Mheshimiwa Engineer Samawati Mbunge!

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
TBC hapa kuna Waziri anatumia muda mrefu kweli kwenye majumuisho ya Wizara yake...
anataja waheshimiwa kibao waliochangia kwenye majadiliano, kwa majina...na kumalizia..Mheshimiwa ....."mbunge".Hii imefanya atumie muda mrefu sana wakati sisi wananchi tunachotaka ni kusikia hoja na siyo majina.

Najiulizayafuatayo:
1. Kuna ulazima gani kuwataja majina na ubunge wao?
2. Je mtu asiye mbunge angeweza kuchangia?
3. Nini mantiki ya orodha hiyo badala ya kujibu hoja?

Tuelimisheni wajuaji wa mambo.

******Niwie radhi bibie Samawati.... nakutakia kila la kher!
 
huu ni utaratibu kuendana na kanuni za bunge, mabadiliko ya kanuni ndo yanaweza leta sura tofauti
 
TBC hapa kuna Waziri akutumia muda mrefu kweli kwenye majumuisho ya Wizara yake...
anataja waheshimiwa kibao waliochangia kwenye majadiliano, kwa majina...na kumalizia..Mheshimiwa ....."mbunge".Hii imefanya atumie muda mrefu sana wakati sisi wanancho tunachotaka ni kusikia hoja na siyo majina.

Najiulizayafuatayo:
Kuna ulazima gani kuwataja majina na ubunge wao?
Je mtu asiye mbunge angeweza kuchangia?
Nini mantiki ya orodha hiyo badala ya kujibu hoja?

Niwie radhi bibie Samawati.... nakutakia kila la kher!

Dada Wos asante kunipandisha cheo. Itabidi nikazane sana nisikuangushe 2015
 
Kumbe kuna mtu kaona hiki kioja. Imekuwa ni desturi kwa mtoa hoja - yaani bajeti (i.e Waziri) wakati wa mahitimisho wa hoja yake anawatajwa wabunge wote waliochangia. Kitu ambacho najiuliza kuna umuhimu gani kuwataja kwa majina wachigiaji? hii time wasting ilitokana na nini hasa? Bado naweza kusema bunge na hata serikali inaendeshwa kwa mazoea, hakuna idea mpya kabisa.
 
Hivi huu mtindo wa kumtambulisha ama kumuita mtu kwa kutumia fani yake mbele ya jina lake umeanza lini? Manake siku hizi mtu ukiwa mhandisi basi utaitwa 'mhandisi' flani wa flani...ukiwa mhasibu utaitwa 'mhasibu' flani wa flani.

Labda mimi kumbukumbu yangu ni ndogo lakini hapo zamani wahandisi, wahasibu, n.k. hawakuitwa kwa fani zao. Ila sasa naona huu utaratibu umeshika kasi sana. Sijui kwa nini tu?
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Kichekesho ni pale wanapesema....fulani fulani - "mbunge'.
Hivi kuna anahudhuria au kutoa mchango kama sio mbunge! vilaza!
 
Hivi huu mtindo wa kumtambulisha ama kumuita mtu kwa kutumia fani yake mbele ya jina lake umeanza lini? Manake siku hizi mtu ukiwa mhandisi basi utaitwa 'mhandisi' flani wa flani...ukiwa mhasibu utaitwa 'mhasibu' flani wa flani.

Labda mimi kumbukumbu yangu ni ndogo lakini hapo zamani wahandisi, wahasibu, n.k. hawakuitwa kwa fani zao. Ila sasa naona huu utaratibu umeshika kasi sana. Sijui kwa nini tu?

Ninavyofikiri mimi ( naweza nisiwe sahihi), enzi za mwalimu, wanasiasa walikuwa wanasiasa na wenye fani zao walikuwa kwenye fani. Ni miaka ya sasa tu tunaona wenye fani wakipigana vikumbo majimboni kugombea ubunge! Na pia ni miaka ya sasa tunaona kila mwanasiasa akihangaika sana kupata shahada ya Uzamivu (PHD) na kufanya PHD iwe kama cheti cha darasa la 12!

