Miaka 50 ya uhuru mnamkumbuka Kigoma Ally Malima?

Miaka 50 ya uhuru mnamkumbuka Kigoma Ally Malima?

Boko haram

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2011
Posts
3,256
Reaction score
1,233
Kigoma Ally Malima alikuwa mwanaharakati mahiri sana alikuwa haogopi mtu penye ukweli alikuwa anasema ukweli lakini fitna alizo kumbana nazo mungu ndio anajua na mkumbuke suala la mwanafunzi kuandika jina lake kwenye mtiani yeye ndie aliye badilisha kutumika namba kwasababu kulikuwa na upendeleo na hilo lilisaidia sana lakini leo hakumbukwi watanzania musipende kusikiliza hoja bila dalili historia ya hii nchi imepindishwa na ndio maana vitabu vingi vilipigwa marufuku. Kwamfano THE DARKSIDE OF MWALIMU JULIUS NYERERE, THE PARTNERSHIP,MWEBECHAI KILLINGS,KANISA KATOLIKI NA SIASA ZA TANZANIA CHA PADRI DR JOHN SIVALONna vingine vingi munavijua
 
Kwakuwa alifanikiwa kuzuia njama chafu za Nyerere kuwabania waislamu, ndio maana historia inafichwa.
 
hata mimi simfahamu inawezekana anamsema yule waziri wa fedha akamwagwa na Mzee Ruksa, kisha akahama CCM na kujiunga na NRA, SIJUI NDIYE HUYO. Hebu tufafanulie , ndiye huyo? mkuu
 
Na mkumbuka kigoma ally malima kwa mengi aliyo tutendea sisi wanafunzi. Mungu amueke mahali pema peponi,Amin
 
Kighoma Alli Malima alikuwa mwanasiasa opportunist wa hali ya juu, kwani katika maisha yake alioa mama wa kihehe wa dini ya kikisto wakati huo alikuwa haujui uislam; baada ya kushindwa kumaliza PH.D yake kule Princeton[ hakuna record kuwa alimaliza huko princeton]alirudi na kufundisha UDSM na baadae akaja kuwa mkurugenzi wa IFM. Aliingia siasa enzi ya mwalimu Nyerere na kujipendekeza sana kwa Mustapha Ny'ang'anyi wakati huo akiwa kipenzi wa mwalimu na mjumbe wa cc ya ccm. Muda si muda akawa waziri na Mwinyi alipopata Urais ndio huyu bwana akaanza mambo ya Udini na kumyanyasa sana yule mama wa kihehe kwa sababu ya madhehebu yake na ndipo akaongeza mke mwingine na kuwa full fledged Mujaheedin na mapete ya fedha mikononi na hata akajenga msikiti pale wizara ya fedha. He was very influential wakati wa mwinyi hata akadhania kuwa angekuwa mgombea wa ccm baada ya Mwinyi!! Alivyoona hakuna jinsi ya kuukwaa urais kupitia CCm ndipo alipohama na kuanzisha NRA ambacho ideology yake principally ilikuwa kutetea Uislam. Mwanae Adam pia alikuwa huko. Akiwa huko NRA mauti ilimfika akiwa London alikokwenda kufuata VIJISENTI vyake alivyoiba akiwa waziri wa fedha bahati nzuri WAHINDI wake wakamuibia fedha zote na ule mshituko wa kudhulumiwa vijisenti ndio uliompeleka mbele ya haki. Huyo Ndio Kighma Allima Malima mzaramo wa mkuranga zamani ikiwa sehemu ya Kisarawe.Hana jema la kukumbukwa alikuwa mtu wa balaa tu!!
 
alikuwa mnafiki na mdini sana aliyehitaji mtu mwelevu kumdhibiti, alitaka kuvuluga mfumo wetu wa elimu kwa kuingiza udini(uislam)
 
Ukiacha kuwatetea waislamu ambalo namsifu na kumkubali,
But hata nae alikua mwizi tu (neno fisadi halikuwapo wakati huo)
Kilichomuua ni presha kupanda baada ya Serikali kuzi-freeze hela zake zilizoko kwenye mabenki mbalimbali huko Nje .
 
