Miaka 30 ya VETA: Yafanya Makubwa, Mazuri Kwa TZ, Rais Samia, Prof. Mkenda, Prof. Mchome, CPA Kasore, Menejimenti, na Wafanyakazi, Wapewe Maua Yao!.

Miaka 30 ya VETA: Yafanya Makubwa, Mazuri Kwa TZ, Rais Samia, Prof. Mkenda, Prof. Mchome, CPA Kasore, Menejimenti, na Wafanyakazi, Wapewe Maua Yao!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,721
Wanabodi,

View: https://youtu.be/OSGYViDqx8Y
View: https://youtu.be/oqwZRhin8ek

View: https://youtu.be/EEMSp2L7MZk
Hii ni makala yangu kwenye gazeti la Nipashe la Leo.
Makala ya VETA.jpg

Hii Makala yangu kuhusu Maadhimisho ya Miaka 30 ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA, kiukweli kabisa, VETA imefanya makubwa, mazuri na ya kupendeza kwa Tanzania.​

Natoa wito kwa Wana JF, kuanzia Jumanne hadi Ijumaa, tujitokeze kwa wingi, katika Viwanja vya JNCC, kwenda kuyashuhudia makubwa hayo ambayo VETA imeyafanya.

Hivyo haya yote makubwa, mazuri, yanayoendelea kufanywa ndani ya VETA, yasingewezekama kama Sio Rais Samia kwa bold decisions kujenga vyuo vya VETA, kila Mkoa na kila wilaya, Waziri wa Elimu, Prof. Adolf Mkenda, sio tuu kwa kuikubali VETA, bali KuuVETISHA mfumu mzima wa elimu nchini kupitia mtaala mpya wa elimu, ambapo sasa unajumuisha mafunzo ya amali (ufundi), Mwenyekiti wa Bodi ya VETA, Prof. Sifuni Mchome, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Kijana CPA Anthon Mzee Kasore, Menejimenti, na Wafanyakazi wote wa VETA, wanastahili wapewe maua yao!, kwa kuifikisha VETA hapa ilipo.​

Kuanzia kesho siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa, itakuwa ni wiki ya VETA, macho na masikio yetu yote tuyaelekeze katika maadhimisho hayo, yatakayo fanyika katika ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam,
Karibuni Sana!.
Paskali
 
VETA NI AIBU KWA TAIFA.
Miaka thelathini huwezi kwenda dukani ukakuta vifaa/bidhaa za veta.

Leo furniture tunaagiza nje,hata tooth pic,hata vibiriti?
Nimtu asiye na aibu anaweza kusifu kazi ndooogo za veta licha ya uwekezaji mkubwa wa serikali.

Wenzetu mfano Rwanda wanatengeneza/wanabadilisha mifumo ya pikipiki/magari kuwa ya umeme sisi veta ni usingizi. Wapi iyo veta?

Wenzetu wanawahudumu wataalamu kwenye malls/mahoteli makubwa hasa ya kitalii sisi wahudumu ni aibu hata lugha hawaijui. Wapi iyo veta?

Wenzetu Wana mafundi wabobezi wa simu, tv, computer nk. Sisi nivishoka wanakaa barazani kutapelitapeli wanajua kufutafuta tuu na kubadili spika na mic. wapi iyo veta? Wengi tumefungia ndani vifaa vilivyoharibika kidogo kwakuwa hatutaki viharibiwe zaidi namafundi uchwara!

Wenzetu wanakilimo Cha kiufundi kuanzia irrigation system nk sisi hakuna wataalam waveta watakufungia ni vijana tuu waliojifunza mtaani.

Wenzetu wanabuni vifaa vya ujenzi vyakisasa kuanzia cement,bati msauzi,wall papers nk. sisi veta hamna wanachogundua chakusaidia sekta.

Tunapigwa jua nchi nzima na kulalama kilaleo nilidhani veta wangetuletea modified solar system lakini waaapi hawana hata dalili hiyo...