Huenda kuna sababu pia ya kujaribu kujitofautisha na wale wasiokuwa na shahada au "professions adimu"!
 
ninavyofikiri mimi ( naweza nisiwe sahihi), enzi za mwalimu, wanasiasa walikuwa wanasiasa na wenye fani zao walikuwa kwenye fani. Ni miaka ya sasa tu tunaona wenye fani wakipigana vikumbo majimboni kugombea ubunge! Na pia ni miaka ya sasa tunaona kila mwanasiasa akihangaika sana kupata shahada ya uzamivu (phd) na kufanya phd iwe kama cheti cha darasa la 12!

Huenda kuna sababu pia ya kujaribu kujitofautisha na wale wasiokuwa na shahada au "professions adimu"!

sababu yeyote ile lazima pia tufanane na dunia inavyokwenda......

Wewe umewahi sikia
mheshimiwa professa condoleeza rice....

Sisi ndo wasomi saaana wa dunia au?????????
 
Huyu waziri amekaa kweli hapa nchini?,hajui hata kutaja majina ya wabunge na hata mawaziri wenzake!
 
Ninavyofikiri mimi ( naweza nisiwe sahihi), enzi za mwalimu, wanasiasa walikuwa wanasiasa na wenye fani zao walikuwa kwenye fani. Ni miaka ya sasa tu tunaona wenye fani wakipigana vikumbo majimboni kugombea ubunge! Na pia ni miaka ya sasa tunaona kila mwanasiasa akihangaika sana kupata shahada ya Uzamivu (PHD) na kufanya PHD iwe kama cheti cha darasa la 12!

Huenda kuna sababu pia ya kujaribu kujitofautisha na wale wasiokuwa na shahada au "professions adimu"!

Hmm..okay!

Kwenye nchi za wenzetu ambazo zimekomaa kisiasa na kidemokrasia, kwenye mabunge yao wabunge huwa hawajitambulishi kwa fani zao. Mfano bunge la Marekani (chemba zote mbili) limesheheni wasomi wa ukweli lakini hata siku moja sijawahi kumuona Newt Gingrich akijitambulisha kama Dr. (wa PhD) Newt Gingrich, Speaker, US House of Representatives au Dr. (surgeon) Bill Frist, Senate Majority Leader, au sijui Advocate Barack Obama, US Senator, Illinois....

Sisi tunapenda sana ujiko wa kwenye makaratasi kuonyesha tumesoma. Hovyo kabisa....
 
sababu yeyote ile lazima pia tufanane na dunia inavyokwenda......

Wewe umewahi sikia
mheshimiwa professa condoleeza rice....

Sisi ndo wasomi saaana wa dunia au?????????

Au umewahi kusikia Advocate Bill Clinton au George W. Bush, MBA? Yaani sisi bana....eti advocate so and so au engineer so and so....hahahahaaa who cares about what they went to school for? Sana sana wanajiaibisha tu kwa sababu hakuna la maana hata walifanyalo huko bungeni achilia mbali majimboni mwao.
 
sababu yeyote ile lazima pia tufanane na dunia inavyokwenda......

Wewe umewahi sikia
mheshimiwa professa condoleeza rice....

Sisi ndo wasomi saaana wa dunia au?????????

Boss,
Kama kuna kitu kinanifanya nione aibu mbele ya wenzetu ughaibuni ni hulka yetu watanzania (hata wanaijeria ) kupenda kujitukuza kwa "credentials' .Haishangazi kuona kila mtu akitaka kuitwa Dr tena kwa muda mfupi sana - miaka 2 !

Siyo siri PHDs siku hizi ni kitu cha kawaida na wengi wanazo tena wanazipata wakiwa na umri mdogo in their 30s na huwezi kuona mtu anajitutumua kujulikana ni Dr X,Y,Z! Na hata hawapendi kuitwa Dr.... kama ni doctoral degree..na wanapenda kujiita kwenye maandishi zaidi -mfano: The Boss..( Phd)!

Inabidia tuanze kampeni kupunguza matumizi mabaya ya "Dr".Wajiite madaktari wa binadamu tu ili tuwatambue kwa urahisi tunapotaka huduma!
 
