JERUSALEMU
JF-Expert Member
- Sep 19, 2012
- 3,106
- 3,523
Naam wanajukwaa,
Mzigo umeletwa tena wa kutosha ni tani kadhaa. Ni solution ya mitishamba kutoka Madagascar. Wanaiita ni dawa ya kufubaza virusi vya corona. Kwa mujibu wa maelezo yao wanasema tumepewa msaada. yaani tumepewa bure kabisa. Umewaamini?
Mimi sijaamini hata kidogo labda mpaka CAG akague ankara za pale Hazina na ile ofisi nyingine. Awamu hii kutumia rupia za wananchi kwa mambo hata ya kisangoma ni kawaida sana. Muda utasema.
Jingine ni kwamba wanasema hatuanzi kuutumia ule mzigo mpaka ufanyiwe utafiti wa kisayansi! Halafu msimamizi ni Kagundi Mwalimu wa Kiswahili! You know why? Wanalenga kuidanganya Dunia na hasa WHO kwamba hawajaanza kutumika kumbe usikute tayari watunga sheria wamepewa ili waendelee na shughuli zao wakiwa wametuluzwa Kisaikolojia.
Kama lengo lingekuwa ni kufanyia utafiti kwanza si wangeagiza lita hata 100 tu ili kubana matumizi? Za kuambiwa changanya na zako.
Mzigo umefika sasa kwanini Kabudi aendelee kuwa msemaji? Kwanini asiupeleke kwa mkemia mkuu au Chakula na dawa huko? You can fool all the people some time and some of the people all the time but you can not fool all the people all the time!
Binafsi nimeijua awamu hii vizuri mno. Kwanza wanaamini fedha za Nchi hii ni zao wanaweza kutumia vyovyote vile.
Pili wanaamini sheria,kanuni na taratibu ziliwekwa kwaajili ya watu vyama vya upinzani. Wao wanaweza wakafanya chocho popote kwa yeyote na wasiulizwe.
Hii dawa haija thibitishwa na mamlaka za tiba za kidunia.Unaanzaje kutumia mamilioni ya fedha za umma kufuata kitu fake?
Mapendekezo yangu ni kwamba kuwekwe Auditing special ya watu wote watakao pewa dawa hii ili madhara ya kitokea basi kuna watu wawajibishwe !
Pili, CAG afuatilie kuona mzigo hautumiki mpaka matokeo ya utafiti yatoke.
Nijuavyo rangi zao hawatakubali.
Mzigo umeletwa tena wa kutosha ni tani kadhaa. Ni solution ya mitishamba kutoka Madagascar. Wanaiita ni dawa ya kufubaza virusi vya corona. Kwa mujibu wa maelezo yao wanasema tumepewa msaada. yaani tumepewa bure kabisa. Umewaamini?
Mimi sijaamini hata kidogo labda mpaka CAG akague ankara za pale Hazina na ile ofisi nyingine. Awamu hii kutumia rupia za wananchi kwa mambo hata ya kisangoma ni kawaida sana. Muda utasema.
Jingine ni kwamba wanasema hatuanzi kuutumia ule mzigo mpaka ufanyiwe utafiti wa kisayansi! Halafu msimamizi ni Kagundi Mwalimu wa Kiswahili! You know why? Wanalenga kuidanganya Dunia na hasa WHO kwamba hawajaanza kutumika kumbe usikute tayari watunga sheria wamepewa ili waendelee na shughuli zao wakiwa wametuluzwa Kisaikolojia.
Kama lengo lingekuwa ni kufanyia utafiti kwanza si wangeagiza lita hata 100 tu ili kubana matumizi? Za kuambiwa changanya na zako.
Mzigo umefika sasa kwanini Kabudi aendelee kuwa msemaji? Kwanini asiupeleke kwa mkemia mkuu au Chakula na dawa huko? You can fool all the people some time and some of the people all the time but you can not fool all the people all the time!
Binafsi nimeijua awamu hii vizuri mno. Kwanza wanaamini fedha za Nchi hii ni zao wanaweza kutumia vyovyote vile.
Pili wanaamini sheria,kanuni na taratibu ziliwekwa kwaajili ya watu vyama vya upinzani. Wao wanaweza wakafanya chocho popote kwa yeyote na wasiulizwe.
Hii dawa haija thibitishwa na mamlaka za tiba za kidunia.Unaanzaje kutumia mamilioni ya fedha za umma kufuata kitu fake?
Mapendekezo yangu ni kwamba kuwekwe Auditing special ya watu wote watakao pewa dawa hii ili madhara ya kitokea basi kuna watu wawajibishwe !
Pili, CAG afuatilie kuona mzigo hautumiki mpaka matokeo ya utafiti yatoke.
Nijuavyo rangi zao hawatakubali.