"alisema kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho.

Kwa upande wa Chelsea ambayo haijawahi kushinda taji kubwa barani Ulaya, yenyewe ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Copenhagen, mabao ambayo yalifungwa na Nicolas Anelka.

Ushindi huo umemsaidia kocha wa Chelsea ambaye alikuwa akilalamikiwa kushindwa kuipa ushindi timu hiyo baada ya Chelsea kutolewa katika mashindano ya kombe la FA wikiendi iliyopita.

"Hii ni soka, unatakiwa ufanye mambo mazuri haraka kama ulipata matokeo mabaya, unatakiwa usitoke nje ya mtazamo wako mzuri, wachezaji wangu walijituma sana, walicheza soka nzuri sana na matokeo ni mazuri,"alisema kocha wa Chelsea, Carlo Ancelotti.

Naye kocha wa Lyon, Claude Puel alisema,"Nimeridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na vijana wangu, pia bado ipo mechi ya marudiano ambayo tunaweza kuitumia vizuri."

Alisema,"bado tuna nafasi ya kufuzu na hilo ni jambo la msingi, itabidi tuwe imara katika mechi ijayo, kwa sababu katika mechi hii tulipata nafasi nzuri, lakini hatukuzitumia vizuri."

Katika mechi ya Chelsea dhidi ya Copenhagen, mshambuliaji mpya wa Chelsea, Fernando Torres alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kufunga bao, lakini alishindwa kutumia nafasi alizozipata.

Lakini katika mechi hiyo aliyetamba alikuwa Nicolas Anelka ambaye alifunga bao la kwanza katika dakika 17, ambapo alifunga bao la pili katika dakika ya 54 pia.

Akimuongelea Torres, kocha wa Chelsea, Carlo Ancelotti alisema,"Jambo la msingi katika mechi hii lilikuwa ni kazi ya mshambuliaji kama alivyoifanya Torres, lakini hakuwa na bahati ya kufunga ingawa alicheza mchezo mzuri sana."

Akizungumzia pambano hilo kocha wa Copenhagen, Stale Solbakken hakulalamikia kichapo alichokipata ambapo alisema,"Walikuwa imara kutuzidi sisi na tulifanya makosa mengi ya kiufundi, walikuwa wana kasi na wepesi, ila wapo wachezaji wangu waliocheza vizuri sana na wengine walijitahidi."

"Labda hatukuwa wazuri kama Chelsea, lakini siku moja tutawakaribia, kwa swababu hivi sasa tumekubali Chelsea wametufunga bao 2-0,"alisema Stale Solbakken.

Timu hizi zitarudiana tena Machi 16.
 
MZFA yaliomba jiji la Mwanza liisaidie Toto

Imeandikwa na Nashon Kennedy, Mwanza; Tarehe: 24th February 2011 @ 09:06 Imesomwa na watu: 12; Jumla ya maoni: 0







CHAMA cha Soka Mkoa wa Mwanza (MZFA) kimeuomba uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuisaidia timu ya Mkoa huo ya Toto African ili iweze kufanya vizuri katika mechi zake za Ligi Kuu zinazoendelea nchini kwa hivi sasa.

Rai hiyo imetolewa jana jijini hapa na Mwenyekiti wa MZFA Jonas Songora muda mfupi baada ya kumalizika kwa hafla ya kutiliana mkataba wa kurusha matangazo ya ligi ngazi ya Wilaya ya Ilemela ya moja kwa moja kutoka katika Kituo cha Runinga cha Barmeda TV.

Kampuni hiyo ilikubaliana na Chama cha Soka cha Wilaya ya Ilemela (NDFA) kuwa inarusha matangazo ya ligi ya soka ya wilaya katika kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia sasa.

Songora aliutaka uongozi wa Halmashauri ya Jiji kutambua kuwa Timu ya Toto African ni kati ya timu za Mkoa wa Mwanza ambazo zimeweza kuzalisha vipaji vya wanamichezo mahiri ambao wameleta mchango mkubwa katika soka nchini na kuwa kuiacha inasuasua ni aibu kubwa kwa taifa na wapenda soka.

"Leo tumemaliza hili la wenzetu kutusaidia katika kuibua vipaji, lakini tunayo Timu yetu ya Toto African ambayo ndiyo inasababisha mechi za Ligi Kuu kuletwa hapa Mwanza, kwa moyo mkunjufu niuombe uongozi wa Jiji letu la Mwanza ujitokeze kuisaidia timu yetu kwa hali na mali ili iweze kufanya vizuri zaidi katika ligi," alisema Songora na kuongeza kuwa kikosi cha Toto kinao vijana mahiri wenye nia ya kulisakata kabumbu lakini wamekuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi.

Alisema, ana imani kubwa na Baraza jipya la sasa la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji, ambao wengi wao wana damu ya kupenda soka na kuwa MZFA imeona ni bora iwasilishe kilio hicho cha Toto kwa uongozi wa Jiji.

"Sasa hivi Baraza letu la Madiwani lina watu ambao ukiwaangalia unaona kabisa wana moyo wa kupenda soka, hivyo nasi MZFA tunawaomba kwa dhati waisaidie timu yetu ya Toto ili iendelee kuubeba mkoa wetu huu kwenye michuano ya Ligi Kuu inayoendelea na hivyo isiweze kushuka daraja,"
 
Gofu waanza maandalizi ya Olimpiki

Imeandikwa na Betram Lengama; Tarehe: 24th February 2011 @ 09:06 Imesomwa na watu: 10; Jumla ya maoni: 0








KLABU ya Gymkhana Dar es Salaam imeanza rasmi programu maalumu ya kufundisha gofu kwa vijana wadogo kwa lengo la kuhamasisha mchezo huo hapa nchini na kuanza maandalizi ya kutengeneza timu ya Olimpiki.

