Michapio hatari

Michapio hatari

Nakumbuka tukiwa form 1 tukawa tunahama darasa...sasa mbele yetu yuko jamaa mmoja anaitwa Samweli...nyuma yuko sister mmoja . Sam akawa kachukua kitu cha mdada then akakimbia mbele...huyo dada akaamua kumuita na kumwambia Sam kwa nguvu...distance ya km mita 20...Nanukuu...
" Samweli tutat...mbanaaa" badala ya tutagombana.


Yaan lipaza sauti mbaya....sijawahi kuisahau hii siku.
 
kunajamaa aliulizwa badili sentesi hii kwa lugha ya kiingereza

swali;kasimu usivute mto wangu.

jamaa kwa kujiamini;
katelephone don't smoke my river
 
Nakumbuka kipindi nipo mdogo mzee wangu aliwahi kuniita sku moja jion akaniambia kwa ujasiri mkubwa..."Kafungie madunge ya ngombe jua linazama" akimaanisha madume ya ng'ombe
 
Miaka ya 80 Halmashauri ya Arusha mjini ilipiga marufuku Wamasai kuingia mjini na Rubega bila kuvaa chupi ndani. Mmasai mmoja akaja mjini, baada ya kumaliza shughuli zake giza limeingia akashikwa na haja kubwa akawa anaingia uchochoro mmoja akakutana na chalii mmoja, akamwambia "Rafiki huko unaingia uwe makini kuna vibaka" Mmasai akapuuza, akaingia akachuchumaa akanyanyua rubega na kujisaidia, baada ya kumaliza akasimama akawasha Tochi akaangalia kinyesi ili afukie na udongo hakukiona akahamaki "Kweli fibaka wapo mtaa huu hata mafi wanaiba"
 
Mwl anamwadhibu dent na kumwambia Fanya adhabu hii '"kichwa chini mijuu guu'".
 
Baada ya kukoswa koswa na ajali mapigo ya mbio yalinienda moyo!!
 
tulikuwa tunacheza mpira sasa jamaa mmoja akasema we f@l@ piga huo mfila tukaanza kucheka sasa jamaa alieambiwa apige mfila akacheka sana kisha akasema 'ha ha haaaa amefapia'...
 
Talhatumbo kanipiga mpira wa hata....Badala ya Talhata kanipiga mpira wa tumbo.
 
Back
Top Bottom