Mheshimiwa Zitto na wana-CHADEMA.....

Engineer Mohamed

JF-Expert Member
Jul 27, 2007
451
9
Mheshimiwa Zitto Kabwe........

kwanaza nakupa kheri ya mwaka mpya 2008 wewe na wana-CHADEMA wote.
kwa vile hapa JF we Dare to Talk Openly...........
kwa heshima na taadhima tunakuomba utuwekee barua ulomuandikia Spika ili tuendelee kumkomalia NYANI na mapema 2008,tujue wapi PUMBA tutoe na tubakiwa na mchele safi.



Zitto: Sijatumia maneno ya kejeli



na Salehe Mohamed



MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), amesema maneno yaliyomo kwenye barua aliyomwandikia Spika Samuel Sitta, ni ya msingi na si kejeli wala dharau kama anavyoeleza spika huyo.
Alisema, mambo hayo ya msingi yanapaswa kufanyiwa kazi na Spika badala ya kukwepeshwa kama anavyofanya sasa kwa kudai barua hiyo imejaa maneno ya dharau na kejeli kwa Bunge.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Zitto alisema hawezi kumwandikia Spika barua ya kejeli kwa kuwa anamheshimu kutokana na umri, cheo na ukomavu wake katika siasa.

Alisema Bunge ni mahali pa heshima, ndiyo maana alitumia busara kuandika barua hiyo akitaka haki itendeke.

"Siwezi kuandika maneno ya kejeli wakati nina hoja za msingi na ninahitaji zifanyiwe kazi ili niweze kupata haki yangu na kusafishwa jina langu," alisema Zitto.

Aidha, Zitto alifafanua kuwa hawezi kwenda mahakamani kama iliyoelezwa na Spika kwa vyombo vya habari hadi atakapopata majibu ya barua yake.

"Mimi nilimpelekea barua kutaka adhabu niliyopewa ya kusimamishwa bungeni Agosti mwaka jana ipitiwe upya hivyo naye anapaswa kunijibu kwa maandishi, baada ya hapo nitajua cha kufanya," alisisitiza Zitto.

Desemba 24 mwaka jana, Zitto aliwasilisha barua kwa Sitta, akitaka kupitiwa upya kwa adhabu aliyopewa ya kusema uongo bungeni.

Alisema kusimamishwa huko kulimfanya aonekane muongo ndani na nje ya Bunge, hivyo anamtaka Spika na baadhi ya mawaziri kuchukuliwa hatua kwa madai ya kuueleza umma kwamba yeye ni mwongo huku wakishindwa kuthibitisha madai yao.

Baada ya kupokea barua hiyo, Spika kupitia Katibu wake, Daniel Eliufoo, alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akieleza kuwa Zitto atapelekwa kwenye Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kuwa barua yake imejaa kejeli, ufedhuli na ubabe dhidi ya Bunge na Spika.


http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/1/1/habari22.php




 
Nami naunga mkono. Mhe. Spika anasema barua ya Mhe. Zitto imejaa maneno ya kejeli. Hivyo, ni vyema Mhe. Zitto akaweka barua yake kwa Spika wazi ili nasi tuweze kuichambua na kujua ukweli uko wapi.
 
Mbona hiyo barua ya Zitto iliwekwa hapa tayati? Iliwekwa na Zitto mwenyewe. Search kwenye threads mbali mbali na mtaiona.
 
Barua hiyo hapo chini na imewekwa na Zitto mwenyewe, cha kushangaza amekanusha kwenye vyombo vya habari kuwa ka post barua hii kwenye net, hii ina maana Zitto wa JF sio Zitto Mbunge somebody ana play na jina lake tu.... hawa ndio viongozi wetu m-badala safari ipo ndefu mbele yetu...

 
Mbona ni barua ya kawaida sana. Sioni matusi au maneno ya kejeli. Nadhani Mhe. Spika ametumia ubabe katika kukataa kujibu barua hii.
 

Tuwekee hiyo 'quote' aliyokanusha nasi tuione.
 
Mbona ni barua ya kawaida sana. Sioni matusi au maneno ya kejeli. Nadhani Mhe. Spika ametumia ubabe katika kukataa kujibu barua hii.

Nina wasi wasi Spika 6 asipo kuwa makini anaelekea kujifunga bao la pili la wazi wazi! kwani hili sakata laweza ibuka upyaaa!, and this time CHADEMA pleeeeeese msipoteze nafasi tena, CHOTA, narudia tena CHOTENI wanachama wa kutosha tayali kwa 2010.
 