Mchezo wa gofu kwa mara ya kwanza utaingia kwenye orodha ya michezo ya Olimpiki ya mwaka 2016 itakayofanyika Rio de Janeiro, Brazil.

Nahodha wa mchezo wa klabu hiyo, Joseph Tango alibainisha hayo alipozungumza na waandishi wa habari jijini jana akisema kuwa programu hiyo ambayo ni ya kudumu imekwishaanza tangu Jumamosi iliyopita na inawalenga vijana wenye umri wa miaka chini ya 18.

Tango alisema kutokana na vijana wengi wenye umri huo kuwa shule katika kipindi hiki programu hiyo itakuwa ikifanyika katika siku mbili za juma, Jumamosi na Jumapili ikisimamiwa na wakufunzi watatu wa mchezo huo akiwepo mchezaji wa kulipwa Hassan Mwanyeza na Bryceson Nyenza na mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa Aidan Nziku.

"Tunawaomba wazazi wawaruhusu watoto wao kwa wingi hasa wale wa kike ambao huwa ni wachache katika mchezo huu wa gofu waje kujifunza namna ya kuucheza ukizingatia mafunzo yenyewe yatakuwa yakitolewa bure hapa klabuni," alisema Tango.

Aliongeza kuwa klabu yake imepokea mabegi sita ya vifaa vya mchezo huo ambavyo vitatumika katika kuwanoa vijana kutoka kwa Chama cha Gofu Tanzania (TGU).

TGU ilipokea zaidi ya mabegi 30 kutoka kwa chama cha kimataifa cha mchezo huo ambacho kipo chini ya Klabu ya Gofu ya Royal Ancient ya Scotland mwaka jana ambavyo vimesambazwa klabu mbalimbali.

Nahodha huyo alisema kuwa wanahamasisha wajitokeze zaidi vijana wa kike kutokana na ukweli kuwa wachezaji wa jinsia hiyo wanaoshiriki ni wachache kiasi cha kufikia kushindwa kupata wawakilishi wa jinsia hiyo katika umri huo wa kushiriki kwenye michuano mbalimbali ya kimataifa.

" Kila mwaka chama cha gofu duniani hutoa udhamini kwa wachezaji wawili kushiriki michuano ya dunia kwa ajili ya vijana wa umri huo, lakini kwa miaka miwili mfululizo tumekosa vijana wa kike ambao wangekwenda kutuwakilisha kwenye michuano hiyo ," alibainisha Tango.

Aidha Tango alisema programu hiyo vilevile itasaidia kujiandaa na kupata wachezaji ambao wanaweza kutuwakilisha kwenye michezo ya Olimpiki ijayo ukiacha ya mwakani ambayo itafanyika jijini London.

Katika hatua nyingine klabu ya Gymkhana ya jijini Dar es Salaam itaanza mradi wa kutandaza mabomba ya umwagiliaji kwenye uwanja wake wa gofu ambayo katika harakati za kukiboresha na kuwa na kijani kibichi muda wote na kufikia viwango vya kimataifa.

Kwa mujibu wa nahodha Tango lengo ni kukifanya kiwanja hicho kiwe na hadhi ya kimataifa ambapo mradi huo unatarajiwa kukamilika baada ya kipindi cha miezi mitatu.

Wakati huohuo, shindano la Kombe la Nahodha litafanyika keshokutwa kwenye Viwanja hivyo vya Gymkhana, shindano ambalo pia litatumika kama sehemu ya kuuaga uongozi unaomaliza muda wao uliokuwa chini ya nahodha Joseph Tango baada ya kuwa madarakani kwa mwaka mmoja.

Uchaguzi wa kupata viongozi wapya utafanyika mapema mwezi ujao.
 
Zanzibar Ocean View yaahidiwa Sh. mil 20

Imeandikwa na Mwandishi Wetu, Zanzibar; Tarehe: 24th February 2011 @ 08:53 Imesomwa na watu: 52; Jumla ya maoni: 0







WAWAKILISHI wa Zanzibar kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika Zanzibar Ocean View wameahidiwa Sh milioni 20 endapo wataitoa AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwenye michuano hiyo.

Ahadi hiyo ilitolewa na Meneja wa Hoteli za Zanzibar Ocean ViewAbdul Hemed kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar wakati timu hiyo ilipokuwa ikiondoka.

"Sisi Hoteli ya Zanzibar Ocean View tutatoa Sh milioni 10 na hoteli yetu iliyopo Pemba pia itatoa kiasi kama hicho kwa wachezaji endapo wataitoa Vita mashindanoni na kusonga mbele,"alisema.

Zanzibar inahitaji ushindi kusonga mbele kwenye michuano hiyo baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1- katika mechi ya kwanza iliyochezwa mwanzoni mwa mwezi huu kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa.

Ikishinda mechi hiyo na kuiondoa Vita kwenye kinyang'anyiro hicho, Zanzibar Ocean View itamenyana na mshindi wa mechi kati ya Vital ‘O' ya Burundi na Coton Sport de Garoua ya Cameroon.