Boss,
Kama kuna kitu kinanifanya nione aibu mbele ya wenzetu ughaibuni ni hulka yetu watanzania (hata wanaijeria ) kupenda kujitukuza kwa "credentials' .Haishangazi kuona kila mtu akitaka kuitwa Dr tena kwa muda mfupi sana - miaka 2 !

Siyo siri PHDs siku hizi ni kitu cha kawaida na wengi wanazo tena wanazipata wakiwa na umri mdogo in their 30s na huwezi kuona mtu anajitutumua kujulikana ni Dr X,Y,Z! Na hata hawapendi kuitwa Dr.... kama ni doctoral degree..na wanapenda kujiita kwenye maandishi zaidi -mfano: The Boss..( Phd)!

Inabidia tuanze kampeni kupunguza matumizi mabaya ya "Dr".Wajiite madaktari wa binadamu tu ili tuwatambue kwa urahisi tunapotaka huduma!

WOS..
I am sure ukisafiri umewahi pia kukuta kwa mfano mtu
ni ceo lakini hata kwenye bussiness cars yake unakuta jina tu na adress ya kampuni..

sasa ukija sisi....

unakuta ceo.director general,dr,shaaban malinyingi,.mjumbe wa nec ccm....

yaani aibu zingine bana....
 
tutaanza kuonekana matapeli kama wa nigeria hata kama sio
kwa upuuzi kama huu...
 
Inabidia tuanze kampeni kupunguza matumizi mabaya ya "Dr".Wajiite madaktari wa binadamu tu ili tuwatambue kwa urahisi tunapotaka huduma!

Hii kampeni isianze na kuishia kwenye u-Dr. tu. Hata wahandisi, wahasibu, mawakili, na wengineo manake huko tunakokwenda sasa hata hakueleweki. Sitashangaa siku moja Michuzi naye akaanza kujitambulisha kama 'Photojournalist Issa Michuzi'.....au Kibonde kuanza kujiita 'Presenter Ephraim Kibonde'.

Mtu ni raisi wa nchi lakini bado unaitwa Dr. tena udokta wenyewe wa kupewa mezani. Sielewi kabisa mimi.
 
Hii kampeni isianze na kuishia kwenye u-Dr. tu. Hata wahandisi, wahasibu, mawakili, na wengineo manake huko tunakokwenda sasa hata hakueleweki. Sitashangaa siku moja Michuzi naye akaanza kujitambulisha kama 'Photojournalist Issa Michuzi'.....au Kibonde kuanza kujiita 'Presenter Ephraim Kibonde'.

Mtu ni raisi wa nchi lakini bado unaitwa Dr. tena udokta wenyewe wa kupewa mezani. Sielewi kabisa mimi.


NN,
Unatangaza vita?....mwendo mdogo mdogo kwanza lol
 
Hii kampeni isianze na kuishia kwenye u-Dr. tu. Hata wahandisi, wahasibu, mawakili, na wengineo manake huko tunakokwenda sasa hata hakueleweki. Sitashangaa siku moja Michuzi naye akaanza kujitambulisha kama 'Photojournalist Issa Michuzi'.....au Kibonde kuanza kujiita 'Presenter Ephraim Kibonde'.

Mtu ni raisi wa nchi lakini bado unaitwa Dr. tena udokta wenyewe wa kupewa mezani. Sielewi kabisa mimi.

mkuu..
mimi nimekutana kabisa na mtu
ambae bussiness card yake amejaza title tele
na title ya mjumbe wa halmashauri kuu ya ccm....
tunapoelekea ni kuwa watu wataanza kuitwa
mheshimiwa mmiliki wa gazeti la ijumaa,john shigongo
mheshimiwa mmiliki a coud media joseph kusaga...

na wengine itakuwa mheshimiwa diwani na mmilikiwa bar ya batotoz john robert...
very upuuzi
 
WOS..
I am sure ukisafiri umewahi pia kukuta kwa mfano mtu
ni ceo lakini hata kwenye bussiness cars yake unakuta jina tu na adress ya kampuni..

sasa ukija sisi....

unakuta ceo.director general,dr,shaaban malinyingi,.mjumbe wa nec ccm....

yaani aibu zingine bana....


Comedian Dr Boss..acha kunichekesha hahahahah
 
Back
Top Bottom