Tuwekee hiyo 'quote' aliyokanusha nasi tuione.

Eeeh jamani. Mshaanza, hebu muacheni Zitto wetu. Ni kweli alisema. Na ni ukweli hakuitoa kwenye internet baada ya kumpelekea spika. Aliitoa baada ya barua yenyewe kuvuja katika vyombo vya habari, kutoka kati ya ofisi ya spika au ya kiongozi wa upinzani. Ndio yeye akamua kuitoa sasa ili wananchi barua yenyewe imesemaje haswa. Kwa hiyo isingevuja kwenye press na kuzua mjadala naye asingeitoa labda. We Masatu, usianzie zodo zodo hapa

Asha
 
Dua na Masatu.....

suali zuri sana hilo,tuwekeeni hizo source na cc tuone wenyewe.


Asha abdallah......

kiongozi wa UPINZANI BUNGENI nani?

Mheshimiwa Zitto......

tunafahamu kuwa sio sana kupitia JF,lakini tunaamini kuwa kuna watu wanakuletea news kama umetajwa ktk JF matokeo yake unakuja kujibu hoja zinazokuhusu,tunaomba na HILI UJE UTUJIBU TAFADHALI.
 

Masatu naye?! Nilitaka kumjibu hivihivi, naona umeniwahi. ahsante sana.
 
Is there anything to discuss here? Au ndiyo Spika 6 alikuwa anataka tuone lile alilosema "standards", sioni la maana la kujadili kama alitaka kutukuzwa kama Mungu basi kwakuwa Zitto hakumuita mtukufu ndio maana anaona hiyo barua ina kejeli! mimi siioni, labda sina busara!
 
Dua source ya habari ya Zitto kukanusha hii hapo chini kupitia gazeti "letu" la TanzaniaDaima unless kama huliamini....


 
Kitila/Asha ulitaka Source...what next? baadhi yetu huwa tunafikiri negative tu...Hata kama mtu analiponda gazeti xyz, lkn si kwamba atakuwa hatetei..au ushamuweka masatu ktk kundi Fulani?
 
kama Zitto kambinga, thats means Zitto anaechangia JF sio ZITTO HALISI ni wa Kuchorwa...itabidi mwanakijiji atutungie msamiati kama alivyomtungia kikwete simba wa kuchora..
Kama hivyo Ndivyo ndio maana binafsi nilipinga wazo la mmoja wetu kuwa JF iendeshwe kama Taasisi then tuwachague watu wenye majina halisi humu JF kuongoza, kumbe wenye Majina Halisi nao wanapokumbwa na kashfa/au Issue HUCHOMOA KUHUSIKA KWAKO HUMU JF...
 
Ha! ndo maana sioni comment za zitto tena! pole sana. wanaposema mitandao ya internet wanamaana JF au? kudadadeki. JF jicho pana hata mzee wa jogoo lilimwona pale J'berg airport.
 
labda kejeli ni kwa "mtu mzima kuambiwa aombe msamaha na akiri kosa" si unajua tamaduni kwamba mtu mzima haambiwi kaj**ba?

aidha inategemea barua iliandikwa kwa nani. yaani spika au mh. sita. sasa kama iliandikwa kwa spika na ikawa imefikishwa ofisi ya spika na kupokelewa na haikuwa imeandikwa "siri/confidential" itabidi tujiulize ni nani aliyeivujisha kwenye vyombo vya habari?

nakumbuka zitto alipoiweka barua hapa jf alisema nia ni kuwapa wanachama kile chote alichoandika badala ya wanatu kutegemea nusu habari za magazeti
 
Masatu

Sasa shida iko wapi hapo. Zito alitoa barua hiyo hapa baada ya kuona kwamba aliyeandikiwa kesha ipata na kumpa muda wa kutafakari. Ulitaka Daily News waitoe ya uongo? CCM na Watanzania MAFISADI ndio wametufikisha hapa wanataka kila kitu kiwe siri. Hakuna ujinga ujinga huu wa siri kila kitu, kwani kuna ubaya gani hata kama hiyo barua ipo kwenye luninga. Technologia mjomba twende na wakati tupo karne ya 21 siyo ya 10.

Waambieni watoe report ya BOT au bado wanaipika. Jamani tuweke Utanzania mbele na tuache longolongo ambazo hazina faida na taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…