Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 4,367
- 2,407
Wengi wameandika baada ya mwaka mmoja na hata miwili ya utendaji wa Rais Magufuli. Sikufanya hivyo, kwasababu sikujua tunakoelekea lakini leo ninajua anakotupeleka na hata jina la kituo au mji ukipenda.
Kwanza nianze kwa kusema ni makosa makubwa kudhani kuwa kinachotokea Ikulu ni mawazo ya Magu tu, nilichokigundua mimi ni kwamba huo ni mpango wa CCM kwa kipindi cha miaka 5. Msiaminishwe hata kidogo kuwa Kinana, Mwinyi, Kikwete, Mkapa na wajumbe wa kamati kuu ya CCM hawakuwa pamoja katika kupanga yote yaliyotokea kipindi cha miaka miwili cha Magu akiwa madarakani. Na ndio maana wamekaa kimya kwa yote yanayotokea.
Kama Nape kwa hasira alivyodokeza kuwa CCM ilikuwa inakwenda shimoni, huu ni ukweli ambao wote wakubwa wa CCM walilifamu kutokana na RUSHWA NA UFISADI vitu ambavyo upinzani ilivipigia tarumbeta. Yafuatayo ndio Maamuzi ya wakubwa CCM.
1) Ni muhimu kuchagua kiongozi ambaye hatakuwa na urafiki na wana CCM, ili avunje mazoea ya kujuana. Akachaguliwa Magufuli
2) Kiongozi huyu apewe majukumu makali na atoe maamuzi makali si yenye tija kwa watanzania ila yawe na tija kwa CCM.
- ahakikishe demokrasia inatokomea, ikiwa ni pamoja na kuzuia upinzani kutoa mawazo yao na watanzania kwa jumla
-Kuzuia haki ya mamlaka ya mihimili mikuu ya nchi
-Kurubuni viongozi wa upinzani kuhamia CCM
- Kuvuruga upinzani kwa kuleta ugomvi ndani ya vyama hivyo.
3. Kuwaaminisha watanzania kuwa huwezi kupambana na RUSHWA NA UFISADI ila sharti uvunje demokrasia.
Hivyo tunakoenda si kwingine ila ni kujenga nchi ya chama kimoja kitachochukua hatamu.
Swali ni kwamba, hivi dunia na watanzania wapo tayari kwa hilo, hata kama tutafanikiwa zaidi kiuchumi?
Kwanza nianze kwa kusema ni makosa makubwa kudhani kuwa kinachotokea Ikulu ni mawazo ya Magu tu, nilichokigundua mimi ni kwamba huo ni mpango wa CCM kwa kipindi cha miaka 5. Msiaminishwe hata kidogo kuwa Kinana, Mwinyi, Kikwete, Mkapa na wajumbe wa kamati kuu ya CCM hawakuwa pamoja katika kupanga yote yaliyotokea kipindi cha miaka miwili cha Magu akiwa madarakani. Na ndio maana wamekaa kimya kwa yote yanayotokea.
Kama Nape kwa hasira alivyodokeza kuwa CCM ilikuwa inakwenda shimoni, huu ni ukweli ambao wote wakubwa wa CCM walilifamu kutokana na RUSHWA NA UFISADI vitu ambavyo upinzani ilivipigia tarumbeta. Yafuatayo ndio Maamuzi ya wakubwa CCM.
1) Ni muhimu kuchagua kiongozi ambaye hatakuwa na urafiki na wana CCM, ili avunje mazoea ya kujuana. Akachaguliwa Magufuli
2) Kiongozi huyu apewe majukumu makali na atoe maamuzi makali si yenye tija kwa watanzania ila yawe na tija kwa CCM.
- ahakikishe demokrasia inatokomea, ikiwa ni pamoja na kuzuia upinzani kutoa mawazo yao na watanzania kwa jumla
-Kuzuia haki ya mamlaka ya mihimili mikuu ya nchi
-Kurubuni viongozi wa upinzani kuhamia CCM
- Kuvuruga upinzani kwa kuleta ugomvi ndani ya vyama hivyo.
3. Kuwaaminisha watanzania kuwa huwezi kupambana na RUSHWA NA UFISADI ila sharti uvunje demokrasia.
Hivyo tunakoenda si kwingine ila ni kujenga nchi ya chama kimoja kitachochukua hatamu.
Swali ni kwamba, hivi dunia na watanzania wapo tayari kwa hilo, hata kama tutafanikiwa zaidi kiuchumi?