Huyu Pesa zake zilichukuliwa na Serikali tena Mbaya wake alikuwa ni Jk Maana Jk alianza uwaziri wa Fedha kwa Mbwembwe Alienda kufunga akaunti ya Kigoma Then ikafuatia ya Msuya.

Siku aliyifunga akaunti ya Kigoma yaliyoendelea ni kusikia kifo chake tu, na Alipofunga ya Msuya Kilichofuatia DTV wakatutangazia Waziri mkuu wa zamani katutoka Baadae walijiwa juu na nusura washitakiwe na Msuya wakaomba Radhi haya mafufu yameisha baada ya kusuluhishwa na kwa ali kuja kupewa unaibu waziri Tuyaacha haya yameshaishi waache watu waishi kwa raha na mustarehe zao sie tuendelee kuteseka tusubiri zamu zetu
 
Japo mara nyingi marehemu husifiwa hata pale ambapo hakufanya vizuri LAKINI kwa Kighoma Malima yatosha kusema kuwa tutamkumbuka kwa maisha ya unafiki tangu ujana wake. Formal education aliyoipata ilikuwa STD IV, kwa unafiki alijiweka karibu sana na Wamisionari hata wakadanganyika kuwa alikuwa mfuasi wao kuliko waumini wao wa wakati ule. Wakamwendeleza mpaka kufikia kumlipia masomo yake ya Chuo Kikuu. Kwa kuendeleza unafiki wake, kwa dhamira maalum, aliamua kumwoa mwanamke mkristo, na Jumapili zote akawa akienda kanisani, na akajifanya mwumini mkubwa wa Mwalimu katika falsafa ya 'serikali haina dini'. Alipoingia Mwinyi akapewa wizara ya Elimu, huko akatangaza kuwa idadi ya wakristo waliosoma inatosha, sasa ni wakati wa kuwasomesha waislam - aliyasema hayo akiamini kuwa atapata uungwaji mkono wa jamii ya kiislam na Rais Mwinyi. Akatenga sehemu ya ofisi za wizara kuwa sehemu ya kuswalia (msikiti). Alipostaafu mkurugenzi wa wizara ya elimu, na msaidizi wake kufariki, alienda msikitini na kusema kuwa, 'kuna mkurugenzi pale mkristo amestaafu, akaniletea taarifa hiyo, nikasema sawa, nikamweka kwenye nafasi hiyo muislam mmoja safi ambaye watu walikuwa wamemkalia; kisha msaidizi akafariki, nikasema naam, na hapo nikamweka muislam mwingine. hatimaye nikaondolewa kupelekwa wizara ya fedha, sikusikitika kwa vile nilikuwa nimefanikisha malengo yangu'.

Akiwa waziri wa fedha, ndipo serikali ilipofilisika kwa namna ambayo haijawahi kutokea, pesa ya misaada iliporwa na kuwekwa kwenye akaunti zake mpaka kufikia mashirika yote ya kimataifa na mataifa ya Ulaya na Amerika kusimamisha misaada yote kwa Tanzania. Baada ya kuvurunda kwa namna ya ajabu, Mwinyi hakuwa na chaguo zaidi ya kumfukuza kazi, aliambiwa ajiuzulu saa 3 asubuhi, na saa 4 asubuhi siku hiyo hiyo ilitangazwa kuwa Rais ameridhia. Baada ya hapo akaanza kwenda misikitini akitangaza kuwa Mwinyi amemwondoa kwa sababu ya kuwatetea waislam. Akajiunga na Chama cha NRA, na akiwa Tabora msikitini akatangaza kuwa angegombea Urais. JK, alipochukua nafasi ya Uwaziri wa Fedha, kama namna mojawapo ya kurudisha imani kwa jamii ya kimataifa alizifunga akaunti zote za nje za Kighoma Malima. Kighoma Malima alipoenda Uingereza kuchukua fedha kwaajili ya kuendeshea kituo chake cha redio kilichokuwa kikihamasisha siasa za kidini, akaambiwa kuwa serikali ya Tanzania imeomba kufungwa kwa akaunti zake za benki nchini Uingereza, siku hiyo hiyo, usiku, Mkuu wa Maisha na pumzi yetu, ambaye ukuu wake hauhojiwi, aliichukua roho ya kiumbe wake.

Tunamwombea kwa Muumba wetu, amrehemu kadiri ya mapenzi yake.
 