Msafara wa wachezaji 19 chini ya kocha wa timu za taifa za vijana Abdulfataha Abbas akisaidiwa na Saidi Kwinzi pamoja na viongozi wanne uliondoka jana kwa ndege ya Shirika la Kenya ambapo ulitarajiwa kulala Nairobi jana kabla ya safari ya Congo mapema leo.

Mechi hiyo itachezwa Jumapili saa 9:30 kwa saa za kule ambapo huku itakuwa saa 10:30. Wawakilishi wengine wa Zanzibar kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho KMKM waliondoka mjini hapa tangu jana na walishafika Congo jana mapema.

KMKM itacheza na DCMP ya hukohuko Congo. Timu hiyo ina wakati mgumu kusonga mbele kwani ilichapwa mabao 4-0 katika mechi ya kwanza iliyochezwa Zanzibar.
 
ZFA yatakiwa kuchagua kocha msaidizi U-23

Imeandikwa na Evance Ng'ingo; Tarehe: 24th February 2011 @ 08:53 Imesomwa na watu: 26; Jumla ya maoni: 0








Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limekiandikia barua Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kiteue kocha msaidizi wa timu ya Taifa chini ya umri wa miaka 23, Vijana Stars.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Ofisa Habari wa TFF Boniface Wambura kocha huyo atakuwa na jukumu la kuteua wachezaji wasiopungua 10 wa wasiozidi 15.

Alisema kuwa wachezaji hao watajiunga na kikosi cha awali cha wachezaji 25 kilichotangazwa juzi na Kocha wa timu hiyo Jamhuri Kihwelo ‘Julio'.

Wambura alisema kuwa baada ya wachezaji hao kutoka Zanzibar kuungana na wenzao kwa ajili ya mazoezi, benchi la ufundi baadaye litafanya mchujo ili kubaki na kikosi cha mwisho cha wachezaji 25 ambacho ndicho kitakachoikabili Cameroon katika mechi ya kwanza na ile ya marudiano itakayochezwa jijini Dar es Salaam.

U-23 inatarajia kucheza mechi mbili za kirafiki kati ya Machi 12 au 13 na 19 au 20 mwaka huu. Safari ya Yaounde kwa timu hiyo inatarajiwa kufanyika Machi 22 mwaka huu.

Mechi hiyo ya mchujo kwa ajili ya kufuzu michuano ya Olimpiki dhidi ya Cameroon inatarajiwa kuchezwa Machi 26 jijini Yaounde.
 
Mashujaa yaibomoa Diamond Musica

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 24th February 2011 @ 08:53 Imesomwa na watu: 20; Jumla ya maoni: 0








BENDI ya muziki wa dansi ya Mashujaa imeiumiza bendi ya Diamond Musica kwa kuwachukulia wanamuziki wake sita.

Akizungumza Dar es Salaam jana alipowatambulisha wanamuziki hao kwa waandishi wa habari Meneja wa Mashujaa Mujibu Taratibu, alisema ametambulisha wanamuziki hao ili kuimarisha bendi hiyo yenye maskani yake Vingunguti jijini.

Wanamuziki hao ni marapa Yanick Noa 'Sauti ya Radi', Mirinda Nyeusi a.k.a Extra Power na safu ya unenguaji ni Salma Bonge, Mariam, Korando, Kevin na Mega.

"Mwaka 2011 tumeamua kujipanga zaidi kuhakikisha tunafanya mambo makubwa na kutoka hatua moja kwenda nyingine," alisema Taratibu.

Alisema, kwa sasa bendi yao inajiandaa kutoa albamu ya pili katikati ya mwaka huu ndiyo sababu ya kuendelea kujiimarisha zaidi ili bendi yao iwe na ushindani ndani na nje ya nchi.

Akizungumza kwa niaba ya wanamuziki wenzake Sauti ya Radi alisema amekuja kufanya kazi Mashujaa kwa kufanya mambo makubwa katika anga za muziki Tanzania.
 
Mtibwa yaikamua Toto

Imeandikwa na Grace Chilongola, Mwanza; Tarehe: 24th February 2011 @ 08:49 Imesomwa na watu: 59; Jumla ya maoni: 0








TIMU ya Mtibwa Sugar ya Morogoro, jana ilitamba ugenini baada ya kuitandika Toto African mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini hapa.

Matokeo hayo yanaifanya Mtibwa Sugar izidi kujiimarisha katika nafasi ya nne kwenye msimamo ikiwa na pointi 30.

Wageni ndio walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza katika dakika ya 47 kupitia kwa Vicent Salamba kabla wenyeji Toto hawajasawazisha katika dakika ya 51 likifungwa na Tete Kanganga.

Salum Machaku aliiongezea Mtibwa Sugar bao la pili katika dakika ya 79 katika mechi hiyo ambayo kipa wa Mtibwa Sugar Shaaban Kado hakuimaliza baada ya kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi Judith Gamba wa Dar es Salaam.

Katika mechi nyingine iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma jana, Kagera Sugar iliendelea kuitambia Polisi ya huko msimu huu baada ya kuifunga bao 1-0.

Bao la Kagera lilifungwa na mshambuliaji wake Gaudence Mwaikimba katika dakika ya 53 na kuifanya timu yake ifikishe pointi 29 katika nafasi ya tano kwenye msimamo.