Tunaongelea nishati jadilifu tueleze veta wamegundia majiko ya gesi? Ama kutoa nuru ya jinsigani gesi yetu itumike kuondoa matumizi ya kuni/mkaa??

Tunakakiwanda hata cha nguo cha wanaveta hata kimoja hii nchi? Aibu! Hadi magereza wanatengeneza viatu veta wameshindwa...hata kutengeneza juisi za veta hawawezi poor veta mnangoja ruzuku tuu ya serikali mfaidi kodizetu.

VETA imefeli kila idara na hakuna taasisi inatuangusha hii nchi kama Veta.Katika zamahizi za ushindani wa teknolojia wameshindwa kuleta wataalamu hata wakichina wakawafundisha vijana kilakitu tunaagiza china hadi maua!!

AIBU KUBWA NA IWAFIKIE NINYI VIONGOZI WA VETA WOOTE TAJWA HAPO JUU NA MAJINAYENU TUTAYAANDIKA KWA SIZI LA MKAA YAPEPERUSHWE MSIKUMBUKWE! MAANA KATIKA ZAMA HIZI ZA TEKNOLOJIA MMETUANGUSHA MMMNO...
SHAME ON YOU VETA!!!
 
Wanabodi,
Hii ni makala yangu kwenye gazeti la Nipashe la Leo.
View attachment 3272183

Hii Makala yangu kuhusu Maadhimisho ya Miaka 30 ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA, kiukweli kabisa, VETA imefanya makubwa, mazuri na ya kupendeza kwa Tanzania.​

Natoa wito kwa Wana JF, kuanzia Jumanne hadi Ijumaa, tujitokeze kwa wingi, katika Viwanja vya JNCC, kwenda kuyashuhudia makubwa hayo ambayo VETA imeyafanya.

Hivyo haya yote makubwa, mazuri, yanayoendelea kufanywa ndani ya VETA, yasingewezekama kama Sio Rais Samia kwa bold decisions kujenga vyuo vya VETA, kila Mkoa na kila wilaya, Waziri wa Elimu, Prof. Adolf Mkenda, sio tuu kwa kuikubali VETA, bali KuuVETISHA mfumu mzima wa elimu nchini kupitia mtaala mpya wa elimu, ambapo sasa unajumuisha mafunzo ya amali (ufundi), Mwenyekiti wa Bodi ya VETA, Prof. Sifuni Mchome, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Kijana CPA Anthon Mzee Kasore, Menejimenti, na Wafanyakazi wote wa VETA, wanastahili wapewe maua yao!, kwa kuifikisha VETA hapa ilipo.​

Kuanzia kesho siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa, itakuwa ni wiki ya VETA, macho na masikio yetu yote tuyaelekeze katika maadhimisho hayo, yatakayo fanyika katika ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam,
Karibuni Sana!.
Paskali
Bidhaa zao wanauzia wapi kwa scale gani na zinaingiza kiasi gani kwenye GDP?Imechangia kupunguza ajira kwa asilimia ngapi? Ubora wa bidhaa wanazozalisha mafundi kutoka hapo ukoje ukilinganisha na nchi za wenzetu? Nadhani hayo ndio yalitakiwa uyaeleze kabla ya sifa nyingi za kua na vyuo vya Veta kila wilaya, kumbuka mtaala wa mkoloni ulikua na somo la study za kazi kama somo na watu walijifunza utaalamu mbalimbali,na hata enzi za mkapa kurudi nyuma kulikua na somo la Kilimo mashuleni ambao hawa unaowapa maua wameyaondosha yote hayo ni jambo jema kusifia kwa merits kwakuonesha mafanikio kwa quality and quantity vinginevyo yanakua yale yale yakina Jaku boy kuhadaa wananchi.
 
CCM imeshindwa kuongoza nchi hii. Nchi yenye ardhi tele yenye rutuba inashindikana vipi vijana wote kujiajiri kwenye kilimo mpk imefika mahalo wanategemea betting na kudanga?
 
