Engineer Mohamed
JF-Expert Member
- Jul 27, 2007
- 453
- 7
Mheshimiwa Zitto Kabwe........
kwanaza nakupa kheri ya mwaka mpya 2008 wewe na wana-CHADEMA wote.
kwa vile hapa JF we Dare to Talk Openly...........
kwa heshima na taadhima tunakuomba utuwekee barua ulomuandikia Spika ili tuendelee kumkomalia NYANI na mapema 2008,tujue wapi PUMBA tutoe na tubakiwa na mchele safi.
Zitto: Sijatumia maneno ya kejeli
na Salehe Mohamed
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), amesema maneno yaliyomo kwenye barua aliyomwandikia Spika Samuel Sitta, ni ya msingi na si kejeli wala dharau kama anavyoeleza spika huyo.
Alisema, mambo hayo ya msingi yanapaswa kufanyiwa kazi na Spika badala ya kukwepeshwa kama anavyofanya sasa kwa kudai barua hiyo imejaa maneno ya dharau na kejeli kwa Bunge.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Zitto alisema hawezi kumwandikia Spika barua ya kejeli kwa kuwa anamheshimu kutokana na umri, cheo na ukomavu wake katika siasa.
Alisema Bunge ni mahali pa heshima, ndiyo maana alitumia busara kuandika barua hiyo akitaka haki itendeke.
"Siwezi kuandika maneno ya kejeli wakati nina hoja za msingi na ninahitaji zifanyiwe kazi ili niweze kupata haki yangu na kusafishwa jina langu," alisema Zitto.
Aidha, Zitto alifafanua kuwa hawezi kwenda mahakamani kama iliyoelezwa na Spika kwa vyombo vya habari hadi atakapopata majibu ya barua yake.
"Mimi nilimpelekea barua kutaka adhabu niliyopewa ya kusimamishwa bungeni Agosti mwaka jana ipitiwe upya hivyo naye anapaswa kunijibu kwa maandishi, baada ya hapo nitajua cha kufanya," alisisitiza Zitto.
Desemba 24 mwaka jana, Zitto aliwasilisha barua kwa Sitta, akitaka kupitiwa upya kwa adhabu aliyopewa ya kusema uongo bungeni.
Alisema kusimamishwa huko kulimfanya aonekane muongo ndani na nje ya Bunge, hivyo anamtaka Spika na baadhi ya mawaziri kuchukuliwa hatua kwa madai ya kuueleza umma kwamba yeye ni mwongo huku wakishindwa kuthibitisha madai yao.
Baada ya kupokea barua hiyo, Spika kupitia Katibu wake, Daniel Eliufoo, alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akieleza kuwa Zitto atapelekwa kwenye Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kuwa barua yake imejaa kejeli, ufedhuli na ubabe dhidi ya Bunge na Spika.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/1/1/habari22.php
kwanaza nakupa kheri ya mwaka mpya 2008 wewe na wana-CHADEMA wote.
kwa vile hapa JF we Dare to Talk Openly...........
kwa heshima na taadhima tunakuomba utuwekee barua ulomuandikia Spika ili tuendelee kumkomalia NYANI na mapema 2008,tujue wapi PUMBA tutoe na tubakiwa na mchele safi.
Zitto: Sijatumia maneno ya kejeli
na Salehe Mohamed
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), amesema maneno yaliyomo kwenye barua aliyomwandikia Spika Samuel Sitta, ni ya msingi na si kejeli wala dharau kama anavyoeleza spika huyo.
Alisema, mambo hayo ya msingi yanapaswa kufanyiwa kazi na Spika badala ya kukwepeshwa kama anavyofanya sasa kwa kudai barua hiyo imejaa maneno ya dharau na kejeli kwa Bunge.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Zitto alisema hawezi kumwandikia Spika barua ya kejeli kwa kuwa anamheshimu kutokana na umri, cheo na ukomavu wake katika siasa.
Alisema Bunge ni mahali pa heshima, ndiyo maana alitumia busara kuandika barua hiyo akitaka haki itendeke.
"Siwezi kuandika maneno ya kejeli wakati nina hoja za msingi na ninahitaji zifanyiwe kazi ili niweze kupata haki yangu na kusafishwa jina langu," alisema Zitto.
Aidha, Zitto alifafanua kuwa hawezi kwenda mahakamani kama iliyoelezwa na Spika kwa vyombo vya habari hadi atakapopata majibu ya barua yake.
"Mimi nilimpelekea barua kutaka adhabu niliyopewa ya kusimamishwa bungeni Agosti mwaka jana ipitiwe upya hivyo naye anapaswa kunijibu kwa maandishi, baada ya hapo nitajua cha kufanya," alisisitiza Zitto.
Desemba 24 mwaka jana, Zitto aliwasilisha barua kwa Sitta, akitaka kupitiwa upya kwa adhabu aliyopewa ya kusema uongo bungeni.
Alisema kusimamishwa huko kulimfanya aonekane muongo ndani na nje ya Bunge, hivyo anamtaka Spika na baadhi ya mawaziri kuchukuliwa hatua kwa madai ya kuueleza umma kwamba yeye ni mwongo huku wakishindwa kuthibitisha madai yao.
Baada ya kupokea barua hiyo, Spika kupitia Katibu wake, Daniel Eliufoo, alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akieleza kuwa Zitto atapelekwa kwenye Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kuwa barua yake imejaa kejeli, ufedhuli na ubabe dhidi ya Bunge na Spika.
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/1/1/habari22.php