Nazo timu za African Lyon na Ruvu Shooting zilirudia matokeo yake ya mzunguko wa kwanza kwa kutoka sare ya bila kufungana katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Matokeo hayo yanaifanya Lyon ibaki nafasi ya nane ikiwa na pointi 20 na Ruvu Shooting ibaki nafasi ya 10 ikiwa na pointi 14.
 
Tenga mambo safi CAF

Imeandikwa na KHARTOUM, Sudan; Tarehe: 24th February 2011 @ 08:20 Imesomwa na watu: 67; Jumla ya maoni: 0








RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodegar Tenga jana alichaguliwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Kanda ya Mashariki katika uchaguzi uliofanyika mjini hapa.

Tenga alipata nafasi hiyo kwa kura 34 na kumbwaga Rais wa Shirikisho la Soka la Rwanda Celestin Musabyimana aliyepata kura 19. Musabyimana alikuwa akitetea nafasi yake.

Tenga ambaye pia ni Rais wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) anakuwa Mtanzania wa pili kuingia kwenye Kamati ya Utendaji ya CAF baada ya Saidi El Maamry kupata nafasi hiyo mwanzoni mwa miaka ya 80 kwa vipindi viwili mfululizo.

Alishindwa kutetea nafasi hiyo katika kipindi cha tatu baada ya TFF wakati huo ikiitwa Chama cha Soka Tanzania (FAT) kutoidhinisha jina lake CAF. El Maamry hivi sasa ni Mjumbe wa Heshima wa CAF.

Mtanzania mwingine aliyewahi kuwania nafasi hiyo mara mbili, lakini hakufanikiwa kushinda ni Mwenyekiti wa iliyokuwa FAT, Muhidin Ndolanga.

Aidha, Kalusha Bwalya wa Zambia amefanikiwa kwa mara ya kwanza kuingia kwenye Kamati ya Utendaji ya CAF baada ya kuchaguliwa jana akiwakilisha Kanda ya Kusini mwa Afrika.

Bwalya ambaye alikuwa mwanasoka bora wa Afrika mwaka 1988 aliwashinda wagombea wengine wanne ambao ni Adam Mthethwa wa Swaziland, Walter Nyamilandu (Malawi), John Muinjo (Namibia) na Justino Fernandes wa Angola.

Nafasi ya Kanda ya Magharibi B ilitwaliwa na Kwesi Nyantakyi wa Ghana na ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ulikwenda kwa Mohamed Raouraoua wa Shirikisho la Soka la Algeria aliyepata kura 39 na kuwashinda Jacques Anouma (Ivory Coast, kura 35), Suketu Patel (Shelisheli, kura 12), Danny Jordann (Afrika Kusini, kura 10), Ibrahim Galadima (Nigeria kura 5). Bwalya alijitoa mapema katika kinyang'anyiro hicho.
 


fscLeagueFrontScoresHdr.gif

Upcoming Games
Today's Games Week 1: 08/07/10 - 08/08/10 Week 2: 08/14/10 - 08/15/10 Week 3: 08/17/10 - 08/22/10 Week 4: 08/28/10 - 08/29/10 Week 5: 09/11/10 - 09/12/10 Week 6: 09/18/10 - 09/19/10 Week 7: 09/25/10 - 09/26/10 Week 8: 10/02/10 - 10/03/10 Week 9: 10/16/10 - 10/17/10 Week 10: 10/23/10 - 10/24/10 Week 11: 10/30/10 - 11/02/10 Week 12: 11/06/10 - 11/07/10 Week 13: 11/13/10 - 11/14/10 Week 14: 11/20/10 - 11/21/10 Week 15: 11/27/10 - 11/28/10 Week 16: 11/27/10 - 12/05/10 Week 17: 12/11/10 - 12/12/10 Week 18: 12/18/10 - 01/22/11 Week 19: 12/21/10 - 12/22/10 Week 20: 01/15/11 - 01/16/11 Week 21: 01/29/11 - 01/30/11 Week 22: 02/05/11 - 02/06/11 Week 23: 02/12/11 - 02/13/11 Week 24: 02/18/11 - 02/20/11 Week 25: 02/26/11 - 02/27/11 Week 26: 03/05/11 - 03/06/11 Week 27: 03/11/11 - 03/13/11 Week 28: 03/19/11 Week 29: 04/02/11 Week 30: 04/09/11 Week 31: 04/16/11 Week 32: 04/24/11 Week 33: 04/30/11 Week 34: 05/07/11 Week 35: 05/11/11 Week 36: 05/15/11 Week 37: 05/21/11 Week 38: 05/29/11​

Saturday, February 26, 2011​
Week 25​

Stade Louis II
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Auguste Bonal
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Route de Lorient
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET

Lens


Goals Cards Substitutions
Geoffroy-Guichard
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Stade Nungesser
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Stade Fernand Fournier
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Stade Chaban-Delmas
Expand
expandInfo.jpg


3:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Sunday, February 27, 2011​
Week 25​

Parc des Princes
Expand
expandInfo.jpg


11:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Marcel Picot
Expand
expandInfo.jpg


11:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Metropole
Expand
expandInfo.jpg


