Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,502
- 911,254
- Thread starter
- #6,441
Simba yaikuna FIFA
na Makuburi Ally
SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (FIFA), limeipongeza Simba ya jijini Dar es Salaam kwa kuvuka hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika na kutakiwa kutokata tamaa mbele ya Mabingwa wa Afrika, TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Simba imevuka hatua hiyo juzi baada ya juzi kuilaza Elan De Mitsoudje ya Comoro kwa mabao 4-2, hivyo sasa kukutana na mabingwa watetezi TP Mazembe kati ya Machi 18 na 20 kabla ya kurejeana Aprili Mosi hadi 3 mwaka huu.
Akizungumza katika uzinduzi wa semina kwa viongozi wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara, Mkurugenzi wa Elimu, Ufundi na Maendeleo ya Soka wa FIFA, Jurg Nepfer, alisema mafanikio hayo ni matunda ya juhudi za wachezaji, makocha na viongozi wa timu hiyo.
Nepfer alisema, Simba wanatakiwa kujiandaa ipasavyo katika michezo yake dhidi ya Mazembe ambayo ni mojawapo ya timu bora barani Afrika.
Aidha Nepfer alisema kwa mpangilio huo Simba ndio klabu mojawapo ambayo ni mfano wa kuigwa kutokana na maendeleo iliyonayo katika mashindano ya kimataifa.
Awali kabla kuanza kwa semina hiyo, viongozi wa klabu za Yanga, Toto Africans, Kagera Sugar na Polisi Tanzania hawakuwepo katika semina hiyo.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange Kaburu, alisema nguvu zao sasa wamezielekeza kwa Mazembe ambayo hawaiogopi kutokana na kuwa na historia bora ya mashindano ya kimataifa kama hayo.
Kaburu alisema, mchezo kati yao na Mazembe unatarajiwa kuchezwa Machi 18 jijini Lubumbashi, DRC ambapo kwa sasa wanajipanga kwa programu ambazo Kocha Mkuu, Patrick Phiri, amewasilisha kwa uongozi.
Kaburu alisema, pamoja na mazoezi kutoka Ligi Kuu Tanzania Bara, Phiri pia atatengeneza vitu vya ziada ambavyo vitafanikisha kuifunga Mazembe.
"Simba ina historia ya mwaka 2003 ilipowaadhibu waliokuwa mabingwa watetezi, Zamalek ya Misri tulipowafunga nyumbani kwao baada ya kuwa mabingwa wa Afrika mwaka 2002, hivyo inaweza kujirudia kwa Mazembe," alisema Kaburu.
Aidha, Kaburu alisema, wanaipa uzito mechi hiyo kutokana na sababu kwamba asilimia kubwa ya wadau wa soka watataka kufahamu kitakachotokea ambapo Simba watatumia upenyo ambao Mazembe hawatosahau.
na Makuburi Ally
Simba imevuka hatua hiyo juzi baada ya juzi kuilaza Elan De Mitsoudje ya Comoro kwa mabao 4-2, hivyo sasa kukutana na mabingwa watetezi TP Mazembe kati ya Machi 18 na 20 kabla ya kurejeana Aprili Mosi hadi 3 mwaka huu.
Akizungumza katika uzinduzi wa semina kwa viongozi wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara, Mkurugenzi wa Elimu, Ufundi na Maendeleo ya Soka wa FIFA, Jurg Nepfer, alisema mafanikio hayo ni matunda ya juhudi za wachezaji, makocha na viongozi wa timu hiyo.
Nepfer alisema, Simba wanatakiwa kujiandaa ipasavyo katika michezo yake dhidi ya Mazembe ambayo ni mojawapo ya timu bora barani Afrika.
Aidha Nepfer alisema kwa mpangilio huo Simba ndio klabu mojawapo ambayo ni mfano wa kuigwa kutokana na maendeleo iliyonayo katika mashindano ya kimataifa.
Awali kabla kuanza kwa semina hiyo, viongozi wa klabu za Yanga, Toto Africans, Kagera Sugar na Polisi Tanzania hawakuwepo katika semina hiyo.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange Kaburu, alisema nguvu zao sasa wamezielekeza kwa Mazembe ambayo hawaiogopi kutokana na kuwa na historia bora ya mashindano ya kimataifa kama hayo.
Kaburu alisema, mchezo kati yao na Mazembe unatarajiwa kuchezwa Machi 18 jijini Lubumbashi, DRC ambapo kwa sasa wanajipanga kwa programu ambazo Kocha Mkuu, Patrick Phiri, amewasilisha kwa uongozi.
Kaburu alisema, pamoja na mazoezi kutoka Ligi Kuu Tanzania Bara, Phiri pia atatengeneza vitu vya ziada ambavyo vitafanikisha kuifunga Mazembe.
"Simba ina historia ya mwaka 2003 ilipowaadhibu waliokuwa mabingwa watetezi, Zamalek ya Misri tulipowafunga nyumbani kwao baada ya kuwa mabingwa wa Afrika mwaka 2002, hivyo inaweza kujirudia kwa Mazembe," alisema Kaburu.
Aidha, Kaburu alisema, wanaipa uzito mechi hiyo kutokana na sababu kwamba asilimia kubwa ya wadau wa soka watataka kufahamu kitakachotokea ambapo Simba watatumia upenyo ambao Mazembe hawatosahau.
PRINT