Miaka 22 kwenye ndoa, kabadilika ghafla!

Miaka 22 kwenye ndoa, kabadilika ghafla!

Mmawia

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
122,521
Reaction score
96,267
Wana JF,

Habari za asubuhi.

Mimi nimeoana na mke wangu na sasa tuna zaidi ya miaka 22 ktk ndoa. Wakati namuoa kipato changu kilikuwa kizuri sana, wakati yeye alikuwa mfanyakazi wa kada ya chini, alikuwa ananipenda na kuniheshimu sana, ila sasa kipato changu kimetoweka na yeye amepata madaraka makubwa ameanza kunidharau.

Nikimkosoa anasema nipe talaka yangu niende kwetu. Haishi kuninunia kila kukicha na tayari tuna watoto sita, nifanyeje?

Naombeni ushauri. Tumefunga ndoa ya kikristu.
 
Pole sana,wewe je labda hukumnyanyasa ulipokuwa nazo?
 
^^
Miaka 22!!
Kuna mtu huwa anafanya maamuzi kwa niaba yako?
^^
 
Ukubali tu kupelekeshwa kama unataka kulelewa au kama laaah basi maamuzi ni yako???????/
 
Miaka 22 katika ndoa bado hujui namna ya kudeal na ups na downs za ndoa hadi uombe ushauri JF? Kama hii ni habari ya kweli basi hazikutoshi upstairs! Kwa mbali naona hii thread haina ukweli wowote bali umeamua kufurahisha hadhira JF!
 
Mpe tu watoto 6 washakuwa hao! Huyo mkeo keshapata kibosile kingne!
 
Back
Top Bottom