3:00 PM ET

 


fscLeagueFrontScoresHdr.gif

Upcoming Games
Today's Games Week 1: 08/28/10 - 08/30/10 Week 2: 09/11/10 - 09/12/10 Week 3: 09/18/10 - 09/19/10 Week 4: 09/22/10 - 09/23/10 Week 5: 09/25/10 - 09/26/10 Week 6: 10/02/10 - 10/03/10 Week 7: 10/16/10 - 10/17/10 Week 8: 10/23/10 - 10/25/10 Week 9: 10/29/10 - 10/31/10 Week 10: 11/06/10 - 11/07/10 Week 11: 11/10/10 - 11/11/10 Week 12: 11/13/10 - 11/14/10 Week 13: 11/20/10 - 11/21/10 Week 14: 11/27/10 - 11/28/10 Week 15: 12/03/10 - 12/08/10 Week 16: 12/11/10 - 12/12/10 Week 17: 12/18/10 - 12/19/10 Week 18: 01/06/11 Week 19: 01/09/11 Week 20: 01/15/11 - 01/16/11 Week 21: 01/19/11 - 02/16/11 Week 22: 01/29/11 - 02/16/11 Week 27: 01/30/11 - 02/28/11 Week 23: 02/01/11 - 02/03/11 Week 24: 02/05/11 - 02/06/11 Week 25: 02/12/11 - 02/13/11 Week 26: 02/19/11 - 02/20/11 Week 28: 03/04/11 - 03/06/11 Week 29: 03/11/11 - 03/13/11 Week 30: 03/19/11 - 03/20/11 Week 31: 04/03/11 Week 32: 04/10/11 Week 33: 04/17/11 Week 34: 04/23/11 Week 35: 05/01/11 Week 36: 05/08/11 Week 37: 05/15/11 Week 38: 05/22/11​

Saturday, February 26, 2011​
Week 27​

Olimpico di Torino
Expand
expandInfo.jpg


2:45 PM ET



Goals Cards Substitutions
Sunday, February 27, 2011​
Week 27​

Angelo Massimino
Expand
expandInfo.jpg


6:30 AM ET



Goals Cards Substitutions
Sant Nicola
Expand
expandInfo.jpg


Bari
9:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Mario Rigamonti
Expand
expandInfo.jpg


9:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Olimpico
Expand
expandInfo.jpg


9:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Renzo Barbera
Expand
expandInfo.jpg


9:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Sant'Elia
Expand
expandInfo.jpg


9:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Dino Manuzzi
Expand
expandInfo.jpg


9:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
Luigi Ferraris
Expand
expandInfo.jpg


2:45 PM ET



Goals Cards Substitutions
Monday, February 28, 2011​
Week 27​

San Siro
Expand
expandInfo.jpg


2:45 PM ET

 


fscLeagueFrontScoresHdr.gif

Upcoming Games
Today's Games Week 1: 01/07/11 - 01/09/11 Week 2: 01/14/11 - 01/16/11 Week 3: 01/21/11 - 01/23/11 Week 4: 01/28/11 - 01/30/11 Week 14: 02/02/11 - 04/13/11 Week 5: 02/04/11 - 02/06/11 Week 6: 02/11/11 - 02/13/11 Week 7: 02/18/11 - 02/20/11 Week 8: 02/25/11 - 02/27/11 Week 9: 03/04/11 - 03/06/11 Week 10: 03/11/11 - 03/13/11 Week 11: 03/18/11 - 03/20/11 Week 12: 04/01/11 - 04/03/11 Week 13: 04/08/11 - 04/10/11 Week 15: 04/16/11 - 04/17/11 Week 16: 04/22/11 - 04/24/11 Week 17: 04/29/11 - 05/01/11​

Friday, February 25, 2011​
Week 8​

Estadio Victoria
Expand
expandInfo.jpg


9:10 PM ET



Goals Cards Substitutions
Saturday, February 26, 2011​
Week 8​

Estadio Victor Manuel Reyna
Expand
expandInfo.jpg


6:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Estadio La Corregidora
Expand
expandInfo.jpg


6:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Estadio Universitaro
Expand
expandInfo.jpg


8:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Estadio Miguel Hidalgo
Expand
expandInfo.jpg


8:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Estadio Jalisco
Expand
expandInfo.jpg


9:45 PM ET



Goals Cards Substitutions
Sunday, February 27, 2011​
Week 8​

Estadio Morelos
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Estadio Olímpico Universitaro
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Estadio Azteca
Expand
expandInfo.jpg


5:00 PM ET

 
Upcoming Games
Today's Games Week 1: 08/28/10 - 08/30/10 Week 2: 09/11/10 - 09/13/10 Week 3: 09/18/10 - 09/20/10 Week 4: 09/21/10 - 09/23/10 Week 5: 09/25/10 - 09/27/10 Week 6: 10/02/10 - 10/03/10 Week 7: 10/16/10 - 10/18/10 Week 8: 10/23/10 - 10/25/10 Week 9: 10/30/10 - 11/01/10 Week 10: 11/06/10 - 11/08/10 Week 11: 11/13/10 - 11/14/10 Week 12: 11/20/10 - 11/22/10 Week 13: 11/27/10 - 11/29/10 Week 14: 12/04/10 - 12/06/10 Week 15: 12/11/10 - 12/13/10 Week 16: 12/18/10 - 12/20/10 Week 17: 01/02/11 - 01/03/11 Week 18: 01/08/11 - 01/10/11 Week 19: 01/15/11 - 01/17/11 Week 20: 01/22/11 - 01/24/11 Week 21: 01/29/11 - 01/31/11 Week 22: 02/05/11 - 02/06/11 Week 23: 02/12/11 - 02/14/11 Week 24: 02/19/11 - 02/21/11 Week 25: 02/26/11 - 02/28/11 Week 26: 03/01/11 - 03/03/11 Week 27: 03/06/11 Week 28: 03/13/11 Week 29: 03/20/11 Week 30: 04/03/11 Week 31: 04/10/11 Week 32: 04/17/11 Week 33: 04/24/11 Week 34: 05/01/11 Week 35: 05/08/11 Week 36: 05/11/11 Week 37: 05/15/11 Week 38: 05/22/11​

