Miaka 15 ya kifo cha Horace Kolimba

Miaka 15 ya kifo cha Horace Kolimba

Nikupateje

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2009
Posts
1,334
Reaction score
990
Leo ni March 13, 2012 ambapo tarehe kama hii kuanzia mida kama hii, Horace Kolimba alifariki ghafla saa chache baada ya kuhojiwa na NEC ya CCM kuhusu matamshi yake kuwa "CCM imekosa dira".

Tunapokumbuka siku ya leo kihistoria, basi tukio hili la kifo cha Kolimba haliwezi kuepukwa na ni kazi yetu kuweka sawa historia kwa kuikumbushakumbusha usahihi wake kama hivi.

Idumu mitandao kama JF inayofanya tuweze kufanya hivi.
 
Marekebisho: ni muda mfupi baada ya kuhojiwa na Kamati Kuu yani Central Committee au CC na sio NEC kama ulivyoandika na alipata shinikizo la damu na sio kuuwawa.
 
Na ukitaka kujua CCM waliamua kumpoteza huyu jamaa yaani hata kwenye historia ya chama chao wamemfutilia mbali kabisa hata picha ya huyu marehemu kwenye maktaba zao wameziDelete kabisa nimezitafuta kwa bidii lakini wapi!
 
kuna muda hua nakaa nakufikiri na vilevile najijibu mwenyewe, SIASA NI UPUMBAVU usio na maana kabisa, embu fikiri maisha ya kolimba na utafakari then utajua ninamaanisha nini.

vilevile chukua muda mtafakari mtu kama Mwakyembe jinsi anavyo teseka maskini mnyakyusa wa watu.
 
Kolimba aliuwawa na system baada ya kuona Mkapa angepata shida katika utawala wake kama angeachwa hai.Kolimba pia alihitilafiana na Nyerere kipindi akiwa katibu mkuu wa CCM baada ya kubariki mpango wa serekali tatu huku akijua sera ya CCM ilikuwa serekali mbili.

Katibu mkuu wa CCM Kolimba na waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais John Malecela wakapigwa chini (wakatimuliwa katika nafasi zao).
 
Ingawa huwa nasikia tu Kolimba kolimba, but May his soul rest in peace
 
leo hii kuikosoa ccm kwa kukosa dira tungeshauawa sijui watu wangapi. ccm then ilikuwa kwenye denials. ilishapoteza mwelekeo lkn ilikuwa haitaki kuabiwa ukweli. labda ingejirekebisha leo hii hizi criticisms za kukosa mwelekeo zisingekuwepo na labda tungekuwa na better tz. ingawa hivyo, kuna vifo vingi sana vimetokea ktk mazingira ya kutatanisha tulipotoka kwenye mfumo wa chama kimoja na kuhamia mfumo wa vyama vingi. iko siku ukweli utajidhihirisha wazi na wauaji kuwekwa bayana
 
Walikufa Wengi, Kina Charles Kabeho,Kighoma Malima, Amrani Mayagila, nk..long time
 
Walijua wakimlaza CCM itafufuka, kumbe ndiyo inazidi kuzama.
Kolimba, tulikupenda lakini CCM ilikupenda zaidi.
R.I.P!
 
Marehemu Horice Kolimba alikuwa amejiandaa kwenda kusema ukweli bungeni kuhusu madhambi ya ccm na akiwa Bungeni akajisikia vibaya kabla hajazungumza. Majamaa yetu yale yalikuwa yamesha mkolimba. Ikawa the end of one of the brave men we ever had inside CCM. Mi nafikiri tusiwalaumu sana magamba wapiga mabenchi na kelele za ndiyo. Wako kwenye mafia squad wakienda oposite tu wanakolombiwa na wale wa vitu vya kuteuliwa wana Chifupaiwa. Usalama utapatikana tu pale mpiga kura atakapotia kura yake ya mabadiliko kwenye box la kura.

Chadema tudeal na kuelimisha tu wananchi na si vinginevyo.
:israel:
 
Una ushahidi ? Watu wengine mnaitafutia serikali lawama ,wangapi wamesema makubwa ndani ya bunge na hadi hii leo wapo ,yaani ukiwa bungeni huwezi kufikiwa na kifo au na maradhi ya ghafla na kupoteza uhai ??? Unataka kuniambia wakubwa vigogo mawaziri raisi hawawezi kufikwa na kifo cha ghafla popote pale wawapo /? Ni mara ngapi mheshimiwa Kikwete ameanguka hadharani ? Mbona hamsemi kama vyama vya upinzani vimemroga,
 
Back
Top Bottom