Watetezi wa Malima kwa Unafiki siwawezi hadi leo hamkubali kuwa kutumia namba kwenye mitihani ni utaratibu uliokuwepo kabla malima hajawa waziri? Kweli nyie vichwa panzi
 
Al Marhuum Kighoma Ali Malima, utakumbukwa sana katika safu za Waislamu. Ulijitoa ,mhanga huku ukijua bei yake. Ni gharama hiyohiyo waliipata kina Kitwana Kondo na Manju Msambia hivi karibuni ya kutaka kuondoa status quo iliyopo nchini na utekelezaji wa mfumo kandamizi 'mfumo kristo'

Majlis za waislamu Tanzania daima zitakukumbuka na Allah atakulipa kheri. Nakumbuka mauti yalivyokukumba siku zile jijini London ulikuwa unatoka kutekeleza ibada muhimu ya umrah nchini Saudia Arabia. Mengia ya uzushi yalisemwa juu ya madai ya wewe kujilimbikizia mali na ufungwaji wa zinazodaiwa ni akaunti zako ughaibuni. Huu ni uzushi na umbea uliotengezwa na mfumo kandamizi.
 
Mhhh, Mkuu kumbe ni wewe ulimpendekeza Mkuu wa Chuo Changu (Technical College Arusha) aitwaye Issa Mushi kuwa Mkurugenzi hapo? Naona enzi hizo ilikuwa ni kupandisha cheo kila Muislaam msomi hata kama uwezo wa uongozi hana. Kuchaguliwa kwake wengi kulitushangaza sana kwa siku za mwanzo ila baadaye ndiyo tukaja kusikia kampeni zinazoendelea hapo Wizara ya elimu.

Kuna wengine wanaenda mbali zaidi hadi kuhusisha ugomvi wa Makamu wa Rais (Dr. Bilal) na Mkapa wakati wakiwa Wizara ya elimu ya juu. Bilal alikuwa na mazoea akikwama, badala ya kumuona Boss wake Mkapa, yeye anatoka nje na kuvuka geti kuingia Ikulu kumuona Homeboy. Kuna mtu pale Wizarani, Mzanzibar anaitwa Rajab, alitengeneza sana hela kwa nafasi za kusoma nje na pia aliwafaidi sana Mabinti wanaotafuta nafasi kusoma nje.
Alipostaafu mkurugenzi wa wizara ya elimu, na msaidizi wake kufariki, alienda msikitini na kusema kuwa, 'kuna mkurugenzi pale mkristo amestaafu, akaniletea taarifa hiyo, nikasema sawa, nikamweka kwenye nafasi hiyo muislam mmoja safi ambaye watu walikuwa wamemkalia; kisha msaidizi akafariki, nikasema naam, na hapo nikamweka muislam mwingine. hatimaye nikaondolewa kupelekwa wizara ya fedha, sikusikitika kwa vile nilikuwa nimefanikisha malengo yangu'.


Tunamwombea kwa Muumba wetu, amrehemu kadiri ya mapenzi yake.
 
Hii thread itafungwa muda si mrefu

sina haja ya kuwaeleza sababu
 
Nasikia kwenye kifo chake kuna mkono wa Jk
 
Kigoma Ally Malima alikuwa mwanaharakati mahiri sana alikuwa haogopi mtu penye ukweli alikuwa anasema ukweli lakini fitna alizo kumbana nazo mungu ndio anajua na mkumbuke suala la mwanafunzi kuandika jina lake kwenye mtiani yeye ndie aliye badilisha kutumika namba kwasababu kulikuwa na upendeleo na hilo lilisaidia sana lakini leo hakumbukwi watanzania musipende kusikiliza hoja bila dalili historia ya hii nchi imepindishwa na ndio maana vitabu vingi vilipigwa marufuku. Kwamfano THE DARKSIDE OF MWALIMU JULIUS NYERERE, THE PARTNERSHIP,MWEBECHAI KILLINGS,KANISA KATOLIKI NA SIASA ZA TANZANIA CHA PADRI DR JOHN SIVALONna vingine vingi munavijua

kwenye hilo (i.e. coloured blue) nasema ........ACHA UONGO NA UNAFIKI
 
Back
Top Bottom