Saturday, February 26, 2011​
Week 25​

Cornellá-El Prat
Expand
expandInfo.jpg


12:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Vicente Calderón
Expand
expandInfo.jpg


12:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
El Molinón
Expand
expandInfo.jpg


12:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Iberostar Estadio
Expand
expandInfo.jpg


2:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Riazor
Expand
expandInfo.jpg


4:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Sunday, February 27, 2011​
Week 25​

Ciutat de Valencia
Expand
expandInfo.jpg


11:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
José Rico Pérez
Expand
expandInfo.jpg


11:00 AM ET



Goals Cards Substitutions
El Sardinero
Expand
expandInfo.jpg


1:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
San Mamés
Expand
expandInfo.jpg


3:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Monday, February 28, 2011​
Week 25​

La Rosaleda
Expand
expandInfo.jpg


3:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Tuesday, March 1, 2011​
Week 26​

Cornellá-El Prat
Expand
expandInfo.jpg


2:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Sánchez Pizjuán
Expand
expandInfo.jpg


4:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Wednesday, March 2, 2011​
Week 26​

Reyno de Navarra
Expand
expandInfo.jpg


2:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Anoeta
Expand
expandInfo.jpg


2:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
El Madrigal
Expand
expandInfo.jpg


2:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
La Romareda
Expand
expandInfo.jpg


2:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Coliseum Alfonso Pérez
Expand
expandInfo.jpg


2:00 PM ET



Goals Cards Substitutions
Mestalla
Expand
expandInfo.jpg


4:00 PM ET

 


fscLeagueFrontScoresHdr.gif

Upcoming Games
Today's Games Week 1: 08/20/10 - 08/22/10 Week 2: 08/27/10 - 08/29/10 Week 3: 09/10/10 - 09/12/10 Week 4: 09/17/10 - 09/19/10 Week 5: 09/21/10 - 09/22/10 Week 6: 09/24/10 - 09/26/10 Week 7: 10/01/10 - 10/03/10 Week 8: 10/15/10 - 10/17/10 Week 9: 10/22/10 - 10/24/10 Week 10: 10/29/10 - 10/31/10 Week 11: 11/05/10 - 11/07/10 Week 12: 11/12/10 - 11/14/10 Week 13: 11/20/10 - 11/21/10 Week 14: 11/26/10 - 11/28/10 Week 15: 12/03/10 - 12/05/10 Week 16: 12/10/10 - 12/12/10 Week 17: 12/17/10 - 12/19/10 Week 18: 01/14/11 - 01/16/11 Week 19: 01/21/11 - 01/23/11 Week 20: 01/28/11 - 01/30/11 Week 21: 02/04/11 - 02/06/11 Week 22: 02/12/11 - 02/13/11 Week 23: 02/16/11 - 02/20/11 Week 24: 02/25/11 - 02/27/11 Week 25: 03/04/11 - 03/06/11 Week 26: 03/11/11 - 03/13/11 Week 27: 03/18/11 - 03/20/11 Week 28: 04/01/11 - 04/03/11 Week 29: 04/09/11 Week 30: 04/16/11 Week 31: 04/23/11 Week 32: 04/30/11 Week 33: 05/07/11 Week 34: 05/14/11​

Friday, February 25, 2011​
Week 24​

Volkswagen Arena
Expand
expandInfo.jpg


2:30 PM ET



Goals Cards Substitutions
Saturday, February 26, 2011​
Week 24​

Fritz-Walter Stadion
Expand
expandInfo.jpg


9:30 AM ET



Goals Cards Substitutions
RheinEnergieStadion
Expand
expandInfo.jpg


9:30 AM ET



Goals Cards Substitutions
Veltins-Arena
Expand
expandInfo.jpg


9:30 AM ET



Goals Cards Substitutions
Millerntor-Stadion
Expand
expandInfo.jpg


9:30 AM ET



Goals Cards Substitutions
Rhein-Neckar-Arena
Expand
expandInfo.jpg


9:30 AM ET



Goals Cards Substitutions
Allianz Arena
Expand
expandInfo.jpg


12:30 PM ET



Goals Cards Substitutions
Sunday, February 27, 2011​
Week 24​

Commerzbank-Arena
Expand
expandInfo.jpg


9:30 AM ET



Goals Cards Substitutions
Weserstadion
Expand
expandInfo.jpg


11:30 AM ET

 
Mghana atumai makubwa kwa Tenga Send to a friend Thursday, 24 February 2011 20:43

tengapongezi.jpg
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Afrika, CAF, na Rais wa TFF, Leodegar Tenga (katikati) akizungumza na Katibu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholaus Musonye baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo jijini Khartoum, Sudan juzi. Kushoto ni Makamu wa Rais wa TFF, Athumani Nyamlani. Picha kwa hisani ya Daily Monitor.