VETA NI AIBU KWA TAIFA.
Miaka thelathini huwezi kwenda dukani ukakuta vifaa/bidhaa za veta.

Leo furniture tunaagiza nje,hata tooth pic,hata vibiriti?
Nimtu asiye na aibu anaweza kusifu kazi ndooogo za veta licha ya uwekezaji mkubwa wa serikali.

Wenzetu mfano Rwanda wanatengeneza/wanabadilisha mifumo ya pikipiki/magari kuwa ya umeme sisi veta ni usingizi. Wapi iyo veta?

Wenzetu wanawahudumu wataalamu kwenye malls/mahoteli makubwa hasa ya kitalii sisi wahudumu ni aibu hata lugha hawaijui. Wapi iyo veta?

Wenzetu Wana mafundi wabobezi wa simu, tv, computer nk. Sisi nivishoka wanakaa barazani kutapelitapeli wanajua kufutafuta tuu na kubadili spika na mic. wapi iyo veta? Wengi tumefungia ndani vifaa vilivyoharibika kidogo kwakuwa hatutaki viharibiwe zaidi namafundi uchwara!

Wenzetu wanakilimo Cha kiufundi kuanzia irrigation system nk sisi hakuna wataalam waveta watakufungia ni vijana tuu waliojifunza mtaani.

Wenzetu wanabuni vifaa vya ujenzi vyakisasa kuanzia cement,bati msauzi,wall papers nk. sisi veta hamna wanachogundua chakusaidia sekta.

Tunapigwa jua nchi nzima na kulalama kilaleo nilidhani veta wangetuletea modified solar system lakini waaapi hawana hata dalili hiyo...

Tunaongelea nishati jadilifu tueleze veta wamegundia majiko ya gesi? Ama kutoa nuru ya jinsigani gesi yetu itumike kuondoa matumizi ya kuni/mkaa??

Tunakakiwanda hata cha nguo cha wanaveta hata kimoja hii nchi? Aibu! Hadi magereza wanatengeneza viatu veta wameshindwa...hata kutengeneza juisi za veta hawawezi poor veta mnangoja ruzuku tuu ya serikali mfaidi kodizetu.

VETA imefeli kila idara na hakuna taasisi inatuangusha hii nchi kama Veta.Katika zamahizi za ushindani wa teknolojia wameshindwa kuleta wataalamu hata wakichina wakawafundisha vijana kilakitu tunaagiza china hadi maua!!

AIBU KUBWA NA IWAFIKIE NINYI VIONGOZI WA VETA WOOTE TAJWA HAPO JUU NA MAJINAYENU TUTAYAANDIKA KWA SIZI LA MKAA YAPEPERUSHWE MSIKUMBUKWE! MAANA KATIKA ZAMA HIZI ZA TEKNOLOJIA MMETUANGUSHA MMMNO...
SHAME ON YOU VETA!!!
Veta waje na;
Mfundishe,
Wanafunzi wafundishwe namna na kuwezeshwa ujuzi wa kutumia tools za kisasa katika fani mbalimbali mfano; Utengenezaji wa furnitures.

Atengeneze,
Baada ya kufundishwa wale wenye uelewa na ubunifu wawezeshwe kutengeneza bidhaa katika viwango vya sokoni na kwa kuwa katika hizo intake za wanafunzi wapo ambao watakuwa cteam basi wajitahidi kupata cream ya wanafunzi hata wawili katika kipindi fulani ili kupata watu competent wanaoweza kukabiliana na soko la bidhaa zilizopo sokoni.

Auze
Baadae wauze bidhaa zile na kidogo kidogo watapenya sokoni na jambo hili litaweza kuajiri wengi katika kila Veta wafanye hivi kwa mgawanyo wa bidhaa za kutengeneza na kwa sbb ya network kubwa basi wanaweza kujikuta wanafanya vzr sana katika soko.
 
Back
Top Bottom