Mheshimiwa Zitto Kabwe


Yeye tangu mwanzo hakusema kama unavyomsemea hapa

Ulichosema Semilong ni sahihi na hakina ubishi, kuwa Zito hakutakiwa kwenda kusoma PhD kwa sababu yuko kazini(kaajiriwa na wapiga kura wake)

Ila naamini kuwa kuwa likizo sio lazima usafiri au uende mbali sana na eneo la kazi. Zito kama wabunge wengine wote-I mean wote (>250) wako likizo kama definition yako ya likizo ni kuwa nje ya eneo la wapiga kura.

Tangu "kuumbwa" kwa taifa hili, wabunge huwa hawakai katika majimbo yao! if are we to use that standard then ni wabunge wote. kama hii ni sawa Tanzania basi Zito hana kosa, kama ni kosa basi wooote wabunge wana makosa.
 


haya ndio matibabu!
 

Hivi kama hamjui mambo si mkae kimya tu kwani mtaulizwa kuwa kwanini hamkuchangia? Kama ulisema kuwa postgraduate ni degree baada ya undergraduate na yeye kasema second postgraduate, hujui kwamba yeye ni masters holder tayari? acheni chuki binafsi za maendeleo ya watu. Kama nyie ubongo umelala na hamhangaiki kutafuta shule mnasubili mletewe kitandani barua za admission na scholarship basi kaeni kimya na walio na juhudi za kutafuta shule wasome. Binafsi kwa kudeclare interest nimesoma masters mbili tena kwa gharama zaidi hata ya huyo Zitto na zote nimepata scholarship. Watu bana, yaani kutafuta tafuta vimaneno tu na kuoneana kijicho. Mbona watoto wa viongozi wenu wanaosomeshwa huku Ulaya kwa kutumia pesa wanazowakwida wananchi huko bongo hamuwasemi. Na huyo anayejiita mmakonde anatuka watu rubbish nadhani una matatizo ya akili. Au Zitto kusoma hapo kumekuuma sana maana hukuweza kupata nafasi hiyo? Masuala ya utawezaje kusoma huku ukitumiakia taifa ni jinsi unavyopanga muda wako na makubaliano yako na mwajili wako. Mnajua Ubunge unatoa taratibu gani kwa mbunge akitaka kujiendeleza kielimu? Au ndo kuzungumza tu bora uzungumze huku hauna data. Au mna hypothesis zenu hapa mnataka kuzitest? Kuweni wawazi bana na acheni hoja zisizokuwa na msingi wowote. Mchango anaoutoa Zitto Bungeni hata kama hahudhurii kwa muda Bungeni nadhani ni mkubwa sana kuliko Mambumbu wa CCM wanaolala humo Bungeni na huku hayana kazi nyingine za kufanya.
 

kazi kweli kweli
 
Piga kitabu kaka, twaitaji wasomi nchi isonge mbele. Big up Dr. Zitto Zuberi Kabwe-PhD/MP/CDM.
 
Zitto kwa nini achague chuo cha Private?
au anataka kuchakachua PhD mwishowe CDM isemwe ni mafisadi wa elimu.

Zitto chagua chuo cha maana uikomboe nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…