KHARTOUM, Sudan
RAIS wa Chama cha Soka Ghana, GFA ambaye alichaguliwa kuingia kwenye Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Afrika, CAF, Kwesi Nyantakyi amesema sura zilizoingia CAF ikiwemo ya Rais wa TFF, Leodegar Tenga ni za matumaini ya kuleta maendeleo ya soka Afrika.

Nyantakyi alishinda nafasi hiyo baada ya kuzoa kura 34 ikiwa ni ushindi wa asilimia 64 ya kura zote akimshinda Anjorin Moucharaf aliyekuwa anatetea nafasi yake.

Nyantakyi anasema kuwa mbinu alizotumia kuhakikisha Ghana inacheza Fainali za Kombe la Dunia mara mbili, atazitoa kwa wenzake Afrika ili kuinua kiwango cha soka katika ukanda huo.

ìNadhani kuchaguliwa kwangu ni kama fursa nyingine kuleta maendeleo. Mimi, Kalusha (Bwalya) na Leodegar Tenga wa Tanzania kwa uzoefu tuliokuwa nao tutahakikisha soka ya afrika inakuwa na sura nyingine.

"Tutahakikisha tunamsaidia Rais wa CAF, Issa Hayatou kuelekea kwenye mafanikio ya kweli,î alisema Nyantakyi.

Katika hatua nyingine, wadau wa soka wamesema wanataka kuona soka ya afrika inapiga hatua za mbali kwa mwaka huu baada ya kufanya vibaya katika mashindano mbalimbali kwa mwaka 2010.

Miongoni mwa mambo yaliyoelezwa ni pamoja na mataifa kushiriki kikamilifu katika michuano ya wachezaji wa Ligi za Ndani, CHAN.

Mohamed Hatimy, Rais wa Chama cha Soka Kenya, KPL, alisema: "Mwaka 2010 ulikuwa wa mafanikio kiasi kwani afrika ilikaribia kuingia nusu fainali lakini isiishie hapo, mafanikio yapo zaidi."

Naye Makamu mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Athumani Nyamlani ambaye alisema: "Nimefurahi kuwepo kwa maendeleo soka Afrika na michuano ya Sudan 2011 imekuwa ya mafanikio.

Wakati huo huo, Kamati ya Utendaji ya CAF, ilikutana kwa mara ya kwanza jana kufahamiana pamoja na kujiweka sawa baada wajumbe wake kuzikwaa nafasi mbalimbali za uongozi katika shirikisho hilo.

Nyantakyi alisema katika kikao hicho, watakutana na Rais wa CAF, Issa Hayatou na wajumbe wengine wa kamati ya utendaji kufahamiana na kuzungumzia hatma ya mashindano ya vijana yaliyopangwa kufanyika Libya mwezi ujao.

Libya ilipangwa kuandaa fainali hizo za vijana na hakuna uhakika wa kufanyika kutokana na migogoro ya kisiasa na kuangalia kama kuna uwezekano wa kuhamishia nchi nyingine.

Mbali na hilo, kikao hicho kitajadili jinsi ya kulishawishi Shirikisho la soka la Kimataifa, Fifa namna ya kuongeza timu katika Fainali za Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil. Kikao cha FIFA kitakaa mwezi ujao nchini Brazil.

Afrika inataka kuwa na uwakilishi zaidi kati ya timu 31. Mwaka jana Afrika iliwakilishwa na timu sita.
 
Moro United waanza kujipanga kwa Ligi Kuu Send to a friend Thursday, 24 February 2011 20:40

Clara Alphonce
UONGOZI wa klabu ya Moro United umeanza mchakato wa kuwanasa wachezaji wa klabu kubwa za Ligi Kuu wakiwemo wakongwe Simba na Yanga kwa ajili ya kujipanga kwa Ligi Kuu msimu ujao.

Moro United iliyokuwa Tanga kucheza Ligi Daraja la Kwanza, ilipanda Ligi Kuu pamoja na Coastal Union waliokuwa wenyeji, JKT Oljoro ya Arusha na Villa Squad ya Dar es Salaam.

Habari ambazo Mwananchi imezipata, zinasema kuwa wafanyabiashara mashuhuri watatu wa Dar es Salaam, wana mpango wa kuchukua wachezaji katika timu hizo lengo ni kuhakikisha Moro United inatoa upinzani na kuendelea kubaki katika ligi hiyo.

Chanzo cha bari kiliipasha Mwananchi kuwa, vibopa hao wameshaanza mazungumzo na wachezaji mbalimbali wakiwemo mabeki wa Simba, Meshack Abel na Amiri Maftah.

Pia katika orodha hiyo, yumo mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete na viungo, Nurdin Bakari na Halfan Razaki.

Mwananchi ilimtafuta mwenyekiti wa Moro United, Rodgers Peter ambaye naye alikiri kufanyika kwa mazungumzo ya awali kwa wachezaji hao.

"Unajua siwezi kusema zaidi kwa kuwa ni mapema mno ila cha msingi elewa kwamba mazungumzo ya awali yamekwishafanyika.

''Wadau mbalimbali Tabata tumeipandisha daraja timu yetu na tunachotaka ni kuibadilisha jina na kuwa Tabata FC na tayari tumekwishaanza mchakato na kinachofuata ni kutengeneza timu halisi kwa ajili ya mikikimikiki ya Ligi Kuu,'' alisema Peter.

