trachomatis
JF-Expert Member
- Jun 7, 2011
- 3,758
- 746
Takribani miaka kadhaa iliyopita,nilikuwa na galfriend ambaye alikuwa akitoka na mzee mmoja mwenye fedha zake. Ilichukua akili,muda na gharama kidogo kumuachanisha na huyo baba,kwa taaluma ni Eng.
Nilipiga sana simu,nilienda baa alizokuwa anakunywa,na kumsihi asimfuate tena yule dada.Alikubali.Akanishauri nimuoe kabisa,nami nikamwambia,ndiyo lengo langu.
Ndipo nilipotangaza nia ya kufunga pingu za maisha na yule dada,vikao vikaanza pale Riverside.
Jumamosi moja kabla ya Jumamosi ya harusi,mi na mchumba wangu tulienda duka moja maarufu kwa mapambo ya maharusi na sherehe kama hizo,ni K'koo jirani na mlango wa magari yanayoingia shimoni..
Nikiwa busy naangalia mapambo,mchumba wangu akiwa na furaha na bashasha tele, akanistua nigeuke,na nilipogeuka,hamadi uso kwa uso na Eng na midevu yake,akiwa na mkewe!
Nilimsalimia ye na mkewe na nikatokomea baa iitwayo Palace nikaanza kunywa kwa hasira.
Nilikumbuka taabu niliyopata kuwaachanisha,nililia na nikamwadithia mbaba wa kaunta..
Nilipiga sana simu,nilienda baa alizokuwa anakunywa,na kumsihi asimfuate tena yule dada.Alikubali.Akanishauri nimuoe kabisa,nami nikamwambia,ndiyo lengo langu.
Ndipo nilipotangaza nia ya kufunga pingu za maisha na yule dada,vikao vikaanza pale Riverside.
Jumamosi moja kabla ya Jumamosi ya harusi,mi na mchumba wangu tulienda duka moja maarufu kwa mapambo ya maharusi na sherehe kama hizo,ni K'koo jirani na mlango wa magari yanayoingia shimoni..
Nikiwa busy naangalia mapambo,mchumba wangu akiwa na furaha na bashasha tele, akanistua nigeuke,na nilipogeuka,hamadi uso kwa uso na Eng na midevu yake,akiwa na mkewe!
Nilimsalimia ye na mkewe na nikatokomea baa iitwayo Palace nikaanza kunywa kwa hasira.
Nilikumbuka taabu niliyopata kuwaachanisha,nililia na nikamwadithia mbaba wa kaunta..