Alisema nia na madhumuni ya kufanya hivyo ni kuhakikisha timuinadumu katika ligi na sio kupanda na kushuka hivyo na wanataka wachezaji watano wenye uzoefu kwa ajili ya kuisaidia timu hiyo na kuleta upinzani.

Mbali na wachezaji wa Ligi Kuu, pia kuna wachezaji wengine ambao walikuwa katika michuano ya ligi daraja la kwanza tisa bora na wengine walioachwa na timu zao kama Temeke United.

Hata hivyo aliwataka wadau mbali mbali kujua timu hiyo pamoja na kutaka kupewa jina la Tabata FC lakini sio ya Tabata peke yao hata kama kutakuwa na wadau wengine kutoka sehemu mbalimbali wanaruhusiwa kuisaidia.

Alisema pia wanajipanga kuleta upinzani mkubwa katika ligi hasa timu kubwa ambazo zimejibweteka na kuona nafasi za juu ni zao peke yao na hakuna mtu anakayewatoa.

''Mfano mzuri umeonyeshwa na Azam na sisi tunafuata kuleta upinzani kwani nia yetu ni kuakikisha Tabata FC inacheza mechi za kimataifa kama klabu bingwa au Shirikisho,'' alisema.

Moro United ni moja ya timu ambazo zimepata tiketi ya Ligi Kuu Bara jioni kwnai mchezo wao wa mwisho walitakiwa kushinda kabla ya kuifunga Morani mabao 2-1.
 
Wasanii kuomba kura hadharani tuzo za muziki za Kilimanjaro


na Mwandishi wetu


amka2.gif
KAMPUNI ya Bia Tanzania kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro wadhamini wakuu wa tuzo za muziki nchini ‘Kili Music Award', wamepanga kufanya maonyesho kadhaa nchini kwa lengo la kuwanadi wasanii na wanamuziki waliopata nafasi ya kuwania tuzo kutokana na kazi zao zilizofanya vema mwaka jana.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, katika semina ya siku moja kwa wasanii hao, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema, wasanii hao wataandaliwa maonyesho mbalimbali katika sehemu ambazo hawajawahi kutumbuiza, kabla ya tamasha kubwa litakalofanyika viwanja vya Biafra Kinondoni Machi 5 mwaka huu.
Aidha, wasanii hao ambao watapanda jukwaani na kujinadi kuomba kura kutoka kwa mashabiki na wadau wao wa muziki, huku ikiwa siyo lazima kwao kuimba.
Alisema, baada ya kuomba kura kwenye viwanja vya Biafra, safari itahamia viwanja vya Mwembe Yanga Temeke na Machi 13 watakuwa ufukwe wa Coco.
Mbali ya kuomba kura katika viwanja vya wazi ambavyo wasanii hao ni nadra kufanya maonyesho, pia wataandaliwa matamasha katika kumbi mbalimbali za burudani zikiwamo Club Bilicanas katikati ya Jiji, Club Maisha uliopo Oysterbay, Sunsiro uliopo Sinza.
Wakati huohuo, TBL wametangaza utaratibu wa kupiga na kutuma kura kwa wasanii hao, ambako kila mtu mwenye simu atakuwa na nafasi moja tu ya kumpigia kura msanii ambaye anavutiwa naye, kwa kutumia namba na siyo kuandika jina, kwani kinyume na hapo itakuwa imeharibika.
Katika utaratibu huo, watakaotuma kura kwa kutumia magazeti na vipeperushi watatumia anuani ya KTMA 2011, Innovex SLP 75297 Dar es Salaam, huku njia ya simu ya kiganjani kwa mitandao yote ni 15747, huku kwa barua pepe ni TEEN TZ na Ktma@innovex.com.
 
Dogo Janja apika video ya Ngarenaro


na Mwandishi wetu


amka2.gif
MSANII chipukizi wa muziki wa kizazi kipya kutoka Arusha, Abdul-aziz Aboubakar Chende 'Dogo Janja' (12), ameanza kutengeneza video ya nyimbo za albamu yake mpya iitwayo 'Ngarenaro'.
Dongo Janja alisema jijini Dar es Salaam juzi kuwa, kwa sasa ameishakamilika albamu hiyo na sasa anasubiri kuiingiza sokoni, hivyo amepanga kutengeneza video ili kuitambulisha albamu hiyo.
Msanii huyo chipukizi alisema kuwa, amepanga kuhakikisha albamu yake inaingia sokoni ikiwa katika kanda za kawaida, VCD na DVD na kuwa, anamshukuru msanii Hamad Ally Seneda 'Madee', aliyesimamia kukamilika albamu hiyo.
"Kwa kweli namshukuru sana Madee kwa kunisaidia kukamilisha albamu yangu, nilipo nasubiri kuiingiza sokoni na tayari tumeanza kujiandaa kutengeneza video," alisema Dogo Janja.
Akifafanua hilo alisema kuwa hana neno zuri la kutumia katika kumshukuru Madee kwa kuamua kumsaidia, jambo ambalo ni wasanii na watu wachache wenye uwezo wa kifedha wanaweza kulifanya kwa msanii chipukizi kama yeye.
Baadhi ya nyimbo za albamu hiyo na wasanii aliowashirikisha ni 'Anajua' ft Tundaman, 'Kama' ft Godzilla, 'Tulia' ft Joh Makini, 'Nikiwa Star' Ft Chegge, 'Wanataka Kunishusha' Peter Msechu, 'Nimefurahi' ft Deso na 'Nitawaambiaje' ft Madee.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom